Mazava chawapa likizo ya kibabe ya miezi 3 isiyo na malipo wafanyakazi wake

Wafanyakazi zaidi ya 1,000 wa kiwanda cha kushona Jezi cha Mazava mkoani Morogoro, wamezuiliwa kuingia kiwandani hapo baada ya kiwanda hicho kutangaza kusimamisha shughuli za uzalishaji kwa kipindi cha miezi mitatu, na kudai kuwa walikubaliana kifungwe Mei 24.

Source: EastAfrica Radio
Mytake - fursa kwa ni bora washone Barakoa kuliko kufunga kiwanda
 
Aisee! Pole nyingi ziwafikie. Kuishi hiyo miezi 3 na kuendelea bila salary siyo jambo jepesi hata kidogo. Kuhusu kubadili matumizi sidhani kama itasaidia maana mtaani zimetapakaa zile barakoa za mafundi cherehani.

Isitoshe tangu serikali ilipoanza kuficha kutoa taarifa za waathirika wa Covid 19, ni ukweli ulio wazi! Baadhi ya Wananchi wameanza kuipuuza Corona na hivyo hawana kabisa muda kuvaa barakoa kwa sasa.

Kwa hiyo hata kama hicho kiwanda kitabadili mbinu, bado kitakutana na changamoto nilizo zitaja hapo juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…