TANZIA Mbeya: Mwenyekiti wa UVCCM Makongorosi, Michael Kalinga akutwa ameuawa na mwili wake kutelekezwa

Inasikitisha sana!
Haya mambo ndio katoka kusema Askofu Yuda Thadeus Ruwa'ichi....
Naona taratibu tunaelekea kwenye matatizo makubwa sana kama Taifa....
Mdogo mdogo tunaelekea kwenye jino kwa jino! Jicho kwa jicho!
Wanaoteka, kutesa na kuua wengine na kunyamaziwa watasababisha madhara kwa wengi!
 
Ccm wakiuliwa hatusikii haki za binadamu wakizungumza ila wakifa vyama vingine

..hakuna anayepiga kelele kwasababu watu wana imani kwamba CCM siku zote wanatendewa haki.

..haki za binadamu wako kutetea wale ambao hawana sauti, wanaonyanyaswa, na hawana watetezi.

..CCM inao makada wake katika vyombo vyote vya dola hapa nchini. Mwenyekiti wa Ccm ndiye Amiri Jeshi Mkuu. Kwa mantiki hiyo mwanaCCM akipatwa na matatizo lazima atasaidiwa na vyombo vya dola.
 
Kumbe na maccm nayo yanakufa? Au ndiyo drama tu kama alivyowahi kusema mwenyekiti wao ili kubalance matukio?
 
Aiseee
Haya mambo yanazidi kupamba moto
Mungu turehemu

Wanaofanya haya, Mungu yupo.
 
Imeniuma sana kumpoteza kijana mtiifu kwa taifa lake na chama chetu .tunatoa wito kwa polisi kufanya uchanguzi wa kutosha kuhakikisha walimuua wanaopatikana na kuchukuliwa hatua stahiki

USSR
View attachment 3168062weny
Huyu sijui chochote juu yake; ndiyo sababu nasita kuchukua upande. Siamini kamwe hata siku moja kwamba waTanzania wote waliomo CCM wana stahili haya yaliyo mtokea huyu.
Lakini, kama alikuwa kama yule UVCCM wa Kagera; nisinge sita kumtakia kheri huko aendako.

Ni bahati mbaya sana kwamba viongozi wa nchi hii wame tufikisha katika hali hii ya mgawanyiko kama taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…