View attachment 2267827
Akihojiwa kwenye kipindi cha kinagaubaga ndugu
Maxence Melo amesema walikuja watu wasiofahamika wakitaka kumchukua ili wakamhoji kwanini amefanya mahojiano na Balozi wa Umoja wa Ulaya, lakini Balozi aliwakatalia katakata akisema hamuwezi kumchukua nikiwa naye mimi.
Kweli nchi ilikuwa ngumu sana
======
Kwenye #KurunziLive leo tunaungana na
Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji wa #JamiiForums (@macdemelo) anayehudhuria kongamano la vyombo vya habari ulimwenguni hapa mjini Bonn.
Tutaangazia baadhi ya masuala yanayojadiliwa kwenye kongamano lenyewe. Vilevile mafanikio na changamoto zinazokumba vyombo vya habari nchini mwako ikiwemo mitandao ya kijamii na majukwaa mengine ya kidijitali.
Je matarajio yako ni yapi kwenye kongamano hilo? Je una swali ungetaka tumuulize Maxence Melo? Na je vyombo vya habari vimefanikiwa kwa kiwango gani kuangazia masuala yanayokugusa?
Tuandikie maoni yako, na usikose kuungana nasi mubashara itimiapo saa kumi kamili majira ya Afrika Mashariki.