Maslahi madogo Clouds yamtoa Ruby Fiesta

Maslahi madogo Clouds yamtoa Ruby Fiesta

Kwani Clouds ndo nini? Wanapata kichwa halafu wawanyonye wasanii wetu!!! Hawana hela za kuwalipa wakae pembeni Hata Diamond alise na aliweka kiwango kuwa chini ya million 15 sifanyi show yoyote ile haijarishi ni nani kaandaa mbona yupo juu bado!!!! Ni wakati wa wasanii kutambua dhamani zao na kujitambua na kuachana na njaaa wataheshimika sanaa

Big up Ruby
 
Hapana hapo sijatumia upenzi kabisa sababu hata mada yenyewe haijaweka team mbili hapa tunaongelea mchango wa clouds kwa wasanii.

Kipimo kizuri cha kupima status ya artiste either anadrop au yupo on ni mauzo ya album (ipo kizamani) shows ( hii ya kisasa) commercials na coverage kwenye media.

Check shows za Jide mikoani tokea atoe ndindi na check za kina Mr II na Professor Juma Nature ambao nao wametoa single zao recently hawa nawaweka sababu ndio wameanza nae mziki au hata uwaweke hawa upcoming bado watatupwa mbali.

hapo ndio utajua status ya Jide na umaarufu wake upoje tokea clouds wambanie for years now.
Jide is Untouchable
 
Clouds ni ngumu kushuka hawa jamaa ni wabunifu tofauti eatv na radio
We angalia hata matamasha wanaoandaa clouds na east africa utaona utofauti katika mafanikio.
East africa wamejaribu kuwashusha clouds wamechemka hata watangazaji wao wazuri wamekimbilia clouds
Labda efm maana nasikia karibu watazindua tv yao pia na wakajitanua mikoani wanaweza kupambana na clouds
We hujui, rates za clouds zinadrop kila kukicha chukua hyo
 
Mkuu....Efm ina miaka mingapi tangu ianze? na imeshaifunika Clouds dar....Huko kwingine haijaifunika kwa sababu bado hawajapata frequency...The moment wanapata frequency clouds wanapotea.

Recently Efm ndio wamekuwa on top of ubunifu hadi Clouds wanahangaika hawajui cha kushika

Nimekwambia miaka miwili kwa sababu ndani ya muda huo TV yao itakuwa imeshaanza na watakuwa na frequency mikoa yote mikubwa.

Clouds hawana muda mrefu kwenye game...wameshafika climax

Na vile wamewekeza kwenye kuwanyanyasa watu...Anguko lao litakuwa kubwa
Sure mkuu watu wanadhani mchezo, luge anahaha now hajui aanze na lipi jide anampumulia huku majizo na efm yake huku eatv wee hana chake tena
 
Hii habari nina mashaka nayo kama ina ukweli wowote! Ruby hawezi kuwa stupid kiasi hicho wakati anafahamu kabisa bado hajaweza kusimama mwenyewe kwa miguu yake! Isitoshe, Ruby yupo na THT na hadi sasa nyimbo alizonazo sidhani kama zinafika angalau 3.

Kwa upande mwingine, zaidi ya 90% ya wasanii wanaishobokea Fiesta na wala si kwa sababu eti wanaogopa Clouds kuwabania bali zinawalipa kutegemeana na status zao! Na ndio maana utakuta wasanii wengi tu wanakuwa kimya kwa muda mrefu lakini wakiona msimu wa Fiesta unakaribia tu, wana-release single ili wakumbukwe! Wasanii wengi hawana show yoyote ya maana zaidi ya Fiesta. Kwa wasanii wengi, Fiesta si tu opportunity ya kutengeneza pesa bali ndio platform pekee kubwa inayowakutanisha na mashabiki wengi. Hawafiki hata wasanii 5 hapa wa kuweza kuidengulia Fiesta! Uzuri ni kwamba, hata wao wenyewe wanafahamu kwamba there's no way Kiba au Diamond apate sawa na Baraka De Prince au Q Chilla!
Acha uoga maisha ya nahitaji uthubutu
 
Mnaonekana hamjiamin NA hii ni hatar sana kwa afya ya maendeleo

Ni jambo zuri NA lenye manufaa pale unapooamua kusimama ww kama ww ktka shughuli zako bila kuwa tegemezi kwa fulan maana siku unayemtegemea akiacha kukusaidia bas unarudi zero and the vice versa is true.....
Me hadi naona aibu kwa uoga wa watu humu ndani, huko maofisini na vyuoni si wananyanyasika sana jamani? Ndio maana wachina na wahindi wanapiga wafanyakazi
 
Mtandaoni wa Tizneez ametoa exclusive ya kwanini Msanii Ruby hakuonekana Mwanza wala kupanda katika jukwaa la Fiesta wakati alikuwa mmoja wa wasanii waliosajiliwa...

Hivi Ndivyo mtandao huo ulivyoandika;
========

Exclusive Ruby Amezungumza mengi ila kati ya machache ni "Maslahi yamenifanya nisiende kwenye Fiesta, Kisa ni Clouds ndio nisiwe free na kuongea, end of the day it's not about clouds it's about my future.Katika shindano la super diva ilikuwa super diva mshindi atafanya Fiesta, wakati umefika lakini ntafanya Fiesta for nothing?

Mimi sitaki kuongelea price ambayo naipata sababu nahisi nikiongea sijui watu watajiskiaje ukubwa wa show ulivyo. ...Tunakuwa na menejiment ambazo zinaendesha wasanii kimabavu, unadhani kwanini @jidejaydee wanamuita komando?? alisema hayo rubby

Nini maoni yako?

Huyu ana safari fupi sana.... Kaanza vindumbwendumbwe mapema sana
 
Me hadi naona aibu kwa uoga wa watu humu ndani, huko maofisini na vyuoni si wananyanyasika sana jamani? Ndio maana wachina na wahindi wanapiga wafanyakazi

Unachanganya mambo! Hakuna aliye na tatizo na Ruby kutofanya show ya Fiesta! Issue ni kwamba, ilikuwaje alisaini mkataba wakati anafahamu maslahi ni madogo?! Ina maana hakusoma mkataba?! Sasa kama hakusoma ni tatizo la nani? Mwenyewe Ruby huyu hapa chini akionesha excitement baada ya kusaini:
Ruby1.png
 
Wabongo wengi waoga kishenzi yaan ndo maana wakija wageni mna nyanyaswa, na huwa mfanyi chochote hivo hivo, kwa sababu uonevu inabidi uwe unakemewa hapo hapo hakuna cha mpaka mtu ajipange
Khaaa!!
 
Wabongo wengi waoga kishenzi yaan ndo maana wakija wageni mna nyanyaswa, na huwa mfanyi chochote hivo hivo, kwa sababu uonevu inabidi uwe unakemewa hapo hapo hakuna cha mpaka mtu ajipange
Khaaa!!

ruby1-png.387442


- Huwezi kuwa Shujaa na things like this, msichana kakosea sana kajiharibia mwenyewe.

le Mutuz
 
Wabongo wengi waoga kishenzi yaan ndo maana wakija wageni mna nyanyaswa, na huwa mfanyi chochote hivo hivo, kwa sababu uonevu inabidi uwe unakemewa hapo hapo hakuna cha mpaka mtu ajipange
Khaaa!!
Afu mchina akimpiga mfanyakazii wake utawaona wanavyoshare video na picha zikizindikizwa na kukemea vikali kumbe kimoyomoyo wanaona ni sahihi
 
Uthubutu upi? Huo wa kusaini mkataba huku ukipiga vigelegele hadi una-post Instagram kwa mbwembwe zote halafu baadae unageuka ndo unasema ujasiri?! Ni nani anataka kufanya kazi na mtu asiyeheshimu makubaliano?!
Wao wamekiuka vingapi? Luge anavopenda ligi tutaona km atampeleka mahakamani
 
Acha ujinga wewe wa kuabudu radio ya mashoga...clouds ni nani mpaka anachotaka yeye ndo watu wakubali. Mziki wetu ulianza miaka mingi hata kabla ya hao clouds na ukasambaa. Na mziki wetu unaweza endelea sana bila hao mashoga. Walamba lips. Kikubwa ni self-determination. Harakati zitaendelea by any means necessary
Twende kwa hoja sio kashfa,maana ukiambiwa hilo jambo uthibitishe utaweza?Suala la msanii kutetea haki yake ni suala lake yeye binafsi hata kama isingekuwa clouds,kwa hilo nampongeza,na lazima tujue jamani risk takers ndio wanaomove kimaisha,kuna wakat hukutana na changamoto ila mwisho wa siku hufanikiwa,me namuona bint yupo sahihi,unakuaje muoga while Tanzania kuna redio zaidi ya 80?na zinaendelea kupata leseni.Kuamini kuwa clouds ndo kila kitu ni ishara ya kwamba hatuna maono.....Msanii atoe wimbo mzuri na atashine tu
 
Being underpaid is one thing,and being ''commando'' is another different story,...Asije tu akafungwa na mkataba waliowekeana awali(kama upo in the first place)..She is obliged to abide by contractual terms and conditions,or else........
Hilo nalo neno
 
Back
Top Bottom