Mazishi ya Dkt. Augustine Philip Mahiga kijijini kwake Tosamaganga mkoani Iringa. Mkewe ashindwa kuhudhuria baada ya kuwa Kenya akiuguza mtoto

seedfarm

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2020
Posts
260
Reaction score
2,655
Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Augustine Mahiga leo atamaliza safari yake duniani kwa kuzikwa kijijini kwake Tosamaganga. Viongozi mbalimbali wa kitaifa wakiongozwa na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu watamsindikiza katika safari yake hii ya mwisho.



Aliyekuwa waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mahiga amezikwa leo kijijini kwake Tosamaganga mkoani Iringa.

Serikali iliwakilishwa na makamu wa Rais mama Samia Suluhu ambaye aliuelezea wasifu wa Balozi.

Bunge liliwakilishwa na Naibu Spika Dr Tulia Ackson ambaye baada ya kumuelezea Dr Mahiga alisema amekuja na rambirambi za wabunge lakini watazikabidhi kwa mke wa marehemu pindi atakaporejea kutoka Nairobi Kenya anakouguza mtoto.

Hata hivyo mwisho wa shughuli za mazishi Waziri wa Ardhi mh Lukuvi aliagiza DC Kasesela wa Iringa Mjini akabidhiwe michango yote ya rambirambi hadi aitunze hadi atakapopewa maelekezo rasmi na familia.

KIFO: TANZIA: Balozi Augustine Philip Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria amefariki dunia - JamiiForums
 
Aisee. Kwa hiyo wengine wanasafirishwa na kuzikwa kiheshima na wengine wanazikwa makaburi ya umma usiku. Mungu anawaona nakwambia. Tumaomba picha za kwenye msiba tuone ni serikali inazka au ni ndugu.
 
Kuvaa mask napo imekuwa taarifa?
 
Lakini huyo alikuwa na nyadhifa kubwa,,halafu Ni kada wetu yule ujue...
Mbele za Mungu hakuna nyadhifa yoyote. Binadamu wote sawa tu. Kama ana nyadhifa kubwa mbona amekufa? Kwanini anazikwa kaburini na tani saba juu yake kama hawa wengine mnaowazika usiku?

Nyadhifa iko wapi hapo? Kila binadamu anapaswa kuheshimiwa hakuna alie juu ya mwingine mwisho wa siku wote kaburi linatuhusu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…