Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

sivyo, unavyofahamu ni makosa kabisa na inabidi usome kuhusu STEM CELLS


You are Just a bush Doctor;;

Soma hapa;

Where's the rest of it going, Rooney? Two years after spending £15k on hair transplant, Wayne needs ANOTHER operation to hide baldness
England striker, 27, has new bald patches following first operation

Asim Shahmalak from Channel 4's Embarrassing Bodies advised another
Rooney's wife Coleen gave birth to second son Klay this week
Dr Shahmalak performs procedures at Crown Clinic, Manchester
Transplant surgeries at clinic shot up by 25% after Rooney had operation


Read more: Two years after spend £15k on hair transplant, Wayne Rooney needs ANOTHER operation to hide baldness | Daily Mail Online
Follow us: mailOnline on Twitter | DailyMail on Facebook
 
Last edited by a moderator:
Mdau: You are hypocrite

Ulianza ku-attack hoja kwa kusema "genetic coucelling" HAIPO NA NI UZUSHI!

nimekupa assignment ya ku-ggoogle umepata majibu.

Sasa unawadanganya umma,wanasiasa, wana JF na medical students kuwa haisaidia tatizo la Albinism.


Nenda tena kwenye Website ya University ya Maryland utakuta fact hizi

Prevention

Because albinism is inherited, genetic counseling is important. People with a family history of albinism or hypopigmentation should consider genetic counseling.


Source: Albinism | University of Maryland Medical Center Albinism | University of Maryland Medical Center
University of Maryland Medical Center I kuwa serikali

Hoja yangu ni kuwa genetic counceling itasaidia na kwamba sirikali na Wizara ya Afya haijafanya kazi ya kutosha katika kukabiliana na tatizo hili kwa kuelimisha umma jinsi ya kuzuia albinism.

Mfano albinos kwa albinos wamekuwa wakioana (aa vs aa) wakati tayari wana phenotypic expression of albinism. Koo zao pia wanaoana. Genotypically you can't identify them 100% bila maabara za kisasa but apperenty you can see it in the colour of carrier eyes and you can trace them through family or descendants history probing as supported by research of Maryland University and others. This is applicable to other inheritable disorders such as epilepsy, ca and congenital heart diseasesCiao ! Na kutafutia data ya population ya albino duniani na utaona tofauti kati ya nchi maskini na tajiri.
Mdau
1. neno "hypocrite" sijui unalitumiaje hapo kuni address mimi, kama hutojali unaweza fafanua.
2. Kama kusema kuwa mimi binafsi sijawahi (sikuwahi) kusikia "genetic counceling" sijui umetafsiri vipi kumaanisha nimesema HAIPO NA NI UZUSHI. Mara ya kwanza nilidhani huelewi vizuri kingereza na hivyo unapat ugumu kutafsiri, lakini baada ya kuona hio post yako hapo juu naona una tatizo la uelewa tu.
 
Mdau
1. neno "hypocrite" sijui unalitumiaje hapo kuni address mimi, kama hutojali unaweza fafanua.
2. Kama kusema kuwa mimi binafsi sijawahi (sikuwahi) kusikia "genetic counceling" sijui umetafsiri vipi kumaanisha nimesema HAIPO NA NI UZUSHI. Mara ya kwanza nilidhani huelewi vizuri kingereza na hivyo unapat ugumu kutafsiri, lakini baada ya kuona hio post yako hapo juu naona una tatizo la uelewa tu.

I task you to look for scientific proof of your argument.JF si kijiwe cha Sangoma. Kuna ma Proffessors na proffessionals.
 


Vick-Ntentema--September22-2014.jpg

Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun, Vicky Ntetema


Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (Shivyawata), limeitaka serikali kupitisha adhabu ya kunyongwa kwa wale wanaohusika na mauaji ya Albino.

Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Amani Kimataifa ya Albino jana jijini Dar es Salaam, Rais wa Chama cha Albino Tanzania (Tas), Joseph Tona, alisema kauli hiyo imetokana na ongezeko la idadi ya mauaji dhidi yao.

Kadhalika, takwimu za kutoka mwaka 2006 zinaonyesha kuwa Albino 74 wameshauawa kikatili, huku 56 wakinusurika kifo, na kati yao 11 wameongezewa ulemavu mwingine wa kudumu.

"Tunaadhimisha siku ya amani Tanzania, lakini hatuna amani kabisa, wenzenu tunakatwa viungo na kuuawa kama kuku bila huruma, kingine cha ajabu makaburi 18 ya albino wenzetu yamefukuliwa na miili yao imetolewa, picha hii inaashiria nini?" alihoji Tona.

Alisema hofu hiyo imesababisha maziko yao kutokuwa na heshima kama wengine kutokana na baadhi ya familia kuwazika wapendwa wao kwa siri na wengine ndani ya nyumba, au kuweka zege nzito katika makaburi kuzuia ufukuaji wa miili yao.

Alisema licha ya serikali kuweka vikosi kazi katika kudhibiti mauaji hayo, bado haisaidii kitu kutokana na baadhi ya polisi na maofisa kuwa miongoni mwa vinara wa kupokea rushwa.

Kwa mujibu wa Tona, matukio zaidi ya 120 ni kesi za mauji ya albino, kati yake 11 ndiyo yaliyofikishwa Mahakama, ambapo kati ya hizo kesi tano tu zimeweza kutolewa hukumu hadi sasa.

Akitoa ushuhuda mmoja kati ya waathirika ambaye mikono yake miwili imekatwa, Mariam Stanford, mkazi wa Ngara, mkoani Kagera, aliwataka wauaji wa albino wanyongwe hadharani ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.

"Japokuwa Tanzania inasifika ndani na nje kama kisiwa cha amani, tafsiri hiyo ni kinyume kwani ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mauaji ya kikatili, hivyo mwito wangu kwa viongozi wa dini tumieni midomo yenu kupinga hali hii kwa sababu na sisi tumeumbwa na Mungu na tunastahili kuisha kama wengine," alisema Miriam.

Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun, Vicky Ntetema, aliishauri serikali kupitia vikosi kazi vilivyochukua jukumu la kuchunguza mauaji na ukatwaji wa viungo kwa albino, kutangaza matokeo kwa umma ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Pia, iuelezee umma matokeo ya kura za siri zilizopigwa katika mikoa tangu mwaka 2009 hadi sasa zibainishwe wazi kwani nyingi zimeonyesha waganga wa jadi kutumiwa na na viongozi wa kubwa katika kuwania nyadhfa mbalimbali serikalini.

Kutokana na hofu hiyo, ameitaka serikali kurejea mkakati wa mwaka 2009 uliotolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ili kupiga marufuku leseni za waganga wa kienyeji na wale wa jadi.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, alizitaka taasisi zilizopewa jukumu la kusimamia vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya walemavu hususani albino kutekeleza majukumu waliyopewa kisheria kwa uadilifu mkubwa jamii ya Watanzania ione haki inatendeka ili kudumisha amani ya nchi.


CHANZO: NIPASHE
 
Imani pototfu, Unyanyasaji, uonevu, ukatili hakuna nafasi hapa katika jamii yetu. Kuheshimu uhai na haki ya kila mtu., Tuache uhuni huo wa mauaji.
 
Tunalazimika kuhoji hivyo kutoka na mwenendo wa chama hicho na wanachama wake huku matukio ya mauaji ya ndugu zetu maalbino yakiendelea bila hatua stahiki kuchukuliwa,

Kumekuwa na minong'ono kwa mda mrefu kuwa chama hiki huabudu imani za kishirikina na kuwa viungo vya maalbino vilikisaidia chama hicho kushinda uchaguzi wa 2010,

Wadadisi wa masuala ya kichawi wanasema kuwa kampeni za uchaguzi wa 2010 chama hicho kilikusanya wachawi karibu 200 toka pande zote za nchi na kutembea nao nchi nzima kila wilaya na kata katika kampeni zao, mabasi madogo 10 aina ya coster ndio ulikuwa udafiri wao,

Ni kipindi hicho ndicho mauaji ya ndugu zetu yalipamba moto, na minong'ono zaidi inasema katika misafara hiyo ilihusisha ushirikina wa kutumia viungo vya ndugu zetu maalbino, fisi na simba.

Taarifa za minong'ono hiyo inapata nguvu kutokana na kigugumizi cha serikali ya chama hicho katika kushughulikia wahalifu hao dhidi ya ubinadamu.

Baadhi ya waganga wa kienyeji waliofanyiwa ma hojiano na shirika moja la kigeni wanakiri kuwa wateja wao wakubwa ni wanasiasa wa ccm na watawala (serikali).
 
100% true na leo kuna mahala nimetoa comment ya hili swala...
_haiwezekani wauliwe na hawakamatwi wauwaji..
 
Nimesikitika sana leo nilivyoangalia Taarifa ya habari ikisema Siku tano ambazo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza alitoa ili awe amepatikana Mtoto Pendo akiwa hai zikiwa hazijazaa Matunda.

Ninasikitika kwa sababu Watu wenye ulemavu wa Ngozi wamekuwa wakiuawa na wauaji kupotea bila kukamatwa na walio kamatwa wanaendelea kula Bata Magereza bila bila Kuhukumiwa.

Kutokuhukumiwa kwa wale waliokamatwa ndio sababu kubwa ya mauaji ya Albino kuendelea.

Mimi nafikiri Viongozi baadhi watakuwa wanahusika na hivi vifo na ndio maana hawataki kuchukua hatua stahili kwa watuhumiwa.

Sababu kubwa ya mauaji ya Albino ni Waganga wa kienyeji ambao wameachwa wakiendelea kufanya ushirikina ndani ya hii Nchi. Ccm ni wadau wakubwa wa hawa waganga wa kienyeji ambao ni chanzo kikuu cha mauaji ya Albino.

Mimi naishauri Serikali sikivu ya Ccm ichukue hatua kwa Waganga wa Kienyeji ambao ndio sababu kubwa ya huu ushirikina wa kutumia Viongo vya Wanadamu.

Hakika Nchi yoyote inayokumbatia wapiga Ramli lazima itakuwa na Balaa siku zote.
 
Mwaka huu wa uchaguzi ni mbaya sana kwa albino, adui za albino ni WANASIASA na WAFANYABIASHARA washirikina.
 
Nimesikitika sana leo nilivyoangalia Taarifa ya habari ikisema Siku tano ambazo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza alitoa ili awe amepatikana Mtoto Pendo akiwa hai zikiwa hazijazaa Matunda.

Ninasikitika kwa sababu Watu wenye ulemavu wa Ngozi wamekuwa wakiuawa na wauaji kupotea bila kukamatwa na walio kamatwa wanaendelea kula Bata Magereza bila bila Kuhukumiwa.

Kutokuhukumiwa kwa wale waliokamatwa ndio sababu kubwa ya mauaji ya Albino kuendelea.

Mimi nafikiri Viongozi baadhi watakuwa wanahusika na hivi vifo na ndio maana hawataki kuchukua hatua stahili kwa watuhumiwa.

Sababu kubwa ya mauaji ya Albino ni Waganga wa kienyeji ambao wameachwa wakiendelea kufanya ushirikina ndani ya hii Nchi. Ccm ni wadau wakubwa wa hawa waganga wa kienyeji ambao ni chanzo kikuu cha mauaji ya Albino.

Mimi naishauri Serikali sikivu ya Ccm ichukue hatua kwa Waganga wa Kienyeji ambao ndio sababu kubwa ya huu ushirikina wa kutumia Viongo vya Wanadamu.

Hakika Nchi yoyote inayokumbatia wapiga Ramli lazima itakuwa na Balaa siku zote.

Mungu asaidie Mtoto Pendo apatikane. Mungu awalaani wote wanao husika kudhulumu haki ya kuishi kwa hawa walemavu.
 
Inasikitisha mtu kutaka utajiri kwa kukata kiungo cha albino......inaniuma sana sana.....!ila hao wahusika waelewe hii dunia ni ya kupita tu.
 
Cha msingi hapa tumuombe Mwenyezi Mungu amnusuru huyu mtoto Pendo apatikane akiwa hai
 
umenikera sana kusema hii ni serikali sikivu,futa usemi wako haraka ndo twende sawa,wewe mwenyewe umekiri kuwa ccm inaua ndugu zetu leo usikivu wa hawa kenge umetoka wapi? mimi ni mbwa nitawala wote hadi kikwete ngoja kichaa cha mbwa kianze.
 
Hili taifa limejaa wapumbavu wengi sana, kama unakata kiungo cha mwili wa mwenzako ili ufanikishe mambo yako wewe ni mpumba.vu mkubwa sana ndiyo matokeo ya kucheleweshwa kwa hukumu za kesi zilizoko mahakamani na kutotoa adhabu kali kwa wakosaji, leo mtoto ananyakuliwa kama kifaranga wa kuku aliyekamatwa na Mwewe huku viongozi wanaleta siasa zao za kipumbavu kwenye roho ya mtu, jiwe la msingi la taifa hili ni ushirikina na uchawi ndiyo maana watawala wanafanya upumbavu na wananchi wanafanya upumbavu tunakuwa na 'taifa la wapumbavu'
 
Serikali inahusika na mauaji haya 100% percent! iko wazi kila mtu sasa amefahamu ni namna gani viongozi wa ccm wameagiza na kusimamia mauji haya ya watanzania wenzetu bila huruma kwa manufaa yao kisiasa.

Wote kwa pamoja tuwalinde na kuwanusuru waTanzania wenzetu kwa kuikataa Ccm.!!
 
Back
Top Bottom