MAYWEATHER vs PACQUIAO - (02 MAY 2015): NANI ATATOKA SHUJAA ???

MAYWEATHER vs PACQUIAO - (02 MAY 2015): NANI ATATOKA SHUJAA ???

EWGM's

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
1,521
Reaction score
2,112
Hatimayeyametimia ni siku tatu tu zimebaki kwa mabondia wawili maarufu dunia kuingiaulingoni kukata ile kiu iliyokuwa inasubiriwa na wapenzi wengi wa ndondiduniani. Nichukue fursa hii kama mpenzi wa ndondi kutoa maoni yangu na wotemnakaribishwa kuchangia kadri mnavyoweza na ni nani unadhani atashinda kwenyempambano wa Mayweather VS Pacquiao, 02 MAY 2015.

Kablasijasema nani atashindwa au kupigwa kwanza niwachambue mabondia hawa wawili.Kwenye ngumi kuna aina tatu za mitindo inayotumiwa na mabondia; Orthodox,Southpaw na Counterpuncher. Lakini pia counterpuncher anaweza kuwa orthodox ausouthpaw. Orthodox wakiwa ulingoni wanatanguliza mguu wa kushoto mbele nawana-jab na mkono wa kushoto wakati Southpaw wanatanguliza mguu wa kulia na kujabna mkono wa kulia. Counterpuncher wao hutumia akili sana na mara nyingi huwawanasubiri mpinzani afanye makosa ili wapate mwanya wa kumdhuru, kwa maananyingine huwa hawafanyi makosa wanapota nafasi.

Nianzena Floyd Mayweather (38) yeye ni orthodox/counterpuncher, mpaka sasaanashikiria rekodi ya mapambano 47 bila kupigwa (47- 0). Kwenye historia yangumi za kulipwa Mayweather hajawahi kupigwa ingawa alishwahi kuonja kipigomara 6 wakati yuko kwenye ngumi za ridhaa. Mayweather ni bondia mwenye akili nashabaha, anayeweza kubadili mchezo wakati yuko ulingoni kutegemeana na mpinzaniwake amekuja vipi. Mayweather hajawahi kupigwa ngumi na bondia yeyote kwenyeulimwengu wa ngumi za kulipwa na kuanguka ulingoni, ijapokuwa hiyo itakuwamajdala mwingine sababu kuna pambano alipigwa konde na glovu yake ikagusa zuriala ulingo lakini mwamuzi hakuona.

Katikahistoria ya mapambano 47 ya Mayweather amepigana mara 8 tu na mabondiawanaotumia mtindo wa southpaw.Mayweather mpaka sasa ameweza kushinda mikandamitano (5) ya WBC uzito mbalimbali kutokea kwenye pauni 130 mpaka 147. Uwezo wakujilinda alikuwa nao Mayweather ulingoni unawapa shida sana mabondiaaliopigana nao kuweza kumfikia kirahisi na kumdhuru.

Sasatuje kwa Manny Pacquiao (36) ni southpaw, mpaka sasa anashikiria rekodi yamapambano 64 na kupigwa matano (57- 5 – 2). Pacquiao kashaonja kipigo mara 5kwenye ngumi za kulipwa na mara 4 kwenye ngumi za ridhaa. Manny Pacquiao nibondia mwenye kasi ya ajabu sana inayoambatana na uwezo wa ngumi kali sana. Piaanamapungufu yake akiwa ulingoni huwa ni rahisi kunogewa na kurusha makonde na huwaanajisahau kwenye kujilinda. Mannyamepigana mara nyingi kwenye ngumi za kulipwa na mabondia tofauti tofautiambayo ndiyo yaliyomwakikishia nafasi na kuandika historia kwenye ulimwengu wangumi za kulipwa. Pacquiao mpaka sasa ameweza kushinda mikanda nane (8) ya WBCuzito mbalimbali kutoka kwenye pauni 108 mpaka 154.

Ukiangaliarekodi za Mayweatherna Pacquiaokirahisi unaweza sema Pacquiao atapigwa. Lakini ukiangalia mabondia Mayweatheraliowahi kupambana nao kwenye hiyo rekodi yake utatambua kuwa siku watakapokutana Mayweather atakuwa na kazi nzito.Sababu Mayweather hajawahi kukutana na bondia mwenye ngumi kali na kasi kamaPacquiao kwenye mapambano yake yote 47. Pia ukiangalia Mayweather alipopiganana Zah Judah (southpaw) alipata shida sana na alipigwa ngumi nyingi japokuwahazikuwa kali za kumletea madhara. Sasa swali linakuja je kama Mayweatherakitoa mwanya kwa Pacquiao kama ilivyokuwa kwa Zab Judah itakuwaje?. Piainaonesha kama pambano litakwenda mpaka raundi ya 12, basi Mayweatheratashindwa sababu Pacquiao ana uwezo wa kutupa ngumi nyingi sana ukilinganishana Mayweather. Hivyo itakuwa rahisi kwa majaji kutoa ushindi kwa Pacquiaosababu ya uwezo wake wa kutupa ngumi nyingi.

Kamanilivyosema mwanzo Mayweather ni counterpuncher hivyo Pacquiao inabidi awemwangalifu sana sababu anaweza kumpigwa kwa kusimamishwa kwa pambano (KO). PiaMayweather ana matatizo sana ya kuruhusu jabs kuwa zinamfikia kirahisi hiyo piainaweza kumletea madhala sababu Pacquiao ana uwezo wa kumdhuru kwa jabs tupekee.

Hivyokwa maoni yangu hayo machache naona mpambano huu uko huru kwa yeyote kushindainategemea na siku hiyo nani atakuwa na ujasiri kwa kuweza kudhibiti ,mbinu zamwenzake. Hawa wote ni mabondia hatari sana hivyo unaweza changia maoni yako nautoe sababui zako ni kwanini unaona nani atashinda kama ikiwezekana ukatoasababu itasaidia sana wengine kukuelewa kwa urahisi.
 

Attachments

  • pacquiao-mayweather-LA-presser.jpg
    pacquiao-mayweather-LA-presser.jpg
    29.6 KB · Views: 825
  • imagesVVTPQMF9.jpg
    imagesVVTPQMF9.jpg
    13.4 KB · Views: 853
  • pm.png
    pm.png
    33.9 KB · Views: 812
  • after-facing.jpg
    after-facing.jpg
    37 KB · Views: 853
Duh hiyo picha ya after facing manny na after facing mayweather inatoa jibu tosha atatota mtu hapo
 
Pacman....huwa hachoki...anarusha ngumi (ndo ulinzi wake) nyingi (combination).....mkono wake wa kushoto utamdondosha kwa mara ya kwanza gaywether.
 
Pacman anarusha ngumi sehemu zote kulia na kushoto bila kupumzisha ila Mayweather watu kama hao anawajulia anajuwa kujilinda ndio uzuri asipojilinda vizuri kapigwa ila Ulinzi ndio muhimu, kwa uzito wa ngumi na kufikisha Usoni ngumi Mayweather ni kiboko mpaka hapo Mayweather anampiga Pacman round Ya 6 utamuona Pacman chiniiiii.
 
Pacman anarusha ngumi sehemu zote kulia na kushoto bila kupumzisha ila Mayweather watu kama hao anawajulia anajuwa kujilinda ndio uzuri asipojilinda vizuri kapigwa ila Ulinzi ndio muhimu, kwa uzito wa ngumi na kufikisha Usoni ngumi Mayweather ni kiboko mpaka hapo Mayweather anampiga Pacman round Ya 6 utamuona Pacman chiniiiii.

Hahhah ......haah! Mkuu umefanya nicheke sana. Hiyo raundi ya 6 kwa mimi binafsi sidhani, lakini lolote linaweza kutokea.
 
Pacman....huwa hachoki...anarusha ngumi (ndo ulinzi wake) nyingi (combination).....mkono wake wa kushoto utamdondosha kwa mara ya kwanza gaywether.

Inawezekana kabisa mkuu ila mwaka jana alifanya makosa kama hayo kwa Marquez akapewa moja chali.
 
Inawezekana kabisa mkuu ila mwaka jana alifanya makosa kama hayo kwa Marquez akapewa moja chali.

Upiganaji wa marquez ni tofauti na Myweather...marquez likes throwing punches unlike myweather mviziaji...unachosahau marquez alishaangushwa na pacman mara nyingi...katika mapambano yao pacman ameshinda mara 3 na marquez mara moja.....watu husawazisha makosa yao.
 
Timu mane.kwasababu huyu jamaa huwa anapenda sana pesa na ni mtu anayependa sifa na ni mtu anayependa kupigana kwa staili yake mwenyewe his fast and his using left hand and fasta more than what you think. Anapenda kusoma game mapema na nu mtundu wa kutumia macho.tekiniki yake iko machoni.anaweza badili game eny time.huyo ndio mane weza.

swissme
 
Paq katika prime angeweza kupambana na May,sasa hivi kachoka May atakuwa too fast for him-hili pambano publicity imelifanya kubwa lakini ukweli ni Paq is past it- May ni mjanja kaona paq is a shadow of himself kakubali kupigana naye for easy money
 
Upiganaji wa marquez ni tofauti na Myweather...marquez likes throwing punches unlike myweather mviziaji...unachosahau marquez alishaangushwa na pacman mara nyingi...katika mapambano yao pacman ameshinda mara 3 na marquez mara moja.....watu husawazisha makosa yao.

Marquez siyo counterpuncher kama Mayweather hiyo ni kweli kabisa.Ila ukiangalia lile pambano Pacquiao alikuwa anaongoza raundi zote. Ila Marquez sijui alipata wapi wazo la kujibadili na kuwa counterpuncher, mimi naweza sema ni uzoefu tu akamvizia na Pacquiao akaingia kwenye mtego pambano na likaisha.
 
Paq katika prime angeweza kupambana na May,sasa hivi kachoka May atakuwa too fast for him-hili pambano publicity imelifanya kubwa lakini ukweli ni Paq is past it- May ni mjanja kaona paq is a shadow of himself kakubali kupigana naye for easy money

Hata Mayweather kachoka pia ni ujio wa umri, hususani hali hiyo inaonekana kwenye pambano na Maidana. Mayweather alikuwa strong sana lakini yale makali yake yamepungua ila anashindia uzoefu kusema ukweli.
 
Back
Top Bottom