Maswali 100 ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022

Maswali 100 ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022

Nimeona utitiri wa maswali.

Hao walioandaa hilo dodoso sijui waliwaza nini, yaani mimi na uzee huu nikae mtu ananiuliza maswali zaidi ya mia, siwezi.

Labda kuwe na posho ya wakuu wa kaya.
Daaah! Eti posho
 
Swali la 59 lakipuuzi sana. Mnataka kujua mitaji yetu ni shs ngapi na tuliipata wapi ili iwe nini?

Naona hilo swali limetungwa na Mwigulu Nchba akishirikiana na Neema Lugangira
Wanataka kuweka tozo hapo
 
Maswali mengi yanaingilia faragha za watu . Mfano mdogo ni huu :

62. Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, Je, ulimiliki au ulitumia vifaa vifuatavyo?
  • Simu janja/Kishikwambi
  • Simu ya kawaida
  • Kompyuta ya mezani (Desktop)
  • Kompyuta mpakato
63. Je, ulitumia kifaa hicho katika matumizi yapi?
Majibu ya maswali ya 62 hadi 63 yataiwezesha Serikali kupata taarifa za asilimia ya watu wanaomiliki na wanaotumia vifaa vya TEHAMA. Aidha, Serikali itaweza kupata taarifa za matumizi makuu ya vifaa hivyo vya TEHAMA kama vile kuwasiliana, kutafuta/kupokea taarifa kwa ajili kuboresha zaidi huduma hizo
Utadhani hiyo internet na GB wanatununulia.!
Hizo anwani za makazi mliziweka lini? Nape ametembea na chopa hatuoni lolote!! WaTz mnaendelea kutufanya mazuzu!?
 
Jamani niuweni Niueniiii......
Man U leo wamekaza kwenye mkesha wa sensaa...
 
Nimeona utitiri wa maswali.

Hao walioandaa hilo dodoso sijui waliwaza nini, yaani mimi na uzee huu nikae mtu ananiuliza maswali zaidi ya mia, siwezi.

Labda kuwe na posho ya wakuu wa kaya.
Kweli kabisa! Ikiwa karani wa sensa analipwa posho kwa kuulizai, vipi anayejibu maswali hayo!
 
Nimeona utitiri wa maswali.

Hao walioandaa hilo dodoso sijui waliwaza nini, yaani mimi na uzee huu nikae mtu ananiuliza maswali zaidi ya mia, siwezi.

Labda kuwe na posho ya wakuu wa kaya.
Sensa lazima iwe na maswali mengi ili kupata takwimu halisi za raia, makazi na shughuli zao za kiuchumi.
 
hao makarani watembee na polisi maana kuna maswali yamekaaa kimchongo ili makarani wapigwe kama hilo swali la 3z😅😅😅
 
Maswali mengine hayakuwa na maana lakini ndio hivyo wenye kujiona wako na akili sana wameona yanafaa kuwepo.

Any way tunawangojea waje, binafsi nitawapa ushirikiano lakini naamini kuna sehemu watajikuta na hali ngumu kutoka kwa watu walio vurugwa.
 
Back
Top Bottom