Mbowe aachiwa huru na wenzake watatu baada ya DPP kuwasilisha hati ya kutotaka kuendelea na kesi

Mbowe aachiwa huru na wenzake watatu baada ya DPP kuwasilisha hati ya kutotaka kuendelea na kesi

Hii inaonyesha nchi hii inamateso sana.

Kama wanafanya haya kwa Mbowe.. Mtu wa kawaida akibambikwa kesi si anafia jela?

Mbowe amesaidiwa sana na Wanasheria kuonyeasha udhaifu wa kesi.. Je ni watu wangapi wapo ndani hawana wanasheria?

Tunalalamika jela zimejaa na mahabusu lakini nina imani kesi nyingi ni za kutengeneza hasa kama mtu anakuchukia.. Anakutengenezea kesi hata ya kubaka au wizi.. Unakwenda na maji.

Tuombe hasa Katiba ibadilike kidogo hata polisi wataogopa kutengeneza kesi
 
shukuru hata katoka sasa akakae na familia sasa..

hizi siasa za tanzania ni za ovyo sana inafika wakati tuelewe tu kwa sasa nchi hii ni nchi ya chama kimoja na hatujafika hatua ya kupevuka kuwa na multi-partism sytem.

hata huo upinzani wenyewe haueleweki na haujielewi kabisa mtu mwenye damu ya upinzani nchii hii walikuwa wawili tu na sasa kabakia mmoja ni maalim seif(marehemu) na lisu hawa watu ni wapinzani wa kweli walibaki ni wachumia tumbo.
Umejibu jambo tofauti na nililoandika!
 
Mbowe na wenzake walikuwa huru siku nyingi sana kabla.

Wenye akili walijua hivyo mapema sana.

Hii kesi ilikuwa inaleta aibu za reja reja.

Ila tumejifunza mengi sana kupitia hii kesi.

Sote ni binadamu na tuna madhaifu mengi sana.

Madhaifu ambayo yameingilia hadi mifumo tuliyojiwekea wenyewe.

Kesi ya Mbowe na wenzake itusaidie kujielekeza, kujiendesha na kujisimamia vizuri.

Kwa pamoja tuhamasishe upatikanaji wa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi
 
Serikali wamekuwa wajanja Sana Mana kupitia kwa mbowe tayari magaidi walikuwa wanatengenezwa kweli na rebels waangekuwa wengi. Tayari hata jeshi lilikuwa limeshagawanyika hivyo mama angepinduliwa soon.
 
Baada ya upande wa Mashtaka kufunga ushahidi wao na kuialika Mahakama kutoa hukumu ndogo na kisha mahakama kuwakuta watuhumiwa na kesi ya kujibu mnamo Februari 18 2022. Leo 04, Machi 2022 ni siku ya watuhumiwa kuanza kujitetea kutokana na tuhuma wanazotuhumiwa nazo.

Awali Mahakama iliwakuta na kesi ya kujibu katika mashtaka 5 kati ya 6 katika kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.

Kujua kesi ilipoishia fungua kiunganishi hiki:Mbowe na Wenzake 3 wakutwa na kesi ya kujibu. Kesi imeahirishwa hadi Machi 04, 2022 watuhumiwa kuanza kujitetea


=========

UPDATES

Jaji anaingia Mahakamani Muda huu Saa 4 na Dakika 52

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Ikupendeze naitwa Robert Kidando Wakili wa Serikali Mwandamizi nipo na

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Mawakili Wa Serikali Waandamizi Tulimanywa Majige
Wakili wa Serikali

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na

Paul Kisabo
Sisty Aloyce
Gaston Garubindi
Iddi Msawanga
Evaresta Kisanga
Maria Mushi
Nashon Nkungu
John Mallya
Jeremiah Mtobesya
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata Ni hayo tu mh Jaji.

Jaji: Shauri lilikuwa lina kuja kwa Utetezi, Je Mnazo habari zozote za Wateja wenu?

Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji ni kweli Kwamba Shauri lilikuwa limepangwa kwa ajili ya Utetezi Kwa Upande wangu tulifanya Maandalizi Mazuri Mimi John Malya, Dickson Matata, Fredrick Kihwelo na

Kibatala: wengine Juzi na Jana tulikuwa Ukonga na Segerea. Tulionana nao wakiwa na Bashasha kabisa, Kwamba Leo tunaendelea na Utetezi Lakini Leo Asubuhi tumepata Taarifa Kutoka Kwa Askari Magereza Kwamba Mbowe amepata Matatizo ya Ki Afya. Kwa hiyo hatuwezi Kuendelea,

Hivyo, Tunaweza Kupanga Kuendelea Jumatatu

Jaji: Jumatatu itakuwa Tarehe ngapi

Wakili Peter Kibatala: Tarehe 07 March 2022

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Utetezi, na tumewasikia Wenzetu Maombi Waliyo Wasilisha Sasa tusingependa Kujibu Hoja hiyo, Kwa sababu na sisi tuna Maombi Mengine Kwa hiyo Kujibu Hoja hiyo haitokuwa na Maana sana

Mheshimiwa Jaji tunaomba Moja la Kufanya Mbele ya Mahakama yako Na Ombi hili Mheshimiwa Jaji ni kwamba Mkurugenzi Wa Mashitaka (DPP) kwa niaba ya Jamhuri anaomba Kuwasilisha Taarifa ya Kutokuwa na Nia na Kuendelea na Shauri hili

Na Taarifa hiyo tunaitoa Chini ya Kifungu cha 91(1) kwa Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai

Jeremiah Mtobesya: Tumesikia Taarifa ya Notes hiyo kutoka kwa Mkurugenzi Wa Mashtaka, na Kwa Bahati Mbaya hatuwezi Kusema lolote zaidi ya Kusema tunaichia Mahakama, sababu Kifungu Kinatoa Maelezo Yote Kwamba Baada ya Kusema hivyo tunaichia Mahakama dhidi ya Amri zake za Mwisho

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Taarifa Hii tunaiwasilisha kwa Njia ya Maandishi, Kwa Maombi hayo ya Kifungu cha 91(1) tunaomba Kuondoa Mashitaka Yote dhidi ya Washitakiwa Wote Sababu zote zipo katika Noel Prosecui ambayo tumeiwasilisha

Wakili wa Serikali Robert Kidando: anapeleka Nyaraka Mbele ya Karani wa Jaji, na Karani anampatia Jaji

Jaji: Je umezungumza kwa niaba ya Defense Wote..?

Jeremiah Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba kila Mmoja aseme

John Malya: Mheshimiwa Jaji notes iliyotolewa inayushuka Mikono wote, pamoja na Kujiandaa kwa ajili ya Kujitetea, Mikono yetu imefungwa na hatuwezi Kusema lolote, Tulitaka sana Warudishe Gharama zetu na Mengine lakini wacha Tusubiri Maamuzi ya Mahakama

Fredrick Kihwelo: Kwa niaba ya Mshtakiwa wa tatu Tumesikia Taarifa iliyotolewa, Tunaichia Mahakama iweze Kutoa Amri

Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Na sisi tunaichia Mahakama, Sheria inajielezea wazi.. Mahakama ipo Kimya Kidogo na Jaji Bado anaandika

Kule Nje ni Kelele za Shangwe na Fifijo watu Wanaimba, Imebidi Mahakama Kufunga Vioo Vya Madirisha ili Kuzuia Kelele Kuingia Mahakamani, Wewe furaha yako ni Kiwango gani? Onyesha emoji ya furaha hapa Chini.. Au picha yako ukiwa na furaha kubwa..

Jaji: Baada ya Mahakama Kusikiliza Hoja iliyoletwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Kwamba Mkurugenzi wa Mashtaka hana nia ya Kuendelea na Kesi, na Upande wa Pili wakaridhia

Mahakama inasema Shauri hili lililo kuwa linawakabili Washitakiwa Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa nakiondosha Mahakamani na Washitakiwa Wanaachiwa huru bila Masharti, sababu Kuna Vielelezo vililetwa Mahakamani, naandaa Amri ya Kuviachia

Jaji: Na hivyo naelekeza Mkuu wa Magereza Kuwaachiwa Mara Moja, Leo na si Vinginevyo Natoa Amri Jaji anatoka Mahakamani Mahakama inaridima Kwa Shangwe.

=======
Freeman Aikael Mbowe na wenzake watatu, wameaachiwa huru leo, na Mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Baada ya DPP Kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo, leo 4.3.2022. Hivyo, Freeman Aikaeli Mbowe

View attachment 2138292
Kufutwa Kwa kesi hii kumeiletea heshima nchi yetu kwa maana haikuwa na afya kwa Taifa letu. Tunaishukuru serikali Kwa kuliona hili. Kazi iendelee na WaTanzania tuimbe wimbo mmoja tu sasa wa maendeleo.
 
Kesi ikifutwa na DPP lifunguliwe shauri la madai ya fidia ya kuchafuliwa jina Mh.Mbowe na wenzake pamoja na CDM kama chama.Maana hawa CCM wametangaza sana kesi hii kwa dunia.

Wakiachwa hivi hivi wataenda na hilo bango towards 2025 kama agenda yao,baadhi ya wananchi wenzetu wamenyimwa ufahamu wa haki za binadamu na hawapatiwi taarifa sahihi dhidi ya uonevu unaoendelea hapa nchini.
Huwezi kufungua kesi ya madai kwenye shauri ambalo final decree haijatolewa. Kumbuka bado nole prosequie is not bar for subsequent proceedings basing on the same fact , hivyo wakikamatwa tena hawawezi kuweka P.O ya autrefois acquit ,autrefois convict au res subjudice , kulikuwa na mswada wa kubadilisha hicho kifungu cha nole kiwe bar sikumbuki kama mswada huo umesainiwa kuwa sheria
 
Usanii ndani ya sanaa

Unamtesa mtu kama utaishi milele wakati wote ni udongo na tunaoza na kuwa funza

Baada ya kuzikwa haufiki mwaka unakuwa umeoza

Tenda wema, Ishi kwa Furaha na Amani
Watu hawajali. Wanapowatesa wengine wao ndio raha yao mkuu
 
Sipendi Mbowe na wenzie waendelee kuwa mahabusu, lakini pia sipendi kusikia ameachiwa kwa MSAMAHA! Kama ni hivyo, basi kesi iendelee tuzijue mbivu na mbichi!

Na nina imani, kwa ushahidi uliotolewa, bila UJAJI WA MCHONGO, kulikuwa hakuna KESI hapo!
Hajaachiwa kwa "msamaha" kutoka kwa yeyote yule.

Kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi kwa DPP sio msamaha,bali inaonyesha ni jinsi gani mtu/watu/kikundi kinaweza kupanga mateso kwa mtu/watu ilimradi tu katiba inawapa nguvu hiyo, bila hata ya kuwa na punje ya ushahidi wa kuishawishi mahakama.
 
Kwa Nchi yetu ilipofikia tupiganie katiba mpya kwa nguvu kubwa zaidi ili asitokee Tena kuongozi wa kuumiza watanzania wenzake kwa mambo ya kisiasa .Napenda Watanzania tuoendane na tusibaguane kwa itikadi za kisiasa.Kama mtu amekosea basi ahukumiwe kwa sheria na sio kisiasa.Tuipiganie nchi yetu ipate katiba mpya kwa maendeleo ya Tanzania.
 
Leo comte na Crimea watajiharishia damu.
Pambafu kabisa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mkuu usiwe pumbavu kiasi hiki!

Mtu kasota rumande karibia mwaka, na ndio lengo la ccm hilo au wewe ulifikiri ccm wanataka nini zaidi ya hicho?

Utakuta mnaanza kushangilia kama mazuzu! Yani ni sawa na mtu anakubutua makofi ya kutosha alafu baadae anakuambia nenda tu, kisha unaanza kushangilia!
[emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Hii inaonyesha nchi hii inamateso sana..
Kama wanafanya haya kwa Mbowe.. Mtu wa kawaida akibambikwa kesi si anafia jela?
Mbowe amesaidiwa sana na Wanasheria kuonyeasha udhaifu wa kesi.. Je ni watu wangapi wapo ndani hawana wanasheria?
Tunalalamika jela zimejaa na mahabusu lakini nina imani kesi nyingi ni za kutengeneza hasa kama mtu anakuchukia.. Anakutengenezea kesi hata ya kubaka au wizi.. Unakwenda na maji..
Tuombe hasa Katiba ibadilike kidogo hata polisi wataogopa kutengeneza kesi
Umeongea point sana Mkuu, niliwahi kwenda Magereza moja hivi kumcheki ndugu yangu aliyekuwa amefungwa huko,nilisikitika sana niliposikia baadhi ya wafungwa kuwa walisingiziwa tu na kwasababu ya kukosa watetezi wamebakia wanaozea Gerezani.Dunia hamna haki,haki inapatikana kwa MUNGU tu.
 
Back
Top Bottom