Mboga zangu 5 simple nizipendazo kulia chakula (hasa ugali) na Jinsi ninavyoziandaa

Mboga zangu 5 simple nizipendazo kulia chakula (hasa ugali) na Jinsi ninavyoziandaa

Ni mazoea mabaya sana kupenda kula mayai kwa wingi na mara kwa mara!

Ni kwa bahati mbaya sana kwenye jamii ama hawana ufahamu juu ya maswala ya lishe salama au wengine wanafahamu athari ya kula mayai mengi mara kwa mara lakini wanapuuza miiko!
Mkuu kuna madhara gani kula mayai ya kienyeji mbona sijawahi sikia boss?!
 
Mimi ni moja ya wale wajuba wasiopenda kula mitaani iwe hotel,cafe,bar,pub,nk sehemu yeyote wanayotoa huduma ya chakula sio mpenzi wa kula sehemu hizo na hii n kwasababu sipendi pikiwa chakula nisichojua kimeandaliwaje,kimepikwa ktk hali gani,nk nk (sababu ni nyingi).

Mimi ni moja ya watu ambao huchelewa sana kurudi nyumbani kutokana na kazi zangu lakini hii hainifanyi niache kupika kwasababu moja ya vitu nivipendavyo chini ya jua basi kupika ni mojawapo ya vitu hivyo.

Unajua kuna watu humu tunawasiliana sana huwa nikirudi home naweza mwambia ngoja nipike kidogo basi wanaishia kucheka na kuniona muongo sazingine wananikubalia ila hawaniamini kbsa kama napika.

Leo nataja mboga zangu pendwa ninazo penda zipika ninapokua nimerudi home,hizi ni baadhi tu ya zile za chap chap ambazo ndani ya dk.10-20 nishaivisha mzigo upo mezani tyr kuelekea tumboni.

1. Mboga ya nyanya

Hii mboga naiita hivi kutokana nyanya ndio kitu pekee kilichotawala hii mboga.

Mahitaji yangu ni:
  • Nyanya
  • Hoho
  • Kitunguu maji
  • Kitunguu swaum (hiki hakikosekan kwenye friji huwa kipo standby maana hamna mboga napka ikose hii kitu hakuna)
  • Tangawizi (niliyoparua) hiii pia ipo standby kwa friji haikosekani maana naitumia ktk kila kitu ninachopka chini ya jua
  • Karot (nakwangua kdg na nyingine nakata kata)
  • Viungo vya pilau (vilivyosagwa)
  • Pilipili mbichi
Huo mchanganyiko naanza kuupika kama mboga zingine naanza kitunguu maji ilaa sisubri mpk ktunguu kiwe brown nakoroga in 1min natia tangawizi,nakoroga naleta karoti zangu zile zakukata kata + hoho (naweka pamoja) nafunikia kama dk kadhaa nakuja naweka nyanya + karoti zile zakukwangua naweka pamoja nakoroga then nafunika baada ya muda kidogo nakuja namalizia kile kitunguu swaum changu na viungo vya pilau masala+ ile plipli yangu kisha nakoroga mboga naifunikia, in 5min nikifunua nikipga mwko kona mbili tatu linatoka sotojo moja tamu sana. Chumvi mimi huwa nawekaga kule mwanzo kabisa wakati wakukaanga vitunguu.

Hii mboga nakulaga nayo ugali mkubwa hata mtto mdogo anaweza asivuke. (ni tamu sana na ni simple sana)

2. Mboga ya Mayai

Hii mboga ya mayai nadhani n mboga ninayoila sana chini ya jua kuliko mboga zingine nadhani n kwasababu ya utamu wake na addiction yangu na mayai kwakweli hata kama n kitambi nahisi hii mboga ndio chanzo cha kitambi.

Mahitaji

Ni yale yale na vile vile kama hapo juu kwenye mboga ya nyaya ila ninapopika mboga ya mayai huwa siweki masala za pilau so ktk mahtaji ondoa pilau masala ila vingine vyote viache kama vilivyo.

Jinsi yakuipika hiii kuna style zangu mbili ambazo napenda

style 1

Nikishaandaa mboga yangu kama nilivyoandaa mboga ya nyanya pale juuu ikiwa jikoni navunjia mayai yangu idadi ninayojiskia kisha nakoroga mpk yale mayai yaive mchuzi wa nyanya nao ukauke.Mboga tyr.

style 2

Napika mboga yangu kama mboga ya nyanya kule juu ila ikifka muda wa kuweka mayai,nakaanga pembeni mayai yangu yenyewe kama yenyewe yakiwa tyr nayaweka kwenye sahani nayakata vipende vidogo vidogo kisha vile vipande vyote namwagia kwenye ile mboga yangu,inakua kama nakula nyama mzeee kumbe n vipisi vya mayai,daah tamu sana na ugali.

3. Dagaa

Bana mimi ni moja ya wale raia ukiwalisha dagaa kila siku ndani ya wiki/mwezi/mwaka mzma hawachoki wala kukinai kila siku hii mboga n kama mpya kwangu kutokana na mapenzi yangu kwa dagaa nmejikuta jikon dagaa hawakauki ila sasa dagaa wengi walio tyr n wale wa mwanza wale wanaokua tyr wamekaangwa.

Mahitaji

  • Nyanya 1
  • kitunguu maji
  • karoti (zakukata kata + za kukwangua)
  • hoho
  • kitunguu swaum
  • tangawizi
  • pilipili
Wakati wakupka kama kawaida naanza na kitunguu changu maji,sisubr kiwe brown naweka karot + hoho nakoroga then nakuja naweka dagaa zangu + ile karot ya kukwangua kwa pamoja na pili pili yangu nakoroga mpk viungo vyangu karot na hoho nione vinakarbia iva kisha mwsho namalizia na ile nyanya yangu 1,nyanya hii nmeiweka mwsho mana haihelewi kuiva nikipga mwko mizunguko miwili mitatu mzgo unatoka unameremeta kbsa. Mboga tyr kuliwa na chakula cha siku hyo.

4. Kachumbari

Mahitaji
  • Nyanya mbichi 1
  • Kitunguu maji
  • Karoti
  • Hoho 1
  • Tango
  • Parachichi 1
  • Limao
  • Pilipili

maandalizi n simple kama yeyote anavyoweza andaa basi ikikamilika namix safi kabsa kitu tyr kuliwa na chakula cha siku husika.

5. Mtindi

Hiii kwangu husimama kama mboga na mara zingine husimama kama chakula kbsa maana kuna siku nakunywa nalala yani friji ikose kila kitu ila sio pakti ya mtindi.

Hizi ni zile za chap chap ambazo at any time naweza ziandaa mtu akala chakula akahisi kala 5 star hotel kwasababu sio masihara msosi ninaopenda kuula huwa najua upika kwa ustadi ule unaokidhi vigezo vyote kuliwa na raia mwenye njaa yake mjini.
Uko vizuri mkuu Mimi napenda kula ila kupika ndo kasheshe ile gesi mtungi mdogo huwa unakaa hata miaka miwili nisipopata mtumiaji huwa siitumii
 
Hapo chini ni list ya baadhi ya mbogamboga, we inaonyesha unapendelea nyanya na kitunguu zaidi.😜

Nyanya,
Kitunguu,
Hoho
Pilipili
Tango
Ndimu
Tembele
Kabichi
Mchicha
Mnafu
Bamia
Ngogwe
Biringanya
Chegere
Harage bichi
Chinese cabage
Sukuma wiki
Etc
 
Napenda sana kujipikia ndizi mshare na nyama. Kingine ni wali na maharage ya nazi 🤭
zamani hizo niko chini ya himaya ya wazazi hamna chakula nilikua sipendi kula kama ndizi,mpk naondoka nyumbani kila mtu anajua sipendi ndizi,lakini sasa hivi sijui ni maisha sijui nini ila nilijaribu jifunza pikaa ndizi tangu hapo hadi leo ndizi ni one of my favourite food.

hasa zikiwa za nazi na zaidi nizipike mwenyewe,nilimpkia mama angu 1st day ananitembelea kwangu tangu nitoke home alifurahi na hakuamini alihisi ni ndoto. Ndizi tamu sana na ndio mana ni moja ya vyakula gharama ktk kuvipika ili vitoke vitamu.
 
Hivi Kuna kitu gani najua kupika zaidi ya chai!! Tena sometime huwa chai inakuwa na mabuja sijui yanatokeaga wapi!.. wataalum hebu nijulisheni hili nakosea wapi
Utakua hauko serios mkuu,chai au uji?!
 
Uko vizuri mkuu Mimi napenda kula ila kupika ndo kasheshe ile gesi mtungi mdogo huwa unakaa hata miaka miwili nisipopata mtumiaji huwa siitumii
zamani hizo nilinunua jiko la gesi ila niilikua nalitumia kuchemshia maji ya kuoga tu lkn baadae niliona ni ujinga nikaanza jifunza kupika na msosi wangu wakwanza pika ni CHIPS japo nilipika kau kau chipsi ila mwanzo mgumu.
 
zamani hizo nilinunua jiko la gesi ila niilikua nalitumia kuchemshia maji ya kuoga tu lkn baadae niliona ni ujinga nikaanza jifunza kupika na msosi wangu wakwanza pika ni CHIPS japo nilipika kau kau chipsi ila mwanzo mgumu.
Kupika najua ila muda na kampani ndo shida
 
Hapo chini ni list ya baadhi ya mbogamboga, we inaonyesha unapendelea nyanya na kitunguu zaidi.😜

Nyanya,
Kitunguu,
Hoho
Pilipili
Tango
Ndimu
Tembele
Kabichi
Mchicha
Mnafu
Bamia
Ngogwe
Biringanya
Chegere
Harage bichi
Chinese cabage
Sukuma wiki
Etc
sili wala sigusi wala kukaribia

hoho
nyanya chungu(ngogwe)
bamia (mlenda kwa ujumla)
biringanya

hizo vitu sigusi kabisa lakini naweza kupika kitu ambacho siwezi pika wala sitokaa nitake kupika ni mlenda,lakini hizo ngogwe,bamia,biringanya kichanganya pamoja ukapika ni mboga ambayo mama angu mzazi anaipenda sana kula na ugali.

ninapopata mgeni nyumbani nikipka dagaa huwa naweka ngogwe au biringanya lakini kwenye kula nampakulia vyote mgeni mimi nakula dagaa tupu.

napenda mboga zote za majani kasoro majani ya maboga (sijawahi yaelewa kila nikijahdi kuyaelewa inakataa)
 
Back
Top Bottom