Uchaguzi 2020 Mbarali: Ngome mpya ya CHADEMA isiyofahamika

Kuna haja ya kutumia chopa kufidia hii wiki iliyopotea ikiwezekana kwa siku mikutano hata 6. Maana bado kanda ya kusini na kaskazini
Inawezekana lakini kwa muda uliobaki itabidi sacrifice baadhi ya mikoa .

Hasa mkoa wa Dodoma, na Ruvuma, Pwani, Dar es salaam,
Badala yake aende Shinyanga, Simiyu, Lindi, Mtwara, Singida, Manyara, Arusha, kilimanjaro na Tanga

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Sijui Ratiba ya NEC vipi. Ni muhimu ku prioritize. Baad ya kutoka Singida bila shaka ataenda Manyala na badae arudi Shinyanga na Lindi. Dodoma na Morogoro hakuna kitu kuna mazuzu tupu.
 
Sijui Ratiba ya NEC vipi. Ni muhimu ku prioritize. Baad ya kutoka Singida bila shaka ataenda Manyala na badae arudi shinyanga na Lindi. Dodoma na Morogoro hakuna kitu kuna mazuzu tupu.
Lindi na Morogoro kuna kura.

Lindi na Mtwara kuna DNA ya upinzani kumbuka CUF 2015 walibeba majimbo 10 kutoka kusini na hata sasa hivi kuna possibility CCM asipate majimbo mengi kanda hiyo

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 

Naomba unielewe vizuri, mimi ninaufahamu upinzani na najua kila mahala penye jumuia yeyote ile ambayo ina watu wengi lazima upinzani uwepo.

Lakini kuna makosa ya organisation yaliyopo upinzani hayawezi kutufikisha kule tunako kutaka tufike. Kuwepo kwa wapinzani wa kweli hakufanyi mnayo yapanga yakatokea, lazima pawepo na hatua za lazima na makusudi ambazo lazima zifuatwe ndio mtapata matokeo mnayoyataka.

1) Mmejipanga vipi kabla ya kwenda kufanya tukio? kupanga vizuri kwa unachotaka kukifanya unakuwa umekwisha tenda 40% ya tukio.
2)Usidharau ubora wa mshindani wako, ukidharau ubora wake unaweza ukatumia silaha hafifu kuliko unazotakiwa kuzitumia kushinda vita.

3) Wapiga kura ni Watanzania, na sio Chadema inawapiga kura wake na vituo vyake, ni pamoja na wapinzani wa Chadema ni wapiga kura wetu, woooote.
4) Kusimamia kila mnacho kifanya, tulipata matatizo kwa ujazaji form wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa, jee tunashindwa kitu gani kuwahimiza wagombeaji waende kwa wanasheria tulio watayarishaa kuwasaidia kama chama na wagombeaji wengi wanauwezo wa kulipia hata kama 50,000/=.

5) Tunaingia uchaguzi bila kampeni materials, kwani tulikuwa hatujui uchaguzi utakuwa lini?
6) Jee tuliendesha hata semina kuwatayarisha wagombea kwenda kwenye uchaguzi huu, hasa wanaoingia kenye uchaguzi huu kwa mara ya kwanza?.
7) Kwa nini utafiti au ushauri hasa wa maandishi haufanyiwi kazi na unatolewa bure ?.

Hali yetu haikuwa nzuri hata 2015, lakini aibu ilifichika baada ya Mzee Lowasa kuokoa jahazi.

8) Kama chama chochote kile ukiona watu wenye ufahamu hawapewi nafasi au wanabezwa lazima ujiulize? kunani? Kila mwaka wa uchaguzi kundi linalo ondoka ni educated Elites kwa nini?

9) Tunaogopa ushindani ndani ya chama? siwezi kueleza sana hichi sio sahihi kuweka mengi wazi ni kipindi cha uchaguzi, lazima niwe na kaba ya roho, Chadema imekwisha pigika ndani na njee tukiendeleza kidogo tutakimaliza.

Na mapungufu yote yanaweza kufanyiwa kazi, Chadema lazima kihakikishwe kinabaki kwa kuweza kupigana vita nzuri na yenye ufundi 2025.
 
Msisahau mbeya vijijini wamama wa sokoni wapo na CHADEMA tu wanamtaka mbunge kijana safari hii yule mzee hana msaada mvua zikinyesha sokoni hakupitiki
 
Ha ha ha ha ha hata Arsenal inawashabiki wafia timu, japo matokeo yamekuwa ya kusua sua. Tungependa wapinzani washinde lakini kwa bahati mbaya, waliobaki mifano mifano ya wapinzani.
Ndo sisi sasa mashabiki wa Arsenal tu wavumilivu tupo tayari kwa majibu yote na hatuhami CHADEMA hata iweje
 
Issue ni siku ya uchaguzi, wakati wa kupiga, kuhesabu, na kutangaza matokeo. Sharti upinzani uwe na mawakala welevu, waliofunzwa, na hodari kuzuia njama chafu.
 
Tuzidishe maombi.Mbarali inahitaji ukombozi wa pili.Mungu ni mwema.tusubiri 28/10
 
Nilikuwa Mbeya mwishoni mwa mwezi wa 9, kuna mwana CCM kindakindaki akaniambia Mbarali kuna upinzani mkali sana... mimi mwenyewe nikabaki nashangaa. Kuna ukweli kwenye hili, wacha tuendelee kutazama.
 
Jimbo lingine ni katoro CDM ikikomaa inachukuwa maana jamaa wanajipanga kupora
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…