Master J aliniambia sijui kuimba kwenye Bongo Star Search– Harmonize

Master J aliniambia sijui kuimba kwenye Bongo Star Search– Harmonize

anajua bwana acheni roho mbaya jamani..
angekua hajui asingehit.
alafu kwanini hamfurahii mafanikio ya wenzenu???
 
mkuu kwa mtu yoyote aliefuzu sound engineering mtu mwenye kuimbia puani kama huyu hawezi kuwa mwimbaji mzuri kwake tena huyu bahati yake siku hizi studio zipo mpaka vichochoroni enzi zile angeishia kuuza madafu na kahawa mziki angebaki kuwa msikilizaji tu
Samahani Mzee je uliwahi kumsikia Suleiman Mbwembwe? Au Hemed Maneti? Au Hassan Rehani Bitchuka? Wote hawa ni watu waoghani sauti zao kwa kutumia sauti ya kwanza au ya pili, mbona wamekuwa ni magwiji wa muziki? Tatizo lipo kwa mahaba ya sauti.
Unawakumbuka Mopero na Josky Kiambukuta. Kuna watu walikuwa ni wapenzi wa Mopero kwa kuwa alikuwa na sauti nene, lakini ukimsikia Kiambukuta yeye alikuwa na sauti kali. Ingawa Mwawaita wabana pua, lakini wanafanikiwa kuteka nyoyo za watu wengi.
Najaribu kumuangalia jinsi King Crazy GK anavyohangaika na muziki wake wa Rap. Pia nikiangalia soko la wanamuziki ambao walikuwa wanasimamiwa na Master J wanavyohangaika kutoboa kwenye soko gumu la muziki wa leo, siipati picha. Ila mahaba ya sauti yasifanye wasimamizi wa muziki kuwaponda baadhi ya vijana, kwani kila binaadamu ameumbwa na bahati yake.
 
Huyu dogo ana sauti kali huenda hata kuliko Diamond. Sauti yake nzuri na bahati ni kwamba kaingia kwenye kampuni inayosaka pesa kwahiyo atafika mbali. Tumuombee
 
Huyu wakuja mtupu kabisa, diamond kamchukua kibiashara ilienda wale wenye dau dogo anawapelekea huyo dogo wahangaike nae
 
Namkubali sana tena sana harmonize anajua anachokifanya anajua kuimba mpaka anaboa ya ni ile sauti ni adimu mpaka imemshinda simba bosi wake..... Big up harmonize kaza buti usikatishwe tamaa na wanafki wachache wanaokuzikilizs kila unapotoa hits song afu wanajifanya kukuponda kwenye social media honestly your the best singer.
 
Kama alishindwa ku-deliver Joakimu angefanyaje sasa..?
 
Kwani Bongo Fleva ina tabu gani, ukiweka maneno mawili Tu, 'Chura anarukaruka' na ukipata promo basi unapiga show za Fiesta.
 
Kwani Bongo Fleva ina tabu gani, ukiweka maneno mawili Tu, 'Chura anarukaruka' na ukipata promo basi unapiga show za Fiesta.
Wenyewe wamevimba vichwa utadhani wasanii wa dunia. Umaarufu umewachanganya...
 
Back
Top Bottom