Maskini Baba Diamond, azidiwa ghafla

Maskini Baba Diamond, azidiwa ghafla

Hapa naona wengi wetu tumekua tunamtupia Baba Tifah lawama kwamba anapaswa kumsamehe baba yake.
Anyway.....
Pengine nianze kwa kuuliza kwambaa.... kwani kuna sehem mzee aliwahi lalamika kwamba alimkosea mwanae?
Na je, nikosagani ambalo mzee alisema kwamba amemkosea mwanae Diamond?
Pengine mimi nipo nje ya ulimwengu wa mwendo kasi ndio maana napitwa na mengi.
Mwenye kujua tafadhali...[emoji101]
 
Mondi alishatamka kuwa alimsamehe baba yake siku nyingi, na hata pesa anampaga, juzi kwenye Father's day pia hakumsahau baba yake.

Ila huyo mzee inaelekea anataka apewe care 100% kama anayopata Mama Mondi kitu ambacho ni impossible. Aliteseka na mama yake wacha ajinome na mama yake.
 
Baba ni bana tu, bila manii zake usingeujua uso wa dunia, bila kujali alikosea wapi, hakuna dhambi isiyosameheka..

Huyo mondi anaacha kumpa hifadhi babae anawapa hifadhi wanawake wa watu... Shule shule shule

Diamond shule ndogo ndio maana anahitaji degree jutambua hili..

Mumshauri
 
Huitaji kumaliza madarasa kuielewa hii habari ipoje,kila kitu hapo kimepangwa kwaajili ya kutangaza biashara kwa kutumia jina la DIAMOND kwa kujificha kwa huyo mzee kwa vile ameshindwa/wameshindwa (huyo mganga sijui Doctor sijui tabibu sijui manyaunyau) kumlipa DIAMOND.
 
Kwahiyo aliita waandishi wa habari wakati anaenda zahanati....? Muache avune alichopanda, diamond hasingekua star leo hii huyo mzee angemkubali ?

Muache asote tu

swali zuri sana, kwa mfano kama daimond angekua chokoraaa tu kule tandale hivi hizi drama zote zingekuepo? wababa jifunzeni kuwa responsible kwa watototo wenu hata kama mna ugomvi na mama zao
 
Mondi alishatamka kuwa alimsamehe baba yake siku nyingi, na hata pesa anampaga, juzi kwenye Father's day pia hakumsahau baba yake.

Ila huyo mzee inaelekea anataka apewe care 100% kama anayopata Mama Mondi kitu ambacho ni impossible. Aliteseka na mama yake wacha ajinome na mama yake.
Nilishawahi kumuona live bado ana nguvu hajafikia umri wa kukaa chini Na kutunzwa ni ugonjwa tu kwasababu hata tembea yake ya tabu,mi ningemshauri D amtibie afanye Kama anatoa msaada kwa Mtanzania yeyote mwenye shida pengine ampeleke hata nje ya nchi pengine akipona akipata nguvu ya kujitafutia ataacha kulialia.
 
Halafu wabongo wako vizuri hasa wale wa kambi nyingine habari ikimuongelea vibaya DIAMOND wataishadadia mpaka basi,lakini habari ikiongelea mazuri ya DIAMOND wao ndio wa kwanza kuyaponda hayo magazeti utasikia "kama habari imeandikwa kwenye gazeti la Shigongo si ya kweli" lakini hapa wanaichukua kama ilivyo bila kuangaliwa imeandikwa na gazeti lipi.
 
Diamond anakosea sana. Yaani anahangaika na Zari halafu anamuacha babake anateseka
Jane, baba yake alimtelekeza na mam a yake akawa na vimada. Nilimsikia Diamond akihojiwa. Akakiri kuwa kila mmoja aende zake maana alishawatupa. Akasema anampenda mama yake maana walihangaika wote mpaka akafikia hapa alipo. Sijui, nami ningelifanya hivyo hakika, potelea mbali
 
Mimi sipendelei mambo ya maselebriti wa bongo wala ulaya....lakini naona hii habari ni kama mtu anatafuta kiki tu au mnaonaje?
Kwani inakuwaje mgonjwa unaenda na kameramani kabisa?
hapa kuna
1. Wenye zahanati wanatafuta kiki
2. Magazeti ya udaku yanatafuta kuuza
3. Huyo mzee pia anatafuta kiki...
Ujumbe: wanaume na wanawake msitupe watoto wala kuwatelekeza hujui una mtupa nani,
pengine ni rais mtarajiwa aisee...
 
Diamond anakosea sana. Yaani anahangaika na Zari halafu anamuacha babake anateseka

Unadhani anafanya yeye kwa maamuzi yake? Mama yake ndo anamkazia, Mama hampendi kabisa huyu mzazi mwenzake, na atakua kamwambia mwanae asimsaidie hata shilingi mia. Diamond hana roho mbaya namna hiyo, anachangia madawati ashindwe kumtoa Baba yake?! Uislam gani huo!? Hivi na yeye anafunga?! Anyway dini inaruhusu kulipiza kisasi.
 
Duh haya mambo bwana tuwaachie wenyewe ila kama ni kweli baba anatia huruma sana.
 
Nakumbuka Qchief nae alikuwa hana mahusiano mazuri na baba kwa sbb kama hizo za kutelekezwa lkn alijiongeza wakayamaliza wakawa washkaji wazuri huyo huyo baba yake ndio akaja kumuokoa na uteja uliotukuka
 
Diamond anakosea sana. Yaani anahangaika na Zari halafu anamuacha babake anateseka
Dr Fadhili Haule anafanya biashara tuu..
Kwa yeyote mdadisi, ni rahisi kugundua kwamba huyo baba wa diamond aliandaliwa kwamba achukuliwe picha huku akionekana kusaidiwa na wahudumu wa hapo hospital, ili kijana apakaziwe na magazeti ya udaku.
Alafu... iweje mzee aende kwenye matibabu huku akiwa amejiandaa na wapiga picha?
Alafu.... kama mzee alikwenda kupata matibabu, kwanini aliwaita makanjanja wa magazeti ya udaku ili wakipake kwa mwanae?
Agghhhh....[emoji51] [emoji51] [emoji51]
 
Kwa nini ugonjwa wa baba asukumiwe lawama mtoto? Kwani Dai ndio kamletea maradhi? Acheni madaktari wamtibu Dai atafute hela ya kuendesha maisha yake.
 
Mmmmh

Promo ya so called dr fadhili tu hii... wamlipe mzee wa watu

Na kwa haya wanaume wanaotelekeza watoto kwa kigezo cha "atanitafuta" akikua mjifunze........
Teh Teh Dr Fadhili Haule ametengeneza scene zake vizuri sana yani hadi nimecheka...! Hivi huyu Baba alimzaa Diamond pekee? Na wengine wote aliwatelekeza kama Diamond?
 
usiangalie matokeo angalia na sababu ya matokeo pia...hawa wazee waliokula ujana enzi zao na kuwaacha watoto wao wakiteseka na mama zao huwaga siwaonei huruma kabisa.

Mimi pia yamenikuta kama hayo..naumwa nimelazwa Amana hospital na bi.mkubwa alikila pembeni uangu hana kitu baba yangu mzazi anashindana kuwatunza hela wakina Tx Moshi na Maalim Gurumo pale Amana Vijana center
asante
 
Back
Top Bottom