Mbaroni kwa kumkamata, kumshambulia na kusambaza picha za utupu za waliyemfumania

Mbaroni kwa kumkamata, kumshambulia na kusambaza picha za utupu za waliyemfumania

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu sita kwa tuhuma za kuwashambulia na kuwarekodi video za utupu watu wawili wanaodaiwa kufumaniwa na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii.

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Jumanne Muliro amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Singiba Buchadi (42) ambaye ni fundi umeme na mfanyabiashara Dephina Buchadi (42).

Kamanda Muliro amewataja wengine kuwa ni Doratea Mathayo (39), Wilbard Teobard (55), Albert Buchadi (30), Valenzi Silvester (40).

Amesema kuwa watuhumiwa hao wote ni wakazi wa Kongowe Wilaya ya Mkuranga.

“Vitendo vya kikatili walivyovifanya watuhumiwa hawa ni pamoja na kutoa adhabu wakati wao si mahakimu wala majaji, vitendo hivi havikubaliki kisheria katika nchi inayofuata mfumo wa utawala wa sheria na kwa sababu hizo watafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo,”alisema Muliro.


wakamatwa-pc-data.png
 
kwa kipigo na manyanyaso alopata jamaa utaishia kubali muke/mume ya mutu sumuuu

Jana saa 12:30-13:00 kulikuwa na maelezo walitoa walopigwa kupitia kipindi cha clouds fm "heka heka"
Leo wataendelea 12:30-13:00

Nilichojifunza hamna nchi ilowahi kaliwa/tawaliwa na wakoloni wakaondoka na kusema uhusiano umeishaaa.
Changamoto watu hatuambizani ukweliii

Yohana 2:17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, "Wivu wa nyumba yako utanila".
 
Back
Top Bottom