Maskini wenye hasira kali Zambia wamuua kwa kumchoma moto Mtanzania

Jamaa ni tajiri ana mali nyingi sehemu mbalimbali za Zambia. Hapo kwenye ajira ndo wengi watapoteza mwelekeo. Inasemwa kuwa wakati wa uhai wake alikuwa kaajiri watu zaidi ya 500.
Huyu mwamba, namuombea akiweka Mambo yake sawa, aje na nyumbani awekeze, maana kitaa pamekuwa pagumu kama jiwe!!
 
Apandacho mtu ndicho atakachovuna.
Marehemu huenda kavuna alichopanda aidha hadharani au sirini
Mungu anapopitisha hukumu hutumia sababu yoyote ile ili uhukumiwe
Ndugu acha kumtaja Mungu kwenye mambo ya kishetani. Mungu ndo alisema maskini wenye hasira wakaharibu mali za watu?
 
Nafikiria hapa tz wapo wa sa na wazambia pia,Moses law should be in action,tumesikia ndugu zetu wakilulumiwa kila mahali tokea huko mocambique ,sa,Zambia ,Kenya n.k
 
Kunywa maji mkuu
 
Ukiwa mtanzania kwa nchi za jirani unachukuliwa kama mbobevu kwenye ushirikina.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matajiri wengi wa Zambia hasa wenye Asili ya Nakonde, ama kutoka miji ya jirani na Nakonde, ama wanaokuja kununua Mzigo Tanzania, Wametajirika zaidi baada kuwa na urafiki na Watanzania!

Watanzania wanawapeleka kwa Waganga hapa Tanzania ili wawe Matajiri....!

Hata kama huamini Uchawi hiyo haindoi Ukweli wa uwepo wake!

Watu hapa wanawaona Wazambia wasio na akili kwa walichokifanya ila wamevumilia sana wakitafuta Mchawi ni nani, mpaka kuja kufanya walichofanya walikua na Ushahidi wa Mazingira!

Zaidi ya watu 100 wameuwawa vifo vikifuatana vikifanana, kunyofolewa viungo vya Binadamu.....! Miezi michache kupita Kaka wa huyo Mzambia Marehemu, anahukumiwa miaka 50 jela kwa kukiri kwake kuhusika na kifo cha Mtu mmoja ambaye nae alinyofolewa viungo vya mwili, majuzi kuna Marehemu amekutwa hana Viungo, wananchi kwa kupepeleza wakapenyezewa habari juu ya uhusika wa huyo Rasta ambaye ni Rafiki wa Tajiri wa Kizambia, ikasemwa kila akionekana eneo flani baada ya siku chake, mwili wa mtu aliyeuwawa unapatikana na yeye kutoonekana tena, wamemfata Raia wenye hasira, kumweka mtu kati anasema yeye anatumwa tu, anatumwa na nani...!?

Akamtaja huyo Tajiri YAKAIPA kwamba ndo huwa anampa kazi, Hasira za Wanachi zikawaka, safari kwenda kwa Tajiri ikaanza, Tajiri kuona Raia wana hasira akataka kuruka Ukuta ikashindikana, akatoa Bastola atishe Raia haikusaidia, yakaanza Maswali, wakambeba yeye na Marasta mpaka ndani ya Nyumbani, kufika ndani wakaanza kufanya Ukaguzi, kuna Chumba kimoja wakakuta Jeneza kufungua Jeneza kuna Vitu vya ajabu.....!

Kilichotokea ndo kilichosikika.
 
Mdogo wa marehemu kahukumiwa miaka 650 sio 50. Wananchi hawakukuta jeneza. Walikuta ottoman couch wakadhani jeneza. Kimsingi maskini wenye hasira hawakuwa na uhakika wa 100%
 

Attachments

  • FB_IMG_1695644008261.jpg
    28.6 KB · Views: 2
  • FB_IMG_1695644012057.jpg
    13.7 KB · Views: 2
matajiri nao wao na adabu,.Reginald mengi kabla ya kufa tweet yake ya mwisho aliandika "matajiri wanaishi kwa amani kwa hisani ya masikini"
We uliiamini hiyo tweets?kaa nao Karibu ndio utajua Wana hisani au vipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…