Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?



Sio kweli mkuu...Tanzania sio nchi inayoongoza kwa uchaw duniani....its Germany instead!!

Afu kwa nn mmeshklia kusem kwmb nowhere else albnhos are killed ispokuw Tanzania? How about Congo? Siung mkon mauaj y albinho, lkn achen kudangny....
 
Sasa umekuwa raia wa wapi? Kwa taarifa yako DRC nao wanaua zeruzeru na leo hii DW wameripoti.
 
Nahama mada.MAN SUBU andika vizuri sijakuelewa,samahani.Narudi kwenye mada;bado nampa muda mkuu!
 
Mi nilijitoa zamaaaaaani alipoingia kipindi.cha pili ndo.namalizia kufungasha nisepe huyu mmmmmm hapana?????
 
Ngoja gharika ya mabonge ya barafu ya kilo 50 yaangushwe kama shinyanga labda watasikia
Ingekua inawezekana mvua ya namna hiyo kunyesha kwenye nyumba za wahalifu na kuwaacha waadilifu ingekua safi sana lkn kwa bahati mbaya haiko hivyo.
 
Nimecheka sanaa baada ya kusoma hii post mwisho nimejikuta nalia kwakuwa siku moja nitakuwa rais wa Tanzania nimeona mzigo mkubwa nitakao kuwa nao kuwafanya wananchi kujivunia utanzania wao..
Huwez kuwa had uwe mshirikina
 
Kiukweli kwenyeuso wa dunia niaibu sana, inatia fedheha kujiita mtanzania. ''Unatokea ile sehemu wanayou uwa watu?'' Ni fedheha sana, njia mbadala na madhubuti inatakiwa ili kudhibiti hii hali isitokee tena nakuliepushia Taifa letu aibu hii kubwa.
Mauaj yabahusishwa na kupata madaraka makubwa ya kisiasa,yataishaje?
 
Amekataa uraia lakini hajakataa ukazi. Kuna watu wangapi wanaoishi Tanzanialakini si raia wa Tz?

Mwanangu kaamua vizuri.

Wengine wanaweza kufanya intercession prayers. "Ikiwa waatu wangu walioitwa kwa jina langu, watajinyeyekesha na kunitafuta kwa bidii nitaiponya nchi yao".

Kinyume cha hapo, Tanzania itegemee maafa ya kutisha. Mnakumbuka Haiti? Naishia hapa kwa leo.


Umechagua Nchi Ya Kwenda Mkuu?
 
Haya ndugu Hamia Somalia ila kweli vibaya kumua albino lakini je, unajua ushenzi wa nchi nyingine? ni pm namba yako ya whatssapp nikupe mambo yalivyo ktk dunia hii kwa nchi tofauti tofauti, uchague kwa kulinga nisha na kwenu TZ.

Ndugu kukimbia janga sivyema yatakiwa ujipange vipi uokoe raia wenzako ufanyeje na si kuwakimbia.
 
Unajaribu kujificha kutoka uhalisia wa nvhi yako.
Haikusaidii sana kuukana U-Tz maana utakakokimnilia utakuta dhambi mbaya zaifi kama za kule sodoma na gomora.
Unatakiwa kusali, tena sana ili watu wajue kuwa kila mtenda dhambi hii mbaya ys ushirikina na mauaji ya albino , atailipia dhambi hiyo kikamilifu.
 

Nakuelewa ndugu wiseboy na wengine wenye mapenzi mema na moyo wa kuguswa na matatizo ya wengine. Sipendi kukuumiza zaidi ila ukweli ni kwamba hayo uliyoyaona ni chembe tu, yapo mabaya kama hayo hayaonekani wala kugundulika.

Nakushauri badala ya kuukana utanzania wako basi jambo hili likufanye uipende Tanzania zaidi kwa kuanzisha harakati za dhati dhidi ya ukatili huu.

Mimi nafahamu jinsi ambavyo vitendo kama hivyo vinafanyika kila mahali duniani ikiwa hata nchi zilizoendelea. Utabisha lakini ushahidi upo japo sio kwa albino lakini hasa kwa watoto wadogo.

Watu fulani fulani huko Ulaya, America, Asia, n.k ambao ni "kizazi cha nyoka" huwateka watoto na kuwachinya baada ya kuwatesa sana malengo yao ni kama ya wale wanaotesha albino, yaani imani za kishirikina. Wengi hamtaamini lakini kwa kifupi sana ukweli ndio huo. Tuombe Mungu sana!
 
mkuu wiseboy umetumia lugha nyepesi sana ndo maana watu wengi wanakushambulia hawajakuelewa, ila ukweli ni fedheha kubwa sana machoni pa mataifa mengine na hata mbele za mwenyezi Mungu, kwa hakika maovu yote yatendekayo kwa ndugu zetu hawa wenye ulemavu wa ngozi malipo yake ni hapahapa duniani, nimeanza kuamini kuwa haya maafa ya ajabuajabu yanayotokea nyakati hizi nchini Tanzania ni malipo kwa maovu yatendekayo kwa ndugu zetu hawa wasio na hatia.
Nawasilisha.
 
Last edited by a moderator:
HAHAHAH KAKA HUWEZI KULIKIMBIS TAIFA BALI TAFUTA SULUHU!HALAFU KUNA MASWALI UNANIACHA NAYO KWELI ULIKUWA MTZ TANGU AWALI?ama mhamiaji
 
Nakukumbusha tu kwamba wakati kama huu mgumu sana kwa ndugu zetu malbino kuukana ukaya wako na kutafuta pengine pakujifichia ni USALITI wa hali ya juu sana kwa ndugu hao.

Kumbuka kisa cha Nabii wa Mwenyezi Mungu Yunus/Yoshua kama wanavyomuita wengine alichofanya na matokeo yake.
Yunus aliletwa na Mwenyezi Mungu aje kuonya waovu waache maovu yao lakini kazi yake haikuzaa matunda yeyote. Alikanwa na kupingwa na wale waovu, hawakumsikia kwa maonyo aliyokuwa anawapa. Mwisho wa siku akaamua kuwatosa na kuondoka na kuicha kazi tukufu ya kukataza maovu. Mwenyezi Mungu akaamua kumuadabisha kwa kumuarisha samaki ammeze na alipojua kwamba amekosea wakati yupo ndani ya tumbo la Chewa akamuambia Mungu, Ee Mola wangu mimi nimeidhulumu nafsi yangu dhulma kubwa kabisa na hakuna mwenye kusamehe makosa ila wewe, nipe msamaha kutoka kwako....

Kwahyo haifai kukimbia tatizo bali endelea kuwa sehemu ya wakemeaji na sio lazima wakusikie wenye kukumewa ila watakaposikia itakuwa jambo jema kwako na kwao. Fikisha ujumbe tu Mungu anaona wauaji hao wote na ipo siku atawadhalilisha sana tena kabla hawajazama makaburini mwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…