Matumizi ya akili bandia (AI) yahofiwa kushusha ubora elimu

Matumizi ya akili bandia (AI) yahofiwa kushusha ubora elimu

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Kongamano la 8 la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu limeanza leo jijini Dar es Salaam ambapo wito ukitolewa kwa wanataaluma kuongeza umakini kukabiliana na changamoto za teknolojia mpya.

Kupitia kongamano hilo lililoandaliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), mada mbalimbali zimejadiliwa ikiwemo maandalizi ya taifa kuingia kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda mojawapo ikiwa ujio wa teknolojia na athari zake chanya na hasi kwenye elimu.

Akichangia mada hiyo leo Juni 14, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma (Udom), Profesa Lughano Kusiluka ameeleza kuwa mapinduzi hayo yamekuja na changamoto ambazo zinaweza kuathiri mifumo mbalimbali ikiwemo elimu.

Amesema ili kuepuka athari hasi ni muhimu kwa wanataaluma kwenda na kasi ya teknolojia hizo ili kubaini udanganyifu unapojitokeza.

Akitolea mfano wa programu rununu ya Chat GPT amesema inatumika vibaya na wanafunzi hivyo ni muhimu kuwa walimu kuwa makini kufanya ufuatiliaji.

“Sasa hivi kuna hii Chat GPT ni teknolojia nzuri lakini matumizi yake yanaweza kuleta shida kwenye elimu yetu, huku vyuoni sasa hivi tuna shida mwanafunzi anaweza kukuletea tasnifu imeandikwa vizuri na akapata 'A' ukiifanyia tathmini utagundua wala hakustahili kupata hiyo alama.

“Hii inatufanya vyuo vikuu na sisi tuone haja ya kuwekeza ili kuzibaini tasnifu zinazofanywa kwa njia hii, tuongeze umakini kwenye tathmini. Teknolojia hizi zipo na hatuna namna ya kuzikwepa lakini tuhakikishe hazitumiki kushusha kiwango cha elimu yetu,” amesema Profesa Kusiluka.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi wa zamani wa Costech Dk Hassan Mshinda amesema teknolojia hiyo ni tatizo kwenye elimu kwani inawawezesha wanafunzi kufanya udanganyifu.

“Mtu anaweza kuandika tasnifu nzuri kabisa ya kurasa tano ndani ya dakika tano. Hata hivyo hatuwezi kupingana na maendeleo haya lazima tuendane na kasi hiyo. Changamoto ni kwamba kama tutaenda taratibu kila siku tutakuwa nyuma lazima kazi kubwa ifanyike kuendana na mabadiliko na maendeleo haya teknolojia,” amesema.
 
Kongamano la 8 la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu limeanza leo jijini Dar es Salaam ambapo wito ukitolewa kwa wanataaluma kuongeza umakini kukabiliana na changamoto za teknolojia mpya.

Kupitia kongamano hilo lililoandaliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), mada mbalimbali zimejadiliwa ikiwemo maandalizi ya taifa kuingia kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda mojawapo ikiwa ujio wa teknolojia na athari zake chanya na hasi kwenye elimu.

Akichangia mada hiyo leo Juni 14, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma (Udom), Profesa Lughano Kusiluka ameeleza kuwa mapinduzi hayo yamekuja na changamoto ambazo zinaweza kuathiri mifumo mbalimbali ikiwemo elimu.

Amesema ili kuepuka athari hasi ni muhimu kwa wanataaluma kwenda na kasi ya teknolojia hizo ili kubaini udanganyifu unapojitokeza.

Akitolea mfano wa programu rununu ya Chat GPT amesema inatumika vibaya na wanafunzi hivyo ni muhimu kuwa walimu kuwa makini kufanya ufuatiliaji.

“Sasa hivi kuna hii Chat GPT ni teknolojia nzuri lakini matumizi yake yanaweza kuleta shida kwenye elimu yetu, huku vyuoni sasa hivi tuna shida mwanafunzi anaweza kukuletea tasnifu imeandikwa vizuri na akapata 'A' ukiifanyia tathmini utagundua wala hakustahili kupata hiyo alama.

“Hii inatufanya vyuo vikuu na sisi tuone haja ya kuwekeza ili kuzibaini tasnifu zinazofanywa kwa njia hii, tuongeze umakini kwenye tathmini. Teknolojia hizi zipo na hatuna namna ya kuzikwepa lakini tuhakikishe hazitumiki kushusha kiwango cha elimu yetu,” amesema Profesa Kusiluka.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi wa zamani wa Costech Dk Hassan Mshinda amesema teknolojia hiyo ni tatizo kwenye elimu kwani inawawezesha wanafunzi kufanya udanganyifu.

“Mtu anaweza kuandika tasnifu nzuri kabisa ya kurasa tano ndani ya dakika tano. Hata hivyo hatuwezi kupingana na maendeleo haya lazima tuendane na kasi hiyo. Changamoto ni kwamba kama tutaenda taratibu kila siku tutakuwa nyuma lazima kazi kubwa ifanyike kuendana na mabadiliko na maendeleo haya teknolojia,” amesema.
Artificial intelligence haizuiliki.
Mapinduzi ya nne ya viwanda yanahusisha vitu kama hivi,
  • Akili bandia za kidigitali AI
  • Fundo tungamo (Blockchain technology)
  • Internet ya vitu (Internet of things) n. K
Ukijifanya wewe hutaki kuzikumbatia utajikuta umepigwa gape moja kubwa sana hapo baadae.

Hivyo tusiwe na hofu na technology.
Hata hii elimu si ajabu ikawa haina mashiko tena kama watafanikiwa mradi wa neural links
 
Hii fourth revolution ndo inaenda kuleta chapa ya mnyama ambapo unique ID zitatumika kuwatambua watu wote duniani ambazo zitakuwa connected na huduma mbalimbali. Kwa maana nyingine binadamu anaenda kufanywa mateka na waabudu shetani ili watimize malengo yao ya giza.​
 
Dah nilitaka kulifungulia uzi suala hili ratiba inanibana, afadhali wameshaliona, na hima walishughulikie haraka.

Chat GPT imevuruga kabisa elimu vyuoni, na imeibuka kwa kasi sana semester hii.

Kama haitopatikana namna bora ya kuishi na hili bomu Kuna wanafunzi watakuwa wanaingia vyuoni na wanatoka empty kama walivyoingia. Hasa ukizingatia vitoto vya siku hizi vipo empty sana vichwani, division I kali ila kichwani zero tupu!
 
Dah nilitaka kulifungulia uzi suala hili ratiba inanibana, afadhali wameshaliona, na hima walishughulikie haraka.

Chat GPT imevuruga kabisa elimu vyuoni, na imeibuka kwa kasi sana semester hii.

Kama haitopatikana namna bora ya kuishi na hili bomu Kuna wanafunzi watakuwa wanaingia vyuoni na wanatoka empty kama walivyoingia. Hasa ukizingatia vitoto vya siku hizi vipo empty sana vichwani, division I kali ila kichwani zero tupu!
Msaada ni kitu gani?
Kinafanyaje kazi?
 
Dah nilitaka kulifungulia uzi suala hili ratiba inanibana, afadhali wameshaliona, na hima walishughulikie haraka.

Chat GPT imevuruga kabisa elimu vyuoni, na imeibuka kwa kasi sana semester hii.

Kama haitopatikana namna bora ya kuishi na hili bomu Kuna wanafunzi watakuwa wanaingia vyuoni na wanatoka empty kama walivyoingia. Hasa ukizingatia vitoto vya siku hizi vipo empty sana vichwani, division I kali ila kichwani zero tupu!
Hilo ndo lengo la waabudu shetani kuwafanya binadamu kama mazezeta ili waweze kutekeleza matakwa yao ya giza.
 
Msaada ni kitu gani?
Kinafanyaje kazi?
In short Artificial Intelligence (AI) ni mfumo wa kikompyuta (ubongo bandia) unaofanya kazi za kibinadamu zinazohitaji kufikiri, ambao umekua kwa kasi hivi karibuni. Mfumo unafanya shughuli nyingi (mara ya kwanza habari zake nimeanza kuziona humu jf kwa wale team Russia vs Ukraine), mara ghafla nikashtuka mzigo upo vyuoni watu wanajiachia tu hawaumizi akili.

Kuna applications zake zinapakuliwa na kuwa installed kwenye simu zina majina tofauti (Chat GPT, Ask AI etc), ni kama mbadala wa Google (maana google sasa imesahaulika ghafla).

Ukihitaji taarifa fulani unakiuliza (Kuna sehemu ya kutype kama unachat na mtu vile). Kinasakua huko chapchap na kukuletea papohapo huku kikichat kama mtu, na kinatype kwa kasi. Ni tofauti na google ambapo ukiuliza unaletewa mambo mengi yanayohusiana na yasiyohusiana ujichambulie.

Sasa shida inapoanzia ni kuwa mwanafunzi mzembe (% kubwa ni wazembe wa kutupwa) akipewa assignment haumizi akili yake, anabeba swali zima kama lilivyo anamuuliza AI, naye AI anatiririka kila kitu chapchap na reference ikihitajika analeta. Mwanafunzi bomu anachukua mzigo anaelekea stationary, anaandika jina na namba ya usajili, anakusanya kazi. Wengine wanatumia mbinu kuingia na simu kwenye tests na UE, hapo kila swali litafanywa na roboti kadri atakavyopata nafasi. Ajabu zaidi hadi research zinaandaliwa kwa AI sasa!
 
In short Artificial Intelligence (AI) ni mfumo wa kikompyuta (ubongo bandia) unaofanya kazi za kibinadamu zinazohitaji kufikiri, ambao umekua kwa kasi hivi karibuni. Mfumo unafanya shughuli nyingi (mara ya kwanza habari zake nimeanza kuziona humu jf kwa wale team Russia vs Ukraine), mara ghafla nikashtuka mzigo upo vyuoni watu wanajiachia tu hawaumizi akili.

Kuna applications zake zinapakuliwa na kuwa installed kwenye simu zina majina tofauti (Chat GPT, Ask AI etc), ni kama mbadala wa Google (maana google sasa imesahaulika ghafla).

Ukihitaji taarifa fulani unakiuliza (Kuna sehemu ya kutype kama unachat na mtu vile). Kinasakua huko chapchap na kukuletea papohapo huku kikichat kama mtu, na kinatype kwa kasi. Ni tofauti na google ambapo ukiuliza unaletewa mambo mengi yanayohusiana na yasiyohusiana ujichambulie.

Sasa shida inapoanzia ni kuwa mwanafunzi mzembe (% kubwa ni wazembe wa kutupwa) akipewa assignment haumizi akili yake, anabeba swali zima kama lilivyo anamuuliza AI, naye AI anatiririka kila kitu chapchap na reference ikihitajika analeta. Mwanafunzi bomu anachukua mzigo anaelekea stationary, anaandika jina na namba ya usajili, anakusanya kazi. Wengine wanatumia mbinu kuingia na simu kwenye tests na UE, hapo kila swali litafanywa na roboti kadri atakavyopata nafasi. Ajabu zaidi hadi research zinaandaliwa kwa AI sasa!
Hizo data za research AI atenda field chap na kukusanya sample, aende maabara kupima, apate majibu aandike na taarifa, vyote kwa chap, kumbe mambo yanaenda kasi sana.
 
Hizo data za research AI atenda field chap na kukusanya sample, aende maabara kupima, apate majibu aandike na taarifa, vyote kwa chap, kumbe mambo yanaenda kasi sana.
Ni hatari. Jamaa ipo speed balaa. Teknolojia haina mchezo.

In fact AI ni nzuri sana kwa kusoma na kujifunzia mambo mengi kwakuwa ina madini sana. Lakini kwa wavivu ambao wanataka copy and paste hapo ni tabu sana.
 
tukiuliza chanzo cha hizi teknolojia ni wapi?majibu hakuna ,inawezekanaje binadamu kuunda kifaa ambacho kinamuzidi akili? 100%? tuwe makini jamani ndo tushafanywa ndondocha ivo.teknolojia gani ambayo haina mechanism? mwalimu wao wa teknolojia ni nanii?
 
Chat GTP ni yakijinga sana, juzi kati nilikuwa semina Sasa mwisho wake kulikiwa na assignment ya kufanya online nikachekelea maana Ili niwe online nahitaji MB's na device yangu yaani hata Haina kujificha ni Mimi ku copy na ku_paste bas bana semina Zima nikawa hata sisikilizi kazi yangu ni kusaini tu nipo,

Kwenye hiyo assignment Kuna swali Moja hata sikulisoma nilifanya tu kulikopi halafu Nika paste kwa AI afanye chap kanipa jibu nikarudi kujibu bila hata kusoma swali, AI kanipeleka Chaka kumbe swali lenyewe rahisi kishenzi kama ningelisoma nigelipata bila hata iyo AI.

Maswali yote alifanya AI kazi yangu ilikuwa ni ku copy na ku paste, bila kujificha maana assignment yenyewe ya online, hakika Hilo dude linafanya tusitumie akili zetu.
 
Artificial intelligence haizuiliki.
Mapinduzi ya nne ya viwanda yanahusisha vitu kama hivi,
  • Akili bandia za kidigitali AI
  • Fundo tungamo (Blockchain technology)
  • Internet ya vitu (Internet of things) n. K
Ukijifanya wewe hutaki kuzikumbatia utajikuta umepigwa gape moja kubwa sana hapo baadae.

Hivyo tusiwe na hofu na technology.
Hata hii elimu si ajabu ikawa haina mashiko tena kama watafanikiwa mradi wa neural links
Neural links inahusu nini?
 
Ukiwa mwalimu unaichukua afu unamwambia ajitetee. Ila mwisho utamdaka Final
 
Hilo ndo lengo la waabudu shetani kuwafanya binadamu kama mazezeta ili waweze kutekeleza matakwa yao ya giza.
Akili finyu wewe... Hiyo smartphone unatumia ya nini?
Hakuna namna ya kupingana na Teknolojia. Leo ni nani anaweza kupigana na matumizi ya simu ama komputa?
 
Back
Top Bottom