Maswali na Majibu kuhusu Kitabu cha Mohamed Said

Maswali na Majibu kuhusu Kitabu cha Mohamed Said

Samahani kulia kwa JKN ni Liwali Ahmed Saleh.

Unaniambia Bilal Mshorwa alikuwa liwale Tb na Ahmed Saleh alikua liwali Dar je kila Mkoa Wa Tanganyika ulikuwa na liwale au nibaadhi tu ya mikoa na kama ilikuwa na maliwali je kazi ya miliwali ilokuwa nini na mikoa iliyo kuwa haikuwa maliwali kwa nini haikuwa maliwali?
 
Sharif kulia kwa JKN ni Bilal Mshorwa liwali kutoka Tabora na kulia Ahmed Saleh liwali Dar. Ntakufahamisha kuhusu Mangara Tabu.

Sheikh Mohamed Said,

Huyo Bwana Liwali Bilal Mshorwa...nafikiri huyo itakua ndo Babuye Bwana Bashir Mshoro...japo sina hakika kubwa kwalo?!

Hawa ndugu zetu kama ndo wao ,basi family yao ina history ndefu pale Tabora khasa kwenye Ilm,biashara na mangineyo!

Nafikiri naliwahi kuzungumza kiduchu na Kahtaan,kuhusu watu/family hiyo...kwenye thread fulani humuhumu-JF!

Bwana Bashir Mshoro,pana wakti alikua ndo Chief Accountant na baadae Branch Manager wa ile NMC pale Arusha.

Pia aliwahi kuwa mmojawapo ya ma-Commisioners wa awali pale TRA...mara ya mwisho nalisikia alikua kwenye shughuli za siasa na aliwahi kugombea Ubunge pale Tabora mjini!?

Nalimfahamu huyo Bwana kupitia mmojawapo ya Uncle zangu...ndo nikapata hiyo history kiduchu ya family yao pale Tabora na ukarimu walokua nao kwa ndugu zao na wageni woote walokua wakipitia pale Tabora zama hizo,kwa shughuli mbalimbali!

Nasikia yakua,pia walikua na Madrasat/Islamic Seminary kubwa pale Tabora zama hizo...na wakitoa Ilm kwa ndugu na jamaa wengi mno kutoka takriban pembe nyingi za hiyo Tanganyika na hata Zanzibar!?

Nitajaribu kumtafuta huyu Bwana Bashir Mshoro ili kuthibitisha haya!?...na kama ndo wao,basi nitakujuza pindi tukikutana penye majaaliwa.

Bakhti mbaya huyo Uncle yangu alokua very close na Bwana Bashiri Mshoro...amefariki/ametangulia mbele ya haki maskini,myka michache ilopita! Maana walisoma woote pale Tabora School,na Wazee Wao/families zao pia zikijuana na kufahamiana kwa ukaribu mno.

Ahsanta.
 
Somo hilo lataka wasaa.

Mzee Said, kwenye kitabu chako kuna picha ya wamama/wadada wengi Waafrika wamekaa kwenye viti na kuvalia nguo za kimagharibi, Mwalimu Nyerere kakaa katikati yao, pembeni kabisa yupo Sheikh Takadir kakaa halafu nyuma wamesimama kina Rupia, Dossa na Sykes; hao kina mama/dada ni kina nani na walikuwa na nafasi gani katika mkutano/jumuiya hiyo?

KK: gombesugu
 
Last edited by a moderator:
20140106_181038.jpg


Ritz,
Picha hii ilipigwa mwaka wa 1968.

Katika picha hii kuna vijana kutoka ukoo wa Tambaza, Sykes, Mwapachu na Mtemvu.
Wazee wa hao wote wameacha alama katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Inawezekanaje mimi nisiijue historia ya watu hawa na mchango wao katika kupigania uhuru
wa Tanganyika?

Mimi ni mmoja wa hao waliopo kwenye picha hiyo.

Dah! hii picha, hawa kaka zangu kabisa. Wengi wao hapo nawaona hivi, nilipokuwa mdogo, huwa nikiwaona sasa hivi nnacheka jinsi nikikumbuka walivyokuwa wakitesa enzi zao na sasa walivyozeeka na kutulizana.

Nilikutana na Wendo juzi juzi alinitia simanzi alipokuwa akibubujikwa na mchozi nilipoongea nae kuhusu Marehem Yusuf Zialor. Inna li Lllahi wa Inna Illahi Rajiun.

Kwa haraka haraka, nimeweza kukutambua Wewe, Wendo, Yusuf, Kleiyst naomba nikumbushe na hao wengine.
 
kwa nini watawala hawataki historia ya kweli? hii inasababisha vijana kuwatukana watangulizi, mwisho tanzania itavurugika
ni vema ukweli ubakie ulivyo.
 
Tunaendelea...

Mkuu Udadisi,

Nakusoma na pia nakufuatiza katika hizi jitihada zako za kujaribu kuleta maboresho katika andiko/kitabu hicho cha Maalim Mohamed Said!

Utakapofikia tamati,mie binafsi tajaribu kumtumia/kumpelekea yeye Maalim Mohamed Said haya masuali kwa mkono!

Nina hakika pindi akipata fursa atakujibu...nami takuletea majawaba/"masahihisho" uloulizia/yalokutatiza!?

Basi shaka isiwepo...shughuli za kitaaluma kama hizi zataka wasaa,kutuama na majadiliano yalo mema!

Nakutakia siku njema!

Ahsanta sana.
 
kwa nini watawala hawataki historia ya kweli? hii inasababisha vijana kuwatukana watangulizi, mwisho tanzania itavurugika
ni vema ukweli ubakie ulivyo.

Mkuu,

Hao watawala,kama wakiamua kuruhusu history ya kweli izungumzwe/isomeshwe...ina maana wao watakuwa wamevuliwa nguo na kubaki watupu,mchana kweupe!

Kwa kifupi,kama historia ya kweli ikielezwa basi hata ile myth tuliyonayo juu ya yule "Baba wa Taifa" na wafuasi wake/watawala wangine itatoweka na watapoteza thamani yoote ya kulazimisha...wanayo enjoy hivi sasa!? Daah!

Yaani history ya kweli imefichwa ili Watanzania waendelee kuwa misukule!? Duuh!

Na excuse ya kitoto inayotumika ni ya kwamba ati Maalim Mohamed Said ni "mdini" na ni mtu "hatari"!? Daah!

Matokeo ya cheap propagandas kama hizi...ndo pia zimewafanza Wanataaluma wangi mno wa khasa kutoka Afrika,kuishia/kutumikia katika Taasisi za Western World! Maana huko ndiko wanakothaminiwa kuliko hata makwao!

Sasa,mfano kiduchu wa karibu ndo kama hivi tuonavyo mnyanyaso afanziwao Maalim Mohamed Said na kutothaminiwa hapo nyumbani na hiyo Serikali yetu!? Daaah!

Ahsanta sana.
 
Maalim Mohamed Said umetiririka vizur mno....endelea kumjibu huyo ndugu Udadis kwan kupitia wewe na yeye wengine tunapata maarifa yasiyokifani. Binafsi maandiko yako sijawahi kuyaona kupitia maswali yake napata burudani makini kuhusu historia yako na wazee wako.
Wewe ni mtu muhimu kutupasha habari zilizofichwa hata hivyo zile makala zako za mambo ya dini zinanihuzunisha sizani kama zinajenga umoja baina yetu.
 
Nimefuatilia kwa Makini saana Toka Hoja hii imewekwa hapa.

Kwanza hongera saana Mdadisi kwa kuthubutu na kuonuesha nia ya kukiosoa Kitabu hicho cha " Mohamed Said" .

1.Umesimamia maswali ambayo mpaka sasa "Mohamed " hajayatolea ufafanuzi kamili.
Mfano swali la kwanza na la pili , lilimuhitaji " Said" kutoa ufananisho kwann aliamua kusema hayo aliyoyasema ,ushaidi ni nn haswa,ila umeshindwa kusema mpaka sasa ..na badala yake umesema kua ,umeandija kama ulivyosimuliwa ba waliokuwepo" statement yako hiyo inadhihirisha ulichokiandika hukikifanyia uchunguzi ,bali ulikiweka kama kilivyo . { Hivyo basi mpaka sasa hakuna ushahidi wowote ( physical evidence) juu ya hayo uliyoyasema .}

2. Uandishi wako kwenye hicho kitabu pamoja na utetezi wako unaondelea hapo JF , nadhani lengo lako halikua kufichua watu waliofichika katika historia ya uhuru wa tanganyika ,bali lengo lilikua ni kuuonyesha mchango wa Dini ya Kiislamu kwenye uhuru wa Tanganyika.
Ulichokifanya ni kizunguka tu.
Nasema hivyo kwani Watu wote unaowataja ni wa Dini ya Kiislamu. Je unataka kuniambia wote ambao hawakusikikia katima historia ya uhuru wa Tanganyika ni Waislamu.
 
Back
Top Bottom