Mbona kila nikiangalia 'Clip' ya Manara akishangilia Ushindi wa Yanga SC Kwake jana nao Furaha yake ni ya Kujilazimisha tu?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"Mwanangu Haji Manara na Mdogo wake wa mwisho wa Kike ndiyo wana Simba SC kindakindaki tokea wakiwa Wadogo ndani ya Familia yangu wakiwa wamemfuata Bibi yao Mzaa Baba ambaye alikuwa ni mwana Simba SC hakuna mfano" amesema Mzazi wa Haji Manara Mzee Manara alipohojiwa na EFM Radio mwaka 2022.

Halafu niulizieni kwa Haji Manara je, ameacha tabia yake ya kuwapigia Simu Wachezaji wa Simba SC (hasa Nahodha Tshabalala, Muzamiru na Rafiki yake mkubwa Kipa Manula) kuwalalamikia kama wakiwa wanapata Matokeo mabaya na huku akiwapongeza pale wakifanya vyema huku akijijua Yeye ni mwana Yanga SC?
 
Unapotoa post kama hii alafu hakuna clip..ni ujinga .
🚮🚮🚮
 
Mmmmmm ajira kakaa.....na njaa iko kichwani acha asogeze siku umri nao....umesonga....
 
Huyu jamaa alikuwa kwenye BAN ama?! Naina tulipumzika na pumba humu jamvini
 
Hizo pigo ni za mademu wa uswazi, watoto wa kiume huwa hawana tabia za umbea umbea. Ulikosa namba ya Manara ukampigia simu ukamuuliza hayo maswali
Aliyekuambia huyo mwanaume ni nani? Huyo ni demu wa kinyarwanda anajifanya tom boi
 
Mnateseka sana na manara yupo sana yanga na tunaimani Naye.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…