Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?

Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?

Ndugu walimtafuta maeneo mbalimbali bila mafanikio. Taarifa ilitolewa Polisi lakini walikanusha kumshikilia. Polisi walisema Robert hakuwa kwenye orodha ya wahalifu wanaotafutwa na Polisi. Na hata angekua mhalifu wangemkamata kwa utaratibu rasmi na kumpeleka mahakamani, sio kumvizia mtaani.
Ooh kumbe utaratibu wa Kukamata unafahamika?
 
Tarehe 13 April, Meya Mastaafu wa Manispaa ya Ubungo, Boniphace Jacob alitoa taarifa ya kupotelewa na ndugu yake Bw. Robert Mushi maarufu kama Babu G, ambaye alipotea mapema mwezi April 2024. Inadaiwa alikamatwa na watu waliojitambulisha kuwa Polisi maeneo ya Kariakoo na baada ya hapo hakuonekana tena.

Ndugu walimtafuta maeneo mbalimbali bila mafanikio. Taarifa ilitolewa Polisi lakini walikanusha kumshikilia. Polisi walisema Robert hakuwa kwenye orodha ya wahalifu wanaotafutwa na Polisi. Na hata angekua mhalifu wangemkamata kwa utaratibu rasmi na kumpeleka mahakamani, sio kumvizia mtaani.

Baada ya hapo Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar likatoa taarifa ya kupotea kwa Robert na kwamba anatafutwa na ndugu zake. Hata hivyo ndugu walipofuatilia waliambiwa Jeshi la Polisi halijapata taarifa wala fununu zozote za alipo kijana wao, hivyo waendeele kuwa wavumilivu, wakati juhudi za kumtafuta zikiendelea.

Ndugu wamehangaika kumtafuta hospitali zote kubwa za jijini Dar, wakihisi huenda alipata ajali na akaumia kiasi cha kushindwa kujieleza hivyo akalazwa kama "unknown patient". Lakini jitihada hizo hazikuleta matokeo.

Leo wakaambiwa "nendeni hospitali ya Polisi Kilwa Road, ndugu yenu amefichwa mochwari pale". Wakaenda. Lahaula! Wakamkuta Robert akiwa kwenye jokofu la baridi. Hakuwa Robert tena bali ni mwili wake ukiwa na majeraha ya kipigo. Ni mauaji ya kikatili. Maskini Robert, hajawahi kuwa na ugomvi na mtu, kwanini atendewe haya?

Ndugu walipouliza wakaambiwa maiti ilipelekwa tarehe 10 April 2024. So ina siku 12 hapo Mochwari. Hii inamaanisha wakati Polisi wakidai kumtafuta Robert, alikua tayari Mochwari 😭.

Watumishi wa Mochwari wanasema maiti ililetwa na Askari. Walipoulizwa majina ya Askari na wanatoka kituo gani, wamewataka ndugu wa marehemu kuuliza uongozi wa hospitali. Viongozi wa hospitali walipoulizwa wakataka ndugu kuwasiliana na Msemaji wa jeshi la Polisi, kwani wao sio wasemaji.

Ni tukio la kinyama linalopaswa kulaaniwa na watu wote. R.I.P Babu G. Gone too soon. Damu yako iwe juu ya wote waliohusika.
View attachment 2971830

Pia soma:

Kamanda Muliro: Malisa GJ, Boniface Jacob wakamatwe kwa tuhuma za kupotosha taarifa za kifo cha Robart Mushi
Je kuna anayefahamu sababu ya dogo kukamatwa?
 
Naungana na Malisa GJ kwamba MULIRO J4 ameingizwa chaka kwenye taarifa au hakuelewa vizuri maelezo ya Malisa .

Maelezo ya Malisa yapo CLear ,hakuna sehemu yeyote alipolaumu jeshi la polisi kuhusika ila Muliro anasema watamkamata Boniface exmayor na Malisa kwa Kupotosha kifo cha "Babu G".

Wakishupaza shingo kuwakamata kina Malisa watajivua nguo kabisa ,inakuwaje Polisi wahifadhi Mwili then ndugu wamtafute kisha waseme hawana taarifa yeyote ina maana vituo havina mawasiliano? Hawana News Bulletin kupeana Update ya kila tukio linalotokea? Kwa ajali ni tukio ambalo lazima Polisi wawe na record ilikuwaje Ndugu wakati wanamtafuta hawakuwaambie siku ile ile au kesho yake kwamba kuna ajali ilitokea waende mochwary kilwa road wakatambue mwili? Taarifa zinasema alikamatwa K/kooo ila Muliro anasema aligongwa "Buguruni - Kimboka".
 
Daah Yan hawa Polisi ni Mbwa kabsa hivi kweli unaenda kumkamata kijana Innocent hivi na kudhulum uhai wake na wakati kuna jitu linasema litapoteza watu juzi tu na liko uraiani
 
Nina wasiwasi huyu kijana alikuwa Sio Raia mwema
Ni Kwa nini Mnalazimishia POLISI Ndio waliomuua? POLISI imekataa wanafamilia wanalazimishia kuuwawa na POLISI
Kuna nini hapa? Kwani Tanzania kuna vijana wangapi walikufa Tarahe hii? Mbona wao hamna shida Huyu vipi?
There is something wrong
 
Kuna watu wa ovyo Sana hapa duniani,Mungu uwalipe kwa matendo yao.
Bila hata kauli hii Karma italipa kwa kila wanachokifanya si unaona yule mwingine kila siku anashinda kwa Wachungaji na masheihk wamuombee ila hakuna kitu anapata kila mwezi anafata viongozi wa Dini anataka kutubia kimya kimya bila kusema alifanya nini...
 
Mama Samia na yeye kaanza kunariki haka ka mchezo ka kutekana, kuumizana na kupotezana kalikoasisiwaga na marehemu.

Kama yeye si sehemu ya huu uchafu basi haraka sana aruhusu uchunguzi HURU ufanyike vinginevyo na yeye anaanza kujipakaza damu za watu.
 
Jitahidi uwe unasoma habar kwa kina kabla ya kukurupuka kuandika utajidhalilisha bure
Nina wasiwasi huyu kijana alikuwa Sio Raia mwema
Ni Kwa nini Mnalazimishia POLISI Ndio waliomuua? POLISI imekataa wanafamilia wanalazimishia kuuwawa na POLISI
Kuna nini hapa? Kwani Tanzania kuna vijana wangapi walikufa Tarahe hii? Mbona wao hamna shida Huyu vipi?
There is something wrong
 
Kuna sababu ya kuangalia upya sheria zetu, hawa polisi ni kama vile wamepewa mamlaka ya kuua raia kwa kisingizio cha kuitwa majambazi.

Sasa panatakiwa itungwe sheria itakayowataka wakuu wa hospitali zote nchini, iwe za wilaya au mikoa, wawe na mamlaka ya kuwahoji polisi pale wanapopelekewa marehemu kwenye hospitali zao kwa ajili ya kuwahifadhi, polisi wakishindwa kutoa maelezo ya kuridhisha, wakuu wa hospitali wawe na mamlaka ya kukataa kupokea marehemu hao.
Point
 
Naomba kujua yule kada wa bukoba alisema tutawapoteza na polisi msimtafute na yeye kashaenda kuhojiwa au uchunguzi unaendelea maana bado watu wanapotea anajua wanakoenda na waliko wengine ambao wanatafutwa ... Polisi mngeenza na huyo mngejua mengi
 
Back
Top Bottom