Mazungumzo ya Alfu Lela Ulela au Siku Elfu na Moja - Kitabu cha Pili

Mazungumzo ya Alfu Lela Ulela au Siku Elfu na Moja - Kitabu cha Pili

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Baada ya kitabu cha nne, sasa tuone kitabu cha pili. Fuatana nami hadi kitakapoisha, pia hivi vyote na vingine vingi unaweza kuvisoma bure ndani ya maktaba app.

ALFU LELA ULELA KITABU CHA PILI.jpg

MAZUNGUMZO YA ALFU LELA ULELA
AU
SIKU ELFU NA MOJA
KIMEFASIRIWA KWA KISWAHILI NA
EDWIN W. BRENN
KITABU CHA PILI

YALIYOMO

UTANGULIZI
SAFARI SABA ZA SINBAD BAHARIA
SAFARI YA KWANZA
SAFARI YA PILI
SAFARI YA TATU
SAFARI YA NNE
SAFARI YA TANO
SAFARI YA SITA
SAFARI YA SABA, YA MWISHO

KISA CHA MBILIKIMO MWENYE KINUNDU

KISA CHA NDUGUYE KINYOZI WA TANO(NDOTO YA ALNACHA)

KISA CHA NDUGUYE KINYOZI WA SITA
 
UTANGULIZI​

HADITHI zinazohadithiwa, zimekuwa kama zile zinazotolewa na wazee wanawake wa nchi mbali mbali wakiwahadithia wajukuu zao. Hapana mtu anayejua ni za tangu lini, au ni nani aliyezitoa kwanza. Labda watoto wa Ham, na Shem, na Japhet (Jaffari) walizisikia katika Safina, siku za Gharika!

Watu wa nchi zingine huzihadithia kwa njia mbali mbali lakini

hadithi ni zile zile moja, hata kwa watoto wadogo wa Kizulu walio Cape, au kwa watoto wadogo wa Kieskimo walio pwani ya kaskazini mwa nchi ya Amerika. Kubadilika huku kumetokea kwa ajili ya tabia na desturi za nchi, kama vile kuvaa au kutovaa nguo.

Katika hiadithi hizi mna wafalme wengi na malkia wengi, kwa sababu hapo zamani kulikuwa na wafalme wengi katika nchi, na yule mtu ambaye sasa ana heshima kwa watu, hapo zamani za kale alikuwa namna ya mfalme. Hadithi hizi za kale haziwezi kusahauliwa kabisa kwa maana ziliandikwa kwa miaka mbali mbali, lakini nyingi ni za karne hii ya sassa ambazo ziliandikwa kwa lugha za kila namna.

Hadithi hizi za "Alfu-lela-ulela," ambazo zingine, ingawa si zote, zimo katika kitabu hiki, ni hadithi za Mashariki. Wahindi na Waarabu na Waajemi, huzitoa kwa namna zao wenyewe, Lakini si kwa watoto, ila kwa watu wazima. Ni kweli kuwa hapo zamani kulikuwa hakuna vitabu vya hadithi, wala vitabu vilivyopigwa chapa, lakini kulikuwa na watu maalum ambao kazi zao zilikuwa ni kuwafurahisha wanawake na wanaume kwa kuwatolea hadithi, nao walikuwa wakiwatolea hadithi kwa kuwasifia vema Waislamu wanaokaa Baghdadi au Bara ya Hindi. Na mara kwa mara hudhaniwa kuwa mambo hayo yote yalitokea zamani za enzi ya Khalifa Mkuu, au Mtawala wa Uaminifu, Harun Rashid, aliyekaa Baghdadi tangu mwaka 786 hata 808, na huyo waziri wake aliyekuwa akia- ndamana naye vile vile alikuwa mtu wa kweli, katika ukoo mkubwa wa Mabamiside. Naye aliuawa na Khalifa kwa ukatili sana, wala hapana mtu ajuaye sababu yake. Katika kulikumbuka deni la mapenzi niliokopeshwa ambalo siwczi kulilipa nafurahi kumsheheneza shukurani za kweli Bwana A. A. M. Isherwood, O.B.E., M.A., Deputy Director of Education Bwana F. Johnson, Esq., Chairman of Publication Committee na mabwana wengine wote walio wanachama wa Publication Committee, na mwenyewe Bwana S. Rivers-Smith, C.B.E, M.A., The Hon'ble the Director of Education, kwa jinsi walivyokuwa radhi kunisaidia kwa mapenzi, katika kukisifia kitabu hiki changu hata kikapatikana kupigwa chapa.

Na hivi natumaini kwamba wasomaji wote watakaokipenda

kitabu hiki, wataungana nami katika kulishuhudia deni langu.


E. W. BRENN​

DAR ES SALAAM,

1st January, 1928.
 
SAFARI SABA ZA SINDBAD, BAHARIA




KATIKA enzi ya Khalifa Harun Rashid, paliondokea mchukuzi mmoja masikini aliyekuwa akikaa katika mji wa Baghdadi, jina lake Hindbad. Siku moja jua lilipokuwa kali mno alitumwa kuchukua mzigo toka mwanzo wa mji mpaka mwisho wa mji, basi kabla hajafika nusu ya safari yake, akatokea katika njia moja iliyonyunyizwa marashi na upepo mzuri ulikuwa ukimpiga usoni,

akatua mzigo wake na kukaa kitako kando ya njia karibu na jumba

kubwa, ili kujiburudisha.

Alipokuwa amekaa hapo, akafurahi sana kusikia harufu za udi na ambari zikitokea mle ndani ya ile nyumba, na zaidi ya hayo alisikia ngoma na sauti za ndege zikiimba vizuri. Pia alisikia harufu ya vyakula vizuri na akafahamu kuwa ndani ya nyumba ile mna karamu. Basi kwa vile alivyokuwa hapiti njia ile mara kwa mara wala hana habari za mtu anayekaa katika jumba lile, akafanya hamu kupeleleza ili ajue, basi alipomwona mtumishi aliyekaa mlangoni akamwendea, na kumwuliza jina la bwana wake.

Mtumishi akajibu akistaajabu, 'Oh! Wewe umekaa hapa Baghdadi kwa siku kadha wa kadha, nawe hata leo hujajua kuwa jumba hili ni la Sindbad Baharia, msafiri mkubwa aliyezunguka dunia?

Mchukuzi aliposikia hivi akakumbuka maneno aliyoyasikia zamani kuhusu utajiri wa Sindbad; akiifikiri hali yake na hali ya Sindbad alimwonea kijicho. Akawaza kuwa kiasi cha furaha ya Sindbad ni sawasawa na kiasi cha taabu zake, naye akajinung’unikia sana hata moyo ukamchafuka, ndipo akainua macho yake mbinguni na kunena kwa sauti kuu, 'Ewe Mwenyezi Mungu, muumba wa vitu vyote, angalia tofauti kati ya Maisha yangu mimi na Maisha ya Sindbad! Kila siku naumia kwa taabu na mashaka hata ule mkate wa kula mimi na watoto wangu ni shida kuupata, huku kumbe Sindbad anatumia atakavyo na maisha yake ni furaha tupu! Amefanya nini hata ukampa raha hii, na mimi nimefanyaje hata nikastahili taabu hizi?'

Alipokwisha kusema hivi akainamisha kichwa kama mtu anayekata tamaa kabisa.



Basi mara ile ile nmtumshi akaja kutoka kwenye ile nyumba kumshika mkono akimwambia ‘Nifutuate, kwani bwana wangu, Sindbad, anataka kusema nawe.’

Hindbad akastaajabu sana maana hakujua analoitiwa, hata alipokumbuka yale maneno aliyokuwa akisema akaogopa sana akifikiri kuwa labda Sindband amesikia na sasa anaitwa kusudi kwenda kuadhibiwa. Kwa hivyo akatoa udhuru na kusema,

‘Siwezi kuacha mzigo wangu njiani’

Lakini watumishi wa Sindbad wakamwambia, ‘Sisi tutakutunzia

mzigo wako’, kisha wakazidi kumshurutisha mpaka akakubali. Basi wale watumishi wakamchukua kumpeleka katika chumba kikubwa ambamo aliona watu waliokaa juu ya meza iliyoandaliwa vyakula vizuri vya kila namna, na mwisho wa ile meza kulikuwa na mtu mmoja mwenye sura nzuri amekaa, naye alikuwa na ndevu nyingi nyeupe. Nyuma yake walisimama watumishi wengi tayari kufanya watakaloambiwa. Mtu huyo alikuwa ndiye Sindbad maarufu. Basi yule mchukuzi alipoona watu wengi kama wale akafanya hofu: akawaamkia huku anatetemeka, lakini Sindbad mwenyewe akamkaribisha akaa upande wa mkono wake wa kulia, kisha akamgawia chakula na mvinyo kwa mkono wake mwenyewe.

Walipokwisha kula Sindbad akawa anaongea naye kama watu waliojuana zamani, akamwuliza jina lake na habari zake. Mchukuzi akajibu, ‘Bwana wangu, Jina langu naitwa Hindbad.’

Sindbad akasema, 'Nimefurahi kukuona, nami nawasemea wote waliopo kuwa nao pia wamefurahi kukuona. Na sasa napenda uniambie yale maneno uliyokuwa ukisema kule njiani,’ maana Sindbad mwenyewe alimsikia akisema chini ya dirisha lake ndiyo sababu akamwita na kumkaribisha.

Alipoambiwa hivi, Hindbad akainamisha kichwa kwa haya, akajibu, 'Bwana wangu, wakati nilipokuwa nikisema maneno hayo nilikuwa nimechoka sana, na sasa naomba uniwie radhi.’

Sindbad akamwambia, ‘Usidhani kuwa raha hii na vitu hivi vya anasa nilivyo navyo sasa, nimevipata bure bila kusumbuka kwa taabu na mashaka ya dunia, la! Osifikiri hivyo, imefika hali hii niliyo, baada ya kuteseka miaka mingi kwa taabu za kiwiliwili na moyo pia.’ Kisha akawageukia watu waliokuwapo akawaambia, ‘Rafiki zangu, matajiri wako wengi-lakini kama wangalipata taabu namna nilivyopata mimi, wangalikata tamaa ya kupata utajiri tangu mwanzo, tena wangalikuwa radhi kurudi makwao katika hali ya umasikini. Labda hamjasikia habari za safari zangu saba za ajabu! Na hatari zilizonipata. Basi maadam leo nimepata nafasi ya kukwambieni habari za safari hizo, nitakwambieni.’ Na kwa kuwa Sindbad alitaka yule mchukuzi naye asikilize habari hizo, akamwamuru mtumishi wake aende kumchukulia ule mzigo wake ampelekee huko alikotaka kuupeleka, kusudi yeye akae kusikiliza hadithi.



SAFARI YA KWANZA​



BASI Sindbad akaanza kutoa hadithi yake hivi: -Babaangu alipokufa aliniachia mali mengi mno isiyo idadi; na fungu kubwa la mali hiyo nililitumia katüka starehe za ujana wangu, lakint halafu yake nikaona kuwa napoteza mali na hali pia, tena nikakumbuka kwamba mtu kuwa mzee kisha masikini ni mashaka makubwa mno. Baada ya kuingiwa na fikira hii, nikakusanya mali yangu yote iliyosalia nikaondoka na kwenda kujipakia chomboni pamoja na wafanyaji biashara, nikaenda Basra.

Tukasafiri kuelekea upande wa Mashariki kupita ghuba ya Ajemi. Awali ya safari yetu nilitaabika sana kwa bahari jinsi ilivyonilevya lakini baadaye nikaizoea, wala sikutaabika tena. Katika kusafiri kwetu tukapita visiwa vingi, tukawahi kuuza bidhaa zetu kidogo na zingine tukazibadılisha kwa vitu visivyopatikana katika nchi yetu. Hata siku moja tukafika katika kisiwa kingine kidogo kilichokuwa kimeinuka kidogo tu juu ya bahari. Basi baada ya kutua matanga, nahodha akatoa ruhusa kwa watu watakao kushuka pwani, washuke, na mimi nilikuwa mmoja wao.

Basi wakati tulipokuwa katika furaha zetu za kula na kunywa, na kujisahaulisha taabu za bahari, mara kile kisiwa kikaanza kuti- kisika sana hata wale wenzetu waliokuwa wamebaki chomboni wakakiona kikitikisika, nao wakatwita turudi upesi ili tujipakie tujiponye, kwani kile tulichodhani kuwa ni kisiwa hakikuwa kisiwa, ila ni mgongo Wa nyangumi. Waliokuwa wepesi wakangia mashuani tulioshukia pwani na wengine wakajitosa baharini kuogelea, na mimi kabla sijawahi kujiponya, kwa ghafla nyangumi akajizamisha baharini na kuniacha nikitapatapa majini kukimbilia kipande cha mti tulichokileta kutoka chomboni kwa kufanya kuni.
 
Nahodha alipokwisha kuwapokea wale waliofika kwa mashua na wale waliokuwa wakiogelea, akatweka tanga kusafiri, maana aliona upepo mzuri unavuma akajua kwamba ataepukana upesi na mnyama huyo. Na mimi nikaachwa peke yangu baharini nikumbane na mawimbi, hata usiku ulipoingia nikakata tamaa ya kunusurika. Hata asubuhi kulipokucha, Mwenyezi Mungu akaleta rehema yake; mawimbi yakanichukua na kunitupa kisiwani, nikalala si hai si maiti, mpaka jua lilipotoka. ljapokuwa nilikuwa ni hoi kwa njaa na taabu nilijikokota hivyo hivyo mikaenda juu kisiwani kutafuta cho chote, mara nikaona majani yanayoliwa na kijito cha maji safi, nikala nikanywa, nikaburudika. Nilipozidi kuendelea mbele mara nikatokea kwenye mbuga kubwa, nikaona farasi wanalisha. Basi niliposimama kuwatazama nmara nikasikia sauti za watu wakisema chini ya ardhi, punde mtu mmoja akatokea na kuniuliza jinsi nilivyofika kule kisiwani, nami nikamweleza mambo yote yaliyonipata. Nilipokwisha kumweleza habari zangu akani- chukua mpaka pangoni kulikokuwa na watu wengine ambao walistaajabu kuniona, kama mimi nilivyostaajabu kuwaona wao.

Basi baada ya kula chakula walichonipa, nikawauliza, ‘Mlipataje

kufika hapa mahali pasipo watu?’

Wakasena, ‘Sisi ni wachungaji farasi wa mfalme wa kisiwa hiki, na kila mwaka majira kama haya huwaleta farasi wa mtalme kuja kulisha katika mbuga hii, na hivi kesho asubuhi tunaondoka kurudi kwa bwana wetu.’ Halafu nao wakaniambia, ‘Bahati yako umetukuta! na kama si hivyo ungalikufa kwa njaa maana wenyeji wa kisiwa hiki wako mbali, nawe hungaliweza kufika huko bila kuongozwa.’

Asubuhi mapema wakafunga safari kurudi kwao na mimi wakanichukua kunipeleka kwa mfalme wao ambaye nilimhadithia habari zangu zote, na jinsi nilivyopata kufika katika nchi yake. Basi naye akanihurumia sana, ndipo akawaagiza watu wake wani-tazame sana tena nisipungukiwe na kitu nitakacho. Na kwa kuwa kazi yangu ilikuwa ya biashara nikawa nazungukazunguka kutafuta watanyaji biashara wenzangu, hasa Zaidi nilikuwa nikiwatatuta wageni, kwa tamaa ya kuwaona watu watokao kwetu Baghdadi nipate kuwauliza jinsi nitakavyoweza kurudi huko. Maana mji huu ulijengwa pwani, tena una bandari kubwa na kila siku huja vyombo vingi vitokavyo pande zote za dunia. Siku moja nilipokuwa bandarini nikaona chombo chatia nanga na kuteremsha shehena, na wafanyaji biashara wenye mizigo wakawa wanaanza kuichukua kupeleka majumbani mwao. Nikasogea karibu kutazama nikaona jina langu limeandikwa juu ya baadhi ya mizigo nikawa na yakini kuwa ndiyo ile niliyoipakia katika chombo chetu huko Basra. Na hata yule nahodha pia nilimtambua. Lakini nilikuwa na yakini kwamba yeye alihidhania kuwa nimekufa.

Nikamwendea kumwuliza, ‘Nani mwenye mizigo hii?’

Akanijibu, 'Alikuwako mfanyaji biashara wa Baghdadi ndani ya

chombo changu, jina lake Sindbad.’ Siku moja yeye pamoja na abiria wengine walishuka mahali tulipopadhania ni kisiwa, lakini kumbe si kisiwa ila ni nyangumi mkubwa mno aliyelala juu ya bahari. Basi walipofika hapo wakawasha moto kupika vyakula vyao, na mara yule nyangumi kuona mgongo wake unapata moto, akajizamisha, na watu wengi waliokuwa juu yake waliangamia majini pamoja na huyo masikinı Sindbad. Bidhaa hizi ni zake, nami nimekusudia kuziuza ili niwapatie faida watu wake kamanikijaliwa kuonana nao.’

Nikamwambia nahodha, ‘Mimi ndiye Sindbad uliyemdhania

amekufa, na hii ni mali yangu!’

Nahodha aliposikia maneno haya akaruka akisema: 'Lo! Hii dunia

gani? Ama siku hizi hakuna hata mtu mmoja aliye mwaminifu. Nimemwona Sindbad akizama kwa macho yangu mwenyewe, leo hivi wajitia macho makavu na kuniambia kuwa wewe ndiye Sindbad! Kwanza nilikudhani mtu mustahiki kumbe vile ni jambazı na mwongo!’

Nikamwambia, Kuwa na subira kidogo, unisikilize habari

zangu. Nahodha akajibu, 'Haya sema, nami ni tayari kukusikiliza.’

Basi nikamweleza namna ya kuokoka kwangu na bahati yangu ya kuonana na mtalme wao wale wachungaji farasi, na jinsi nilivyo pokelewa kwa wema. Nikaona yale maneno nimwelezayo yanamwingia akilini hata walipokuja wafanyaji biashara wengine wa mle chomboni ambao walinitambua, wakafuralhiwa mno kuniona ni hai. Ndipo sasa nahodha aliposema kuwa naye pia anitambua Akanikumbatia na kunena, ‘Mungu kakuokoa na hatari kuu. Chukua mali yako uiuze kama upendavyo.’ Nikamshukuru sana sana na kumsifu kwa uaminifu wake, nikamsihi akubali kupokea zawadi ya mitumba ya bidhaa za namna mbali mbali, kuwa ndiyo dalili ya shukrani zangu, lakini akakataa kabisa asichukue hata kitu kimoja. Nikachagua Vitu vilivyo thamani nikampa mfalme zawadi. Naye akafurahi sana, kisha na yeye akanipa zawadi nyingi za thamani zaidi kuliko zile nilizompa mimi; ndipo nikamwomba ruhusa ya kurudi kwetu. Basi nikanunua vipande vya sandali, udi, karafuu maiti, kungumanga, karafuu, pilipili na tangawizi, nikapakia chomboni, huku nakwenda nikiuza, hata nilipofika Basra nilikuwa nimepata reale kadiri ya elfu moja.

Mke wangu na watoto walinipokea kwa furaha kuu kama ile niliyokuwa nayo mimi kwa kuwaona tena, basi nikanunua shamba tena nikajenga na nyumba kubwa, nikakaa kitako kwa raha na kutumia mali yangu.



Sindbad alipomaliza kusema maneno haya akanyamaza. Akaamrisha wapigaji vinanda wapige, na waimbaji waimbe. Hata ilipopata jioni Sindbad akatwaa mfuko wa reale mia za dhahabu akampa Hindbad, na kumwambia, 'Chukua mfuko huu kwako, lakini kesho njoo tena usikilize zaidi habari zangu zingine.’

Mchukuzi akatoka kwa turaha (basi kisia mwenyewe jinsi alivyopokelewa vema nyumbani kwake). Na alipowaeleza Watoto wake kisa cha Sindbad wakafurahi sana, na zaidi ya hayo wakamshukuru Mwenyezi Mungu aliyemjalia Sindbad kuwa na moyo wa ukarimu. Siku ya pili yake Hindbad akavalia nguo zake nzuri, akaenda nyumbani kwa mfadhili wake, naye akakaribishwa kwa wema.



Hata wageni wengine wote walipokuja chakula kikaandaliwa kama siku ya kwanza wakala na kufurahi. Walipokwisha kula Sindbad akawaambia, 'Rafiki zangu, natumai kwanmba mtasikiliza vizuri habari za safari yangu ya pili, ambazo nina yakini kuwa mtaziona za kustaajabisha zaidi kuliko za safari ya kwanza.
 
SAFARI YA PILI



BAADA ya safari yangu ya kwanza kama mjuavyo, nilikusudia kukaa Baghdadi nitumie siku zangu zilizobaki raha mustarehe,

lakini mara nikaanza kuchoka kukaa bure, nikatamani kusafiri tena kwa bahari. Basi nikanunua bidhaa zinazofaa katika nchi nilizokusudia kwenda, safari hii nikajipakia katika chombo kizuri pamoja na wafanyaji biashara wengine niliowajua kuwa ni maaruufu. Tukasafiri kutoka kisiwa hata kisiwa tukifanya biashara na kila mara tukipata faida sana, hata siku moja tukashukia mahali ambapo hapakuwa na nyumba wala watu, ijapokuwa palijaa miti ya matunda ya kila namna na kulikuweko chemchemu ya maji mazuri.

Wakati wenzangu walipokuwa wakizunguka kuchuma maua na matunda, mimi nilikaa kivulini chini ya mti kula chakula, na kunywa kwa furaha mvinyo niliokuwa nao. Basi kwa kule kuchoka kwa safari na kwa mvinyo niliokunywa, mara usingizi ulinishika nikalala, nikawa ninabembelezwa na sauti ya kijito cha maji safi yanayopita karibu yangu. Kiasi nilicholala sikijui, lakini nilipoamka na kusimama nikafanya hofu kwa kujiona ni peke yangu, na kile chombo chetu kimekwisha kwenda. Nikakimbia huku na huko kama mwenye wazimu nikitafuta wenzangu, huku nalia kilio cha kukata tamaa kabisa. Hata nilipokwenda pwani nikaona chombo kwa mbali upeo wa macho kinakwenda kasi, sasa nikasema kwa uchungu, 'Laiti kama ningelikuwa radhi kukaa mjini salama haya yote yasingalinipata.’ Lakini kuona masikitiko yangu hayafai kitu, nikaanza kujipa moyo na kutazama huku na huku kutafuta njia ya kukimbilia, hata nilipopanda juu ya mti mrefu, kwanza nikaangalia baharini lakini sikuona kitu cha kukitumai, nikageuka kuangalia upande wa bara, na huko nilitaharuki kuona kitu cheupe cha ajabu kwa mbali, wala sikuweza kukitambua ni kitu gani.

Nikashuka chini ya mti kwa haraka na kukusanya vyakula vyangu vilivyosalia, nikakimbilia upesi upesi kule kwenye kilekitu nilichokiona. Nilipofika karibu yake nikaona ni donge jeupe kubwa mno lililo refu, na nlipoligusa, nikaliona laini tena lateleza sana. Kisha lilikuwa halipandiki-kwani halikuwa na chakupandia- nikalizunguka-zunguka kutafuta palipo wazi lakini sikuona. Lakini pamoja na hayo nililıpima. Duara yake ilikuwa haipungui hatua hamsini.

Wakati huo jua lilikuwa karibu kutua, na punde kwa ghafla kukawa giza, nikaona kitu Kama wingu jeusi kubwa mno likija upesi na kusimama juu yangu, nilipotazama juu nikastaajabu kuona ni dege kubwa mno la ajabu, lililokuwa likishuka kwa karibu yangu. Sasa nikakumbuka kuwa mara nyingi nimesikia mabaharia wakizungumza habari za dege moja la ajabu linaloitwa Rok, labda kile kitu cheupe nilichokiona na kunifadhaisha sana ni yai lake. Nalo lilikuwa ndilo kweli maana lile dege lilishuka chini pole pole likalilalia na kulifunika mbawa zake kusudi lipate uvuguvugu, nami nikawa nimejikunyata kwa hofu kando ya yai karibu na guu lake lililokuwa mbele yangu, ambalo lilikuwa kubwa kama shina la mti. Nikavua kilemba changu nikajifunga na guu lake barabara kwamba kesho asubuhi Rok akiruka ataruka nami na kunitoa katika kisiwa kile cha ukiwa, na hivyo ndivyo ilivyokuwa. Asubuhi kulipokucha dege likaruka likanichukua juu kwa juu hata mwisho sikuweza kuona ardhi, na halafu yake kwa ghafla likashuka chini kwa upesi kama upepo, nikawa sina fahamu kabisa. Basi nilipopata fahamu ya kujua kuwa sasa Rok ametua nami nimefika chini tena, nikajifungua upesi upesi; na mara ile ile haikupata hata dakika, dege likavamia joka kuu. Likamdonoa utosini kwa mdomo wake mkali likamwua, kisha akalishika na kuruka nalo tangu nikiliona hata nisilione tena.
 
Baada ya kitabu cha nne, sasa tuone kitabu cha pili. Fuatana nami hadi kitakapoisha, pia hivi vyote na vingine vingi unaweza kuvisoma bure ndani ya maktaba app.

View attachment 2125601
MAZUNGUMZO YA ALFU LELA ULELA
AU
SIKU ELFU NA MOJA
KIMEFASIRIWA KWA KISWAHILI NA
EDWIN W. BRENN
KITABU CHA PILI

YALIYOMO

UTANGULIZI
SAFARI SABA ZA SINBAD BAHARIA
SAFARI YA KWANZA
SAFARI YA PILI
SAFARI YA TATU
SAFARI YA NNE
SAFARI YA TANO
SAFARI YA SITA
SAFARI YA SABA, YA MWISHO

KISA CHA MBILIKIMO MWENYE KINUNDU

KISA CHA NDUGUYE KINYOZI WA TANO(NDOTO YA ALNACHA)

KISA CHA NDUGUYE KINYOZI WA SITA

Hiyo app haipo kwenye IOS eeh jamani natafuta story za bulicheka
 
Bonde nililokuwamo sasa (ambamo ndimo nilimoachwa na Rok), ilikuwa jembamba tena limekwenda chini sana, kisha limezungu-kwa na milima mikubwa mikubwa iliyokwenda juu mawinguni, nayo ilikuwa imechongoka sana kwa magenge wala haipandiki. Basi nikawa nazungukazunguka kwa taabu na mashaka mle bondeni kutafuta njia ya kutokea, ndipo nikaona almasi zimeta-wanyika chini, na zinginezo zina ukubwa wa kustaajabisha. Kuona hivi nikafurahi sana, lakini nilipoona majoka mengi marefu makubwa na yanayotisha mno furaha yangu iliyeyuka. Hata wale wadogo wangaliweza kumeza tembo mzima pasipo shida.
 
Ilikuwa bahati yangu kuwa yale majoka mchana mchana yalikuwa yakijificha mapangoni hayatoki ila usiku; nadhani labda ni kwa sababu ya kumwogopa adui wao Rok. Basi siku ile kutwa nikawa nazungukazunguka huku na huku mle bondeni, na magharibi ikiingia hutafuta kijipango nikaingia na kuziba mlango kwa jiwe, nikala chakula changu kidogo nikalala. Na ingawa nililala hivyo, lakini kwakule kutambaa kwa majoka na milio yao ya kutisha sikuweza kupata usingizi kwa woga. Hata asubuhi jua likichomoza huwa na furaha sana na kushukuru, tena ninaposikia kimya-a hujua kwamba majoka yamerudi mapangoni mwao, nami hutoka kijipangoni mwangu kwa kutetemeka sana na kuanza kutembea tembea tena huku na huku mle bondeni. Na zile almasi zilizokuwa mle njiani nipitamo nilikuwa nikizipiga mateke kwa kuzidharau, maana niliona kuwa hazifai kitu kwa mtu aliye mahali pale. Mwisho nikachoka, nikakaa juu ya jabali, punde kidogo nikastuliwa na mshindo wa kitu kilichoanguka chini kando karibu yangu. Na hicho kilikuwa kipande kikubwa cha nyama, na nilipokuwa nakitazama mara mapandee mengine yakabingirishwa katika magenge yakiangukia chini kwa mahali mbali mbali. Na kila siku nilikuwa nikifikiri hadithi za bonde la almasi lililojulikana sana na kuzungumzwa habari zake na mabaharia, na jinsi wafanyaji biashara walivyobuni njia ya werevu ya kupatia almasi hizo. Hapo kwanza nilidhani kuwa ni hadithi tu walizozitunga wasafiri kwa kusudi ya kuwafurahisha wasikizaji, ila sasa naona kuwa ni kweli. Wasafiri hao walikuwa wakifika katika bonde hilo wakati tai waliojenga

Viota vyao magengeni wameangua watoto; nao hutupa manofu makubwa ya nyama mle bondeni. Manofu hayo huanguka kwa nguvu juu ya almasi nayo humkini kuambatana na mawe ya almasi, basi wale tai wanapoyavamia kuwapelekea makinda yao, ndipo wafanyaji biashara wanapowafukuza kwa makelele mpaka wayaangushe kusudi wapate kuchukua almasi. Na kila nikitazama mle

bondeni nilijiona kama niliye kaburini, maana sikuwa na njia ya kutokea nje mzima, lakini nikajipa moyo na kuanza kutafuta njia ya kuokoka. Kwanza nikaanza kuokota mapande makubwa makubwa ya almasi nikiyawcka vizuri ndan1 ya mkoba wangu wa ngozi limokuwa na chakula changu, nikaufunga barabara na ukanda wangu. Halatu nikachagua pande la nyama nililoliona kuwa litafaa kwa makusudio yangu, nikalifunga barabara mgongoni kwa kilemba changu; hata nilipokwisha kufanya hivyo nikalala

kifudifudi kungonjea tai waje. Mara nikasikia kwa juu yangu

mvumo wa mbawa zao zenyc nguvu, na mmoja wao aliliona na kulitamani lile pande la nyama nililojifunga nalo, akalinyakua na mimi pamoja, akaruka pole pole mpaka kwenye kiota chake akanibwaga.

Kwa bahati nzuri kumbe wale wafanyaji biashara walikuwa wakiangalia, mara wakaanza kupiga kelele zao za desturi wakikimbilia kule kiotani kwenda kumfukuza yule tai. Ama kwa kweli mastaajabu yao yalikuwa makubwa mno waliponiona mimi; na sasa walivunjika nguvu, kisha wote kwa umoja wakaanza kunitukana wakisema ati nimewaibia chumo lao la siku zote. Nikamwambia yule mmoja wao aliyekuwa zaidi akinitia uchungu, ‘Laiti kama ungalijua masaibu yaliyonipata, nina yakini kuwa ungalinihurumia, na ikiwa ni almasi, mimi ninazo nyingi zilizo nzuri sana zinazokufaa wewe na wote waliopo, na mimi mwenyewe pia.’ Kusema hivi nikazitoa kuwaonyesha. Wale wengine wotebwakakusanyika 1na kunizunguka na kustaajabu mambo yalivonipata na huku wakinisifu kwa ile akili niiiyoifanya hata nikatoka katika lile bonde. Basi waliponichukua kunipeleka kambini kwao ili wazidi kutazama almasi zangu, wakanihakikishia kuwa katika miaka yao yote waliyofanya kazi hawakupata kuona mawe ya almasi yaliyo makubwa na mazuri kama yale.

Basi ikawa kila mfanyaji biashara kwenda kubahatisha kuangalia

katika viota vya ndege, kwa tamaa ya kuona kitu ndani yake, Ndipo nilipomwambia yule aliyepanda kile kiota nilichokuwamo mimi achukue almasi zangu kwa kadiri awezavyo, lakini kwa radhi yake mwenyewe akachukua jiwe moja tu ambalo hilo ndilo lililo kuwa kubwa kabisa. Halafu akaniambia kuwa amebahatika kupata kitu cha thamani kama kile, wala hana haja tena ya kufanya kazi ya taabu. Basi nikakaa nao kwa siku kadha wa kadha; na walipokuwa wakisafiri kurudi kwao nikataka kuandamana nao. Njia yetu tuliyopitia ilikuwa yenye milima mikubwa mirefu iliyojaa majoka yanayotisha, lakini kwa bahati tulisalimika na mwisho wake tukafika pwáni salama. Kutoka huko tukasafiri kwa chombo mpaka kisiwa cha Roha, kunakoota miti mikubwa ya mikarafuu maiti, hata watu mia huweza kujificha chini ya mti mmoja kwa nafasi bila shida. Na kama ukiugonga utomvu wake hufurika na kwenda juu ya mti kulikotundikwa chombo kusudi utone humo, na mara hukauka ukafanyika kitu kinachoitwa karafuu maiti.

Katika kisiwa hicho tuliona faru, nyama ambaye ni mdogo wa tembo lakini ni mkubwa zaidi ya mbogo (nyati). Ana pembe moja ngumu inayopata urefu wa dhiraa moja, na mwili wake una mikunjo mikunjo toka kichwani hata mkiani, na juu yake ilionekana mistari mieupe ya umbo la mtu. Faru huyo hupigana na tembo naye humchoma kwa pembe yake na kumchukua kichwani mwake, lakini kisha naye hupofuka kwa damu ya adui yake, basi huanguka

chini akawa hana nguvu, halafu huja Rok, huwakamata wote wawili kwa kucha zake, na kuruka nao kuwapelekea makinda yake. Bila shaka naona haya yanawastaajabsha mno, lakini kama hamsadiki maneno yangu nenden Roha mkaone wenyewe. Na kwa hivi sipendi kukuchokesheni, sitakuungumzieni mambo mengi mengine ya ajabu niliyoyaona katika kisiwa hicho. Basi kabla hatujaondoka nikatwaa alnmasi yangu moja nikaibadilisha kwa bidhaa zilizo bora ambazo zilinipatia faida kubwa humo njianl, wakati tukisafiri kurudi kwetu. Mwisho tukawasili Basra nilipofika kitendo changu cha kwanza nilichotenda nilitoa fungu kubwa la mali yangu kuwapa masikini. Baada ya hivyo nikakaa raha mustarehe nikifurahia utajiri nilioupata kwa taabu na mashaka.



Basi hivi ndivyo Sindbad alivyohadithia mambo ya safari yake ya pili, na halafu yake akampa tena Hindbad mfuko wa reale mia za dhahabu, kisha akamwalika aende tena siku ya pili, akasikilize jinsi alivyosafiri safari yake ya tatu. Na wale wageni wengine pia wakaondoka kwenda majumbani mwao, lakini siku ya pili kwa wakati ule ule wote wakarudi, pamoja na yule mchukuzi. Na baada ya kwisha kuliwa karamu iliyoandaliwa, Sindbad akawataka radhi wageni wake, ndipo akaanza kutoa habari za satari yake ya tatu.
 
SAFARI YA TATU



BAADA ya kitambo kidogo ile raha na starehe niliyoipata, ikanisahaulisha taabu na hatari zote zilizonikuta katika safari zangu mbili. Tena, kwa kujiona bado ningali na nguvu nikaanza kuchoka kukaa bure bila kazi, basi nikanunua bidhaa nzuri nzuri za Baghdadi, nikasafiri kuzipeleka Basra. Nilisafiri pamoja na wafanyaji biashara wengine. Tukapita nchi nyingi tukifanya biashara zetu. Siku moja tulipokuwa baharini tulikumbana na dhoruba kali ambayo ilitutoa katika njia yetu, na ikatupeleka katika bandari ya kisiwa kigeni ambacho hatukupenda kutia nanga.

Nahodha wetu akasema, 'Afadhali ningetia nanga mahali popote

pengine kuliko hapa, kwani kisiwa hiki na vingine vyote vilivyo kizunguka vina vijitu vikali mno namna yao kama vibushuti, navyo kwa yakini vitatushambulia.’ Basi kama vitakavyofanya tusijaribu kupigana navyo, maana ni vingi kama nzige, na kama tukikiua kimoja na tufahamu kuwa sisi sote tutaangamia. Basi tulipotazama maneno aliyosema nahodha tukaona kuwa ni kweli, na muda si muda mara vikatokea kundi kubwa mno, urefu wao wapata mikono miwili, vimejifunika ngozi zenye manyoya laini mekundu, vikawa vinatujia kwa kuogelea na kukizunguka chombo chetu. Vilipotukaribia vikasema nasi lakini lugha yao hatuku.

Baada ya kutafutatafuta kwake kwa bure, likapapasapapasa mpaka likafika mlangoni, likatoka nje na kugumia kwa kitisho sana kama mbwa. Basi tulipoona kuwa limekwisha kwenda zake tukafanya haraka kulitoka lile jumba la mauti, tukaenda pwani tukakaa kando karibu na vyelezo vyetu, kuangalia itatokea nini. Nia zetu zilikuwa hivi: kama jua likitoka, nasi hatuoni lo lote wala hatusikii tena mgumio wake, ambao hata sasa ulikuwa ukisikilizana kwa mbali, tutajua limekufa, na hivyo tutaweza kukaa kisiwani salama wala hatutakuwa na haja ya kupoteza maisha yctu baharini kwa vyelezo vile hafifu. Lakini lo-o! Masalale! kule kupambazuka tu, tukaona kundi la maadui linatujia: na lile jitu limeshikwa mkono na wenziwe wawili wa kimo kimoja, na kundi jingine likifuata nyuma yao. Kuona hivi hatukusita tena, tukapanda juu ya vyelezo vyetu na kuvuta makasia kwa nguvu zetu zote kujipeleka baharini. Mijitu ilipoona nyama zao zikikimbia ikachukua mapande ya mawe na kuingia majini kutuvurumishia. Na kwa jinsi ilivyokuwa na shabaha vyelezo vyote vya wenzangu isipokuwa kile kimoja nilichoingia mimi, vilipinduliwa na jamii ya mabaharia wao wakazama, wala nasi hatukuweza kufanya lo lote la kuwasaidia. Basi mimi na wenzangu wawili tukafanya bidii ili ile mijitu isitupate, na tukavuta makasia kwa nguvu mpaka tukafika bahari kuu. Hapo tukapata msukosuko wa bahari kutwa kucha kwa upepo mkali na mawimbi, lakini asubuhi yake tukaangukia kisiwani, tukashuka pwani kwa furaha na kutafuta matunda mazuri tukala, kisha halafu tukajinyosha kupumzika.



Mara kwa ghafla tukagutushwa na sauti kubwa ya kitu kinachotambaa juu kisiwani, kutazama tukaona ni joka kubwa mno la ajabu, linalotiririka mchangani kutujia. Likaruka kama mshale likamkamata mwenzetu mmoja kabla hajawahi kukimbia, na hata ijapokuwa alipigana nalo lakini mara lilimbana na kumpiga mapindi likammeza. Wakati huo mimi na yule mwenzangu wa pili tukakimbia juu ya mti mrefu. Hata usiku ulipoingia tukalala, lakini punde si punde nikaamshwa tena kwa mlio wa joka lile lile litishalo likizungukazunguka chini ya mti ule ule, mwisho likapanda juu na kumshika mwenzangu aliyckuwa amelala chini yangu likamla. Ndipo likashuka na shibe likaenda zake, likaniacha mimi si hai si maiti kwa kihoro.

Asubuhi jua lilipotoka nikashuka chini hali sina tamaa sana ya kupona na mauti yale yanayotisha yaliyowapata wale wenzangu wawili: lakini roho ni tamu, basi nikafanya vyote niwezavyo nijiokoe nafsi yangu. Siku ile kutwa nikawa nakusanya haraka haraka mabiwi mengi ya miba nikayazungusha chini ya ule mti, nikayapanga moja juu ya moja hata ikawa kama kibanda madhubuti, ambamo humo nilijikunyata kama panya amwonapo paka akija. Basi kisia mwenyewe jinsi nilivyoupitisha usiku ule wa kutisha, kwani lile joka lilirudi tena kuja kunimaliza, likipita mbio na

kuzungukazunguka pale pale nilipojificha likitafuta mlango wa kuingilia, na kila likizungukazunguka hivyo roho sina naona litafaulu tu, lisukume mabiwi ya miba upande mmoja lipenye, lakini halikuweza. Hata kulipokucha likarudi pangoni mwake kwa njaa na kutahayari, na mimi nilikuwa ni maji, natetemeka kwa hofu na pumzi zimenisonga rohoni kwa ajili ya zile pumzi

zake za sumu. Basi nikatoka kibandani mwangu nikajikokota mpaka pwani, nikaona afadhali nisimame juu ya jabali nijitupe baharini nife kabisa kuliko kulala tena usiku mwingine unaotisha. Basi wakati nilipokuwa katika msiba wangu huo, mara nikaingiwa na furaha kwa kuona chombo kikipita karibu, nikakipigia ukulele kama nilivyoweza huku nikikipungia kwa kilemba changu. Ishara hii iliwafahamisha jamii ya mabaharia waliokuwamo na mashua ikateremshwa upesi kuja kuniokoa. Nilipofika chomboni nikazungukwa na kundi la mabaharia na wafanyi biashara waliokuwa na hamu kutaka kujua yaliyonipata hata nikafika katika kisiwa kile, chenye majoka makubwa yanayokula watu. Bası baada ya kuwaeleza habari zangu wakanikaribisha vizuri kwa chakula chema cha jahazini, na yule nahodha kuona sina nguo, akafanya jamala kuvua koti lake na kunipa.

Na baada ya kusafirisafiri kwa siku kadha wa kadlha tukipitia bandari yingi mwisho tukafika kisiwa cha Salahat, kinachoota miti ya sandali. Hapa tukatia nanga, nikaondoka nikasımama kuwaangalia wafanyi biashara wakiteremsha mali zao kuuza na kuzibadili kwa bidhaa zingine, ndipo nahodha aliponijia na kusema, ‘Ndugu yangu, mimi nina bidhaa za abiria mmoja aliyekufa. Je, utanitany1a hisani ya kuziuza? Na hapo nitakapojaliwa kuonana na warithi wake nitaweza kuwapa fedha zao hata kama itapatikana ie mali tu; na wewe utapata sehemu kwa kazi yako.’

Nikakubali kwa furaha kwani sikupenda kusimama kivivu. Basi akanionyesha mitumba ya mali, kisha akatuma kuitwa mtu ambaye kazi yake ilikuwa ya kuandika orodha ya mali iiyomo jahazini. Huyo mtu alipokuja akauliza, ‘Bidhaa za jina gani niandike kitabuni kuwa zinmeteremka?’



Nahodha akajibu, 'Hizo zilizoandikwa jina la Sindbad, baharia Kusikia hivi nikastaajabu sana na wakati nilipomtazama vizuri nikamtambua kuwa ndiye yule nahodha wa chombo nilicho safiria safari yangu ya pili, ingawa alikuwa amebadili sura sana tokea siku hizo tulizoonana mwanzo. Na kwa yeye kunidhania nimekufa si ajabu, maana hakunitambua.



Basi nikasema, 'Nahodha, huyo mfanyi biashara mwenye

mitumba ile alikuwa akiitwa Sindbad?’ Akajibu, Ndiyo, alikuwa akitwa hivyo. Ni mtu wa Baghdadi, naye alipanda chomboni mwangu toka Basra, lakini kwa bahati mbaya tulimwacha katika jangwa la kisiwa alichoshuka ili kujaza maji ndani ya mapipa yetu, nayo hayakujaa upesi maana tulimngoja mda wa saa nne hakutokea, kwa hivyo alichelewa. Na hasa zaidi

wakati huo kulikuwa na upepo mwingi nasi hatukuweza kumrudia.

Nikamwuliza, 'Basi wewe wamdhania amekufa?

Akajibu, 'Naam.

Nikasema, Nahodha, hebu nitazame vizuri! Kwani mimi ndiyeyule Sindbad aliyekuwa amelala kisiwani, na alipoamka akajiona ameachwa.

Nahodha akanikodolea macho kwa kustaajabu, na baadaye akaona nimesema kweli, naye akafurahi sana. Akaniambia, ‘Sasa chukua mali yako na faida yote niliyokupatia, nami nakuombea heri na baraka.’

Basi nikachukua mali yangu kwa shukrani kuu, na ilivyokuwa tukisafiri kutoka kisiwa hata kisiwa, nikawa nanunuanunua karafuu na midalasini na vitu vinginevyo nikiweka. Mahali pamoja nikaona kasa, urefu wake dhiraa ishirini, tena nikaona samaki kama ng’ombe ngozi yake ilikuwa nene hata watu walikuwa wakiitumia kwa kufanya ngao. Pengine niliona mnyama aliyefanana na ngamia kwa umbo na kwa rangi pia. Basi ikawa tunarudi kidogo kidogo mpaka Basra, ndio nami nikarudi Baghdadi na fedha nyingi zisizo idadi, mbali hazina isiyo kikomo. Nikatoa fedha nyingi kwa

masikini, tena nikanunua na shamba kubwa kuongezea lile nililokuwa nalo, na hivi safari yangu ya tatu ikaisha.



Basi Sindbad alipomaliza habari zake, akampa Hindbad mfuko wa reale mia za dhahabu, halafu akaondoka, akaaga pamoja na wageni wengine kila mtu akarudi kwake; lakini siku ya pili yake wote wakakusanyika tena. Hata karamu ilipokwisha uliwa mwenyeji wao akaendelea kuhadithia mambo yaliyompata.
 
SAFARI YA NNE​



BASI ile mali na raha niliyoipata baada ya safari yangu ya tatu, haikuweza kabisa kuniweka nyumbani. Moyo wangu ukapenda sana kufanya biashara na kupambana na masaibu kama yale niliyozoea kupambana nayo, basi nikaanza kutengeneza safari yangu ya kupitia katika nchi za Ajemi. Kwanza nikatanguliza bidhaa zangu kila mahali nilipokusudia kwenda ili ziende zikaningojee huko mpaka nifike mwenyewe, na kwa zile nchi zilizokuwa mbali nilikuwa nikijipakia chonmboni. Basi kwa muda wa siku kadha wa kadha mambo yote yakawa yanaendelea vema, lakini mwishowe bahari siku moja ikachafuka vibaya sana hata chombo chetu kikazama, na watu wengi wakafa maji, ila mimi na wenzangu wachache tu tukapata bahati ya kushika vapande vya mbao vilivyokuwa vikielea: na hivyo tukawa tunapigwa na mawimbi kupelekwa ufukoni, na upepo ukituvutia karibu na kisiwa. Basi tukajikokota mpaka juu kusikofika mawimbi, tukajilaza chini tu hoi, ikawa tunangojea kuche.

Kulipokucha tukawa tunazungukazunguka kisiwani mara tukaona nyumba kwa mbali. Hata tulipoikaribia, wakatokea watu wengi wakatukamata na kutupeleka majumbani mwao, ikawa tunagawanywa kwa mabwana zetu. Mimi na wenzangu watano tukachukuliwa katika nyumba moja na kuambiwa tukae kitako, kisha tukaletewa majani na kufanyiwa ishara tuyale. Lakini kuona wenyewe hawayali na mimi nikaogopa kuyala, ila wale wenzangu kwa njaa waliyokuwa nayo wakayala yote na mara ile ile wote wakawa na wazimu, wala yale maneno niliyokuwa nikisema nao hawakuyasikia. Sasa ikawa wale wenyeji wetu kutuletea sinia ya wali uliopikwa kwa mafuta ya naz1, na kwa kuwa wale wenzangu walipotewa na akili wakaula wote lakini mimi niliuonja kidogo tu, na hapo nikafahamu waziwazi kuwa hawa bwana zetu wanataka watunenepeshe upesi kwa vyakula vyao kisha watule, na hivyo ndivyo ilivyokuwa hasa. Masikini wenzangu walipotewa na akil wakawa hawana wasiwasi wala woga, wakala kwa ulafi kile chakula walichopewa na baada ya siku chache wakanenepa, ikawa ndiyo mauti yao. Ama mimi niliyekula kidogo kila siku nikawa nakonda kwa hofu ya hayo yaliyo mbele yangu. Bası walipoona kuwa sipatikani kwa hila zao wakanipa ruhusa ya kutembeatembeamwenyewe. Hata siku moja watu hao wote walipokua wamekwenda safari, wakamwacha mzee mmoja kunilinda, na siku hiyo ndiyo niliyopata fursa ya kukimbia na kuingia mwituni, na yule mzee akanifukuzia sana huku akinipigia kelele nirudi, lakini wapi! Hakuniona tena.



Muda wa siku saba nikawa nakimbia tu wala sipumziki, na kama nikipumzika huwa kumeingia giza, chakula changu kilikuwa nazi na maji yangu ya kunywa ni maji ya nazi. Hata siku ya nane nikafika pwani nikaona kundi la wazungu wakichuma pilipili zilizoota kwa wingi. Wakaniamkia kwa maneno ya kikwetu na kuniuliza mimi ni nani na wapi nilikotoka. Ama siku hiyo furaha yangu ilikuwa kubwa kwa kuwasikia wakisema lugha ya kikwetu. Basi nikawaeleza habari za kuzama chombo chetu hata tukakamatwa na wale watu waliotukamata. Wakasema, ‘Lakini watu hao wanakula watu! Ehe, wewe umeokokaje?’ Nikawaambia kama hivi nilivyowaambia ninyi, nao wakastaajabu sana. Basi nikakaa nao mpaka walipokwisha kuchuma pilipili kwa kiasi walichotaka, ndipo wakatunga safari ya kurudi kwao, wakanichukua na mimi

kunipeleka kwa mfalme wao ambaye alinipokea na kunikaribisha

kwa wema. Halatu nikamzungumzia na mfalme wao mambo yaliyonipata ambayo yalimstaajabisha sana, na nilipokwisha kumzungumzia habari zote akaamrisha nipewe chakula na nguo.

Kisiwa hicho nilichokuwako sasa kilikuwa kimejaa watu na kila

namna ya vitu, na biashara nyingi zilifanyika ndani ya mji, na mimi

nikaanza kupapenda na kuona kama kwetu. Na zaidi ya hayo yule mfalme alinıpenda sana, na kila mtu wa mji au wa kikao cha baraza ya mfalme alifanya urafiki nami. Jambo moja nililoliona geni katika mji huo ni hili: kuwa toka wakubwa hata wadogo, wote hupanda farasi bila matandiko wala hatamu. Hata siku moja nikamwuliza mtalme sababu gani ya kutotumia matandiko wala hatamu juu ya farasi wake, akanijibu, ‘Leo umeniambia mambo ambayo sikupata kuyasikia.’ Kwa hiyo nikawa na nia ya kumfanyia

tandiko na hatamu, nikampata fundi hodari aliyenikatia Ngozi va kufanyia tandiko kama vile nilivyomwonyesha mwenyewe nikafanya moja lililo zuri sana na kulipamba kwa nyuzi za zari na hariri. Kisha nikampata na fundi wa chuma akanifulia jozi mbili za vipi vya kumtekenyea farasi, nikampelekea mfalme na kumwonyesha namna ya kutumia kwake. Basi halafu nikamtandikia farasi wake akampanda na kutembeatembea huku na huku hali

amefurahiwa mno na vitu vile vipya, na akanipa shukrani zake na zawadi nyingi.

Baada ya hivi nikafanya matandiko mengi mengine nikawapa masheikh na maliwali, nao wote wakanapenda wakanipa zawadi za mali, na mara nkawa tajiri na mtu maarufu katika mji. Hata siku moja sultani akaniita na kuniambia, 'Sindbad, ama mimi na raia zangu wote tunakupenda, basi ukae na kuishi pamoja nas1, na kwa sababu hii nitakutafuutia mwanamke mzuri mwenye mali nikuoze, ukae ustarehe, wala usifikiri tena kurudi kwenu.’ Basi maadam jambo analopenda mfalme ni halali, nikamkubali bibi mzuri niliyeletewa, nami nikaishi kwa furaha pamoja naye. Walakini nilikusudia kukimbia kama nikipata nafasi ili nirudi kwetu Baghdadi, maana mtu kwao ni kwao, ijapokuwa ni katika pango. Basi kwa muda wa siku kadha wa kadha mambo yakawa yanaendelea vema, hata siku moja mke wa jirani yangu akaugua, akafa. Nikaenda nyumbani kwao nikamwona jirani rafiki yangu yu

katika msiba mkuu, nikamfariji.

Nikamwambia, ‘Mwenyezi Mungu akuweke, tena akupe na umri mrefu!’

Akajibu, ‘A, ndugu yangu! Ni faida gani kusema maneno hayo hali nimebakiza saa moja tu ya kuishi duniani?’ Nikamwambia, 'La hivyo sivyo! Mungu aepushe mbali!’ Mungu ajaalie uwe hai, tukae sote miaka mingi.’

Naye akajibu, ‘Mungu ajaalie umri wako uwe mrefu zaidi, lakini kwa wangu mimi, umekwisha! Nimetengeneza nyumba yangu na kila kitu nimekiweka vema, kwani hivi leo nitazikwa pamoja na mke wangu. Hii ndiyo sheria ya kisiwa chetu iliyowekwa tangu kale mume azikwe pamoja na mkewe aliyekufa, na mke azikwe pamoja na mumewe aliyekufa. Hivi ndivyo walivyofanya

babu zetu, nasi hatuna budi kufanya Vivyo. Sheria hii haibadiliki,

na sisi sote imetupasa kuishika.’

Alipokuwa akinena hivi, ikawa ndugu na rafiki zake huyu aliyefiwa wameshughulika kutengeneza mazishi. Yule maiti akavikwa nguo zake za thamani na kupambwa vyombo vya dhahabu na johari. Kisha halafu wakamtia jenezani, wakamchukua kwa mwendo wa taratibu wakienda kwenye mlima mkubwa mrefu ulio kuwa mbali na mji. Na yule mume aliyefiwa alijifunika ushungi wa hguo nyeusi toka kichwani hata miguani, akifuata kwa msiba mkuu.

Walipofika mahali pa kuzikia wakaondoa jiwe kubwa lililozibiwa mlango wa shimo hilo kuu, na yule maiti akateremeshwa ndani yake. Baada ya hivi mume naye akawaaga rafiki zake kisha akajinyosha mwenyewe ndani ya jeneza lingine ambamo mliwekwa mikate saba na gudulia la maji, akateremshwa chini!! chini !!! mpaka mwisho wa shimo lile linalotisha, halafu jiwe likazibwa, na jamii ya watu wenye msiba wakarudi mjini.
 
Mambo hayo yalinihuzunsiha sana; amaa kwa wengine wote ilikuwa si neno maana wameyazoea tangu utoto wao, lakini kwa mimi yalinisikitisha mno hata sikuweza kujizuia kumwambia mfalme jinsi mambo yale yalivyoniathiri. Nikasema, ‘Seyid yangu ama desturi hii mpya inayofanyika katika nchi yako inanistaajabisha mno: ya mtu kuzikwa mzima pamoja na wafu. Katika safari zangu zote sikupata kuona sheria ya ukatili na ya kutisha Zaidi kuliko hii.’

Mfalme akajibu, 'Utafanyaje, Sindbad, na sheria hii ni ya kila

mtu? Mimi mwenyewe nitazikwa mzima pamoja na mke wangu ikiwa yeye ndiye atakayetangulia kufa.’

Nikasema, Seyid yangu, je, sheria hii inawahusu hata wageni?

Mfalme akacheka na kujibu, 'Naam, kwa kawaida, hapana tofauti kama wakiwa wameoana hapa.’

Niliposikia hivyo nikaenda nyumbani kwangu hali sina nguvu,

na tangu siku hiyo moyo wangu ukawa hauna starehe. Hata kama mke wangu akiumwa na kidole, nilikuwa nikiona kuwa atakufa tu. Basi naam, hazikupita siku nyingi mara mke wangu akawa mgonjwa kweli, na baada ya siku chache akafa. Hofu yangu ikawa kuu, nikaona kuzikwa mzima ni kifo kibaya mno kuliko kile cha kuliwa na watu wanaokula watu, lakini nifanyeje, sikuwa na njia ya kuokoka. Marehemu mke wangu akavikwa nguo zake za mali na kupambwa vyombo vyake vyote vya johari na almasi alivyovaa siku ile ya harusi yake; kisha akatiwa jenezani kwenda kuzikwa na mimi nikifuata kwa msiba. Na nyuma yangu kulikuwa kunakuja watu wanaokwenda mwendo wa taratibu pamoja na mfalme mwenyewe na watu wake wote walio watukufu na hivyo tukafika katika mlima huo wa kaburi.

Sasa pale mlimani nikajaribu kujitia wazimu ili angalau nistue

huruma ya mfalme na wale waliosimama karibu naye, nikitumaini katika kufanya hivyo huenda nikaokoka katika dakika ile ya mwisho, lakini haikufaa kitu. Wala hamna aliyesema nami ila walionekana kushughulika haraka haraka kufanya kazi yao ya kutisha. Na muda si muda nikajiona nateremka ndani ya shimo ya giza, pamoja na mikate yangu saba na guduria la maji.

Basi kabla sijafika chini kabisa, lile jiwe likabingirishwa kuziba mlango, nami nikaachwa mumo humo. Sasa nilipofika chini nikaona nuru ndogo ukutani ikilikamulika mle shimoni, na nilipofanya bidi kuangalia nikajiona kumbe nimo ndani ya shimo kubwa mlimotawanyika mifupa na maiti. Na ijapokua niliona na kusikia mikoromo ya kukataa roho ya wale wenzangu kama mimi waliozikwa wizima ndani ya shimo hilo la giza, nikaona ni kazi bure kupiga kelele za uoga wa kufa. Ila nilijilaumu, nikasema, ‘Kupenda kwangu mali ndio asili ya mambo haya kunifikia.’ Lakini mwisho nikatulia. Nikala mkate wangu na kunywa maji, halafu nikajifunika uso kwa ule ushungi wa ada, nikaondoka na kupapasapapasa njia kuelekea mwisho wa lile shimo, ambako kulikua hakuna uvundo. Huko nikakaa kwa unyonge sana nikawa nikila vyakula vyangu, mpaka vilipo niishia, lakini nilipokuwa karibu kufa kwa njaa, lile jiwe lililozibiwa mlango wa shimo likaondolewa: nikaona jeneza likiteremshwa shimoni, na maiti aliyekuwemo ndani yake alikua mwanamume. Nikakumbuka kuwa huyo mwanamke atakaye mfuata atakua hana utarajialo ili kufa tu, na kama nikimpunguzia shida zake, nitaweza kujisaidia. Basi kile kiasi cha kuteremshwa tu, roho yake ikawa imekwisha mpaka kwa hofu nami nilikua tayari nikimngojea huku nimeshika silaha ya mfupa mkubwa wa mtu, nikampiga dharuba moja nikamwua nikatwaa ile mikate nikala na maji nikanywa nikashukuru nikatumai nitaishi.
 
Basi kwa siku hizo kadhaa wa kadha nilizokuwemo kifungoni ndani ya shimo hilo, nikaona ni afadhali nitende kitendo hicho cha uovu ili nipate kuishi. Hata siku moja nikajiona kama niliyesikia kitu karibu yangu kikivuta pumzi. Nikageuka kuangalia huko kunakotokea pumzi, nikaona kwa giza giza kitu kama kivuli, hata nilipo kikaribia kikakimbia, na kujipenyeza kwa shida ndini ya ufa wa ukuta. Nikakifuatia kwa haraka sana, na punde si punde, nikajiona katika njia ya ufa mwembamba uliotokezea juu ya miamba, nikaifuata kwa kitambo hata mwisho kwa mbele yangu nikaona nuru ya taa ikamulika wazi wazi kisha mara ikisinzia, vivyo hivyo mpaka nikatokea pwani. Ah! Niliona furaha kuu hata siwezi kueleza. Basi nilipokua na yakini kuwa yule ni kweli wala si ndoto, nikasadikisha kuwa kile kivuli nilicho kiona kilikua ni mnyama mdogo aliyetoka baharini kuja kuelekea shimoni, na pale nilipo mshtusha alikimbia kunionyesha njia ya kuokoka ambayo kwa mimi mwenyewe tu, singali igundua. Basi nikasimama kutazama huku na huku nikajiona ni salama, wala hakuna mtu atokaye mjini kunifuatia.

Milima iliyokuwako kule pwani ilikuwa mikubwa tena yote imechongokachongoka sana wala haipandiki. Kuona hivi nikarudi tena kule shimoni nikakusanya vyombo vyote vya mali vilivyokuwa vimevaliwa na wale maiti, dhahabu, na lulu, na johari na almasi, na vinginevyo vyote vilivyokuwa vimetawanyika chini, nikavifunga mitumba. Nikaichukua salama mpaka pwani na huko nikakaa kwa kutumai chombo kipitacho, Na baada ya siku mbili nikafurahi sana kuona chombo kinapita karibu na nilipokuwa

nimekaa. Nikakipigia kelele na kuwapungia mikono jamii ya mabaharia, na mara ile ile ikaletewa mashua. Mabaharia waliponiuliza jinsi nilivyopatikana na masahibu hata nikafika kule, nikawaambia kuwa siku mbili kabla, chombo chetu kilizama, lakini Mungu alinijalia kufika pwani salama ijapokuwa kwa shida, pamoja na ile mitumba yangu (ambayo niliwaonyesha). Ni bahati yangu walinisadiki na kwa hivyo wakanipakia mashuani mwao pamoja na mitumba yangu kunipeleka chomboni. Nahodha

aliponiona akanishughulikia sana na kwa ukarimu wake alikataa kabisa kupokea chombo cha mali nilichompa kwa kujilipia nauli yangu. Basi safari yetu ikawa ya heri, tukapitia bandari kadha wa kadha, na katika kila bandari nikawa nanunua bidhaa nyingi zilizo nzuri nikiweka, hata mwisho nikajiona nimewasili Baghdadı mara nyingine, pamoja na kila aina ya mali.

Nikatoa tena fungu kubwa la mali yangu nikawapa masikini na kuipamba misikiti yote ya mjini, na baada ya hivyo nikakaa na ndugu zangu pamoja na rafiki zangu wote tukila karamu zetu na kufurahi.

Sindbad alipokwisha kunena maneno haya akanyamaa, na wale wasikilizaji wake wote wakanena kuwa mambo yaliyompata katika safari yake ya nne yamewapendeza zaidi kuliko yale waliyo yasikia kabla. Halafu wote wakaondoka wakiaga, na yule Hindbad, aliyepewa tena mfuko wa reale mia za dhahabu, akaambiwa arudi tena pamoja na wenziwe siku ya pili, asikilize habari za satari ya tano.

Siku ya pili wakati ulipotimia kila mtu akawa amekaa mahali pake anakula, hata walipokwisha kula na kunywa vyote valivyoandaliwa, Sindbad akaanza kutoa hadithi yake.
 
SAFARI YA TANO​



BASI baada ya haya yote yaliyonikuta, sikuwa radhi kukaa nitulie. Nilichoka nazo upesi tafrija za mjini nikatamani kuondoka mara moja tena, kwenda kubadili hewa na kuona mambo ya ajabu. Safari hii nilisafiri kwa jahazi yangu mwenyewe niliyoiunda karibu na bandari, maana nilipenda kupitia katika bandari yo yote niitaayo, kwa wakati wo wote nitakao mwenyewe. Basi kwa kuwa safari hii sikukusudia kuchukua mali mengi za kutosha kufanya shehena kamili, nilipatana na wftanyaji biashara wengine wa mataifa mbali mbali, waje wapakie mali zao.

Haya basi! tukaondoka tukasafiri kwa upepo mzuri, na baada ya safari ya kutwa tukafika bahari kuu, tukaegesha katika kisiwa kisichojulikana. Tukashuka tukaona hakina watu, lakini tukakusudia

kukizunguka. Basi kabla hatujafika mbali mara tukaona yai la ndege aitwaye Rok, ukubwa wake ulikuwa kama lile nililoliona zamani na kwa dalili yake lilikuwa karibu kuanguliwa, kwani mdomo wa mtoto ulikuwa umetokeza nje. Wale wafanyaji biashara wenzangu waliokuwa pamoja nami, ijapokuwa nilisema nao Sana kuwakataza wasiliguse, hawakunisikia, wakalingilia kulipiga kwa mashoka hata wakalivunja, na kumwua mtoto wa Rok. Halafu wakawasha moto na kumkatakata vipande vipande kuvikaanga, hali mimi nimesimama kwa hofu kuu.

Basi kabla hawajamaliza kula karamu yao hiyo mara tukaona huko juu hewani kumetanda giza kwa vivuli vya madege mawill makubwa. Na yule nahodha wa jahazi yangu, kwa maarifa yake aliyokuwa nayo akajua maana yake, ndipo akatwambia, ‘Wazazi wa ndege wanakuja, basi fanyeni muingie jahazini tujiponye.’ Nasi mara tukaingia na matanga yakatwekwa, lakimi kabla hatujafika po pote madege yakafıka na kutua juu ya jumba lao liliovunjwa. Hata yalipoona vipande vilivyobaki vya nyama ya mwana wao aliyepasuliwa, yakalia kilio cha kutisha mno. Punde kidogo yakaruka kwenda zao tukawa hatuyaoni tena ikabakı sisi kujisifu kuwa tumepona, lakini yalipotokea tena mara ya pili hali yanaruka juu hewani kulenga sawasawa na jahazi yetu, tukaona kila moja imechukua pandikizi la jiwe katika kucha zake, tayari kutupona nalo. Kuona vile tukawa na wasiwasi, ndipo lile dege moja likaachilia pande la jiwe lililoteremka likivunja anga, nami nashukuru kwa kuwapo mshika sukani hodarı aliyeigeuza jahazi yetu kwa kuelekea upande mwingine, ikaangukia baharini kando karibu yetu, nalo lilirusha maji kwa nguvu juu sana, hata ilikuwa karibu tuone chini ya baharı.
 
Back
Top Bottom