Pre GE2025 Mbinu za wizi wa kura zinazotumiwa na CCM zabainika; ni hizi hapa

Pre GE2025 Mbinu za wizi wa kura zinazotumiwa na CCM zabainika; ni hizi hapa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
baseless. mwaka 2020 sisi pia tulisimamia uchaguz.sio kwel hakuna aliyelazimishwa. sema nyie vijana hampigag kura. sisi tumekaa pale kituon ni wazee wanaletwa wengine hawez hata kutembea vizur ila anajikongoja anapiga vijana wako zao vijiwen wanachek ball.
 
Hii nondo imetulia.

Siwezi kupoteza muda kushiriki chafuzi. CCM acha iibe, iharibu, kisha wananchi watakapochoka wataamua cha kufanya huko mbeleni wao wenyewe. Lakini CCM kamwe haitoki madarakani kwa chafuzi
Wewe unafikiri wananchi "watachoka" lini , mkuu 'Missile'. Hivi hadi tulipo fikia sasa hivi kweli tunaweza kusema wananchi hawajachoka?

Sasa hivi kinacho kosekana ni njia za kuwapanga na kuwaongoza wananchi hao tu basi ili waifanye hiyo kazi ya kuwaondoa CCM.

Ngoja nieleze kidogo. Haya wanayo fanya CCM sasa hivi tukielekea kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa, wananchi wanajua kila kitu kinacho pangwa na CCM. Wananchi wanajuwa kwamba uchaguzi/uchafuzi huu ni maandalizi ya uchafuzi wa mwakani (uchaguzi mkuu). Hawa wanao pachikwa kwenye nafasi hizi za uongozi huko mitaani ndio wakala wakuu wa kuchafua uchaguzi mkuu kuiwezesha CCM kuendelea. Wananchi wanayajuwa haya, na baadhi yao, ndio hao, kama wewe mnao amua kususia uchafuzi huu wa mwanzo.
Kwa bahati mbaya sana, CCM haijali, tena ndiyo furaha yao kuu kwa wananchi kutojitokeza; kwa sababu hiyo tayari ni njia ya wao kuendelea.

Ina faida gani kujiandikisha na kwenda kupiga kura ikijulikana tayari kuwa CCM ni washindi kwa njia haramu?

Kama kuna faida, moja ni kuwaonyesha CCM kuwa watu hawawataki; pamoja na kura zao kuharibiwa, lakini ukweli huo utakuwa upo wazi mioyoni mwao, na hata machoni mwa watu (hata wakiuficha ukweli huo). Hivi 'guilty consciousness' haiwezi kupunguza, au hata kutia uoga wasifanye baadhi ya maovu yao?

Lakini, tukiachana na hiyo sababu moja hapo juu; baada ya wananchi wengi kujiandikisha na kupiga kura na kura zao kuharibiwa, na wanbanchi hao wakaona ukweli huo. Hivi hatua hii haiwezi kuwa njia nzuri ya kuwapanga na kuwaongoza wananchi kutoka kwa wingi zaidi na kupiga kura wakati wa uchaguzi mkuu; na kuhakikisha kwamba safari hii kura zao watakataa zisichezewe?
Ni njia ipi iliyo rahisi kumshawishi mwananchi kukataa uharibifu wa kura yake; badala ya kutojishughulisha kabisa na kwenda kupiga kura (kususa)!

Mkuu 'Missile of the Nation', ninakuomba ujaribu kuweka fikra zako hapa, ili sote tujaribu kupata njia inayo weza kusaidia kuwa ondoa hawa CCM. Kususia uchaguzi siyo njia sahihi hata kidogo.
 
Hii nchi imeoza sana kwenye masuala ya uchaguzi. Wizi uliofanyika mwaka 2020 umewakatisha tamaa wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapigakura.
Uzuri ni kwamba hawa hawa wanaotumika kuiba baada ya uchaguzi tunaishi nao mitaani na hali ya maisha inapokuwa mbaya kwa sababu ya viongozi waliopata uongozi bila kuwa na sifa na wao wanaathirika. Yaani mtu unapewa kisu unaambiwa jikate mwenyewe na wewe unajikata. Ndiyo maana tunafananishwa na manyani.
 
Mbinu za wizi wa chaguzi zote unafanana mkuu.
Hili ninalielewa vizuri sana mkuu'tpaul', na nikushukuru sana kwa kufanya uchambuzi makini kama ulivyo uweka hapo juu.
Lakini naomba unisome vizuri maana yangu katika bandiko hilo nililo mjibu mkuu 'Erythro'. Sikuwa na maana kuwa kuna njia tofauti kati ya maovu wayafanyayo CCM. Pengine itakusaidia kidogo kunielewa ninacho lenga ukinisoma kwenye majibu niliyo yaweka kwenye bandiko linalo mjibu mkuu 'Missille' ambaye yeye , kama walivyo wengi, mipango yake ni kususia kujiandikisha na kupiga kura; kwa mategemeo tu kwamba siku moja CCM itawaonea huruma waTanzania. Hili kamwe halitatokea.
 
Narudia tena, hatupaswi kulalamika tu bali tuchukue hatua kudhibiti ujinga na uhayawani huo wa CCM....

Wananchi wote tuliokwisha kuchoshwa na kuichukia CCM tunatakiwa, kuhamasishana na kujitoa hata bila kusubiria kulipwa ingalau kwa hiyo siku moja ya uchaguzi kuhakikisha kuwa tunazuia kila mbinu ya wizi wa kura na uchaguzi inayofanywa na hawa hayawani wa CCM...
Nami ninakubaliana na wewe mia kwa mia,kwamba wananchi ndio wenye uwezo wa kuzuia CCM wasifanye uharibifu, na wakati mzuri wa kufanya hivyo ni huu wa uchaguzi wa viongozi.

Toka mwanzo kabisa, 2020, tuli washauri CHADEMA waanze maandalizi ya kuwapa elimu wananchi huko vitongojini/mitaani kwa lengo hili hili, lakini kwa bahati mbaya sana naona ushauri haukukubaliwa, na sasa tupo hapa; hali ikiwa mbaya zaidi hata kuliko ile ya 2020!
 
Mkuu,
Bandiko zuri, umejadili vizuri mbinu za hao wezi.

Swali, je kama nchi tunatokaje hapo tulipofikishwa na hicho kikundi cha wezi kinachoongoza nchi bila ridhaa ya wananchi?!!
Kwa maoni yangu, hii sasa hivi ndiyo ingekuwa ni "MADA KUU" nchi nzima. Na huko ndani ya vyama vya upinzani kwenyewe sasa hivi ingekuwa ni kupanga mikakati ya kuwawezesha wananchi kukataa ujinga unaofanywa na CCM.
 
Hiyo mbinu ya kuletewa matokeo ndio hutumika zaidi. Mnakuta tu mtendaji kabandika matokeo ambayo hata hamjui yametoka wapi
 
baseless. mwaka 2020 sisi pia tulisimamia uchaguz.sio kwel hakuna aliyelazimishwa. sema nyie vijana hampigag kura. sisi tumekaa pale kituon ni wazee wanaletwa wengine hawez hata kutembea vizur ila anajikongoja anapiga vijana wako zao vijiwen wanachek ball.
Kwa hiyo wewe ulishudia nini 2020 nkuu?
 
Ikiwa leo ni siku ya mwisho ya uandikishaji wa watu watakoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, CHADEMA wanahamasisha wananchi wajitokeze kujiandikisha lakini CCM wanaendelea kuimarisha mbinu zao za wizi wa uchaguzi. Kama ulikuwa huju mbinu za wizi wa uchaguzi zinazotumiwa na CCM, hasa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 na hatimaye uchaguzi mkuu mwaka 2020, basi mbinu hizo ni kama ifuatavyo:

1. Ulegezaji wa masharti ya kujiandikisha
Ulegezaji wa masharti ya kujiandikisha uliobuniwa na CCM kwenye uchaguzi wa mwaka huu, haujawahi kutokea. Wameweka mfumo huu ili wawatumie wafuasi na makada wao kujiandikisha mara nyingi kadri iwezekanavyo ili kuongeza idadi ya kura zao na kujishindia uchaguzi kiulani. Kwa mfumo huu, ambao mtu anatakiwa kutaja tu umri na kutia saini kwenye daftari la uandikishaji bila kuhitajika kwanza kutambuliwa na uongozi wa mtaa/eneo husika, CCM wamepiga hatua kubwa sana katika wizi wa uchaguzi wa mwaka huu.

Mtu mmoja anaweza kujiandikisha hata mara 1000 kwenye vituo tofauti. Kwa mwanya huu, makada wa CCM makumi kwa maelfu wanazunguka kila kituo kujiandikisha bila wasiwasi wowote. Kwa mfano makada 700 wa CCM wakijiandikisha kwenye vituo 1000 watakuwa wameongeza idadi ya kura hewa 700,000. Fikiria mgombea wa CCM anakuwa na akiba ya kura hewa 700,000 mgombea wa CHADEMA au wa chama kingine cha upinzani anashindaje kwa mfano?

2. Kuteua makada wa CCM kusimamia uchaguzi
Tume ya uchaguzi huwatumia wakurugenzi wa halmashauri, ambao ni makada maarufu wa CCM kusimamaia uchaguzi. Aidha, wakurugenzi hawa huhusika moja kwa moja kuwateua wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Tukumbuke uchaguzi unapoitishwa, wakurugenzi, huwaalika “wananchi” kutuma maombi ya kusimamia uchguzi. Hapa sasa ndio patamu!

Kinachofanyika katika zoezi hili la uteuzi ni kiinimacho tu. Kabla ya hao wanaoitwa wananchi kuandika barua za kuomba kazi ya muda ya kusimamia uchaguzi, makada wa CCM tayari wanakuwa wameishaelekezwa kuandika baraua kwa wingi sana na kwa kuwa wanafahamika, wakati wa uchambuzi wa majina ya watakaosimamia uchaguzi, 99.99% ya “wananchi” wanaoteuliwa, ni makada wa CCM. 0.01% inayobaki kukamilisha 100% ya wasimamimizi, huwaendea walimu, tena wale ambao ni makada wa CCM. Kwa hiyo, utaona kwamba vituo vya kupigia kura vinakuwa vimesheni makada wa CCM tupu. Hapo sasa nieleze nini zaidi? Si tayari CCM wamejihakikishia ushindi?

3. Kupiga kura baada ya kura
Mwaka 2020, wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, wengi wao wakiwa walimu na makada wa CCM, walishurutishwa na wakurgenzi wa halmashauri kuwapigia kura wagombea wa CCM baada ya zoezi la uchaguzi kukamilika na vituo kufungwa. Katika halmashauri moja nilishuhudia wasimamizi wa vituo wakifungiwa kwenye chumba maalumu ambapo kila mmoja alielekezwa kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa idadi iliyoelekezwa na mkurugenzi wa halmashauri ili kuongeza idadi ya kura.

Timu ya ushindi iliyoteuliwa na mkurugenzi ilikuwa akiwasiliana na wasimamizi wa vituo na kuwauliza kama wagombea wa CCM wameshindwa au kushinda kwa asilimia ngapi. Katika kituo kimoja, mgombea wa CCM alipata 51% ya kura zilizopigwa. Mkurugenzi alikasirika sana akamuagiza msimamizi kuboost hizo kura hadi 99% kwa kuongeza idadi ya kura za mgombea wa CCM bila kupunguza zile za wagombea wa upinzani.

Mbinu hii hutumika pale kunapokuwa na idadi ndogo ya watu waliojiandikisha na idadi ndogo zaidi ikajitokeza siku ya kupiga kura. Hata ikiwa idadi ya “waliopiga kura” itatofautiana na idadi ya waliojiandikisha, potelea mbali (Nape, 2024). Hii mbinu ilitumika zaidi mwaka 2019 baada ya wagombea wote wa CHADEMA kujitoa na kubakiwa wagombea wa CCM na vyama vingine ambavyo ni matawi ya CCM, hivyo kupelekea hata wapiga kura wa CCM kutojitokeza kupiga kura, baada ya wagombea wa chama chao kuwa na uhakika wa ushindi.
View attachment 3130687

Wananchi wakipiga kura kwenye kituo cha kupigia kura (Chanzo: Mtandao)

4. Kuandika idadi bandia ya kura zilizopigwa
Hii ndio ile mbinu aliyoisema Nape Nnauye na ndiyo iliyotumika kwa kiasi kikubwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu wa 2020. Katika mbinu hii, kura zinazopigwa ndani ya vyumba vya kupigia kura hazihesabiwi. Kinachotokea ni kwamba mkurugenzi wa halmashauri, ambaye ni returning officer (RO) hujifungia kwenye chumba na timu yake ya ushindi na kutengeneza kura bandia kwa kila kituo cha kupigia kura (kulingna na idadi ya wapiga kura) akimchuanisha kwa mbali mgombea wa CCM na wagombea wa vyama upinzani.

Kwa mfano, ikiwa kituo A cha kupigia kura kina jumla ya wapigakura 300 na wagombea wa vyama vya CHADEMA, CCM, ACT, CUF na CHAUMA, kura za bandia kwa wagombea zinaweza zikatungwa kama ifuatavyo:

CCM =290
CHADEMA =7
ACT =2
CUF =1
CHAUMA = 0

Mfumo huu wa wizi hutumiwa kwenye kila kituo cha kupigia kura kwa kumpaisha mgombea wa CCM mbali kabisa na wagombea wa vyama vingine. Kwa mfano wa hapo juu, mgombea wa CCM anakuwa ameshinda kwa 96.7%.

Wizi huu hufanikishwa na mtendaji wa kata, ambaye kwa nafasi yake hupewa cheo cha Asisitant Returning Officer (ARO). Watendaji hawa hupita kila kituo na kukabidhi matokeo bandia kwa msimamizi wa kituo kwa kutumia mbinu ya kujificha mahali na kumuita msimamizi aje kuchukua matokeo. Polisi pia hutumiwa kupeleka matokeo kwa wasimamizi.

5. Matumizi ya polisi wanaolinda vituo vya kupigia kura
Aghalabu polisi hutumiwa kuwatoa nje wagombea wa upinzani ili CCM wapate kuingiza kura bandia kwenye masanduku ya kura. Kinachotokea ni kwamba msimamizi wa kituo cha uchaguzi (ambaye ni kada wa CCM) huanzisha ugomvi wa lazima dhidi ya mawakala wa vyama vya upinzani na kisha kuwaita polisi kuja kutuliza ghasia. Polisi wanapokuja huwachota mawakala wa upinzani na kuwapakia kwenye gari, hivyo kumuachia mwanya msimamizi wa kituo kuingiza kura bandia kwenye masanduku.

Baadaye polisi huwaachia huru wale mawakala kurudi ndani ya vyumba vya kupigia kura. Kufuatia, kadhia hii, mawakala wa vyama vya upinzani hugoma kusaini hati za uchaguzi wakati wa kufunga vituo lakini kugoma kwao hakusaidii chochote kwani tayari uchaguzi unakuwa umeibiwa na CCM.

6. Kuwazubaisha mawakala
Wengi wa mawakala wanaosimamia kura za wagombea wa upinzani, huletewa chakula na mgombea husika. Ikiwa mgombea atachelewa kuleta chakula, fedha zilizotolewa na mkurugenzi hutumika kuwanunulia chakula mawakala wote bila kuwabagua kivyama. Wakati mawakala wote wameenda kula, msimamizi wa kituo cha kupigia kura hutumia mwanya huu kuingiza kura bandia kwenye masanduku ya kura. Ikifika muda huu wa kula, wakala wa CCM naye huzuga kuambatana na mawakala wa upinzani kwenda kwenye chakula huku akiwa anafahamu fika mchezo utakaoendelea nyuama ya pazia.

7. Kuwanunua au kuwateka wagombea wa upinzani
Mtindo wa ununuzi wa wagombea wa upinzani hauna haja ya kuueleza hapa kwani kila mtu anafahamu jinsi wagombea wa upinzani wanavyonunuliwa kujitoa kwenye uchaguzi au kupotea siku ya kurudisha fomu.

8. Ulaghai na kuficha taarifa za uchaguzi au taarifa binafsi za wagombea
Aghalabu CCM hutumia mbinu ya kuficha taarifa za uchaguzi kwa kushirikiana na tume ya uchaguzi ambayo huteuliwa na Rais, ambaye naye huwa ni miongoni mwa wagombea. Hii ni sheria ya ajabu kabisa katika nchi hii ya kusadikika.

Katika ngazi ya kata, watendaji wa kata hutumika kuficha fomu za wagombea wa upinzani kwa makusudi au kujificha siku wagombea wa upinzani wanaporejesha fomu. Tukumbuke kuwa watendaji wa kata kwa sasa hivi huajiriwa kwa misingi ya kiitikadi. Watendaji wanaoajiriwa kwenye kata sasa hivi hupangiwa vituo moja kwa moja kutoka makao makuu ya CCM, Dodoma. Kwa hivyo, hawawezi kwenda kinyume na maagizo au maelekezo ya CCM hata siku moja.

N.B: Ikumbukwe kwamba siku chache kabla ya tarehe ya uchaguzi wasimamizi wa vituo vya uchaguzi kwenye kila kata huitwa kupewa semina ya wizi na kiongozi wa ushindi aliyeteuliwa na mkurugenzi wa halmashauri.

Nawasilisha
Well narrated. Tatizo sijui kwa nini CDM wanashindwa kusoma mchezo huo na kuwathibiti wahuni hao.
 
Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho Muda utasema Tusubiri. Na Kila afanyaye siku zake duniani zinahesabika hakuna atakaye dumu
 
Safari hii patachimbika
Tumesubiri sana tuone palipochimbika lakini wapi. Maneno mengi vitendo zero, wakati wahuni wanafanya kweli na mnabaki kupiga kelele tu. Viongozi wa CDM wanatekwa badala na nyie kufanya kweli kuwathibiti wahuni mnabaki kupiga kelele kwenye majukwaa.

Siku CDM mkiamua utashangaa wananchi wengi watakaoungana na nyie. 2015 wananchi waliamua na wakawa tunawasubiri CDM mseme kitu ili shughuli ianze mkajifanya waungwana na white hair wenu.
 
Tatizo sijui kwa nini CDM wanashindwa kusoma mchezo huo na kuwathibiti wahuni hao.
Jibu lipo kwenye namba 5 mkuu.
Kwa mujibu wa maelezo ya mtoa mada, polisi hutumika kifanikisha wizi kwa shuruti.
👇
5. Matumizi ya polisi wanaolinda vituo vya kupigia kura
Aghalabu polisi hutumiwa kuwatoa nje wagombea wa upinzani ili CCM wapate kuingiza kura bandia kwenye masanduku ya kura. Kinachotokea ni kwamba msimamizi wa kituo cha uchaguzi (ambaye ni kada wa CCM) huanzisha ugomvi wa lazima dhidi ya mawakala wa vyama vya upinzani na kisha kuwaita polisi kuja kutuliza ghasia. Polisi wanapokuja huwachota mawakala wa upinzani na kuwapakia kwenye gari, hivyo kumuachia mwanya msimamizi wa kituo kuingiza kura bandia kwenye masanduku.

Baadaye polisi huwaachia huru wale mawakala kurudi ndani ya vyumba vya kupigia kura. Kufuatia, kadhia hii, mawakala wa vyama vya upinzani hugoma kusaini hati za uchaguzi wakati wa kufunga vituo lakini kugoma kwao hakusaidii chochote kwani tayari uchaguzi unakuwa umeibiwa na CCM.
 
Jibu lipo kwenye namba 5 mkuu.
Kwa mujibu wa maelezo ya mtoa mada, polisi hutumika kifanikisha wizi.
👇
Wizi wa kura ni mchakato (process) kama alivyosema mtoa hoja.

CDM walitakiwa wapinge kwa nguvu zote utaratibu mbovu na wa kihuni na kanuni zake wakati wa kujiandikisha kwenye daftari. Wapiga kura wengi wana vitambulisho kwa nini mtu haombwi uthibitisho wowote (Kitambulisho cha kura, taifa, leseni, kadi ya benki etc) wa kuthibitisha kuwa anayeandikisha ndo mwenye jina halisi.

Pili kwa nini CDM hawakukomaa ili daftari la wapiga kura linalotumika uchaguzi mkuu, hilo ndo liboreshwe na litumike kwenye kupiga kura badala ya utaratibu wa hovyo na wa kihuni uliofanywa safari hii.
 
Back
Top Bottom