Pre GE2025 Mbowe: Ilikuwa ghafla sana Lissu kutangaza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mh. Mbowe ana busara sana - si mkurupukaji na ndiyo kinamfanya aitwe jabari la siasa Tanzania na Africa.
Hakuna cha jabali wala gogo, akae pembeni....fikra zake kuendeleza chama zimefika mwisho sasa baada ya miaka 21 kwwnye kiti!.
 
Kwahiyo Mhe Mbowe ni kwamba hiyo nafasi ya Uenyekiti ni kwamba alijipanga kugombea
Na siyo kweli kwamba alilazimishwa na ile nyomi ya watu iliyovamia nyumbani kwake na kumshauri agombee?
Tuamini lipi kati ya haya mawili aliyoyasema?
 
Kwahiyo Mhe Mbowe ni kwamba hiyo nafasi ya Uenyekiti ni kwamba alijipanga kugombea
Na siyo kweli kwamba alilazimishwa na ile nyomi ya watu iliyovamia nyumbani kwake na kumshauri agombee?
Tuamini lipi kati ya haya mawili aliyoyasema?
Njia ya muongo huwa ni fupi na pia ukiwa muongo uwe na kumbukumbu!
Mbowe gafla amesahau aliandaa igizo lowasa style eti wanachama wameenda nyumbani kwake KUMLAZIMISHA agombee uenyekiti!
 
Njia ya muongo huwa ni fupi na pia ukiwa muongo uwe na kumbukumbu!
Mbowe gafla amesahau aliandaa igizo lowasa style eti wanachama wameenda nyumbani kwake KUMLAZIMISHA agombee uenyekiti!
Maana mwanzo alisema familia yake imemshauri apumzike
Mara kaja na uvamizi wa wafuasi wa chadema nyumbani kwake, wakimshinikiza agombee
Akaamua tu kugombea kutokana na wale watu kumlazimisha.
Leo Mheshimiwa Mbowe anasema alikubaliana na Lissu. .
Ikumbukwe alianza Lissu kutangaza nia,mbowe ametoa msimamo wake late sana,..sasa walikubaliana saa ngapi?

Kwakweli Mbowe anatuchanganyia mafile
Mimi nilikuwa mmoja kati ya watu walioamini lile tukio,licha ya wafuasi wengi kusema ni igizo..
Sasa anaanza kututoa kwenye reli.
 
Na mimi nimeshangazwa sana na kauli hii ya Mwamba...

Hakuweka wazi walipatana nini juu ya nani agombee...

Je, Tundu Lissu alikubali Freeman Mbowe aendelee...?

Ni kwanini Tundu Lissu akafanya U-TURN ya ghafla kwa kufuta nia yake ya kugombea Umakamu mwenyekiti badala yake kuutaka uenyekiti kabisa na hivyo kwenda kinyume na makubaliano yao na Mwenyekiti wake? Mbowe kakiri kuwa hata yeye alishangaa...!!!

Hebu media Jambo TV au maria Space mtafuteni Tundu Lissu ajibu swali hili...

Pamoja na haya, kumbukumbu zinaonesha, Tundu Lissu alishaligusia na kuitolea ufafanuzi hoja hii..

Za kutoka ndani ya CHADEMA zinasema, mpango wa Freeman Mbowe ni kugombea U - Rais. Hawezi kuitekeleza nia yake hiyo kwa ufanisi akiwa nje ya uongozi kama mwanachama wa kawaida tu..

Na kumbe haya ni Moja ya makubaliano yake na Bi Samia Suluhu Hassan (Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT) ktk kilichoitwa "maridhiano"

Ameambiwa ahakikishe huyu mwamba (Tundu Lissu) is completely out of the picture ndani ya CHADEMA kwa kutokuwa na nafasi yoyote ya uongozi. Ndiyo maana kwenye Umakamu mwenyekiti akawekewa Hezekiah Wenje..!

Na Tundu Lissu kuliona hili, akasema namfuata huko huko juu aliko. Huyu ndiye Tundu Lissu bhanaπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…

Lengo la Freeman Mbowe kugombea u - Rais ni kumpa unafuu Samia mgombea wa CCM kutopitia mikikimikiki ya mgombea wa aina ya Tundu Lissu...

Tuendelee kufuatilia...
 
Hawa bora wametifuana....tuelekeze nguvu zetu zote kwenye kulisaka tonge....wanasiasa ni walewale
 
Mkiwa Nyuma ya keyboard mnataype mafichoni mnakua majasiri kweli kweli πŸ˜€ na kujifanya mna uchungu na nchi
Kwani kusema FAM amekataliwa ni ujasiri? wakati jambo ambalo lipo wazi tuu huku mtaani
 
Mbowe ana busara gani? Sasa kaunda kamati ya Roho mbaya ikiongozwa na Mdee, Boniface, sugu na wenje kwa ajili ya kumdhoofisha Lisu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…