Mayai yamefurika Dar es salaam, Soko hakuna wafugaji ni Msiba

hali ni tete kwa wafugaji maana mtu anarundika mayai hawezi kuuza mwishowe anashindwq kulisha kuku wake.

soko la mayai liko congo,kuna mzungu iringa anaitwa hoffmann yeye anakusanya maelfu ya trey za mayai inatia fusoni huyoo congo,na inamlipa balaa,
 
soko la mayai liko congo,kuna mzungu iringa anaitwa hoffmann yeye anakusanya maelfu ya trey za mayai inatia fusoni huyoo congo,na inamlipa balaa,

Tatizo ni mtaji ndg kama unao njoo tukuuzie ...
 
wewe hata ukiacha kula, kama afya yao ni mgogoro itaendelea kuwa hivyo hivyo tu.
 

That is one way of thinking LAKINI pia ni vema kujiuliza.., ukizingatia wakulima /wafugaji wa hapa nao hawalipi hizo kodi kwahio cha kujiuliza ni kwamba iwapo mtu bado anaweza kuagiza mzigo nje plus cost za transport na bado akaweza kuuza kwa bei ndogo kuliko wewe uliyopo ndani ni vema kujiuliza ni njia gani wanazotumia kuweza kuzalisha mzigo wao kwa bei nafuu (kama quality ni ile ile...) na kama quality yao ni mbaya bado wewe uliyepo ndani unaweza ukauza mzigo wako kwa bei ya juu kuliko wao kwa kuuza mzigo wako kwa kuwafahamisha watu kwamba wewe wako ni wa ubora zaidi...

Utaona haya yote kuyafanya kwa ufasaha inahitaji muugano wa watu ili kuuganisha nguvu zao kitu ambacho wanaweza kuongeza value ya bidhaa zao.

Pia kumbuka huu ushindani na ushukaii wa bei bado ni faida kwa mlaji (unless bidhaa ni duni) kwahio hizo ndio changamoto zinazokuja/zitakazokuja baada ya dunia kuwa kijiji na ushindani kuwa maradufu.., hapo itabidi waliopo ndani nao waanze kuangalia na masoko ya nje na sio ndani tu
 
Mi situmii hizo vitu cauz ni cancer tupu..mi ni mwendo wa kienyeji..over
 
umefanya research kwamba wote wanaoungua cancer wanakula mayai ya kisasa? acha kupotosha umma weye!! kama huna cha kuongena ni vizuri ukakaa kimya ili watu wasijue kichwani umehifadhi nini.

Ina maana hujui kua hayo mayai ni sumu na yana madhara makubwa tu kwa afya? Nenda Ocean road watakuambia. Acha ubishi wa kikuda
 
kuku mmoja kwa wiki?!!
 
na sisi wabongo tupunguze biashara za kuigana,sometime tuwe creative.tumerundikana sana kwenye ufugaji kuku sasahivi ndo maana supply imekua kubwa na bei zimeshuka.wengine tufuge mbuzi,tulime mihogo na matunda matunda,soko ni kubwa sana la maembe,na mananasi.
 
Unashangaa Mayai.....:wacko::wacko::wacko:

Njoo mikoani huku uone watu wamevuna mavuno kibao,maghala yamefloats hakuna hata pa kuweka tena na mbaya zaidi soko hakuna:embarrassed:
 
Jaribu kuboresha bidhaa zako,
kwa kufungasha na kuunganisha watu katika vikundi kisha kuuz nje.
 

Hii inathibitisha kwamba hali ni ngumu mno purchasing power ya watu ni ndogo mno, hata uwapunguzie wanakuangalia tu! Vinginevyo wangeyakimbilia kwa bei hiyo.
 
Hayo mayai ya kidhhungu huwa yana vunjanguvu za kiume kama hamfahamu mulezi dokta yaani toka alfajiri hadi usiku ni kazi moja tuu ya kuwatilea dawa hadi kuwa yai si tatito hilo jamani ni bora ya kiyenjeji ndo huwa na ubora wa nguvu za kiume

Mkuu mayai pekee hayahusiki na nguvu za kiume bali na life style nk

 
He 4500!leteni leteni huku zenjiberi haraka !huku tunapenda pizza,vileja keki,cutles,kila siku .leteni tununue huko dar wake zenu wavivu wa kuoka oka! leteni bwana huku 8000 na hatujapunguza kasi ya kuyanunua!
 
Naibu I moja tu kutokana na ugumu wa maisha sasa hivi mayai ni luxury food kwa watanzania
 

unashangaa hilo mbona vitunguu swaumu na samaki wanaimport angali uwezo wa kuzalisha upo na vilivyozalishwa vimo ila tu kwa maslahi ya ccm na viongozi wake
 
Sidhani kama kuna ukweli wowote juu ya kuingizwa kwa mayai kutoka nje ya nchi, yawezekana hizi ni hisia tu.
Ukweli ni kwamba biashara ya mayai hasa kwa dsm ilianza kuyumba kipindi kile cha mwezi mtukufu baada ya mfungo kuisha biashara ikatengamaa ila kwa kuwa uzalishaji umeongezeka kupita mahitaji ndio maana soko limefurika...

Ushauri wangu watu wasikimbilie tu kufuga kuku kwa kuwa jirani yako nae anafuga, na kama ukiamua kuiga basi tafuta hata hotel au mlaji wa uhakika uingie nae mkataba, pia wafugaji wawe wamoja kusaka masoko. Pia kufuga mifugo mingine kama ngombe mbuzi, sungura n.k
 
Mkuu mayai pekee hayahusiki na nguvu za kiume bali na life style nk

mkuu kuna watu huongea bila hata kufanya utafiti hata kidogo - matatizo ya nguvu za kiume yanatokana na kula mayai ya kuku wa kisasa? this is very weak argument - hili ndilo taifa letu na hawa ndio wananchi tunaowategea ku argue points with some supporting justification.

Achana naye tusonge mbele ya mada yetu mkuu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…