Mbowe: CHADEMA haiko tayari kupokea Ruzuku inayotokana na Kura za Wizi!

Chama cha siasa kikishindwa uchaguzi mara 3 kinageuka kuwa cha kigaidi..

Ndiko hii saccos chadema inakoelekea
 
Mwamba yupo committed sana ,nilivyoona walivyoporosha Billcanas ,wakavunja Shamba lake la maua/mboga mboga ,wakambambikizia kwamba ajalipa kodi,wakamnyima mshahara ,wakamfunga still mwamba hajaunga mkono juhudi.

Heche,Sugu,Msigwa ni baadhi ya wabunge walioshawishiwa waunge mkono juhudi wengine walipewa blank cheque wajaze mpunga wao wenyewe wanaotaka lakini hawajaunga!! Ukiunga mkono juhudi maana yake umejimaliza kisiasa eg Covid19,Silinde,likualibutu,nasari and the like washajimaliza kisiasa!! Ngoja wamtumikie kafiri kisha warudi mtaani kuungana na lipumba,mrema ,cheyo etc
 
Kwani huko siasani kinatafutwa nini zaidi ya fedha na vyeo?
 
Kwani huko siasani kinatafutwa nini zaidi ya fedha na vyeo?
Vyeo kwa kuuza UTU? (Samahani lakini)kwahiyo akitokea mshefa akasema akupelekee moto kwa MPALANGE akupe CHEO utakubali? Kuuza Utu kwa vipande 30 vya FEDHA ni sawa?
 
Vyeo kwa kuuza UTU? (Samahani lakini)kwahiyo akitokea mshefa akasema akupelekee moto kwa MPALANGE akupe CHEO utakubali? Kuuza Utu kwa vipande 30 vya FEDHA ni sawa?
Sasa mbona hapo Ufipa mnauzana kwa CCM?!
 

Mie nina swali la udadisi wa kimahesabu tu, kama ifuatavyo:

1. Chukulia kwamba, kama CDM walipata kura P, basi walistahili ruzuku Q;

2. Chukulia kwamba, kama waliibiwa kura R, basi waliibiwa ruzuku S;

3. Chukulia kwamba, baada ya wizi huo kutokea, basi walibakiza kura T ambazo zinazoendana na ruzuku U;

4. Kwa hiyo, salio la ruzuku U linakuwa limetokana na kura halali zilizobaki baada ya wizi kufanyika.

5. Kwa hiyo, kama zile kura za Chadema zilizotangazwa na NEC hazikutokana na wizi uliofanywa na Chadema kwa kukwapua kura za CCM, basi, ruzuku U itakuwa ni halali, na utimilifu (integrity) wa Chadema haumeguki kwa sababu ya Chademakuchukua ruzuku hiyo.

SWALI: Kwa hiyo nisaidieni: ruzuku hiyo anayoikataa Mbowe ina tatizo gani hasa?
 
Labda TAL aliiba kura!
 
Kwenye msafara wa Mamba kenge hawakosekani Mkuu , kenge kama likualikali,silinde,kovid19 etc wameondoka wamebaki makonki Heche,Sugu,Msigwa ambao hawajakubali kununulika kwa vipande 30 vya fedha.
CCM wakifika bei hapo Ufipa hatabaki Freeman wala Sugu wote watavaa kijani!
 
Brilliant. Inaelekea Mbowe hajui kura halali walizopata CHADEMA na ruzuku halali wanayotakiwa kuchukua ili kubaki na utimilifu (integrity) wao.

Mpelekee hiyo hesabu (with exact figures) awasilishe serikalini ombi rasmi la CHADEMA kulipwa ruzuku yake halali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…