Matokeo ya Maalim Seif Kumtambua Karume

Nyie wazanzibari mnajidanganya tu; mkibakia peke yenu bila sisi wabara mtachinjana kama kuku wa kienyeji!! Huyo mtoto wa Sultani anawachanganya tu.
Wewe Bulesi - ya Ngonswe mwachie mwenyewe Ngoswe!!!!
 
hapana haukuwa mchezo wa kuigiza, unakosea kitu kimoja tu ndugu yangu, wanachama hawakutaka kumpiga, kilichotokezea ni baadhi ya wanachama kutopendezewa na kauli ile, hasa kutokana na mtiririko vile maalim alivyokuwa akielezeya, hivyo kupiga makelele ya "haiwezekani, hatumtambii, viongozi mshanunuliwa n.k" ...nilikuwepo na sikushuhudia mtu yeyote aliyekuwa na lengo la kumpiga maalim ...ni jambo kubwa sana kwa huku kwetu hilo, twaheshimiana sana!

walioathirika kwa kipindi chote kwa kweli ni wananchi wa kawaida, wote wa CUF/CCM n.k ... inshallah tutegemee mabadiliko makubwa baada ya mapatano haya, and this time it's really serious, labda kutokana na kutoshirikishwa kwa vyama, especially CCM.
 
cuf waigizaji wazuri tu.
CCM wanamtayarisha Seif kuwa rais wa Zanzibar 2010 kupitia chama chao....
Akishindwa maalimu kama kawaida wakati watu wanauana yeye atapanda dege kwenda ulaya na atatoa kauli zake akiwa ulaya.
Subiri wapigwe chini tena 2010 utasikia zao tu................. tumeonewa.......wameiba kura and the like!
 
Point less afadhali ungenyamaza..pumba tupu..unatetea uwizi wa kura unaofanywa na CCM ambao kila mtu anajua? kichwa kiko salama au ushabiki imekuondoa akili..mgonjwa wewe
 
Wewe na nani? wenye kutaka vyeo hurekebisha njia kwanza bara zanziba wanaenda kumalizia kusafari..ukishajua wapi kuanzia safari ni rahisi kujua wapi kumalizia..
Ni kweli kabisa lakini kumbuka hao walioanza kurekebisha njia bara walikuwa na mizizi Zanzibar...wanajuulikana mpaka na watoto wadogo...hata kwa wizi wizi walikuwa wanaelekea elekea kukubalika na wezi wenzao its different case for Khatib "Msakatonge"
Nenda zako wewe upemba utakuua ukipewa dozi yako unafuka kama joka kifutu! Seif hana jipya uroho wa madaraka ndo unampeleka puta yeye alisimamia hayo yote kutendeka na iwaje leo hii awe mkali wa urasimu wake! huu twaita kuunyea mkono!
Sijakuelewa vizuri..notwithstanding that...you dont know Maalim Seif the way Zanzibaris know him...he is the man of the people...the lack of only one man one vote election denies him the state house.
 
UHUSIANO kati ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Dk Amani Karume na Chama cha Wananchi (CUF), unaonekana kuendelea kuimarika baada ya viongozi wa chama hicho jana kumsindikiza rais huyo katika hafla ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu Maalim Seif jana walimsindikiza Karume katika kutunukiwa shahada hiyo iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki.
Baada ya rais huyo wa Zanzibar kutunukiwa shahada hiyo, mshereheshaji alitangaza makundi ya picha za pamoja ambapo kundi la kwanza lilikuwa la Karume na viongozi wa siasa; Kundi hilo ndilo lililowashirikisha pia viongozi wa CUF.
Kabla ya kupiga picha Maalim Seif alikwenda kumpa mkono wa kumpongeza Karume akafuatia Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na wakafuatia wengine.
Hata hivyo, viongozi hao wote jana hawakuwa tayari kuzungumzia kwa undani walichozungumza wakati walipokutana.
Rais Karume alisema tofauti kubwa iliyokuwepo visiwani humo ni ya kiitikadi za kisiasa hali ambayo alibainisha kuwa sasa imekuwa historia kutokana na CUF, kutangaza kumtambua rais huyo.
Novemba saba mwaka huu, Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif aliwatangazia mamia ya wafuasi wa chama hicho kisiwani Pemba kwamba chama hicho kimeamua kumtambua rasmi Rais Karume.
Pamoja na hatua hiyo ya CUF, kupongezwa na watu mbalimbali zikiwamo taasisi za kimataifa na mabalozi, ilikuwa mwiba kwa wanachama wa CUF, ambao wengi wao waliangua vilio baada ya kusikia kauli ya Seif.
Kauli hiyo mpaka sasa imeibua makundi miongoni mwa wanachama wa CUF, huku baadhi ya wanachama hao wakimuunga mkono Seif na wengine kumpinga.
Akizungumzia hali hiyo jana, Seif alisema kulikuwa na chuki ya dhahiri miongoni mwa Wazanzibari kwa misingi ya kisiasa na kuwa hali hiyo ndiyo iliyofanya watu wakalia kama watoto wadogo, baada ya kusikia kiongozi wao huyo kutangaza kumtambua Rais Karume.
“Kwa hatua tuliyofikia tutaiepusha nchi yetu na mambo mengi mabaya, hatua hii imefikiwa kwa maslai ya Zanzibar, tumechoswa na migogoro Zanzibar, nyiye waandishi simnajua kuwa sisi wazanzibar tuna matatizo yetu wenyewe,… basi hayo ndo tunataka tuyamalize,†alisema Karume.
Alisema anaamini kuwa yeye na Seif ndio viongozi wakubwa Zanzibar hivyo hatua yao ya kuamua kumaliza tofauti zao za kisiasa itasaidia kuchochea maendeleo ya visiwa hivyo.
Katika hali ambayo haikuzoeleka hapo awali kwa viongozi hao wa CUF wote kwa pamoja walimpongeza Rais Karume kwa kutunukiwa shahada hiyo ya heshima na kusema kuwa alistahili kutokana na juhudi zake za kuvipatia visiwa hivyo amani na maendeleo.
Katika siku za nyuma viongozi hao wa CUF, walionekana kupinga na kukejeli kila kitu kilichokuwa kikifanywa na Serikali ya Mapinduzi na wakati mwingine hata vilivyokuwa vikifanywa na Serikali ya Muungano.
Kwa upande wake Karume alisema kwa sasa wameamua kuachana na siasa ya zamani na kuwa lengo lao ni moja tu la kuipigania Zanzibar na wananchi wake.
Alisema wameamua kushirikiana ili kuhakikisha kuwa chaguzi mbalimbali zinazo fanyika visiwani humo, haziwi chanzo cha mitafaruku bali kuwaunganisha wazanzibari.
Chama cha Wananchi CUF kila wakati kimekuwa kikipinga matokeo yatokanayo na chaguzi mbalimbali hali ambayo wakati mwingine ilisababisha umwagikaji wa damu visiwani humo.
Katika siku za hivi karibuni kulikuwa kunamsuguano mkubwa uliohusu uandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura, hali iliyofanya CFU kutisha umwagikaji mwingine wa damu endapo matakwa yake yasingetekelezwa...

source:hakinaumma.wordpress.com
 
Viongozi wa CUF wameshaahidiwa nyadhifa.....Maalim....Waziri Kiongozi katika serikali ya mseto. Mchezo ni ule ule, kudumaza demokrasia kwa kisingizio cha serikali ya mseto. Ukishaamua kupigania haki na hasa kile unachoamini, unatakiwa kupambana mpaka mwisho na si kuwa ndumilakuwili. Maalim na uongozi wa juu wa CUF wameamua kula matapishi yao kwa ahadi zitakazowatokea puani siku za usoni. Sasa ndio wamehalalisha CCM waendelee kutawala kwa mizengwe mpaka hapo kitakapokuja kizazi kingine baada ya kizazi cha Maalim na Prof kuishia.
 
HAKUNA MASHARTI TULIYOWEKEANA NA SEIF-KARUME

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume, amesema hakuna masharti waliyowekea na Katibu Mkuu wa Chama cha CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, walipokutaka hivi karibuni, Ikulu ya Zanzibar.
Amesema hakuna masharti isipokuwa sharti lao kubwa ni kusameheana na kusahau yalitopita kwa kurejesha udugu katika kudumisha utulivu na amani kwa ajili ya kuwaletea maendeleo ya wananchi wa Zanzibar.
Rais Karume aliyasema hayo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar mara baada ya kuwasili akitokea Dar es Salaam, kwa ajili ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Falsafa ya Udaktari wa Sayansi na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, shehere zilizofanyika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Aidha alimpongeza Maalim Seif Sharif kwa ujasiri mkubwa wa kwenda kuwatangazia wanachama wake katika mkutano wa Jumamosi iliyopita uliofanyika Kibandamaiti ya kumtambua Rais Karume.
Alifahamisha kuwa Seif baada ya kukaa na Baraza kuu la CUF, na kuona kuona Wazanzibari wote ni wamoja na inafaa washirikiane kuleta maendeleo na kulinda utulivu na amani nchini.
"Wazanzibar wote ni ndugu wasikubali kutofautishwa na visiwa vya Unguja na Pemba, na visiwa vidogo vidogo vya Tumbatu, Kojani, Fundo na Uzi, kwa vile kila mmoja anazunguka katika familia hizo hizo na wengine kuoana", alisisitiza.
Dk. Karume alieleza siku zote anaomba dua nchi hii iendelee kuwa ya amani na utulivu, ambapo hadi sasa hakuna mtu anayebughudhiwa.
Alifahamisha kuwa, anaomba dua uchaguzi wa mwakani ufanyike kwa utulivu na amani, ambapo mtu atakayeshindwa au kushinda wapeane mikono kwa kupongezana kwa ajili ya maendeleo ya mustakabali wa Zanzibar.
Hata hivyo, aliongeza kuwa yupo tayari kuteuwa nafasi mbili za wajumbe wa CUF kuingia katika chombo cha kutunga sheria cha Baraza la Wawakilishi iwapo atapelekewa majina.
Rais Karume akiwa na mke wake, Mama Shadya Karume, walipokewa na viongozi mbali mbali wa serikali, Chama Cha Mapinduzi na vyama mbali mbali vya upinzani katika uwanja wa ndege wa Zanzibar.
CHANZO: ZANZIBAR LEO
 
Huku mnakoelekea mmeanza kukosa dira...mapenzi ya form two-three...motomoto...mkikua mtaacha halafu msitushirikishe mkifarakana tena 2010 ....kichekesho kwelikweli..mnasindikizana hadi kwenye mambo yasiyo na maana ala!
 
wazanzibari wengi hawajali kitu, wanajali utu. naamini wazanzibari wengi tunafurahishwa na haya makubaliano kwasababu tunatamani mapatano na mapenzi baina yetu. mimi binafsi sifurahii makubaliano haya kwa ajili ya kutaraji kitu bali nayafurahia kwasababu naona utu wetu na heshima yetu wazanzibari ipo kwenye umoja wetu. Mungu ayatie baraka makubaliano haya iwe ndo mwisho wa kubaguana zanzibar.amen
 
....kichekesho kwelikweli..mnasindikizana hadi kwenye mambo yasiyo na maana ala!
Sijakuelewa vyema hapa,unakusudia kueleweka kuwa mambo ya elimu ndo hayana maana????
 
Sijakuelewa vyema hapa,unakusudia kueleweka kuwa mambo ya elimu ndo hayana maana????
Elimu ipi kaka/ndugu?...kutunikiwa...embu ungeleeni tume huru na uchaguzi wa haki...wasije kufa watu tena hayo ndiyo mambo ya msingi..
come 2010 ndoa hii itaisha...watu watanyimwa haki zao watauliwa wengine..etc...halafu watataka watanzania tuwauunge mkono ..ala!
 
1-wote hawautaki Muungano

2.wote wana common enemy-yaani wabara wanaowaingilia mambo yao

3.kuna potential kubwa ya mafuta sasa ya nini kugombana

4.Muungano unanganganiwa na watu wa bara

5.In the next 15-10 yrs time huu muungano unaweza usiwepo kabisa na kama ukiwepo utakuwa very weak

6.Its about time wa Tanganyika wakala silver bullet na kukubali hali halisi kuwa viability ya hii project ya Muungano ni kama story ya Cinderella na kuamua kuwa na PLAN B baada ya Muungano kuvunjika

7.Ile theory kuwa waPemba na wa ZNZ watapata tabu kwa sababu wana business interest umepitwa na wakati in this day and age ya GEO-ECONOMICS badala ya GEO-POLITICS za akina Poooool soziiiigwa
 
Game Theory,
Mkuu wangu usidanganyike hata kidogo.. Karume anawekwa na Bara hawezi kuzungumza kwa maslahi ya Zanzibar ikiwa yeye mwenyewe mguu nje ndani. Maalim Sief always stands for his own interest. Anasema saaana kuwavuruga vichwa tu, na kama alivyokosolewa huyu alikuwa Waziri kiongozi, na kisha waziri wa Elimu hatumsikia hata siku moja akipinga Muungano..mbali na hayo hakufanya lolote la maana kw Wazanzibar alipokuwa madarakani.

Mkuu wangu wazee waliopinga Muungano Zanzibar wanajulikana toka siku ya kwanza na wengine kutokujiunga na baraza la Mapinduzi. Na hakuna chombo chenye nguvu Zanzibar na bara kama baraza hilo kwani wasemavyo wao ndivyo itakavyokuwa.

Kama umesoma vizuri taarifa iliyotolewa ni kwamba hakuna masharti baina yao, meaning uchaguzi ujao ngoma ni ile ile..Na kutokana na mfumo wa serikali ya leo hata kama CUF watachukua uongozi Zanzibar, Wazanzibar wtaendelea kuwa ktk hali hii hii kwa sababu tatizo sii kuongozwa na CCM ila mfumo mzima wa madaraka.

Nimewahi kusema kama kweli kuna kiongozi yeyote Zanzibar mwenye nia ya kuvunja Muungano, iwe CUF au baraza la Mapinduzi basi hatua ya kwanza sii kuweka Muafaka baina yao ila kuitisha Refendum, kuwapa wananchi wa Zanzibar nafasi ya kuchagua kuwa huru kujitenga ama laa! Matokeo ya referendum hiyo ndiye yatakayo jenga misingi ya muafaka baina ya bara na visiwani na sio Karume na Maalim Seif..
Imefanyika hivyo nchi zote zilizotaka kuvunja muungano kwa amani, iweje Zanzibar viongozi wake wasifikirie kabisa njia hii isipokuwa zile zinazohusu nafasi zao za kazi?..
 
.

Mkuu Mkandara, Wanzanzibari waone hivyo hivyo, tena haswa inapotokea ni waarabu wa Pemba. Pamoja na Karume kuwa sio chaguo la Komandoo, ni Chaguo la Bara, kilichotokea anakijua, game lilivyochezwa kumdhibiti Komandoo na chaguo lake, analijua, na kilichomkuta Komandoo na chaguo lake na timu yake nzima sote tunakijua, (complete cut off).

Sasa Karume hataki yamkute yaliyomkuta mtangulizi wake, yeye naye analo chaguo lake, huku kukutana na Maalim ni caveat dhidi ya bara, just incase bara ina chaguo tofauti, then watamback Maalim moja kwa moja to hell with Muungano.

Karume has nothing to loose, siku zake zinahesabika anyway, hivyo kaamua bora Seif kuliko mgombea wa bara. Masharti ya siri baina yao yapo!. Anaeutaka urais wa Znz sio Karume ni Seif, aliyeumia ni Seif, aliyelialia ni Seif leo hawezi kwenda kumlamba miguu Karume for nothing huku watu wake wakiendelea kunyimwa Zan ID na japo walijitokeza kwa wingi day one baada ya mapatano, kesho yake waliendelea kususa kusubiri kauli. Mpaka sasa hakuna kauli yoyote kwa Seif waende, its not for nothing.

Seif naye hii ndiyo karata yake ya mwisho, bado anaamini alikuwa mshindi akipokwa tonge mdomoni, safari hii, alishajipanga sio asipokwe tena, bali kuwahamasisha Wapemba kususia kujiandikisha na kuhakikisha Pemba hakuna kitakachoendelea bora wakose wote at the expense ya damu za Wapemba. Walijipanga kufanya kitu mbaya, Huku kumuangukia Karume sii bure bali ni kuepusha yale yote waliyoyapanga.

Hapa sasa wanaozugwa ni Bara, lets wait for much surprises ahead.
 
Pasco,
Mkuu wangu nawaelewa vizuri Wazanzibar na hasa viongozi wake..Huyu Maalim Seif atalamba miguu ya wangapi? Toka nimjue kila mara hutafuta mbinu ya kumwingiza ktk utawala wa Zanzibar ili apate nafasi yeye kwa ajili maalum ya haki za Wapemba. That is a fact, hana zaidi ya kutazama kwao na rangi yake kama ulivyosema.

Hata kwa huyo Komandoo alijaribu akakuta ukuta mzito.. Matatizo ya Komandoo yalikuwa within Baraza la Mapinduzi alipotaka kuongeza muda na pia alokusudiwa na wengi hakuweza kushika madaraka kwa sababu bara waliingilia kati kumweka Karume.
Hii ni kanyanga tu mkuu wangu, mtoto wa Mwinyi ana chance kubwa ya kuchukua Zanzibar kuliko Maalim Seif.. mnachoshindwa kuelewa ni kwamba huwezi kuwa rais wa nchi yoyote ikiwa wewe haupo ktk System... iwe bara au viziwani ni lazima uwe mwanachama wa KGB ya nchi hiyo..
Labda Mapinduzi yenyewe yaanze na wananchi kama kule Poland na Nchi za Amerika ya kusini. Ikiwa baraza la mapinduzi hawamtaki Salim kuwa rais wa Jamhuri ya muungano, leo unataka kunambia watampa baraka zao Maalim Seif! mtu ambaye ni hatari kwao kuliko hata Salim akiwa rais wa Jamhuri. Jamani msijidanganye hata kidogo na Siasa hizi.
Kweli Wapemba wanajuana kwa Vilemba, lakini sii Karume kwani yeye sii Mpemba wala hana asili hiyo..
 
CUF kumtambua Karume sidhani kwamba ni muhafaka umefikiwa bali ni mbinu za kujitenga. Zanzibar iwe Serekali/Nchini kamili na si sehemu TAnzania/Tanganyika. Hapo naona ni chenga wanampiga JK na serikali yake. Labda tuangalie 2010 kutatokea nini.
 

Game;

Ukitulia una akili sana. Naomba us stick kuwa Gametheory wa aina hii. Toka jana unaporomosha ma vituuuzzzz tu.

Keep it up bro na next time ukirudi Dar tutafutane.

FP
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…