Mbona Waziri Dorothy Gwajima yupo kimya sakata la Pauline Gekul?

Mbona Waziri Dorothy Gwajima yupo kimya sakata la Pauline Gekul?

We nae sijui wa wapi wewe, Rais asingemtumbua huo uchunguzi ungefanyikaje? Uliwahi kusikia waziri anachunguzwa na kushtakiwa

Sasa hivi tu katumbuliwa ila RPC akiongea anamuita muheshimiwa na body language Inaonekana kabisa ameegemea upande gani huyo RPC

Kuendelea kumuacha akiwa waziri na mbunge ni kusababisha kuharibu hii kesi na kumlalia Hashim
Nijuavyo mimi ni Rais tu ndiye hawezi kushitakiwa (Sasa hivi ninasikia wameongezeka Spika, CJ, n.k.)

Maana yake wengineo wote (akiwemo NW) wanashitakika and so wanaweza kuchunguzwa vizuri kabisa hata wakiwa na nyadhifa zao.

Hiyo aya ya mwisho ninafikiri ni mahakama tu ndiyo inapaswa kuthibitisha. Otherwise, haumtendei haki. Tuhuma zinapaswa kuthibitishwa kabla ya kuanza kumshushia hizi nyuzi.

Siku moja nawe utatuhumiwa (bila kujali una hatia) halafu jamii nzima ikuhukumu, ndipo utajua umuhimu wa presumption of innocence mpaka mahakama iamue vinginevyo. That's karma.
 
Waziri hupaswi hata kutuhumiwa, ni vile tu viongozi wa Kiafrika hukaza mafuvu sababu ya kiburi na uchu wa madaraka wa kutokujiwajibisha

Mahakama ikimsafisha ataweza kupewa dhamana ya uongozi tena...
Usafishaji wa mahakama unakuja baada ya presumption ya innocence yake. Nyuzi zenu humu zipo kimhemuko sana. JF imekuwa ya vilaza siku hizi.
 
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum mbona upo kimya sana kuhusu hili sakata la Naibu waziri wa katiba na sheria Pauline Gekul?

Dorothy Gwajima hujawahi kukaa kimya kiasi hiki linapotokea jambo la kuzalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia kiasi cha kijana mdogo kuingiziwa chupa sehemu ya haja kubwa na Naibu waziri!

Dorothy Gwajima kama uliweza kujitokeza kwa mbwembwe za hali ya juu na kuwananga na kuwasema walimu eti kisa tu wameruhusu kuucheza wimbo wa Zuchu wa Honey. Mbona hili jambo la Gekul umekaa kimya kama vile hulioni?

Wewe huwa unajinasibu kuwa unapinga sana unyanyasaji wa kijinsia na hupendi kuona raia akifanyiwa kitendo cha kinyanyasaji. Sasa mbona hili la Gekul umekausha kimyaaaaa?

Zile mbwembwe zako za kwenye media hasa linapotokea jambo lolote la unyanyasaji wa kijinsi mbona kwa Gekul hatukuoni!

Mbona hutoi matamko yako ya mbwembwe nyingiiiiiiiiiiiiiiii kama tulivyokuzoea!

Kuna siri gani kati yako na Pauline Gekul mpaka "umeufyanta"?
Nadhani yuko kimya sababu suala lipo ktk mikono ya Police, asije akaharibu upelelezi.
 
Rahisi ❌️
Rais ✅️

Kama kuandika tu ni shida, comment yako haishangazi.
Yes, nimekosea nakubali. Lakini huo ndio ukweli na ndivyo katiba yetu ilivyo. Imempa madaraka makubwa raisi ya kufanya hivyo. Kuteua na kutengua anavyojisikia wale aliowateua bila hata kutoa sababu. Wengine utasikia watapangiwa majukumu mengine ila huyu sababu haikutajwa na huo mstari wa atapangiwa majukumu mengine haukuwepo.
Hivyo upende au usipende, ndivyo ilivyo.
 
Right to presumption of innocence until the court proves otherwise. Ninashangaa Samia ametumia kigezo gani kumtumbua! Sifa za kijinga na mob psychology zinatuharibu Watanzania.
Kiongozi hupaswi kutuhumiwa au ata kuhisiwa kuwa unafanya jambo la utovu wa kimaadili.Yeye Gekul kama alikuwa na ushahidi yule dogo anapanga kumuua angeripoti kwenye vyombo vya usalama.Unakuaje Naibu Waziri wa sheria alafu unakuwa namba moja kuvunja sheria!
Kama yule dogo angekufa mbele yake Gekul,ungekuja hapa na huu utetezi?

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Huyo Gekul hakubaliki hata hapa babati huwezi kuleta bifu na mamalishe yeye ndio alilianzisha na atalinywa zitaletwa Hadi picha hapa akiwa na Serengeti boys sa hv ni kuwalipua tu tumechoka sasa
 
Double standard.
Dkt. Gwajima D
Please.
Sidhani kama mfumo wa kiuongozi unamruhusu Waziri kutolea tamko tukio lililofanywa na Waziri mwenzake. Hivyo msitegemee tamko lolote lile kutoka kwake. Kuna kitu kinaitwa collective responsibility. Ndicho kitakachomzuia kuongea chochote kumhusu Waziri mwenzake.

Na isitoshe hilo suala lenyewe tayari lipo kwenye vyombo vya dola(polisi) kwa ajili ya uchunguzi. Hivyo hao ndiyo wenye mamlaka na jambo hilo kwa sasa.
 
Kiongozi hupaswi kutuhumiwa au ata kuhisiwa kuwa unafanya jambo la utovu wa kimaadili.Yeye Gekul kama alikuwa na ushahidi yule dogo anapanga kumuua angeripoti kwenye vyombo vya usalama.Unakuaje Naibu Waziri wa sheria alafu unakuwa namba moja kuvunja sheria!
Kama yule dogo angekufa mbele yake Gekul,ungekuja hapa na huu utetezi?

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
Ninakubaliana na wewe. Na kwa kuwa viongozi wetu wote, kuanzia CCM hadi upinzani, wana tuhuma za kutosha sote kwa umoja wetu tupaze sauti waachie nafasi zao za madaraka... Tusimng'ang'anie Gekul pekee.
 
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum mbona upo kimya sana kuhusu hili sakata la Naibu waziri wa katiba na sheria Pauline Gekul?

Dorothy Gwajima hujawahi kukaa kimya kiasi hiki linapotokea jambo la kuzalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia kiasi cha kijana mdogo kuingiziwa chupa sehemu ya haja kubwa na Naibu waziri!

Dorothy Gwajima kama uliweza kujitokeza kwa mbwembwe za hali ya juu na kuwananga na kuwasema walimu eti kisa tu wameruhusu kuucheza wimbo wa Zuchu wa Honey. Mbona hili jambo la Gekul umekaa kimya kama vile hulioni?

Wewe huwa unajinasibu kuwa unapinga sana unyanyasaji wa kijinsia na hupendi kuona raia akifanyiwa kitendo cha kinyanyasaji. Sasa mbona hili la Gekul umekausha kimyaaaaa?

Zile mbwembwe zako za kwenye media hasa linapotokea jambo lolote la unyanyasaji wa kijinsi mbona kwa Gekul hatukuoni!

Mbona hutoi matamko yako ya mbwembwe nyingiiiiiiiiiiiiiiii kama tulivyokuzoea!

Kuna siri gani kati yako na Pauline Gekul mpaka "umeufyanta"?

---
Pauline Gekul ambaye ni Mbunge wa Babati Mjini anatuhumiwa kumfanyia unyanyasaji vijana wawili ambapo inadaiwa akishirikiana na watu wengine waliwadhuru mwili na kumuingiza chupa sehemu ya haja kubwa ili wakiri kutumwa kufanya uhalifu. Zaidi soma Naibu Waziri na Mbunge Pauline Gekul adaiwa kumfanyia Ukatili wa Kimwili Mtoto

Saa chache baada ya habari kusambaa kuwa Pauline Gekul amefanya uhalifu, Rais Samia alitengua uteuzi wake wa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, lakini barua ya Ikulu haikuelezea sababu ya utenguzi wake. Zaidi soma Rais Samia atengua uteuzi wa Pauline Gekul saa chache baada ya kutuhumiwa kufanya unyanyasaji kwa mtoto

Baada ya Pauline Gekul kutenguliwa, wanaJF walisema asiishie hatua hiyo bali anatakiwa kuvuliwa uanachama na kufikishwa mahakamani. Zaidi soma Pauline Gekul anastahili kuvuliwa uanachama na kufikishwa mahakamani haraka sana. Amekichafua na kukipaka matope chama


Habari nyingine soma viunganishi hapa chini
Anasoma upepo kwanza!!
 
Yaani unataka waziri mzima aje aropoke hapa jamba ambalo liko polisi tayari? Tuache ujuaji wa kipopoma!
Kwani taasisi na makundi mbalimbali yanayoongelea jambo hilo unadhani hawajui kuwa liko polisi? Aacheni utoto, ni sheria ipi inakataza kuongelea jambo kama hilo likiwa polisi?
 
Back
Top Bottom