KERO Mataa ya Bagamoyo Road yamekuwa Kero kwa watumiaji wa barabara hiyo

KERO Mataa ya Bagamoyo Road yamekuwa Kero kwa watumiaji wa barabara hiyo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

DMN

Member
Joined
Jun 13, 2020
Posts
21
Reaction score
19
Habari Zenu,

Mimi ni mkazi wa Dar es Salaam na ni mtumiaji wa barabara ya Bagamoyo Road. Kila siku napita kwenye barabara hii kwenda katika majukumu yangu ya kila siku, lakini aisee, mataa ya barabara hii, kuanzia njia panda ya Goba Masana hadi hapa Tanki Bovu na njia panda ya kwenda Kawe, hayafanyi kazi kwa muda sasa. Hali hii si salama kwa watumiaji wa barabara hii, kwani ajali zimekuwa nyingi kutokana na kila mtu kujaribu kuwahi.

Wahusika, tafadhali tunaomba marekebisho ya mataa sehemu hizi ili kuondoa kero hii na kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara.
 
Kama taa haziwaki, na iwapo hakuna traffic, sheria inasema umpe nafasi wa kulia kwako apite.

Mfano, wewe unayetokea Tegeta kwenda Mjini unapaswa kumpa kipaumbele yule anayetokea Goba.

Tatizo madereva wengi mnataka mashindano na ubishoo barabarani.

Mkiambiwa msome sheria za usalama barabarani hamtaki.

Ndiyo maana huwa ninawazodoa kila mara.

Acheni ujinga wenu!
 
Kama taa haziwaki, na iwapo hakuna traffic, sheria inasema umpe nafasi wa kulia kwako apite.

Mfano, wewe unayetokea Tegeta kwenda Mjini unapaswa kumpa kipaumbele yule anayetokea Goba.

Tatizo madereva wengi mnataka mashindano na ubishoo barabarani.

Mkiambiwa msome sheria za usalama barabarani hamtaki.

Ndiyo maana huwa ninawazodoa kila mara.

Acheni ujinga wenu!
Nisawa unayo sema hivi hawa boda boda na bajaji akili zao unazijua viziri na wawo ndo wanaongoza kugogwa au kuganga mtu kwenye mataa.. lakini pia sio sawa unakaribia mwezi au wiki kadha mataa kuto kufanya kazi tena barabara kubwa kama ile
 
Back
Top Bottom