Maulizo ya mshahara kila mwezi - Watumishi wa Umma

Maulizo ya mshahara kila mwezi - Watumishi wa Umma

Basi msiwe mnauliziaulizia sana mishahara jamani kha kwani mnaotoa picha mbaya sana kwamba mnafanya kazi kwa kujilazimisha tu na sio kwa wito kama ulivyosema na hiyo mishahara mnayolipwa ni kiduchu sana haiwezi kuwatosheleza kwa mwezi mzima.
Any way poleni nawaonea huruma jamani mnavyolalamikalalamika kuulizia mishahara.
Nakumbuka nilivyokuwaga muajiriwa mshahara wangu nilikuwa nautumia kukopea benki na kufanya uwekezaji tu nilikuwa sina time na mshahara kwa kweli.
Nawashaurini kopeni kwenye mabenki mfanye biashara muwe mnaingiza kipato kingine.
Naamini kabisa katika mazingira unayoishi huwezi shindwa kubuni biashara yeyote , jaribuni hata biashara ya bodaboda huwezi kosa kijana mwaminifu wa kufanya hiyo kazi.
Na pia jitahidini kuishi maisha ya kujibana ya kujinyima vitu ambavyo sio vya msingi ili kupunguza matumizi yasiyokuwa na ulazima.
Nawashauri msome kitabu kinaitwa the richest man in babylon na uzifanyie kazi theory zake, nyingi ni simple na zipo kiuhalisia kabisa na maisha yetu ya kila siku.
Nyie ndio injini ya Serikali mnapokuwa na malalamiko madogomadogo haya ya kulalamikia mishahara kuchelewa wakati mwisho wa mwezi haujafika mnatia mashaka kwa sisi wananchi wa kawaida kwamba injini ya serikali yetu haipo sawa.
Eeh Mungu Baba Mwenyezi liangalie kundi hili la hawa watumishi wa umma wanaouliziaulizia mishahara kabla ya mwisho wa mwezi na kwa jinsi itakavyoona inafaa waondokane na kero hii .Amina
Maskini mnaongozaga kwa kutoa ushauri butu
 
Maskini mnaongozaga kwa kutoa ushauri butu
Poleni sana , na Mungu Baba Mwenyezi mjinga kama huyu endelea kumweka hapohapo awe tegemezi wa mshahara na huku ikifika tarehe 20 ya mwezi mshahara uwe umekwisha ateseke yeye na vizazi vyake 4 wawe wategemezi ya mishahara ya serikali ya ngazi ya tgos.
 
Hahaha na iyo ndio raha ya kazi. Raha ya kazi ni kuulizia mshahara unatoka lini 😀😀
Sema labda raha ya kazi kwa nyie waajiriwa msiojielewa.
Kwangu mimi raha ya kazi ni kukamilisha tasks na kutimiza malengo ya shughuli na mipango iliyowekwa
 
hivi kuulizia mshahara wangu huwa inamaanisha nina maisha magumu.
Kuulizia mshahara kabla ya mwisho wa mwezi?
Kiutaratibu mtu anatakiwa kudai mshahara na sio kuulizia .
Sasa mwisho wa mwezi haujafika unakuwa na nguvu gani ya kuulizia mshahara kama sio kujizalilisha na kuonyesha kwamba hauna pesa.
Inatakiwa kama mwezi umepita na hujalipwa ndio unakwenda kudai mshahara kwani hapo unakuwa na haki.
Kama unaulizia mshahara na mwisho wa mwezi haujafika wewe utakuwa na maisha magumu ndugu. Mshahara umekata na hauna chanzo kingine cha fedha kwa kifupi wewe ni maskini .
Poleni sana watumishi na mnatakiwa mfahamu kwamba karibia 85% ya watumishi wa serikali wapo kwenye kundi la watanzania maskini
 
Poleni sana , na Mungu Baba Mwenyezi mjinga kama huyu endelea kumweka hapohapo awe tegemezi wa mshahara na huku ikifika tarehe 20 ya mwezi mshahara uwe umekwisha ateseke yeye na vizazi vyake 4 wawe wategemezi ya mishahara ya serikali ya ngazi ya tgos.
Endelea kushobokea mambo ya watu, utat*mbwa
 
Twendeni tukapige moja baridi moja ya moto tayari mshahara umetoka
 
Back
Top Bottom