Masimango na kejeli kwa wanaoonekana wamechelewa kuoa/ kuolewa na kupata watoto uzeeni au umri ukiwa umekwenda

Masimango na kejeli kwa wanaoonekana wamechelewa kuoa/ kuolewa na kupata watoto uzeeni au umri ukiwa umekwenda

Mtu asipooa au asipoolewa hafanyi kosa lolote kimaadili. Hilo si kosa la kimaadili wala la kisheria.

Sio dhambi kutokuoa au kutoolewa.

Lililo kosa la kimaadili au kosa dhidi ya akili yaani dhambi ni: KUVUNJIKA KWA NDOA au TALAKA, UZINZI NA UASHERATI; PONOGORAFIA, MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE. Haya ndio mambo watu tunatakiwa tutafakari, tuyachunguze, tufuatilie; tujue yanasabishwa na nini, na kwa nini; halafu tuamue.

Hebu fikiria ni ndoa ngapi zinavunjika? Jiulize: ni ngapi? Jiulize; ni mateso kiasi gani watoto wanapata na kupitia kiakili na kimwili kwa wazazi kutalakiani? Ni wangapi wanateseka kwa makosa haya ya wazazi kutalakiana, magonvi, au kutengana? Madhara yake ni nini? Jiulize!!

Kwa kufanya uzinzi na uasherati, ni wanawake wangapi wamezalishwa na kutelekezwa? Wanawake wangapi wamepigwa mimba na kutelekezwa? Wangapi? Hao watoto wanatunzwa na nani? Haya sio mateso? Huu sio uuaji? Na hivi ndivyo mambo au mpango unapaswa kuwa? Hili ndilo lengo?

Huyo Mungu ambae waafrika mnapenda kumrejelea na kuficha udhaifu au ukatili au ubaya au mapungufu yenu, kwa kukosa kwenu uelewa wa mambo na elimu ya vitu, hakuna mahali amesema watu lazima waoe na kuolewa au wazaee. Hakuna!

Mwenye huu uthibitisho alete hapa.

Watanzania ni watu ambao hawatumii akili kabisa, ukiacha hekima na busara. Wanafungisha ndoa huko wanakoita makanisani na misikitini, lakini hawasimamii hizo ndoa walizozifungisha. Watu wanatalakiana, wanaachana kila siku. Kila uchao ni ugomvi, mafarakano kwenye hizo ndoa.

Wasivyo na akili, hekima, na busara, wameshindwa kushughulikia matatizo ya ndoa, sasa wanataka kuwabagua watu wasio na kosa kimaadili, yaani wale wasiooa na wasioolewa.

Huu ni wendawazimu mkubwa.

Ndugu zangu watanzania acheni kushikilia mambo na kudhani kwamba haya ni mambo yetu; na yale ni mambo yao.

Tupende kufikiri, kuchunguza, kufuatilia na kisha kuamua. Tuache kuchukua mambo kama yalivyo bila kujua yalianza vipi, wapi na kwanini.

Hivi kweli suala la mtu kutokuoa au kutoolewa nalo ni jambo zito linalohangaisha jamii au familia, kwamba mtoto wangu hajaoa au hajaolewa?

Mtu asieoa au asieolewa ana kosa nini kimaadili au kiakili; au hata kimwili?
Hapo unakosea kusema kutooa au kutokuolewa sio kosa. Ni kosa.

Ni sawa na kusema kutengeneza silaha na anayezitengeneza sio shida shida ni matumizi ya hiyo silaha. Sasa hiyo silaha isingetengezwa madhara ya silaha yangekuwapo?

So kimsingi nataka ufahamu jambo moja, kuna maisha nje ya mfumo wa Ndoa ambayo ndio haya yaliyotapakaa sasa na kuna maisha yaliyo ndani ya mfumo wa ndoa.

Ukisema sio kosa kuishi nje ya ndoa jua unahalalisha na kusema sio kosa kuwa single mother, sio kosa kulala na wanaume wengi, sio kosa kutembea na kuwapa mimba wanafunzi, sio kosa kuwaharibia mabinti wadogo direction kwa kulala nao kisha kuwatema na kwenda kutafuta binti mpya wa kumharibu, unasema ni sawa kutoa mimba, unasema ni sawa maisha ya kufanya kazi kwa bidii halafu pesa inaishia kununua makahaba na kulewa vitu ambavyo baadae ndio chanzo kikuu cha maradhi ya kuambikizwa na yasiyo ya kuambukiza mwilini.

Kwa kifupi unaposema ndoa sio necessary kwenye maisha ya kijana au binti maana yake unafungua mjadala mpya kabisa wa namna ya kuishi kwenye ulimwengu nje ya kanuni tulizowekewa za kimaadili. Hauwezi ishi nje ya mfumo wa ndoa halafu ukawa mstaarabu na kuwa comfortable at the same time. Pia mfumo wa maisha nje ya ndoa ndio huo huo mfumo unawaletea shida sana waliopo ndani ya Ndoa kushindwa kutulia na kufanya maisha yao kwa umakini na kuendelea kuimarisha jamii.

So tengua kauli yako kuwa ndoa sio lazima, cha msingi fanya kwenda kujielimisha kwann kuna ndoa na nini kinatokea kusopokuwa na ndoa.
 
Hapo unakosea kusema kutooa au kutokuolewa sio kosa. Ni kosa.

Ni sawa na kusema kutengeneza silaha na anayezitengeneza sio shida shida ni matumizi ya hiyo silaha. Sasa hiyo silaha isingetengezwa madhara ya silaha yangekuwapo?

So kimsingi nataka ufahamu jambo moja, kuna maisha nje ya mfumo wa Ndoa ambayo ndio haya yaliyotapakaa sasa na kuna maisha yaliyo ndani ya mfumo wa ndoa.

Ukisema sio kosa kuishi nje ya ndoa jua unahalalisha na kusema sio kosa kuwa single mother, sio kosa kulala na wanaume wengi, sio kosa kutembea na kuwapa mimba wanafunzi, sio kosa kuwaharibia mabinti wadogo direction kwa kulala nao kisha kuwatema na kwenda kutafuta binti mpya wa kumharibu, unasema ni sawa kutoa mimba, unasema ni sawa maisha ya kufanya kazi kwa bidii halafu pesa inaishia kununua makahaba na kulewa vitu ambavyo baadae ndio chanzo kikuu cha maradhi ya kuambikizwa na yasiyo ya kuambukiza mwilini.

Kwa kifupi unaposema ndoa sio necessary kwenye maisha ya kijana au binti maana yake unafungua mjadala mpya kabisa wa namna ya kuishi kwenye ulimwengu nje ya kanuni tulizowekewa za kimaadili. Hauwezi ishi nje ya mfumo wa ndoa halafu ukawa mstaarabu na kuwa comfortable at the same time. Pia mfumo wa maisha nje ya ndoa ndio huo huo mfumo unawaletea shida sana waliopo ndani ya Ndoa kushindwa kutulia na kufanya maisha yao kwa umakini na kuendelea kuimarisha jamii.

So tengua kauli yako kuwa ndoa sio lazima, cha msingi fanya kwenda kujielimisha kwann kuna ndoa na nini kinatokea kusopokuwa na ndoa.
Kweli kabisa na ndio maana wanalalamika kwa nini wazazi, ndugu na jamii inawauliza, kama hilo jambo la kutokuwa na ndoa si kosa la kimaadili kwa nini nafsi yako inakuuma kama huna kosa au hatia na wengine wamethibitisha kuwa kuwa wanaumia kuulizwa.

Ni bora mtu useme bado hujajipanga lakini sio eti sio lazima kuoa na ili hali unaonekana unaingiza wanawake tofauti tofauti kila kukicha.

Mimi nilipofika umri wa kuanzia miaka 28 wazazi na ndugu wa jirani walinishauri sasa na vizuri upate ndoa nikajipanda nilipofika miaka 30 nikaoa.
 
Nakutana nazo sana kwenye matukio ya kijamii,kiukweli niliplan kuoa 2014 ila niiyekuwa nae alimpata mwengine alivyo enda kusoma nikaplan tena 2017 still demu akarudi kwa ex-wake. Yaani mpaka sasa sijui nitaoa lini kwani hawa ambao ninao kutana nao wote vichomi, unaweza ukasema wanatumia template moja ya ujinga,kuendesha mahusiano.

Kuna dem mmoja tu alikuwa rafiki yangu kipindi nipo O-Level na Advance, yule nahisi ndiye kama alikuwa mke wangu. Sema ndio hivyo uoga plus udomo zege kipindi hiko,baadae tukawa tunasoma sehemu tofauti then sasa hivi kaolewa.

Ila swala la kuoa nimemuachia Mungu, sometimes unataka kuforce ila vichomi unavyo kutana navyo bora ubaki single.
 
Kuoa ni heshima full stop

Kuona kwako walevi wameoa haimaanishi kuoa siyo kitu cha maana na heshima.
Tusipingane na ukweli ,ili tujue mwanaume umekamilika kuoa hakukwepeki familia ni nguzo muhimu sana msichokijua vijana hakuna raha Kama umetoka kazin umerud na kimfuko cha mazaga madogo wanakimbia baba baba cha kumuomba mungu ni akupatie mke sahihi vyote vitajiset alafu Sasa mungu anakuangalia kwa jicho la pekee kwenye ridhiki bachela kulala njaa ni kawaida Ila si kwa Alie na familia anaechakalika oeni vijana na Kuna baadhi ya madili yanahusisha mpunga mrefu unaweza pishana nayo Kama huna family jamii inakuchukulia mhuni tu
 
Hapo unakosea kusema kutooa au kutokuolewa sio kosa. Ni kosa.

Ni sawa na kusema kutengeneza silaha na anayezitengeneza sio shida shida ni matumizi ya hiyo silaha. Sasa hiyo silaha isingetengezwa madhara ya silaha yangekuwapo?

So kimsingi nataka ufahamu jambo moja, kuna maisha nje ya mfumo wa Ndoa ambayo ndio haya yaliyotapakaa sasa na kuna maisha yaliyo ndani ya mfumo wa ndoa.

Ukisema sio kosa kuishi nje ya ndoa jua unahalalisha na kusema sio kosa kuwa single mother, sio kosa kulala na wanaume wengi, sio kosa kutembea na kuwapa mimba wanafunzi, sio kosa kuwaharibia mabinti wadogo direction kwa kulala nao kisha kuwatema na kwenda kutafuta binti mpya wa kumharibu, unasema ni sawa kutoa mimba, unasema ni sawa maisha ya kufanya kazi kwa bidii halafu pesa inaishia kununua makahaba na kulewa vitu ambavyo baadae ndio chanzo kikuu cha maradhi ya kuambikizwa na yasiyo ya kuambukiza mwilini.

Kwa kifupi unaposema ndoa sio necessary kwenye maisha ya kijana au binti maana yake unafungua mjadala mpya kabisa wa namna ya kuishi kwenye ulimwengu nje ya kanuni tulizowekewa za kimaadili. Hauwezi ishi nje ya mfumo wa ndoa halafu ukawa mstaarabu na kuwa comfortable at the same time. Pia mfumo wa maisha nje ya ndoa ndio huo huo mfumo unawaletea shida sana waliopo ndani ya Ndoa kushindwa kutulia na kufanya maisha yao kwa umakini na kuendelea kuimarisha jamii.

So tengua kauli yako kuwa ndoa sio lazima, cha msingi fanya kwenda kujielimisha kwann kuna ndoa na nini kinatokea kusopokuwa na ndoa.
Nadhani ingekuwa vema tukaelewa nini maana ya kutooa au kutoolewa.

Kufafanua hilo, naomba nirejelee Agano Jipya.

Yesu anawaambia wafuasi wake kwamba, (si nukuu rasmi) "kama mtu ataweza kuishi kama mimi (Yesu) atakuwa ametenda jambo njema sana duniani".

Aidha, Petro katika Agano hilohilo anawaambia wafuasi haohao kuwa, mtu asieweza kudhibiti au kukabiliana na tamaa za mwili, basi na aowe na aolewe.

Kutooa au kutoolewa maana yake ni kutoshiriki kufanya mapenzi au ngono, ni kutojamiana.

Kwa hiyo, hayo uliyoyataja hapo juu kwenye comment ni makosa dhidi ya ndoa. Yeyote aliye katika hali hiyo, amefanya kosa dhidi ya akili.

Kama mtu anazini, au anafanya uasherati, ni single mama au baba, huyo ameoa na ameolewa. Mtu yeyote aliye katika hali hii hawezi kusema hajaoa au hajaolewa.
 
Habari za muda huu marafiki,

Siku za hivi karibuni kumekuwa na hali ya kushangaza kustaajabisha kwenye jamii yetu na hasa huku mitandaoni.

Kumekuwa na wimbi la watu kuwasimanga, kuwakejeli na hata kuwacheka ndugu zetu, jamaa zetu na marafiki zetu wanaoonekana kwa vigezo, mitazamo na viwango vilivyowekwa kwenye jamii kuwa wamechelewa kuoa au kuolewa hivyo kuonekana wamepata watoto wa uzeeni.

Ni jambo linaloonekana kama la kawaida lakini kwa upande mwingine linasononesha na kuvunja mioyo ya watu walioamua kujenga familia.

Ni kauli za kitoto zinazoonyesha kuwa bado hawajakomaa kiakili kwenye ulimwengu huu uliojaa harakati na purukushani za kila aina.

Ningependa kuchukua nafasi hii kuwakumbusha hao wenye kuwakejeli wengine kwenye hili ya kuwa.

1) Maisha ni fumbo zito Sana ambalo mara nyingi ni wachache Sana wenye kufumbua. Mara nyingi mipango yako inaweza ikapishana na mipango ya Mungu.

2) Uhai na kifo ni vyake Mungu mwenyewe kwani hakuna ajuaye kuwa amebakisha muda gani wa kuishi hapa duniani. Wapo vijana wengi wametangulia mbele za haki wakiacha watoto wao na familia zao zikiteseka na kuwaacha wazee wakiendelea kulea watoto wao wa uzeeni mpaka wakijitegemea na kufurahia matunda yao. Hivyo kusema kuwa mwanaao akifika miaka kadhaa wewe utakuwa umeshachoka au umeshakufa ni maneno ya kufuru au ya mtu asiye na Imani kwa mola wake mlezi.

3) Kwenye maisha kila mtu Mungu amemuwekea wakati wake wa kufanya jambo lake kwa rehema zake. Wapo watu waliowahi kuoa lakini Mungu akawanyima watoto mpaka wanazeeka na wengine wanawapata uzeeni kabisa. Wapo watu wamejikuta wapo jela wakitumikia vifungo virefu na mpaka wanatoka umri umekwenda na wanaamua kujenga familia. Wapo watu walikuwa wanaugua kwa muda mrefu na hatimaye wakapona na kuanzisha familia. Hivyo basi kama wewe umewahi ni sahihi kwako lakini haiwezi kuwa makosa kwa anayeonekana amechelewa.

4) Changamoto za kifamilia na vifo.
Kuna mwingine anawahi kuoa lakini Kati Kati ya safari anawapoteza mke na watoto wote kwa pamoja Kwa ajali au maladhi ya kawaida na anaamua kuoa na kuanzisha familia upyaaa.

Kwa kifupi mambo na changamoto za kidunia ni nyingi zinazopelekea watu kuonekana wamechelewa kupata watoto au kuoa na kuolewa. Tujifunze kuwa wastaarabu kwenye maisha ya watu kwani hatujui matamshi yetu yanawaathiri vipi wenzetu.

Niko tayari kusahihishwa.

Nawasilisha.
Mkuu fanya I'ma uoe fanya jui chini uoe najuta kuchelewa kuoa japo Nina mtoto ambae hatuelewani nae
 
Back
Top Bottom