Mauaji Moshi: RC Mghwira asema utaratibu wa kukanyaga mafuta uliandaliwa vizuri ila vibaka walivamia kutokea nje na kusababisha maafa

Mauaji Moshi: RC Mghwira asema utaratibu wa kukanyaga mafuta uliandaliwa vizuri ila vibaka walivamia kutokea nje na kusababisha maafa

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amesema paliwekwa mabeseni ya mafuta katika mageti yote ila cha ajabu katika geti moja palitokea kundi la vijana kutoka nje ya uwanja na kulazimisha kuingia ndani kwa nguvu ndipo watu wakaanza kukanyagana.

Akizungumza katika ibada ya kuwaaga marehemu mama Mghwira amesema vijana hao hawaeleweki walikuwa wanaingia uwanjani kufanya nini kwani ibada ilishamalizika, yawezekana walikuwa vibaka.

Mkuu wa mkoa amewataka vijana hao wasiofahamika hadi sasa kutubu mbele za Mungu kwani dhambi waliyoitenda ni mbaya sana.

Mama Mghwira amesema Huduma za kiimani zitaendelea kama kawaida na kwamba mikutano ya Injili kuanzia sasa itaratibiwa kwa makini na ameomba kukutana na viongozi wote wa dini mkoani humo.

Mama Mghwira amesema aliongea na Rais Magufuli leo asubuhi na kwamba Rais alimtaka kutositisha shughuli za kidini bali waweke utaratibu mzuri wa kuzimonitor.

Source: TBC
RC amenikwaza, angekaa kimya ingesaidia-onye wenye akiri timamu waepuke ibada za namna hii
 
Yamekuwa hayo tena, anamanisha kuwa vibaka walikuwa wamekwenda kukwapua upako?.
 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amesema paliwekwa mabeseni ya mafuta katika mageti yote ila cha ajabu katika geti moja palitokea kundi la vijana kutoka nje ya uwanja na kulazimisha kuingia ndani kwa nguvu ndipo watu wakaanza kukanyagana.

Akizungumza katika ibada ya kuwaaga marehemu mama Mghwira amesema vijana hao hawaeleweki walikuwa wanaingia uwanjani kufanya nini kwani ibada ilishamalizika, yawezekana walikuwa vibaka.

Mkuu wa mkoa amewataka vijana hao wasiofahamika hadi sasa kutubu mbele za Mungu kwani dhambi waliyoitenda ni mbaya sana.

Mama Mghwira amesema Huduma za kiimani zitaendelea kama kawaida na kwamba mikutano ya Injili kuanzia sasa itaratibiwa kwa makini na ameomba kukutana na viongozi wote wa dini mkoani humo.

Mama Mghwira amesema aliongea na Rais Magufuli leo asubuhi na kwamba Rais alimtaka kutositisha shughuli za kidini bali waweke utaratibu mzuri wa kuzimonitor.

Source: TBC

Vibaka?? wangapi? Dhidi ya waumini wangapi?? Aisee
 
Back
Top Bottom