Udadisi,
Unachofanya sio kuuliza kwa ajili upate jawabu ya maswali, unachokifanya ni cross examination ya kumsuta Maalim Mohammed Said. Kama bingwa wa kufanya research kwanini hufanyi yako kwa nguvu zako halafu ukatoa counter sessith au rebutal book dhidi ya kitabu chake? Ninachokiaona hapa ni kama vile undegraduate anafanya utafiti lakini wakati huo huo unqogopa kutumia marejeo ya kitabu chake kwa sababu yana maana na humpendi au umeshawishiwa kuwa usitumie marejeo katika maandishi yake lakini moyo haukupi.
Pls jifunze kujieleimisha kwa upole na juhudi sio kukebehi kazi za watu na hali wewe mwenyewe ni mwanagenzi bado.
Averoes,
Mambo haya yana matatizo yake kwa hawa ndugu zetu.
Kilipochapwa hiki kitabu Uingereza kikaja nchini na kuanza kusambazwa kilileta
mtafaruku mkubwa.
Kubwa zaidi cha kwanza ni kuwa ''brains'' nyuma ya TANU hakuwa Nyerere
bali Abdulwahid Sykes.
Wapenzi wa Mwalimu Nyerere walipigwa na mshtuko mkubwa wa kufa mtu.
Kiasi kitabu na mimi nikajadiliwa katika ngazi za juu kuwa huyu Mohamed Said
ni nani?
Nikafahamika kuwa ni kijana wa Kidaresalama na wazee wake walikuwa ndani
ya harakati za uhuru na wakifahamiana na Nyerere toka alipofika Dar es Salaam.
Kuna waliotaka ''nishughulikiwe'' kwa kuandika kitabu hiki.
Kuna mmoja akauliza, ''Huyu Mohamed aliandika hiki kitabu kwa Kiswahili
kwanza kisha kikatafsiriwa?''
Hii ilikuwa husda.
Hata huyu Mswahili atakuwa na Kiingereza hiki?
Kuna katika jamaa zetu heshi kuandika akisema kuwa, ''Ukisoma kitabu
cha Mohamed Said utajua kuwa kimeandikwa na ''native speaker.''
Hasad inakula moyo wake.
Alichokiona katika kitabu kizima ni hicho Kiingereza basi na kikamuuma.
Nakala moja ya kitabu hiki kipo East Africana Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Wanafunzi wanakatazwa na walimu wao wasikiweke katika rejea zao kwa
kuwa Mohamed Said si ''academician.''
Kwa utangulizi huu unatosha kuelewa vipi ndugu zetu wanavyokitazama
kitabu hiki na wanavyotuangalia.
Kwa hiyo basi kwa haya niliyokuwekea hapa nadhani wewe utakuwa na maswali
mengi ya kujiuliza.
Hii cross examination mimi hainipi tabu hata kidogo.
In Sha Allah nitatoa ushirikiano wa kutosha kabisa kwa
Mdadisi.
Nina kitabu cha shule za msingi, ''Torch on Kilimanjaro,'' Oxford University Press,
Nairobi toka 2007.
Oxford kwa utaalamu wao huwa hawachapi kazi mbovu.
Hiki ni kiabu cha mwanafunzi wa msingi kujifunza Kiingereza na wakati huo huo
kusoma historia ya nchi yake.
Huu ni mradi wa Afrika ya Mashariki na Kenya wanavyo vitabu kama hiki cha kwangu
maarufu ni, ''The Kapenguria Six,'' kuhusu kifungo cha Kenyatta na wenzake.
Wizara ya Elimu wamekipiga vita.
Hasad inawala na mfumo uko kazini.