Karibu kwenye ukurasa wa maswali na majibu kuhusu Kitabu cha 'The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968): The Untold Story of the Muslim Struggles Against British Colonialism in Tanganyika'. Ukurasa huu ni tofauti na ile mingine hivyo tunaomba isiunganishwe. Hapa tunajikita katika kuhakiki maandishi halisi yaliyomo humo ili kukiboresha kitabu n.k.
Hivyo, ni ukurasa unaoratibiwa. Nitakuwa naweka maswali yanayohitaji ufafanuzi/uthibitisho. Tuanze na hayo hapo chini.
1. "Aziz Ali Dosa was the first African to own a car and was always chauffer driven" (p. 30)
2. "The two [Kleist Sykes and Aziz Ali] were the only Africans in Dar es Salaam permitted by the government to drink beer" (p. 31)
3. "The Germans halted fighting [in World War 1] throughout Tanganyika for seven days in honour of Affendi Plantan [a.k.a. "Mohosh", "Chief of the Imhambane" and husband of "Sykes Mbuwane's sister"] (p. 35)
4. "In a strange twist of fate, Abdulwahid's driver [?] in Burma came to be one of the top brass in the Tanganyikan army" (p. 55)
5. "It was here [Imphal, Burma] on Christmas eve of 1945 that Abdulwahid and other askaris, including his young brother Ally and James Mkande, made a pact to found a political party when they returned home after the war...The name of the party was to be Tanganyika African National Union (TANU). Ally Sykes remembers that Abdulwahid wrote the name of the proposed party in his diary" (p. 57-58)
6. "he [Abdulwahid], certainly no match for [Erika] Fiah" (p. 69)
7. "Stanley [Street] (called Aggrey Street after independence in honour of Dr Aggrey, and later to be renamed Makisi Mbwana Street after one of the founding fathers of TANU" (p. 71)
Mdadisi,
Kuhusu TANU na Abdulwahid Kalieni Camp, India baada ya Vita Kuu
ya Pili wakati wanasubiri kurudhishwa Tanganyika hili wala si kubwa.
Labda ungeniuliza jinsi alivyowaoganaizi askari wa Burma Infantry 6
Battalion wengi wao wakiwa kutoka Tanganyika na kuwaambia kuwa
wakirudi nyumbani waanzishe chama cha siasa.
Labda swali lako lingeanzia hapo.
Au ukipenda uanze na baba yake Kleist Sykes na kuasisi African
Association mwaka wa 1929 na Al Jamiatul Islamiyya 1933 fi Tanganyika
vyamaviwili ambavyo ndivyo vilivyokuja kutoa uongozi katika TANU 1954.
Mdadisi,
Pole sana najua shida na tabu iliyokufika na hii si wewe peke yako.
Unawaza vipi mbona historia imerokodi Nyerere ndiye aliyeanzisha TANU?
Mbona kwa miaka hii yote haya asemayo Mohamed Said hayakufahamika?
Mimi msimamo wangu siku zote umekuwa kuwa inawezekana Nyerere alikuwa
na TANU katika kichwa chake toka yuko Butiama.
Hili halina tatizo, tatizo ni pale ''version'' nyingine ya TANU hii ya Abdu Sykes
inapopigwa vita.