Matumizi ya mafuta kwenye Altezza

nyambari

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
355
Reaction score
171
Habari ya hapa jamvini wadau?
Tafadhali naomba kujulishwa wastani wa lita kwa kilometa kwa gari ya alteza gita 6c and 4c asanteni!
 
Watakuja wataalam,
Ila kibongobongo,hii inatagemea mambo mengi,kwanza foleni ya jiji yenyewe inakula mafuta,na pia uendeshaji wa mtu pia ni kigezo kingine.
Ila kitaalam zaidi watakuja wadau.
 
Reception
14 /100
lita 14 kwa km mia
katika hali ya kawaida
 
Spreads,brevis ,verossa sio magari mazuri kwa watu wa hali ya chini
 
Altezza zenye injini ya 3S-FE (four cylinders) hutumia wastani wa lita moja kwa kila kilomita 9 au 10 kwa mizunguko ya mjini (stop and go) lakini kama ukikwama kwenye foleni na kuacha injini ikinguruma basi unaweza kwenda chini ya kilomita 9 kwa lita kutegemea na ubaya wa foleni (unaweza kumaliza lita moja bila kwenda kokote). Kwenye safari ndefu katika barabara nzuri Altezza zenye 3S-FE huenda kati ya kilomita 13 na 15 kwa kila lita moja kutegemea na uendeshaji. Lita 13 zinatosha kukutoa Dar mpaka Moro (umbali wa kilomita 190).
 
Nasisitiza tena. Altezza four cylinder inakwenda Moro kwa lita 13 za petroli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…