Matumizi sahihi ya Dabo indiketa, gia L,2,3 na O/D katika gari za Automatic

Matumizi sahihi ya Dabo indiketa, gia L,2,3 na O/D katika gari za Automatic

Mkuu na kigari changu Auto kimeandikwa kina 4WD lkn sioni sehemu yoyote ya Ku activate. Always huwa nafikiri hiyo L ndo sehemu ya ku activate hiyo four wheel. Na hii nilipata nguvu baada ya kuiweka hiyo L na kuona garo haibadirishi via, iko constant kwenye gia Moja. Je nipo sahihi juu ya hilo?

Ukiweka L maana yake isibadiri gia zaidi ya namba 1, na siku zote namba 1 ndo gia yenye nguvu zaidi na ndo maana tunaitumia unapkuwa umekwama, lengo la kuweka L ni kuwa gear box isijibadirishe gia yenyewe automatically kwa kufuata RPM yake, maana kila gear ina ingia kutegemeana na mzunguko wa injini/RPM. Sasa hili linakuwa tatizo kama umekwama maana unataka gia namba moja itumike kwa nguvu zaidi ili utoke kwenye kwamo let's say wa umbali labda wa mita 100 au zaidi, ambapo ukiwe D basi unaweza kujikuta by the time RPM imefika 3000 uko gia namba 4 ambapo gari inakuwa nyepesi na haina uwezo wa kukutoa kwenye tope au mchanga.

4WD ina maana Four Wheels Drive au mengine huandikwa Full Time Four Wheels hasa kwa gari ndogo, hii inamaana muda wote inakuwa kwenye 4WD haihitaji kubonyeza chochote kwa kuiweka au kuitoa, yaana tairi zote nne zinazunguka kwa mzunguko mmoja na hii inakuwa imetengenezwa moja kwa moja toka kiwandani, uzuri wake zikuwa hazikwami hovyo hovyo na hazina usumbufu wa kuweka au kutoa 4WD, ni nzuri kwa akina mama au watoto hasa wa kike japo ulaji wake wa mafuta ni juu kidogo maana muda wote inakuwa nzito kuliko gari ambayo sio Full Time 4WD ila uzuri mwingine zinanguvu sana
 
Kwahiyo mkuu akohi kwenye dashboard ikiwaka taa ya O/D OFF = ON; na kama haipo ni sawa na O/D iko OFF??

Ikizima ndo iko ON, ikiwaka ndo iko OFF

ku prove hilo fanya hivi:

Endesha wakati taa ya OD imewaka then nenda kasi mpaka speed 60 au zaidi, utasikia muungurumo umekuwa mzito na engine inapiga kelele/vuma/vibrate sana na RPM iko juu zaidi ya 3000, maana yake uko speed lakini gear box iko namba 4 na haiwezezi kuingia gia namba tano sababu umeweka OD OFF, basi hapo weka OD ON wakati uko speed then yafuatayo utaona:-

1. RPM itashuka mpaka 2000
2. Muungurumo wa Engine utarudi normal
3. Gari ita ingage gia namba 5
4. Speed itaongezeka zaidi
5. Gari itatulia au kuacha kuvibrate na hata mkononi utaisikia imetulia
6. etc
 
Katika gari zingine kuna N/P ukipress P kwenye Dashbord inawaka POWER hii inasaidia nini na inatumikaje?


ELCT au P=Power ya kwenye dashboard kazi yake ni kuipa gari nguvu zaidi na inatumika unapotaka kumaintain speed zaidi ya 140km kwa saa au zaidi ila kufanya hivyo inabidi uwe na uzoefu wa kukimbia na kumaintan hiyo speed lakini pia kiwango cha mafuta kitaongezeka takriban mara mbili ya kawaida...hahaha

Mi naitumia sana hasa ninapokuwa nasafiri kwenda mikoani na nina haraka
 
Fuatilia nyuzi kuna sehemu nimefafanua ila si kosa japo inaweza kusababisha ajari


alfredmkohiatgmaildotcom

Kuweka N wakati uko kwenye mwendo ni hatari sana maana unakuwa wewe huiendeshi gari na ni rahisi kupoteza control maana mf ikizima gafla ni kila kitu kika jilock mf steering au break zika fail basi hapo unaweza hata kupoteza maisha
 
Mkuu ukiona gari imekuandikia 'ECONO' maana yake ni economy, huwa inatokea pale ambapo kiwango cha mafuta kinachoingia kwenye injini ni kidogo kulinganisha na kiasi cha hewa kinachoingia kwa hiyo mafuta yanayotumika ni kidogo sana.Kifaa kinachofanya hiyo balance kinaitwa THROTTLE na kuna baadhi ya mafundi hukichezea kwenye baadhi ya magari ili ulaji wa mafuta upungue ila usijaribu kufanya huo mchezo ni hatari unaweza ukaharibu injini. Hali ya ECONOMY hutokea gari inapokuwa kati ya speed 60-90. Ni function ambayo ni common sana kwenye gari za CARINA

Well said Chief, labda kuongezea tu.

kama una balance vizuri mafuta kwa kukanyaga huku unatizama RPM isizidi 3000 pale gia inapotaka kuingia na hasa unapokuwa safairini basi utaweza kukuta taa ya ECONO inawaka uko speed 120 bila tatizo chamsingi usiwe unakanyaga mafuta kwa nguvu, kanyaga kidgo tu halafu gari yenyewe itaongeza speed taratibu unless kama unaharaka hapo ndo inabidi ukanyage mafuta mengi of which taa lazima itazim
 
Sahihi kabisa, CControl inasaidia sana hasa unapokuwa Off Road maana ukiisha ingage, katika speed unayotaka basi huna haja ya kukanyaga mafuka, so utakuta hata mwili ume relax, japo pia ina option ya kuongeza na kupunguza speed hapo hapo kwenye steering kwa alama ya + kwa maana ya kuongeza au - kwa maana ya kupunguza speed na hii utaitumia zaidi either kwenye kona au unapotaka kupunguza kwendo maana si kila muda ukanyage break, so unachofanya ni kubonyeza alama - kwa idadi ya speed unayotaka, sijui gari yako maana kuna ambazo kila kubonyeza inaongeza au kupuza speed 5 na zingine speed 10 na zingine speed 20
Mkuu me hyo nilitumia kwa Brevis la CC 3000 Aisee Ile Gari imetulia sana yani Raha
 
ELCT au P=Power ya kwenye dashboard kazi yake ni kuipa gari nguvu zaidi na inatumika unapotaka kumaintain speed zaidi ya 140km kwa saa au zaidi ila kufanya hivyo inabidi uwe na uzoefu wa kukimbia na kumaintan hiyo speed lakini pia kiwango cha mafuta kitaongezeka takriban mara mbili ya kawaida...hahaha

Mi naitumia sana hasa ninapokuwa nasafiri kwenda mikoani na nina haraka
Mkuu nashukuru sana kwa kuanzisha uzi huu, utakuwa umetusaidia wengi wetu. Mimi kwenye gari yangu (AUTO) kuna button mbili ambazo sijiu matumizi yake, moja imeandikwa PWR (inawezekana ikawa Power kama ulivyoeleza hapa), lakini kuna nyingine inafuatia imeandikwa MANU. Naomba unieleweshe kama unafahamu kuhusu hizi.
Pili ni kama sijakupata vizuri kuhusu matumizi ya 2 na L kwenye hizi gari za AUTO, hivi ulisema unaweza pia kuzitumia kama unashuka mteremko mkali? Asante.
 
Dabo indiketa inashauriwa itumike wakati una dharula kubwa mf: Ajari au gari Mbovu maana lengo lake ni kuwataarifu madereva wenzako kuwa gari yako inatatizo so wapite kwa uangalifu zaidi lakin utakuta wengi wetu tunatumia visivyo mf; katika kupita njia panda au ukipaki pembezoni mwa barabara. Pia niongezee kuna ambao aki over take gari anawasha indiketa ya kulia (hiyo sawa kabisa ila sasa unapotaka kurudi upande wako wa kushoto hunahaja yak u indiketa tena unless kama kuna gari nyuma yako na iko jirani sana sio
Hata uko pekee yako unawasha indiketa tu.

Katika gari za Automatic kuna gia za L, 2, 3 na O/D.
Kwanza ujue kabisa katika hali ya kawaida gari yako inapaswa kuwa katika D kwa maana ya Drive na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali yali ya hewa kama ni nzuri ila 2, 3 hutumika tu pale unapokuwa either unashuka au unapanda mlima/mteremuko mkali sana na mrefu mf’ sekenke na unataka ushuke au upande kwa speed ile ile ila isizidi 40/60 basi ndo unaruhusiwa kutumia 2, 3. Namba 2, 3 na L inamaana kuwa ina inalock gear box ili gear zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili toka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe speed zaidi ya 40/60 maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disks) zilizomo ndani ya gearbox kufanya gazi nah ii upelekea ile hydrolic iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha gear box kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndo maana ukiweka 2, 3 au L gear box inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolick kupoa pia na ndo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla. L inatumika pale unapokuwa either umekwama au unavuta gari jingine au tera ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana inanguvu sana na pia inaongeza ulajo wa mafuta, so kama ukiishatoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huohuo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau speed 40/60 au zaidi kama utaweka D. kwa maana rahisi zaidi kwamba 2,3,na L inafanya kazi kama gari ya Manual nah ii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

Over Drive inatumika pale gari inapokuwa speed zaidi ya 60/80 kutegemeana na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe ndo inafanya nan do maana unashauriwa iwe on muda wote kusudi gari ichague ni wkati gani iweke on au of maana uukiwa chini ya 60/80 hata kama umeweka on bado inakuwa haifanyi kazi.
Cha mwisho ndugu zangu ni kwamba OD unaweza kuitumia kama break/stop engine hasa unapokuwa zaid ya 80 na wakati huo iko ON yaan katika dashboard taa ya OD izime ikiwaka maana yake iko OFF, basi ili upunguze mwenda kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga break taratibu utaona mwenyewe gari lako linavyopunguza mwendo tartibu na wakati mwingine si lazima ukanyage break, we iweke OFF tu halafu toa mguu katika pedal ya mafuta gari lazima li slow down na kama lilikuwa ni tuta na umeliisha lipita basii iweke tena ON ongeza mafuta auu unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi na ikiisha changanya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida.

Tahadhari: never ever kata kona wakati uko speed kubwa na gear namba tano (Kwa manual) au rpm iko 3000 Kwa automatic hii husababisha kupitiliza maana gari inakuwa nyepesi sana. Hakikisha ume slow down mpaka gia namba nne na break kidogo na Kwa autimatic either uweke 2 au 3 ila lazima weka OD off na break kidogo

Sijui kama ntakuwa nimeeleweka maana Kiswahili na lugha yetu ila mmh …!
Thanks!
 
Mkuu naomba unieleweshe kitu kimoja...ni hivi. Mimi gari yangu siku zote naendesha nikiwa nimebonyeza kile kitufe cha OD. Hivyo pale kwenye dashboard inawaka taa ya orange inasoma O/D OFF sasa hapo inamaanisha nini na je ni sawa?
Hapo unakosea. Inatakiwa kile kitaa cha o/d kizimike...
 
Hapana enhe si sawa kabisa maana lengo la over drive ni kuongeza ufanisi wa injini na pia kupunguza ulaji wa mafuta Kwa maana kwamba ukiweka OD ON taa inazima na ikiwa OFF taa inawaka inapokuwa ON gia zitawahi kufika namba nne au tano na injini itakuwa nyepesi so ulaji wa mafuta unakuwa mdogo lakin pia hata injini inakuwa na maisha marefu maana rpm haiwezi kuzidi 3000 na labda nishauri Kuwa ili u save mafuta make sure rpm isizi 2000 unless kama uko safarini na unaharaka other wise usiilazimeshe injini kuanza na Kasi zisizo na lazima, weka D then ondoka taratibu huku unaangalia rpm yako isizidi 2000 utaona gari inaongeza mwendo yenyewe mpaka spidi kubwa kabisa hata 140kph na sana sana rpm wakati huo itasoma 3000 ambayo bado ni fuel efficient.

Ukidrive wakat OD iko OFF maana yake ulaji wa mafuta unakuwa Mkubwa sana na pia gari haiwezi kuchanganya haraka lakin pia unaua injini unless huzidi speed 60kph

Here is the trick part, weka OD off kama uko offroad au kuna utelezi na hutaki gari iwe nyepesi ila unataka ikimbie maana inakuwa nzito so ni nzuri Kwa barabara za vumbi lakin make sure huzidi 60kph maana OD inafanyakazi ktk speed kuanzia 60/80kph



alfredmkohiatgmaildotcom
Alfred asante sana kwa mada yako vipi elect pwr?

Dabo indiketa inashauriwa itumike wakati una dharula kubwa mf: Ajari au gari Mbovu maana lengo lake ni kuwataarifu madereva wenzako kuwa gari yako inatatizo so wapite kwa uangalifu zaidi lakin utakuta wengi wetu tunatumia visivyo mf; katika kupita njia panda au ukipaki pembezoni mwa barabara. Pia niongezee kuna ambao aki over take gari anawasha indiketa ya kulia (hiyo sawa kabisa ila sasa unapotaka kurudi upande wako wa kushoto hunahaja yak u indiketa tena unless kama kuna gari nyuma yako na iko jirani sana sio Hata uko pekee yako unawasha indiketa tu.

Katika gari za Automatic kuna gia za L, 2, 3 na O/D.
Kwanza ujue kabisa katika hali ya kawaida gari yako inapaswa kuwa katika D kwa maana ya Drive na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali yali ya hewa kama ni nzuri ila 2, 3 hutumika tu pale unapokuwa either unashuka au unapanda mlima/mteremuko mkali sana na mrefu mf’ sekenke na unataka ushuke au upande kwa speed ile ile ila isizidi 40/60 basi ndo unaruhusiwa kutumia 2, 3. Namba 2, 3 na L inamaana kuwa ina inalock gear box ili gear zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili toka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe speed zaidi ya 40/60 maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disks) zilizomo ndani ya gearbox kufanya gazi nah ii upelekea ile hydrolic iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha gear box kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndo maana ukiweka 2, 3 au L gear box inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolick kupoa pia na ndo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla. L inatumika pale unapokuwa either umekwama au unavuta gari jingine au tera ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana inanguvu sana na pia inaongeza ulajo wa mafuta, so kama ukiishatoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huohuo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau speed 40/60 au zaidi kama utaweka D. kwa maana rahisi zaidi kwamba 2,3,na L inafanya kazi kama gari ya Manual nah ii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

Over Drive inatumika pale gari inapokuwa speed zaidi ya 60/80 kutegemeana na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe ndo inafanya nan do maana unashauriwa iwe on muda wote kusudi gari ichague ni wkati gani iweke on au of maana uukiwa chini ya 60/80 hata kama umeweka on bado inakuwa haifanyi kazi.
Cha mwisho ndugu zangu ni kwamba OD unaweza kuitumia kama break/stop engine hasa unapokuwa zaid ya 80 na wakati huo iko ON yaan katika dashboard taa ya OD izime ikiwaka maana yake iko OFF, basi ili upunguze mwenda kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga break taratibu utaona mwenyewe gari lako linavyopunguza mwendo tartibu na wakati mwingine si lazima ukanyage break, we iweke OFF tu halafu toa mguu katika pedal ya mafuta gari lazima li slow down na kama lilikuwa ni tuta na umeliisha lipita basii iweke tena ON ongeza mafuta auu unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi na ikiisha changanya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida.

Tahadhari: never ever kata kona wakati uko speed kubwa na gear namba tano (Kwa manual) au rpm iko 3000 Kwa automatic hii husababisha kupitiliza maana gari inakuwa nyepesi sana. Hakikisha ume slow down mpaka gia namba nne na break kidogo na Kwa autimatic either uweke 2 au 3 ila lazima weka OD off na break kidogo

Sijui kama ntakuwa nimeeleweka maana Kiswahili na lugha yetu ila mmh …!
 
Nimefurahi sana kuhusu double indicators. Utaona watu wengi ambao ulidhani ni wazoefu sana wa magari wakiweka hizo taa ati kuonesha wanaenda mbele kwa mbele sio kupinda. Nikajiuliza, mbpna njiani tunapita barabara nyingi tu zenye muingiliano na tunayoipita lakini hatuweki hizo indicators??
Umewafafanulia vizuri sana mkuu. Aksante kwa somo.
 
Mkuu, Unaweza ukatoka kwenye D - ukenda kwenye 3 au 2 ikitegemeana na Spidi.

L- Inatembea mpaka 60km/hr
2 - Inatembea mpaka 120km/hr
3 - Inatembea mpaka 180km/hr
4 - inatembea mpaka 240km/hr - ( ikiwa imefungwa speed gorvenor itafika 220km.hr atleast)

In that case, kama umeweka D na umefika 160 km/hr unaweza ukashift kwenda 3rd gear bila tatizo lolote, ukifanya ivi utaona gari ikiwa inaongezeka nguvu kidogo.

Ila huwezi ukatoka kwenye D wakati upo 160, ukarudi kwenye 2nd Gear, safe mechanism ya gari inatakiwa ikate mafuta at once na gari kuzima kabisa.... sijawahi kujaribu kufanya ichi kitu 😀 wala sitojaribu.... lakini in theory it is suppose to cut off fuel mpaka pale gear itakapoweza kuendana na mzunguko wa engine.

Pia some of the info unazotoa hazipo sawa kuhusu OD. Unasema kuwa unaua gari ukiwa una drive wakati OD ikiwa Off? Na pia Suala la unywaji mafuta ukoje? Kuna baadhi ya vitu ni lazima uelewe theory yake ikoje.

OD kukaa off maana yake ni kuwa hio ni normal driving mode, wewe umeekewa option ya ku OVER DRIVE the Factory set limit tu. Na hapa ndio unywaji wa mafuta unaongezeka, kwa sababu, kwanza utakuwa umejihold kwenye lower gear for a period of time without efficiently using it. Pengine wewe unakwenda 60km/hr ndio mwendo wa kila siku, Over drive for what? unapoweka on, unapunguza efficiency ya gari. Kwa sababu gari automatic wakati unaendesha, huwa inakwenda kutulia kwenye higher gear kwa ajili ya kupunguza ulaji wa mafuta, higher gear haitumii ulaji mkubwa wa mafuta kwa sababu engine inakuwa nyepesiiiii mzunguko wake. Ndio maana utaona gear zinajibadilisha RPM ikiwa somwhere between 2000-3000.

In Theory, ukibonyeza zaidi accelerator, throttle body inazidi kufunguka, hii hupelekea hewa nyingi kuingia, manake na mafuta zaidi yataingia, na maanake mzunguko wa engine utaongezeka (RPMs). Sasa ukiweka Over drive on, practical kabisa, utaona kuwa utajikuta upo kwenye lower gear kisha rpm inaongezeka, ikiongezeka rpm basi ujue kuna ongezeko la hewa na mafuta ndani ya engine. Sasa ukinambia kuwa Over drive inasaidia kuokoa mafuta hapo itabidi unieleweshe hio engine inafanya kazi vipi?

Lengo la OD, sio efficiency ya mafuta kwenye gari. Lengo lake ni kukupa more power in the lower gear. Mfano wakati upo normal driving without OD on na uko kwenye 70km/hr, mbele yako kuna gari, unataka kuipita, hii gari nayo labda ipo kwenye 60km/hr, unajaribu ku overtake, bila ya OD, utajikuta kuwa unachukua mda kumpita huyu jamaa wa mbele, bila OD unaweza kumpita, lakini itachukuwa mda, sasa unapoweka OD, wakati una overtake halafu umekanyaga mafuta, maanake unaiambia engine kuwa, give me the most power i can get with the force i push the accelerator, engine nayo inajibu kwa kushusha gear ya chini yake ili kukupa nguvu zaidi, Tena hapa itategemea how hard you press the gas pedal, what speed you are into, hio hio OD inaweza ikashift from 4th Gear to 2nd Gear straight.

I hope nimeeleweka kama kuna hitajika ufafanuzi nipo
 
Asante kwa elimu nzuri mleta mada,
Nini kazi ya ECT SNOW?
 
Back
Top Bottom