Pre GE2025 Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

Pre GE2025 Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametoa masaa 24 kutiwa mbaroni Kwa Kijana mmja huko Wilayani Rungwe ambae inadaiwa amemkashifu Rais Samia na Kuichoma Picha yake.

My Take
Naunga mkono hoja, upumbavu wa tabia za kihuni za kuiga ukomeshwe na usiruhusiwe hapa Tanzania.

Mnaweza kupinga Kila kitu kadiri inavyowezekana lakini kwa namna ya kuwaheshimu hao msiokubaliana.

Tanzania haiwezi na haitakuja kuwa Taifa la wahuni.Safi sana Polisi Kwa kumtia nguvuni,alijikuta Gen Z sana.

Ni vyema ikaeleweka kwamba Watanzania tuelewe nafasi ya Rais kama Kiongozi wa nchi na tumheshimu Rais Samia Suluhu Hasani

====


Mkuu wa mkoa wa mbeya cde: Juma Z. Homera amemuagiza Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya SACP Benjamini kuzaga kumsaka na kumkamata kijana anayepatikana Ntokela Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya kwa kosa la kumkashifu Rais Samia kwa maneno makali na kisha kuichoma moto picha inayomuonyesha Rais.

RC Homera amelaani vikali kitendo hicho kuwa si cha maadili wala uungwana na kiko tofauti na utamaduni halisi wa wananchi mkoani Mbeya.

Hata hivyo ametoa masaa 24 kwa Kamanda Kuzaga kumkamata kijana huyo ili alisaidie Jeshi la Polisi juu ya tuhuma hizo na mashambulizi hayo ambayo kayaelekeza moja kwa moja kwa Rais Samia.

Mwisho RC Homera amewasihi wananchi mkoani Mbeya kutojiingiza kwenye vitendo viovu kwa kukashifu viongozi makusudi badala yake wajikite katika utafutaji na uchapa kazi kwa manufaa ya familia zao na Tanzania kwa ujumla.


Video ya Kijana akichoma moto picha ya Rais Samia.

Pia soma==>> Aliyekamatwa kwa kuchoma picha ya Rais Samia ahukumiwa faini Tsh. Milioni 5 au miaka miwili jela
 
Hiyo picha ni mali yake ana haki ya kuifanya atakavyo

Bendera za Israel na Marekani kila mara zinachomwa moto ndio sembuse.

Yupo mwamba mpaka nakala za Qurani kapiga moto ni mali yake huwezi kumpangia.
 
Hiyo picha ni mali yake ana haki ya kuifanya atakavyo

Bendera za Israel na Marekani kila mara zinachomwa moto ndio sembuse chura kiziwi.

Yupo mwamba mpaka nakala za Qurani kapiga moto ni mali yake huwezi kumpangia.
Rais ni Mali ya Umma sio yake ,kuharibu Mali ya Umma ni kosa na vibaya kimaadili.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametoa masaa 24 kutiwa mbaroni Kwa Kijana mmja huko Wilayani Rungwe ambae inadaiwa amemkashifu Rais Samia na Kuichoma Picha yake.👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/C86M9wSCkcp/?igsh=em1heXI4NHgybw==

My Take
Naunga mkono hoja, upumbavu wa tabia za kihuni za kuiga ukomeshwe na usiruhusiwe hapa Tanzania.

Mnaweza kupinga Kila kitu kadiri inavyowezekana lakini kwa namna ya kuwaheshimu hao msiokubaliana.

Tanzania haiwezimkiwa Taifa lawahuni.

Hebu na sisi tuione hiyo picha
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametoa masaa 24 kutiwa mbaroni Kwa Kijana mmja huko Wilayani Rungwe ambae inadaiwa amemkashifu Rais Samia na Kuichoma Picha yake.👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/C86M9wSCkcp/?igsh=em1heXI4NHgybw==

My Take
Naunga mkono hoja, upumbavu wa tabia za kihuni za kuiga ukomeshwe na usiruhusiwe hapa Tanzania.

Mnaweza kupinga Kila kitu kadiri inavyowezekana lakini kwa namna ya kuwaheshimu hao msiokubaliana.

Tanzania haiwezimkiwa Taifa lawahuni.

Mbona picha inaonesha ni uchina, huyo mkuu wa mkoa amri hiyo ameitoa akiwa China? Na picha husika si ya mama Samia kwani picha yake amevaa ushungi mwekundu si mweusi kama ambavyo picha inaonesha.
 
Back
Top Bottom