Mawazo, Stori na historia ya maisha yangu

sanalii

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,639
Reaction score
5,767
Kwanza mimi huwa najiulizaga, hivi mawazo yanatoka wapi? Inakuaje unatokea kuwaza tu mfano unawaza ngoja niandike uzi.

Japo sijapata jibu lakini naamini mawazo/thought are social influenced thing, mazingira yanayotuzunguuka ndo yana determine sana kile kinacho kua generated akilini, how are they generated and where? I don't know.
 
Anyway, nikikumbuka kipindi niko chuo mwaka wa tatu then nilikua bado nikidhani internet ni km mawingu yani ni kama kitu kinaelea juu juu tu, huwa nacheka sana
 
Lengo sio kua na pesa ila pesa ikusaidie kufikia malengo kwa mfano kua na mahitaji ya msingi, kusaidia wenye uhitaji na kadharka, sasa ukikutana na mtu ambae lengo lake ni kua na pesa ni hatari sana.

Huyu ktu anaweza kua na hela bank then ndufu yake anaumwa hamsaidii,

Raha ya kutafuta pesa ni ipi? Uone zero nyingi bank? Then?
 
Siku ya kesho nataka niitumie kufikiria maisha nitakayoishi km nitajaaliwa kuishi miaka 50, 60 70...

Nataka niwaze nikiwa na umri huo
1. Nitakua naishi wapi
2. Nitakua naishi na nani ( aina ya familia)
3. Nitakua nafanya kazi gani
4. nitafikaje nikiwa na Afya njema
5. cycle ya watu wangu itakua ni ipi
Na mambo mengine,
Nikipata majibu nitafikiria mikakati ya kufikia ayo maisha nitayofikiria
 
kwa hiyo mkuu kila siku utakuwa unaanzisha nyuzi za kuongea mwenyewe?
 
Niliwaza kujiua nilipokua mdogo.

Yani ilikua mtu akinifanyia kosa hasa family member, basi nawaza, nikijiua kwa kunionea watu watamlaumu sana kwa kunifanyia makosa hadi nijiue then atakua anajilaumu sana na atakua anajuta kwanini amenifanyia kosa, sikua nawaza zaidi mimi kupoteza maisha ila nilikua nafikiria alienionea ata feel guilt.

sasa nimekua nagundua kua kumbe watu wengi ni waovu, wanaweza kukufanyia uovu na sio tu wakakumbuka kua wamekuafanyia uovu bali wakawa wanafurahi kabisa kwa uovu waliokufanyia
 
The facts that kuna familia Tanzania hii hata mlo mmoja ni shida ni jambo la huzuni sana. May God forbid ila ikinitokea na familia yangu ni bora niende sehemu kijijini niwe nalima familia ipate chakula, life has so many colors
 
Baada ya kuwaza sana nimeona kabisa kua naweza jifunza kua mtu mzima nikiwa bado kijana, mtu mzima in sense that niko na busara, uchumi uliotulia nk.
Katika kufikia malengo ya kuishi kama mtu mzima mwenye busara na heshima huku nikiwa mdogo nitafanya yafuatayo

1. Nitaanza kuvaa nguo za heshima, sio vimodo vilivyobana na jinsi za kuchanika ( sijawahi kuvaa vimodo tho)
2. Nitajifunza ujuzi ambao utanipatia kipato na nitaifanyia kazi kwa muda mrefu hasa upande wa cyber, like cyber security
3. Nitakua nafanya mazoezi na kula vyakula visivyo na athali sana kiafya, nitaepuka procecced sugar, mafuta mengi nk
4. Nitaepuka madeni kwa gharama yoyote
5. Nitaanza ku invest na kununua ardhi
6. Nitatulia na mwenza wangu mmoja
7. Nitajiepusha na dhulma na maovu, kuwatendea watu wema na kujitenga na watu waovu as soon as i can.
8. While I do all that, nitajitahidi ku enjoy life as much as i can with peace to be the my priority.
 
Mtu yoyote ambaye yuko vizuri katika jambo fulani ni matokeo ya mambo mawili
1. Amepata mtu anaefahamu akamfuza
2. Ametumia muda wingi kufanya jambo hilo.

Hakuna shortcut katika maarifa au ujuzi. Kwa sababu hiyo nimedhamilia kutumia muda mwingi nisome computer security. Then nione nitakapofikia. Kila kitu ni juhudi tu huhitaji kua genius kufanikiwa
 
0 x any number is 0, hii nakubali
Lakini namba yoyote ukizidisha kwa 0 kwanini isiwe namba ile ile? Yani nina 10 then nisiizinishe na chochote (neutral) kwanini isiwe 10? Whyyyyy?
 
ukiwa masikini uamue uchelewe kulala au uwahi kuamka katika kufanya kazi ulioamua ikutoe kimaisha not otherwise
 
Ukipata muda jibanze sehemu ambapo watoto wanacheza, itakua vizuri kama hawatakuona, tulia then wasikilize, kuna kitu utajivunza kuhusu hawa tunaoita watoto, it ks very interesting experience
 
"Wazuri ni wengi ila kumpata mwenye mapenzi ya kweli ndo balaa"
 
Kadri unavyokua na shauku na nia ya kusaidia watu ndio Mungu anakupa njia mbali mbali za kutafuta hela
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…