nergomafioso
Senior Member
- Apr 3, 2024
- 109
- 284
Mimi kama kijana ninaye jitafuta bado ninaishi na mama yangu mzazi pamoja na mdogo wangu ambaye kwa sasa yupo kidato cha nne, dada yangu wa kwanza ameolewa yupo na familia yake yeye kaniacha miaka 6 ndio nikafuatia na mimi nimemuacha mdogo wangu wa mwisho kwa miaka 10.
Katika swala la maadili nashukuru mungu uyu bi mkubwa alijitahidi kutuweka kwenye mstari na alikuwa mkali mno unapoenda kinyume na matakwa yake, mkono ulihusika ili kuhakikisha tunakaa kwenye mstari sababu sisi wote tumelelewa bila ya baba, angalau mimi mshua kidogo alikuwa na nafasi nzuri kielimu na kiuchumi ila sikuwahi kupata walau malezi upande wa baba tulikuwa tukionana nilipokuwa mdogo kama na umri wa miaka kama 8-9 kushuka chini ila sikuwahi kujua kwanini hatuishi na baba.
Ukiwa mdogo sometimes na malezi niliyolelewa sikuwa mtu wa kujudge mambo kwa upana wake niliishia kuliacha hewani tu lipite as long as napata mahitaji yangu ya msingi ayo mengine watajua wenyewe.
Chekechea nilisoma shule za kulipia ila sikuwa na moment nzuri kabisa upande ule kwasababu ya lifestyle niliyokuwa nayo na shule uzungu ulikuwa mwingi mnoo nakutana na vitoto vya kishua, tambo zao na majivuno yakanifanya niingize miss kidogo na kucompare na maisha ya nyumbani ambapo kipindi hicho mama ni personal secretary wa wa wakili flani maarufu kidogo mkoani hapo na mdingi sikuwa najua kazi yake nikimuuliza mama ananijibu kwa utani mara kada wa ccm, mara aniambie tapeli basi shida tupu.
Mzee mwenyewe akija na kigari chake akiniletea na vizawadi nasahau maswali yangu yote naishia kufurahi tu na namuacha aende bila kunipa majibu ya kueleweka ya maswali yangu.
Kimbembe nikienda uko shule tulikuwa na kipengele cha kujitambulisha mwenyewe pamoja na wazazi wako na wadhifa wao apo ndo nakuwa na kiwewe na kukosa jibu zuri la kuwapa sababu nilikuwa naogopa sana kusema uongo kwahiyo ikifika sehemu ya kuwatoa wasifu wa wazazi upande wa mama ntatiririka vizuri tu ila ukifika upande wa mzee ntaishia kutaja majina yake na kabila tu maswali yanayofuata ningekaa kimya tu sasa ile kitu ilikuwa inawachekesha wanafunzi wenzangu na kuonekana sijui ilikuwa inanikata sana na kidogo kidogo nikaanza kuichukia shule. Jambo ambalo sitokuja kusahau mpaka uzee wangu kipindi hicho nasoma utaratibu ulikuwa kama shule nyingine tu za kawaida kwamba ukihitaji kwenda chooni unapaswa kuomba ruhusa kwa mwalimu husika anayefundisha tena kwa lugha ya kingereza "please teacher may i go out?" Mwalimu akikubali unaenda kiroho safi akigoma inabidi utulize mshono mpaka muda wa mapumziko.
Kuna kitoto kilikuwa kinaitwa Recho kina asili ya kiarabu na kaumbo kadogo ila kalikuwa kajanja sana chenyewe kanaweza kwenda chooni hata x2 kabla ya kengele ya break kugonga kalikuwa kanaomba ruhusa kama mara 3-5 mwalimu akigoma utashanga kimtu kimechomoka nduki hicho bila ruhusa kikirudi pale mwalimu akianza kugomba kanajua kujieleza na kiasi chake upande wa ngeli kaliijua si haba basi mwalimu mwenyewe atasanda.
Shida ilianzia hapo sielewi ni uoga tu au kuna kitu kilikuwa kinanisumbua ila mpalianda nilikuwa nikiomba ruhusa ninyimwe naogopa kutoka darasani ata kama mkojo umenibana to the maximum mi nilikuwa naendelea kuomba ruhusa mpaka nikubaliwe na mwalimu akikataa basi nitaishia kuomba mpaka mkojo unatoka nimekaa hapo hapo kwenye kiti mwalimu mdadisi ndiye angejua kama ichi kitoto kinakaribia kushusha mzigo maana sauti inabadilika kadri uvumilivu ulivyo nishinda, ningekibinya Kibamia kwenye kaptura mwishoe kojo lingenitoka hapo hapo kwenye kiti na ruhusa ndo zingekomea hapo na kujiandaa kwa aibu mpya🥺
Tulikuwa tunatumia viti vidogo vya plastic size kama ile wanayo tumia kutengeneza ma pot ya kujisaidia watoto wadogo miaka ya sasa, nikishajikojolea hapo ningeuchuna kimya mpaka wambea wa darasa waniripoti kwa mwalimu.
Nae mwalimu angeishia kunisema na kumtolea mifano Recho mtoto mdogo ananizidi akili hii kitu iliniumiza sana na tukio lilijirudia mara 2 ndani ya muda tofauti na ni tukio limeacha alama kwenye maisha yangu sababu shule ilipo na nyumbani umbali haukuzidi 2 km kwahiyo sikuwa napanda school bus asubuhi nilikuwa naenda na mmaza anapoenda kazini ila mchana hakukuwa na haja ya kufatwa na dada wa kazi sababu tulikuwa wanafunzi wengi tunatembea kwa miguu mpaka nyumbani wanaotoka mbali ndio walilipiwa usafiri na wazazi wao.
Kwahiyo ninapojikojolea ilinipasa kutembea hivyo hivyo mpaka nyumbani na hiyo siku wenzangu wangenitenga na kutembea la mmoko kama Rambo yupo vitani njiani nilikuwa nakutana na bullying kutoka kwa watu mbalimbali na maoni hasi juu yangu iliniumiza sana na ikanifanya niichukie shule kabisa ikifika asubuhi nakuwa mtata sana kwenye suala la kwenda shule bila sababu ya msingi.
Namshukuru mungu upande wa taaluma nilikuwa vizuri na niliwanyoosha haswa hao watoto wa vibopa sababu ya uelewa niliokuwa nao na nilikuwa miongoni mwa watoto ambao wangepewa nafasi ya kufanya presentation tunapoenda kwenye ziara za shule kama redioni au kwenye maonyesho mbalimbali ila sikuwahi kuwa proud na hiyo kitu mpaka nimemaluza ile shule na kuingia darasa la kwanza nikiwa na umri wa miaka 7 ndo nakutana na viyande wenzangu watoto wa walala hoi katika shule ya kayumba...
Itaendelea chapter 2
www.jamiiforums.com
Katika swala la maadili nashukuru mungu uyu bi mkubwa alijitahidi kutuweka kwenye mstari na alikuwa mkali mno unapoenda kinyume na matakwa yake, mkono ulihusika ili kuhakikisha tunakaa kwenye mstari sababu sisi wote tumelelewa bila ya baba, angalau mimi mshua kidogo alikuwa na nafasi nzuri kielimu na kiuchumi ila sikuwahi kupata walau malezi upande wa baba tulikuwa tukionana nilipokuwa mdogo kama na umri wa miaka kama 8-9 kushuka chini ila sikuwahi kujua kwanini hatuishi na baba.
Ukiwa mdogo sometimes na malezi niliyolelewa sikuwa mtu wa kujudge mambo kwa upana wake niliishia kuliacha hewani tu lipite as long as napata mahitaji yangu ya msingi ayo mengine watajua wenyewe.
Chekechea nilisoma shule za kulipia ila sikuwa na moment nzuri kabisa upande ule kwasababu ya lifestyle niliyokuwa nayo na shule uzungu ulikuwa mwingi mnoo nakutana na vitoto vya kishua, tambo zao na majivuno yakanifanya niingize miss kidogo na kucompare na maisha ya nyumbani ambapo kipindi hicho mama ni personal secretary wa wa wakili flani maarufu kidogo mkoani hapo na mdingi sikuwa najua kazi yake nikimuuliza mama ananijibu kwa utani mara kada wa ccm, mara aniambie tapeli basi shida tupu.
Mzee mwenyewe akija na kigari chake akiniletea na vizawadi nasahau maswali yangu yote naishia kufurahi tu na namuacha aende bila kunipa majibu ya kueleweka ya maswali yangu.
Kimbembe nikienda uko shule tulikuwa na kipengele cha kujitambulisha mwenyewe pamoja na wazazi wako na wadhifa wao apo ndo nakuwa na kiwewe na kukosa jibu zuri la kuwapa sababu nilikuwa naogopa sana kusema uongo kwahiyo ikifika sehemu ya kuwatoa wasifu wa wazazi upande wa mama ntatiririka vizuri tu ila ukifika upande wa mzee ntaishia kutaja majina yake na kabila tu maswali yanayofuata ningekaa kimya tu sasa ile kitu ilikuwa inawachekesha wanafunzi wenzangu na kuonekana sijui ilikuwa inanikata sana na kidogo kidogo nikaanza kuichukia shule. Jambo ambalo sitokuja kusahau mpaka uzee wangu kipindi hicho nasoma utaratibu ulikuwa kama shule nyingine tu za kawaida kwamba ukihitaji kwenda chooni unapaswa kuomba ruhusa kwa mwalimu husika anayefundisha tena kwa lugha ya kingereza "please teacher may i go out?" Mwalimu akikubali unaenda kiroho safi akigoma inabidi utulize mshono mpaka muda wa mapumziko.
Kuna kitoto kilikuwa kinaitwa Recho kina asili ya kiarabu na kaumbo kadogo ila kalikuwa kajanja sana chenyewe kanaweza kwenda chooni hata x2 kabla ya kengele ya break kugonga kalikuwa kanaomba ruhusa kama mara 3-5 mwalimu akigoma utashanga kimtu kimechomoka nduki hicho bila ruhusa kikirudi pale mwalimu akianza kugomba kanajua kujieleza na kiasi chake upande wa ngeli kaliijua si haba basi mwalimu mwenyewe atasanda.
Shida ilianzia hapo sielewi ni uoga tu au kuna kitu kilikuwa kinanisumbua ila mpalianda nilikuwa nikiomba ruhusa ninyimwe naogopa kutoka darasani ata kama mkojo umenibana to the maximum mi nilikuwa naendelea kuomba ruhusa mpaka nikubaliwe na mwalimu akikataa basi nitaishia kuomba mpaka mkojo unatoka nimekaa hapo hapo kwenye kiti mwalimu mdadisi ndiye angejua kama ichi kitoto kinakaribia kushusha mzigo maana sauti inabadilika kadri uvumilivu ulivyo nishinda, ningekibinya Kibamia kwenye kaptura mwishoe kojo lingenitoka hapo hapo kwenye kiti na ruhusa ndo zingekomea hapo na kujiandaa kwa aibu mpya🥺
Tulikuwa tunatumia viti vidogo vya plastic size kama ile wanayo tumia kutengeneza ma pot ya kujisaidia watoto wadogo miaka ya sasa, nikishajikojolea hapo ningeuchuna kimya mpaka wambea wa darasa waniripoti kwa mwalimu.
Nae mwalimu angeishia kunisema na kumtolea mifano Recho mtoto mdogo ananizidi akili hii kitu iliniumiza sana na tukio lilijirudia mara 2 ndani ya muda tofauti na ni tukio limeacha alama kwenye maisha yangu sababu shule ilipo na nyumbani umbali haukuzidi 2 km kwahiyo sikuwa napanda school bus asubuhi nilikuwa naenda na mmaza anapoenda kazini ila mchana hakukuwa na haja ya kufatwa na dada wa kazi sababu tulikuwa wanafunzi wengi tunatembea kwa miguu mpaka nyumbani wanaotoka mbali ndio walilipiwa usafiri na wazazi wao.
Kwahiyo ninapojikojolea ilinipasa kutembea hivyo hivyo mpaka nyumbani na hiyo siku wenzangu wangenitenga na kutembea la mmoko kama Rambo yupo vitani njiani nilikuwa nakutana na bullying kutoka kwa watu mbalimbali na maoni hasi juu yangu iliniumiza sana na ikanifanya niichukie shule kabisa ikifika asubuhi nakuwa mtata sana kwenye suala la kwenda shule bila sababu ya msingi.
Namshukuru mungu upande wa taaluma nilikuwa vizuri na niliwanyoosha haswa hao watoto wa vibopa sababu ya uelewa niliokuwa nao na nilikuwa miongoni mwa watoto ambao wangepewa nafasi ya kufanya presentation tunapoenda kwenye ziara za shule kama redioni au kwenye maonyesho mbalimbali ila sikuwahi kuwa proud na hiyo kitu mpaka nimemaluza ile shule na kuingia darasa la kwanza nikiwa na umri wa miaka 7 ndo nakutana na viyande wenzangu watoto wa walala hoi katika shule ya kayumba...
Itaendelea chapter 2
Mbona kama mama kanilengesha kwa huyu binti! Ndo tulipofikia huku
Mimi kama kijana ninaye jitafuta bado ninaishi na mama yangu mzazi pamoja na mdogo wangu ambaye kwa sasa yupo kidato cha nne, dada yangu wa kwanza ameolewa yupo na familia yake yeye kaniacha miaka 6 ndio nikafuatia na mimi nimemuacha mdogo wangu wa mwisho kwa miaka 10. Katika swala la maadili...