KISA CHA TATU.
KISA CHA KIJANA BAROBARO NA MAISHA YA CHINI KABISA (FUKARA) KUMBE NI TAJIRI MKUBWA.
Kisa hiki chamhusu kijana mmoja shababi mwenye nguvu zake za kutosha kumsukuma tembo kwa mikono yake.
Kisa hiki kilitokea kwenye jiji la maraha, jiji lililoporwa ukuu wa nchi na kubaki kuwa makao makuu ya ubuyu na Visa vya kina Manunu, Mkadeda,
Mshana Jr na wengine wengi walio maarufu. Makao Makuu ya Masupa Staa wa
instagram.
Huyu kijana tumuite Mr. Mbunye, yeye alikuwa ni mwajiriwa wa shirika moja kubwa la mifuko ya hifadhi za Jamii.
Shirika hili lilikuwa mahiri kwa kununua ardhi kwa Bei ndogo kisha Hudanganya kwamba wamenunua kwa Bei kubwa, chenji ziliingia mikononi mwa wajanja wachache na miongoni mwao alikuwa ni huyu Mr. Bunye.
Walichokuwa wakifanya mbali na kudanganya gharama za manunuzi, ni pamoja na kuchelewa mafao ya wastaafu, zile hela za wastaafu zilikuwa zikiingizwa kwenye akaunti binafsi za wajanja wachache akaunti za fixed account, hela ikisha mature riba huliwa na wajanja wachache.
Waliendelea na mchezo huu kwa miaka mingi sana ya ule utawala wa Chukua Chako Mapema
uncle SCAR na rafiki zake mafisi wenye uchu na uroho wakiongozwa na Shenzi, Banzai, na Ed.
Alipo ingia mtawala mpya
Simba, alianza kufukua makaburi, kuanzia mradi ule mkubwa uliopo ng'ambo ya Bahari, majengo marefu katikati ya jiji, na sehemu nyingine.
Uchunguzi huo ukagundua madudu ya kutisha, Mr Mbunye naye alikuwa na magunia ya mapesa kayahifadhi nyumbani.
Mr. Mbunye machale yakamcheza, akaenda kununua kigari kikirikuu, akachukua nyraka zake zote muhimu, akazitia kimpangilio kwenye gari, akachomelea bodi lote kimadhubuti, akazuga na kakufuli.
Akaendesha hicho kigari Hadi kwa mjomba wa mke wake huko Ngudu, akamwambia hii gari nimeinunua kwa jamaa yangu ni mbovu, nikiitengeneza hapo nitakapo pata pesa nitaitengeneza kisha wewe itakuwa unitumia.
Jamaa akaing'oa hiyo gari magurudumu yake. Akaiweka juu ya mawe, ikapigwa na vumbi la kutosha.
Kamatakamata ikaanza Mr. Mbunye naye akakamatwa, uchunguzi ukafanyika, wakampekua kila mahali, kila ndugu na jamaa yake akapatwa misukosuko, lakini hakuna aliyekashtukia kale ka gari kabovu juu ya mawe.
Muda mrefu wa uchunguzi ukapita na hakukuwa na ushahidi wa kumtia hatini.
Mr. Mbunye akaachiwa huru, akarudishwa kazini.
Kazini akaomba apunguzwe kazini ili akapate nafasi ya kujitibu.
Akalipwa mafao yake yote. Akakarudia kagari kake kwa shangwe.
Mr. Mbunye akaibuka kidedea bila kushitukiwa.
Sasa ana biashara zake halali za uchukuzi na clearing and forwarding akiwa na malori mengi sana ya mizigo na mafuta, ana kampuni kubwa ya kuzimisha mitambo ya ujenzi, anakula hela yake kiulaini.