Mayai yalivyonitesa katika mimba yangu ya kwanza

Mayai yalivyonitesa katika mimba yangu ya kwanza

Daisy Llilies

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2019
Posts
1,017
Reaction score
2,158
Nilishika ujauzito tukiwa Honeymoon Mombasa. Nilistuka baada ya kurudi na kuanza kazi hali ya kutapika ilipoanza . Vyakula vingi vilinikataa, niliishi kwa banana milk shake. First trimester nililazwa siku tatu hospitali hakuna kilichokaa tumboni.

Nikisikia harufu ya mayai hata kama jirani anakaanga nitatapika vibaya sana. Mwisho ilikua hata nikiyaona tu. Mayai yalikua adui mpaka siku ninajifungua. Baada ya mama mkwe kupata habari ya uzazi kesho yake alikuja hospitali na chai, mayai, mikate na nguo za mtoto pamoja na madera ya mzazi.

Nilipoona mayai nilimwambia mama si unajua mayai siwezi kula. Alicheka sana alinijibu kula tu ugonjwa umepona. Niliyala na wala sikutapika.

Mimba ya pili ilinitesa kwa miezi mitatu ya kwanza lakini ya tatu nilikula kila kitu mpaka muda wa kujifungua.

Tupe experience yako ya mimba.
 
Yaani nilivyoelewa mimi hiki kichwa cha thread....tofauti kabisa na nilichosoma lakini nimeelewa.
Pole sana
 
Ndio niko first trimester at first nilikua nakula kitu Yani mm kila muda njaa nisione mtu anakula kitu chochote na mm kinakaa rohoni mpaka nile hicho kitu

Sasa tangu juzi nasikia mdomo mchungu Yan nakula kidogo sana najisikia kichefuchefu pia hali kama ya kutapika hivi ila najizuia, napenda sana mkate na blueband tu na chai ya maziwa hicho ndio chakula changu cha tangu juzi, nikila kitu kingine ni kidogo sana Yan najisikia hovyo

Ila nimeambiwa hiyo hali itaisha baada ya hii miezi 3 ya mwanzo[emoji25]
 
Miezi mitatu ya mwanzo ilikua hata nikiona nyama iko buchani Mimi Ni kutapika tu,baada hapo nkawa nakula nyama ila iwe imekaangwa,nilikua natapika sana[emoji17]nakula nashiba vizur tuu ila baada ya mda naenda kutapika chakula chote hadi nkawa natapika damu[emoji17]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sitasahau maumivu ya chuchu baada ya kujifungua aisee niliumwa chuchu mpaka vidonda alf unaambiwa dawa ni kumyonyesha apo apo kwny kidonda jamn mtoto alikuwa akiamka tu moyo unafanya paa mapigo ya moyo yanaenda kazi namyoyeshaje mtoto..sitasahau ilo aisee
 
Ndio niko first trimester at first nilikua nakula kitu Yani mm kila muda njaa nisione mtu anakula kitu chochote na mm kinakaa rohoni mpaka nile hicho kitu

Sasa tangu juzi nasikia mdomo mchungu Yan nakula kidogo sana najisikia kichefuchefu pia hali kama ya kutapika hivi ila najizuia, napenda sana mkate na blueband tu na chai ya maziwa hicho ndio chakula changu cha tangu juzi, nikila kitu kingine ni kidogo sana Yan najisikia hovyo

Ila nimeambiwa hiyo hali itaisha baada ya hii miezi 3 ya mwanzo[emoji25]
Pisi kali anamimba ndio basi tena mipango yangu ishafeli subira yangu ndio iliyoniponza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio niko first trimester at first nilikua nakula kitu Yani mm kila muda njaa nisione mtu anakula kitu chochote na mm kinakaa rohoni mpaka nile hicho kitu

Sasa tangu juzi nasikia mdomo mchungu Yan nakula kidogo sana najisikia kichefuchefu pia hali kama ya kutapika hivi ila najizuia, napenda sana mkate na blueband tu na chai ya maziwa hicho ndio chakula changu cha tangu juzi, nikila kitu kingine ni kidogo sana Yan najisikia hovyo

Ila nimeambiwa hiyo hali itaisha baada ya hii miezi 3 ya mwanzo[emoji25]
Usiogope tena kitakuwa kitoto cha kike hicho. Katazaliwa kembamba ila baada ya wiki 3 tu kataongezeka saana uzito. Je, Mr ukimuona roho yako husuuzika?? Mpende zaidi asijewakumbuka ma x
 
Usiogope tena kitakuwa kitoto cha kike hicho. Katazaliwa kembamba ila baada ya wiki 3 tu kataongezeka saana uzito. Je, Mr ukimuona roho yako husuuzika?? Mpende zaidi asijewakumbuka ma x

Kila mtu ananiambia ni cha kike[emoji1] Mzee baba nampenda tunapendana tena naona ndio mapenzi yamezidi zaidi japo yupo mbali kidogo ila very soon tunaenda kumlea pamoja kijacho wetu, naona yeye yuko makini sana na k kuliko hata mimi mwenyewe
 
Kila mtu ananiambia ni cha kike[emoji1] Mzee baba nampenda tunapendana tena naona ndio mapenzi yamezidi zaidi japo yupo mbali kidogo ila very soon tunaenda kumlea pamoja kijacho wetu, naona yeye yuko makini sana na k kuliko hata mimi mwenyewe
Usijali hakika k ni cha kike hicho ndo maana mapenzi yamezidi from Mr. Angalieni, mnapokutana tena asiongeze sikio la 3.
 
Back
Top Bottom