Mbeya: Hakimu wa Mahakama ya Wilaya auawa kwa kipigo kutoka kwa Wananchi wenye hasira kali

Mbeya: Hakimu wa Mahakama ya Wilaya auawa kwa kipigo kutoka kwa Wananchi wenye hasira kali

Naona imani za kishirikina ndio chanzo cha tatizo.
 
Kuna vijiji hawana macheko na hawatak madharau,sijui hata waliwezaje kujikusanya fasta hvyo na kufanya jambo.

Ila hicho kijiji watateseka mpaka wajute kuna nyumba zitabaki na wanawake tu
 
Juu ya kanisa katoliki au CCM kuchukua maamuzi ya kuua au ugomvi wa kuumizana ,nakataa kabisa. Kama ni wewe umepanga kufanya fujo kulisingizia kanisa au CCM na kuja kusema niliwaambia ,acha wazo hilo.
Umeona eenhh?!.Barikiwa sana mkuu.
 
Duh hii imetokea Kijiji cha Kibole, Kata ya Itete.. Halmshauri ya Wilaya ya Busokelo.

Nilimpigia Afisa Mtendaji wa Kijiji icho cha Kibole na kumpa pole kwa kilichotokea.

Kwakweli inashangaza sana Hakimu kutoheshimu maamuzi ya Mahakama.
 
Nimekutana na hili andiko kwenye mitandao yetu hii, naamini mamlaka zitatuambia ukweli wa hii kitu....

Anaandika Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mh. Siriel Mchembe👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿

Niimepokea taarifa kutoka kwa DC Rungwe Dkt. Vincent Anney kwamba alfajiri ya leo, Hakimu Joakim Mwakyolo wa Mahakama ya Wilaya hapa Handeni ameuawa na wananchi wenye hasira kali huko Busokelo Tukuyu/Rungwe.

Marehemu alikuwa likizo maana huko Rungwe ndipo anapotokea.

anzo cha kuuawa ni Mgogoro wa Ardhi kati yake na wanakijiji hicho anachotoka.

Alishindwa kesi ya ardhi Mahakama Kuu dhidi ya kijiji, lakini baada ya muda akaonekana kwenye eneo la Mgogoro akiwa ameongozana na Watu wawili.

Inadaiwa kuwa yeye na watu hao wawili kuna vitu walikuwa wanavichimbia ardhini kwenye eneo hilo la mgogoro jambo ambalo lilitafsiriwa na wanakijiji kwamba ni ushirikina.

Wananchi walipowazonga watatu hao na kuwahoji kuhusu suala hilo, ugomvi ukatokea kati yao, jambo lililopelekea mmoja wa watu waliokuwa na Hakimu huyo kuwapiga risasi wanakijiji wawili miguuni.

Baada ya hapo wananchi wakapandwa hasira na kumshambulia kwa mawe na silaha mbalimbali Hakimu huyo pamoja mmoja wa watu aliokuwa nao, huku mwingine akitoweka kuelekea kusikojulikana.

Hivyo vifo vilivyoripotiwa ni viwili. Hakimu pamoja na mmoja wa watu alikwenda nao kwenye eneo la mgogoro.

Pole sana Mhimili wetu wa Mahakama, hasa Hakimu wa Wilaya Handeni Mhe.Sabuni kwa kuondokewa na mtumishi huyu.Poleni ndugu zangu wa Handeni.

Tuwaombee pumziko la amani - Amina.

===================

TAARIFA RASMI YA MKUU WA WILAYA

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Dkt. Vincent Anney amesema “Ni tukio la kweli, Hakimu alikuwa na mgogoro na Wanakijiji, yeye si mwananchi wa Rungwe ila alinunua eneo Rungwe.

“Zamani baba yake alikuwa anaishi Rungwe akahamia Kyela, hata yeye Hakimu alizaliwa hukohuko Kyela. Hapo kati alianzisha mgogoro na wananchi akisema anataka eneo la babu yake lakini hiyo ni sehemu nyingine, si seheu amayo tukio limetokea.

“Eneo ambalo limesababisha auawe ni kubwa kuna karibia ekari 1000, ni msitu na ni hifadhi ambayo imekuwa ikisadia mvua, alinunua kinyemela, wananchi wakamshtaki Mahakamani.

“Akashindwa kesi, alikuwa katika harakati za kukata rufaa, kesi ikiwa imeisha akaenda shambani akiwa na watu wengine wawili akaanza kuchimbachimba, inasemakana alikuwa anachimba dawa.

“Yakatokea majibizano kati yake na Wananchi waliofika eneo hilo, akatoa bastola na kuwapiga risasi Wananchi wawili miguuni.

“Wananchi wakakasirika na kuanza kumpiga kisha kusababisha kifo chake pamoja na mmoja kati ya wale watu wawili alioongozana nao, mwingine mmoja alitokomea haijulikani alipokwenda.

“Tumeshawakamata watu kama saba hivi kutokana na tukio hilo na uchunguzi unaendelea.”
Kutokana na simulizi ya tukio hao wananchi walikuwa kwenye self defence kwa sababu marehemu alishaanza kuwadhuru kwa silaha ya moto.

Reasonably silaha walizotumia wananchi ni kiwango cha chini dhidi ya marehemu.

Hakimu amepoteza maisha kwa ardhi inayoenda kummeza milele yote
 
Duh hii imetokea Kijiji cha Kibole, Kata ya Itete.. Halmshauri ya Wilaya ya Busokelo.

Nilimpigia Afisa Mtendaji wa Kijiji icho cha Kibole na kumpa pole kwa kilichotokea.

Kwakweli inashangaza sana Hakimu kutoheshimu maamuzi ya Mahakama.
Hapo ndipo utafakari usahihi wa hukumu wanazotoa mahakimu wetu dhidi ya wananchi wanaobambikiziwa hujumu uchumi
 
Siku zote napinga suala la kumiliki silaha, ukiwa na silaha za moto unakuwa ni mwenye kijiamini kupita maelezo, hapo hakimu asingekuwa na silaha pengine wangeweza kuzungumza na yakaisha.

Jambo lingine, serikali iangalie hawa watu waliopewa Mamlaka ya uamuzi. Hakimu mzima umeshindwa kwenye kesi badala ukate rufaa unalazimishia mabavu, yawezekana hata hukumu zake ni za kijanjajanja.

Wananchi waliotenda jinai hiyo pia ni wahalifu. Kuua mtu sio suluhisho ila ni kuongeza ukubwa wa tatizo. Hao wahalifu wasakwe.

Yote kwa yote , Mungu azipumzishe roho za Marehemu mahali pema peponi na majeruhi awape uponyaji wa haraka.
Ikiwa tayari hakimu alishawavunja wawili miguu huoni kama wananchi walikuwa wanajitetea na wameua bila kukusudia?
 
Hii nchi ina ardhi kubwa kwa nini ugombane na watu na mwishowe kuuwawa kizembe? Mimi natokea Kilimanjaro ambako ardhi ya familia nzima ni ekari 15 tuu na tuko zaidi ya 30. Nimeenda zangu Morogoro nimepata ardhi nzuri kwa kilimo, ufugaji na hata makazi, tena kwa bei ya kutupa kabisa na wenyeji wangu ni watu wakarimu sana. Yaani hata ukitaka ekari 100 unapata bila zengwe unaenda ofisi ya Kijiji mnaandikishiana, unalipa ushuru wa kijiji unapewa risiti maisha yanaenda.
 
Siku zote napinga suala la kumiliki silaha, ukiwa na silaha za moto unakuwa ni mwenye kijiamini kupita maelezo, hapo hakimu asingekuwa na silaha pengine wangeweza kuzungumza na yakaisha.

Jambo lingine, serikali iangalie hawa watu waliopewa Mamlaka ya uamuzi. Hakimu mzima umeshindwa kwenye kesi badala ukate rufaa unalazimishia mabavu, yawezekana hata hukumu zake ni za kijanjajanja.

Wananchi waliotenda jinai hiyo pia ni wahalifu. Kuua mtu sio suluhisho ila ni kuongeza ukubwa wa tatizo. Hao wahalifu wasakwe.

Yote kwa yote , Mungu azipumzishe roho za Marehemu mahali pema peponi na majeruhi awape uponyaji wa haraka.
Hawa wananchi, ukiondoa tukio la kumtoa roho Mhe hakimu, wsnajitambua kwa kitendo cha kufungua kesi huku wakijua jamaa ni hakimu na pengine angetumia nafasi yake kushawishi kesi ipindishwe. Pia nimpongeze hakimu aliyesimamia hiyo kesi kwa kusimamia haki bila kumpendelea hakimu mwenzake kama tunavyoona kwenye baadhi ya matukio ya Polisi,ambao wanapenda sana kulindana na kuonea watu.
 
Hii nchi ina ardhi kubwa kwa nini ugombane na watu na mwishowe kuuwawa kizembe? Mimi natokea Kilimanjaro ambako ardhi ya familia nzima ni ekari 15 tuu na tuko zaidi ya 30. Nimeenda zangu Morogoro nimepata ardhi nzuri kwa kilimo, ufugaji na hata makazi, tena kwa bei ya kutupa kabisa na wenyeji wangu ni watu wakarimu sana. Yaani hata ukitaka ekari 100 unapata bila zengwe unaenda ofisi ya Kijiji mnaandikishiana, unalipa ushuru wa kijiji unapewa risiti maisha yanaenda.
Mkuu ni wapi huko na wanauzaje??
 
Yale yale ya Mabima na wananchi wenye hasira kali huko Mwanza.... vibastola vinawapa watu jeuri wakidhani wanaweza kutisha kila mtu. Haya sasa akazikwe na kabastola kake!
 
Nimekutana na hili andiko kwenye mitandao yetu hii, naamini mamlaka zitatuambia ukweli wa hii kitu....

Anaandika Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mh. Siriel Mchembe[emoji1541][emoji1541][emoji1541][emoji1541][emoji1541]

Niimepokea taarifa kutoka kwa DC Rungwe Dkt. Vincent Anney kwamba alfajiri ya leo, Hakimu Joakim Mwakyolo wa Mahakama ya Wilaya hapa Handeni ameuawa na wananchi wenye hasira kali huko Busokelo Tukuyu/Rungwe.

Marehemu alikuwa likizo maana huko Rungwe ndipo anapotokea.

anzo cha kuuawa ni Mgogoro wa Ardhi kati yake na wanakijiji hicho anachotoka.

Alishindwa kesi ya ardhi Mahakama Kuu dhidi ya kijiji, lakini baada ya muda akaonekana kwenye eneo la Mgogoro akiwa ameongozana na Watu wawili.

Inadaiwa kuwa yeye na watu hao wawili kuna vitu walikuwa wanavichimbia ardhini kwenye eneo hilo la mgogoro jambo ambalo lilitafsiriwa na wanakijiji kwamba ni ushirikina.

Wananchi walipowazonga watatu hao na kuwahoji kuhusu suala hilo, ugomvi ukatokea kati yao, jambo lililopelekea mmoja wa watu waliokuwa na Hakimu huyo kuwapiga risasi wanakijiji wawili miguuni.

Baada ya hapo wananchi wakapandwa hasira na kumshambulia kwa mawe na silaha mbalimbali Hakimu huyo pamoja mmoja wa watu aliokuwa nao, huku mwingine akitoweka kuelekea kusikojulikana.

Hivyo vifo vilivyoripotiwa ni viwili. Hakimu pamoja na mmoja wa watu alikwenda nao kwenye eneo la mgogoro.

Pole sana Mhimili wetu wa Mahakama, hasa Hakimu wa Wilaya Handeni Mhe.Sabuni kwa kuondokewa na mtumishi huyu.Poleni ndugu zangu wa Handeni.

Tuwaombee pumziko la amani - Amina.

===================

TAARIFA RASMI YA MKUU WA WILAYA

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Dkt. Vincent Anney amesema “Ni tukio la kweli, Hakimu alikuwa na mgogoro na Wanakijiji, yeye si mwananchi wa Rungwe ila alinunua eneo Rungwe.

“Zamani baba yake alikuwa anaishi Rungwe akahamia Kyela, hata yeye Hakimu alizaliwa hukohuko Kyela. Hapo kati alianzisha mgogoro na wananchi akisema anataka eneo la babu yake lakini hiyo ni sehemu nyingine, si seheu amayo tukio limetokea.

“Eneo ambalo limesababisha auawe ni kubwa kuna karibia ekari 1000, ni msitu na ni hifadhi ambayo imekuwa ikisadia mvua, alinunua kinyemela, wananchi wakamshtaki Mahakamani.

“Akashindwa kesi, alikuwa katika harakati za kukata rufaa, kesi ikiwa imeisha akaenda shambani akiwa na watu wengine wawili akaanza kuchimbachimba, inasemakana alikuwa anachimba dawa.

“Yakatokea majibizano kati yake na Wananchi waliofika eneo hilo, akatoa bastola na kuwapiga risasi Wananchi wawili miguuni.

“Wananchi wakakasirika na kuanza kumpiga kisha kusababisha kifo chake pamoja na mmoja kati ya wale watu wawili alioongozana nao, mwingine mmoja alitokomea haijulikani alipokwenda.

“Tumeshawakamata watu kama saba hivi kutokana na tukio hilo na uchunguzi unaendelea.”

Mahakimu na majaji wafe tu maninaaa zao wanatumiaga sheria kama fimbo sana! Watu wengi wamefungwa kijinga tu
 
Back
Top Bottom