MB 1 iliuzwa senti 65, sasa tunakamuliwa shilingi 1 na senti 77, elfu 2 ilitupa GB 3 lakini sasa ni gb 1. Kenya na Zambia wametupindua

MB 1 iliuzwa senti 65, sasa tunakamuliwa shilingi 1 na senti 77, elfu 2 ilitupa GB 3 lakini sasa ni gb 1. Kenya na Zambia wametupindua

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Ndani ya muda mfupi kabisa gharama za internet zimepanda mara 2.7 yani tatu kasoro.

Ni mwaka jana tu hapo kabla ya mabadiliko machunu ya vifurushi tulikuwa tunaweza kununua mb moja kwa senti 65 (shilingi 0.65) lakini sasa ni takribani shilingi 1.8.

Hii elfu 2 tunayotumia kwa sasa kununua gb 1 ilikuwa inatosha kununua gb 3.

nchi yetu ilisifika kwa kuwa na gharama nafuu katika ukanda huu lakini kwa haya mabadiliko hata Kenya na Zambia wametuidi.
 
Nijuavyo mimi, MB huuzwa kwa Shilingi 1 hadi 2 point something. Ulichofanya wewe ni umeconvert BANDO LA INTERNET kwa pesa uliyonunulia.

Kumbuka hivyo vifurushi just an offer, yaan ni ofa tu kutoka kwenye mitandao na wala sio agizo au sheria wakupe bando.

Mitandao ya Simu hutoza pesa kwa Dk/sek kwa kupiga simu, kwa SMS kwa pale utumapo SMS na kwa KB au MB kwa pale utumiapo Internet.

Kutokana na ushindani ndio wakabuni VIOFA unavyotumia hapo ili kuvutia wateja wao, kwamba sasa ukilipa 500 utapata MB 300 au utapata Sms 500 kwa wiki, au utapata dk 20 kwa saa 24 nk nk.

Hiyo ni Offer tu na wala sio agizo kwao. Zamani tulilipa kwa Dk na Sms 1 ilikuwa karibu Tsh 40-60 kila utumapo.

Nadhani nimekupa mwanga na upunguze kulalamikia hisani. Watanzania Hisani tunafanya kuwa ni haki yako.
 
Watanzania wengi tushazoe vifurishi kwa hio ndio vimetumika kwenye hesabu, Ni ngumu sana kukuta mtu anaevijua vifurushi kumkuta anatumia internet kavu kavu bila kujiunga bando.
 
Watanzania wengi tushazoe vifurishi kwa hio ndio vimetumika kwenye hesabu, Ni ngumu sana kukuta mtu anaevijua vifurushi kumkuta anatumia internet kavu kavu bila kujiunga bando.
Sasa hizo ni hisani, usichukulie ndio haki yako. Haki yako ni kuuziwa MB 1 kwa Tsh kadhaa Sms na Dk hali kadhalika kwa Tsh kadhaa, hivyo vifurushi ni just an offer. KUZOEA MAANA YAKE NINI??
 
Sasa hizo ni hisani, usichukulie ndio haki yako. Haki yako ni kuuziwa MB 1 kwa Tsh kadhaa Sms na Dk hali kadhalika kwa Tsh kadhaa, hivyo vifurushi ni just an offer. KUZOEA MAANA YAKE NINI??
Huwezi Ukaita Package Ni Offer. Mfumo Wa Vifurushi Upo Rasmi Na Unajitegemea. Uko Sahihi Kwenye Bei. Bei ya MB 1 Ndani ya Kifurushi Ambayo Bei chini Tsh 1.75 Ni Tofauti Na Bei Ya Mb Nje Ya Kifurushi Ambayo Ni Tsh 9.35 Kwa Hi Mitandao Mitano Mikubwa. So Vifurushi Ni Mfumo Rafiki Na Nafuu Kwa Wateja Ila Sio Ofa. Ofa Ni kitu Kingine khabisa.
 
Nijuavyo mimi, MB huuzwa kwa Shilingi 1 hadi 2 point something. Ulichofanya wewe ni umeconvert BANDO LA INTERNET kwa pesa uliyonunulia...
Acha kupotosha. Hakuna kampuni inayotoa ofa. Iwe kifurushi au kitu kingine chochote ni biashara kama biashara. Kama unapewa hisani nadhani ni wewe peke yako.
 
Acha kupotosha. Hakuna kampuni inayotoa ofa. Iwe kifurushi au kitu kingine chochote ni biashara kama biashara. Kama unapewa hisani nadhani ni wewe peke yako.
Kasome sheria za hiyo mitandao, afu urudi tena hapa.
 
Ndani ya muda mfupi kabisa gharama za internet zimepanda mara 2.7 yani tatu kasoro.

Ni mwaka jana tu hapo kabla ya mabadiliko machunu ya vifurushi tulikuwa tunaweza kununua mb moja kwa senti 65 (shilingi 0.65) lakini sasa ni takribani shilingi 1.8.

Hii elfu 2 tunayotumia kwa sasa kununua gb 1 ilikuwa inatosha kununua gb 3.

nchi yetu ilisifika kwa kuwa na gharama nafuu katika ukanda huu lakini kwa haya mabadiliko hata Kenya na Zambia wametuidi.
Lini buku 2 ikikupa GB 3 ? Mitandao unatumia peke yako?
 
Mwaka Jana nilikua najiunga Halotel 5000 unapata 7GB Kwa siku 7. Leo hii unapata 2.7GB lakini Bei ni ileile 5000. Hili ni ongezeko la zaidi ya 130%
 
Nijuavyo mimi, MB huuzwa kwa Shilingi 1 hadi 2 point something. Ulichofanya wewe ni umeconvert BANDO LA INTERNET kwa pesa uliyonunulia.

Kumbuka hivyo vifurushi just an offer, yaan ni ofa tu kutoka kwenye mitandao na wala sio agizo au sheria wakupe bando.

Mitandao ya Simu hutoza pesa kwa Dk/sek kwa kupiga simu, kwa SMS kwa pale utumapo SMS na kwa KB au MB kwa pale utumiapo Internet.

Kutokana na ushindani ndio wakabuni VIOFA unavyotumia hapo ili kuvutia wateja wao, kwamba sasa ukilipa 500 utapata MB 300 au utapata Sms 500 kwa wiki, au utapata dk 20 kwa saa 24 nk nk.

Hiyo ni Offer tu na wala sio agizo kwao. Zamani tulilipa kwa Dk na Sms 1 ilikuwa karibu Tsh 40-60 kila utumapo.

Nadhani nimekupa mwanga na upunguze kulalamikia hisani. Watanzania Hisani tunafanya kuwa ni haki yako.
Hakuna cha ofa mkuu, soko linaamuliwa na mivutano katika soko ya uhitaji na supply, Hivi vifurushi ndivyo watu tunavihitaji ndio maana wanaviweka,,, hakuna cha ofa hapo, ni biashara mtindo moja ndio maana hakuna mtandao usio na vifurushi, usipouza vifurushi wakati wenzako wanauza jihesabie kukosa wateja, ni rahisi kama hivyo
 
Sasa ambapo hatutumii Zantel? Na kama ni promotion unawezaje kusema ni straight policy?

Mbona Saizi kuna mitandao inakukipia tozo Kwa hiyo tuje tuseme tuliokuwa tunatoa pesa bila tozo?
Kama wewe ulikuwa hutumii Zantel, hayo yalikuwa ni maamuzi yako, hili ni soko huru hakuna kulazimishana, tuliozihitaji hizo gb 3 kwa elf 2 tulitumia Zantel kwa miaka.
 
Kama wewe ulikuwa hutumii Zantel, hayo yalikuwa ni maamuzi yako, hili ni soko huru hakuna kulazimishana, tuliozihitaji hizo gb 3 kwa elf 2 tulitumia Zantel kwa miaka.
Basi kinachoangaliwa ni yule mwenye share kubwa Sokoni alikuwa ana charge kiasi gani na hapa ni Voda, Airtel na Htel kidogo na Tigo hao wengine akina Zantel sijui TTcl ni very minor
 
Hakuna cha ofa mkuu, soko linaamuliwa na mivutano katika soko ya uhitaji na supply, Hivi vifurushi ndivyo watu tunavihitaji ndio maana wanaviweka,,, hakuna cha ofa hapo, ni biashara mtindo moja ndio maana hakuna mtandao usio na vifurushi, usipouza vifurushi wakati wenzako wanauza jihesabie kukosa wateja, ni rahisi kama hivyo
Kaa na mavi yako kichwani, maana unaeleweshwa unalazimisha ofa iwe haki yako.
 
Watanzania wengi tushazoe vifurishi kwa hio ndio vimetumika kwenye hesabu, Ni ngumu sana kukuta mtu anaevijua vifurushi kumkuta anatumia internet kavu kavu bila kujiunga bando.
naomba mungu huyu jamaa akuelewe!!!! hii OFA kwake imekuwa HAKI
 
Back
Top Bottom