Mauaji ya Karume 1972: Je, muuaji aliwahi kukamatwa na kushitakiwa?

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Nimekuwa nikipata habari kuwa jabali la siasa za Zanzibar aliuliwa na Askari jeshi nje ya makao makuu ya chama cha ASP majira ya jioni tarehe 07/04/1972 alipokuwa akicheza bao. Mauaji yake yalifanyika kwa njia ya kupigwa Risasi.

Ni upi wasifu wa askari huyu muuaji wa shujaa huyu na je alikamatwa na kushitakiwa? Alifungwa au alinyongwa?

Pia Soma
- Utata kifo cha hayati Abeid Karume
 
Jay One,
Suala la Lisu liweke pembeni shoga yangu. Mimi nimekuja na mauaji ya Jemedari na mwanamapinduzi Mzanzibari Abeid Karume.
 
Hii kesi haina umuhim tena maana hata huyo alietuma (master mind) kuuliwa kwa Karume naye ni marehemu. Siku kama ya leo ni vyema kukumbuka kauli za marehemu Karume " Muungano ni kama koti likikubana unaweza kulivua"
 
Askari huyo aliuawa katika majibishano ya risasi na vyombo vya ulinzi alipokuwa akijaribu kutoroka...wahusika wenzie walikamatwa na kusota gerezani...wengine waliachiwa baadaye..

ila baadhi ya watuhumiwa ambao wakati wa tukio walikuwa Bara Nyerere alikataa kuwarejesha Zanzibar, maana inawezekana wangekula risasi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…