Wikiendi inaanza tena.
Mkuu inaonesha unaanza kuota...
Maalim Seif alikuwa miongoni mwa waanzilishi na waasisi wa CCM Zanzibar...anaijuwa CCM kuliko hata Jakaya Kikwete..anajuwa nje ndani ya CCM...ndiyo Maana alikubali jeuri ya Mwalim Nyerere kuwa "bora uwe mpinzani nje ya CCM kuliko ndani yake..." na Maalim akachkuwa ustaarabu wake...unajuwa alipokelewa vipi na Wazanzibari...kwa kishindo kikubwa hakijawahi kutokea,mpaka mshairi mmoja maarufu visiwani akamtungia shairi lililoimbwa na Naad Ikhwan Safaa(Malindi musical club),akatunga na watu wakaimba:
Mtajirusha wenyewe, roho na akili zenu
Kisemeni msizuwe, kilichomtoa kwenu
Na huku kaja mwenyewe, kajuwa hamna lenu
Ya bure yenu mayowe, huyu sasa siye wenu.
Chorus:Mtajirusha wenyewe roho na akili zenu na msema msizuwe kilicho mtoa kwenu.
Sasa Maalim arudi CCM akatafute nini...wazanzibar hawajasahu ahadi yake ya mwaka 1989 katika uwanja wa Tibirizi,Pemba...alisema "...nitakuwa pamoja nanyi hadi mwisho wa maisha yangu na sitawasaliti..."
Na mwenyewe Maalim heshi kutukumbusha ahadi hiyo mara kwa mara...akionyesha kuwa ni mtekelezaji wa ahadi zake na si mnafiki...ipo siku yatatimia kama si leo kesho
Endelea kuota.