Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Mimi ni mmoja wa walioamini katika story ya Majaliwa Jackson kijana wa kihaya aliyeokoa abiria siku ile ya ajali ya Ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nilipomuona anaongea katika runinga akihojiwa na mtangazaji wa TBC asubuhi baada ya ajali kutokea jana yake nikaamini nilichokiona.
Kijana ameucheza vizuri uhusika wake kadri script ilivyomuelekeza kucheza, mpaka akaalikwa bungeni na akapiga selfie nyingi na warembo wa Sinza, akawa maarufu ghafla na ajali nzima na vifo vya abiria vikapoteza umaarufu.
Serikali imefunika hii aibu kwa gharama za Majaliwa. Na hata kama amepewa pesa za wasamaria wema, ni pesa ambazo hazilingani na fedheha nzima ya ndege kuzama pasipo muokoaji wa maana aliyesomea uokoaji kusogea karibu kabisa na Ndege ile!.
Uokoaji ni jukumu la serikali, na halikwepeki hata siku moja. Anaweza kutumika Majaliwa anayepatikana karibu na tukio na akatumika kuzima uzembe mzima, lakini bado ukweli unasimama kama ukweli kuwa uokoaji ni jukumu la kiserikali.
Ni kazi ya kwanza kufanywa na serikali kwa mlipa kodi anayetoka jasho mchana na usiku ili achangie mfuko wa hazina. Uokoaji sio suala la kuchukuliwa kama ni ziada, hapana, ni jukumu la kiserikali kulinda maisha ya raia wake.
Bima wamesema watalipa, lakini hii haiondoi ukweli kwamba ile ni ajali ya pili kutokea ndani ya Ziwa Victoria, ya kwanza ikiua watu wasiopungua 1,000 mwaka 1996. Hii ni ya ajali ya pili na hakuna chombo cha uokoaji chenye kufanana na serikali.
Yanapotokea matukio kama haya ndipo watu huwa wana haki ya kuhoji manunuzi ya magari ya milioni 400 yanayopishana barabarani nchi nzima na anasa nyingi halafu hakipo kinachomfikia mtu wa kawaida akiwa anasisitiziwa kila mara juu ya umuhimu wa kulipa kodi kila mara!.
Safari hii ametumika Jackson Majaliwa 'kuuwa soo" lakini ni suluhisho dogo na la muda mfupi tu. La kufanyiwa kazi ni suluhisho lenye kueleweka na kukubalika miongoni mwa walipa kodi. Miongoni mwa wanaoumia kugharamia matanuzi ya kila siku ya serikali.
Kijana ameucheza vizuri uhusika wake kadri script ilivyomuelekeza kucheza, mpaka akaalikwa bungeni na akapiga selfie nyingi na warembo wa Sinza, akawa maarufu ghafla na ajali nzima na vifo vya abiria vikapoteza umaarufu.
Serikali imefunika hii aibu kwa gharama za Majaliwa. Na hata kama amepewa pesa za wasamaria wema, ni pesa ambazo hazilingani na fedheha nzima ya ndege kuzama pasipo muokoaji wa maana aliyesomea uokoaji kusogea karibu kabisa na Ndege ile!.
Uokoaji ni jukumu la serikali, na halikwepeki hata siku moja. Anaweza kutumika Majaliwa anayepatikana karibu na tukio na akatumika kuzima uzembe mzima, lakini bado ukweli unasimama kama ukweli kuwa uokoaji ni jukumu la kiserikali.
Ni kazi ya kwanza kufanywa na serikali kwa mlipa kodi anayetoka jasho mchana na usiku ili achangie mfuko wa hazina. Uokoaji sio suala la kuchukuliwa kama ni ziada, hapana, ni jukumu la kiserikali kulinda maisha ya raia wake.
Bima wamesema watalipa, lakini hii haiondoi ukweli kwamba ile ni ajali ya pili kutokea ndani ya Ziwa Victoria, ya kwanza ikiua watu wasiopungua 1,000 mwaka 1996. Hii ni ya ajali ya pili na hakuna chombo cha uokoaji chenye kufanana na serikali.
Yanapotokea matukio kama haya ndipo watu huwa wana haki ya kuhoji manunuzi ya magari ya milioni 400 yanayopishana barabarani nchi nzima na anasa nyingi halafu hakipo kinachomfikia mtu wa kawaida akiwa anasisitiziwa kila mara juu ya umuhimu wa kulipa kodi kila mara!.
Safari hii ametumika Jackson Majaliwa 'kuuwa soo" lakini ni suluhisho dogo na la muda mfupi tu. La kufanyiwa kazi ni suluhisho lenye kueleweka na kukubalika miongoni mwa walipa kodi. Miongoni mwa wanaoumia kugharamia matanuzi ya kila siku ya serikali.