Pre GE2025 Mbowe iokoe CHADEMA kwa kuchukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Lissu, usisubiri kesho!

Pre GE2025 Mbowe iokoe CHADEMA kwa kuchukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Lissu, usisubiri kesho!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa hoja hii mimi si CDM wala sipo hata karibu na ofisi zao. Sijui nini kilijiri lakini nadhani kulikuwa na ku bulldoze waliokataa. Sijui kama kura zilitumika na sijui kama hoja za waliokataa ziliangaliwa kwa ubora. Sijui
Ninachokijua, waliokataa ni vigogo waandamizi ! na hili linaeleza jambo.
Mimi nilidhani una access ambayo wengine hatuna. Vigogo waandamizi ni binadamu na huwa wanakosea. Ndio maana katika kamati kila upande inapata nafasi ya kuwashawishi waumbe ili wakubali hoja yake. Baada ya hapo mawezi ya waliowengi ndio yanayokuwa ndio msimamo wa Kamati. Nijuavyo mimi katika Kamati kura zote zina uzito bila kujali nafasi ya mpiga kura, ubobezi wake n.k. Ikiwa mawazo ya vigogo waandamizi yanakubaliwa tu hata kama ni minoity basi ina maana kuwa hiyo Kamati imekuwa "animal farm ya George Orwell". Wale wasio vigogo wataona hamna sababu ya kuchangia mawazo yao. Hiyo inakuwa ni cabal. Na Makamu Mwenyekiti inaelekea hulka yake ndio hiyo. Anachotaka yeye ni lazima kiwe ndio msimamo wa wote maana yeye anajua kuliko wengine na tusisahau anatembea na risasi mwilini mwake.
Mazungumzo (dialogue) hutokea kati ya wawili au zaidi katika kubadilishana fikra na mawazo
Maridhiano (reconcilliation) ni upatanishi unaoleta muafaka baada ya pande husika kuhitilafiana

Hili la MARIDHIANO hatukulizua, tumeliazima kutoka kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh FAM
Maridhiano ni sawa na upatanisho. Mara nyingi yanafanyika pale pande moja inapoona kuwa mwenye nguvu anamuonea na hamtendei au hakumtendea haki. Kuna mtu atabisha kuwa CDM ilikuwa haitendewi haki? Kuna mtu atabisha kuwa CCM imeshika mpini? Mbowe alikosea nini kutaka upatanisho ambao utawarudisha katika hali ya ushindani na sio uadui?
Kwa mujibu wake, kulikuwa na Maridhiano 1, wakati wa JPM ambayo hayakuwa na matunda
Alichokwenda kuongea na Mh Rais ilikuwa kutafuta maridhiano 2 ya kisiasa nchini. Ni kwa mujibu wake

Kwa Maana ya maridhiano hapo juu, tuna maswali; ni pande ngapi zilihitifiana, je zilihitilafiana kwa jambo gani, na wahusika ni akina nani.
Hili nimelijibu hapo juu. Inawezekana kuwa wakati wa JPM palifanyika majadiliano ambayo walitegemea yatale maridhiano. Nakumbuka Mbowe alienda na viongozi wenzake Mwanza na kumuomba hadharani Rais wa wakati ule wakae pamoja ili kupoza hali iliyokuwepo nchini. Alimuomba kwa sababu alitambua kuwa wao wameshika makali katika suala hilo na mtu pekee mwenye mamlaka ya kupunguza maumivu yao alikuwa Rais. Na hilo lilikuwa linawezekana kwa sababu wakati wa marais waliotangulia waliweza kufanya siasa za upinzani kwa uhuru zaidi.
Hapana, lengo la mazungumzo ni kuwa na Muafaka! consensus
Sio consensus. Consensus ( kukubaliana kila kitu) inatafutwa ndani ya chama henye msimamo mmoja na sio baina ya washindani maana pakiwa na consensus hamna ushindani. Lengo la mazungumzo ni kufika mahali ambako mtakubali kutofautiana kwa heshima na amani. Kila mmoja ataheshimu haki ya mwenzake kutofautiana nae. Consensus ingeweza kutafutwa ndani ya chama kwa kujadiliana mpaka wanafikia muafaka unaokublika na kila mmoja wao. Mwalimu alikuwa anasema hivyo ndivyo ilikuwa demokrasia ya kiasili ya kiafrika. Wale wenye mamlaka ya kutoa maamuzi walikaa chini ya mti na kujadiliana mpaka wote wanakubaliana. Ambacho hakusema ni kuwa sehemu kubwa ya jamii ( haswa wanawake) hawakushirikishwa katika majadiliano hayo kwa hiyo ilikuwa demokrasi ya baadhi ya watu.
Hapa unanioea ! Aliyeleta neno Maridhiano katika kikoa (Domain) ni FAM.
Amelitumia katika kila mkutano. Tafadhali rejelea clip zake
Hakukosea. Nimeangalia maana yake na nimetambua hakukosea.
Of course, baada ya kuwa na Muafaka (concensus) kuhusu South Africa ikiwemo Katiba, iliundwa timu ya Maridhiano(reconciliation) chini ya Askofu D.Tutu (R.I.P) iliyoitwa Truth and reconciliation Commission. Kwa S.Africa Maridhiano yali conclude the process. Kwa FAM alianza na Maridhiano ndio maana tnapata shida ya kumwelewa
Hapakuwa na consensus kuhusu Katiba Mpya ya Afrika Kusini. Bunge lilipiga kura na walio wengi walikubali kuwa kuna haja ya Katiba Mpya wakati kuna baadhi walikataa wazo hilo kwa sababu waliona hamna haja ya Katiba Mpya wakati wanaweza kuirekebisha iliyokuweko. Hapakuwa na consesus kama unavyodai maana walioikataa waliendelea kuikataa lakini walikuwa wachache kuliko walio ikubali. Kama ilivyokuwa katika Kamati Kuu ya CDM, msimamo wa wengi ndio ukawa msimamo wa Bunge.
Kuna siku Rais alibadili njia na kutokea uani. Ilikuwa notable . Tu criticise na kutoa credit inapobidi
Hicho ni kitu cha kawaida. na kwa sababu ya uchache wao hao waandamanaji walishindwa kumzuia asitoke. Walibaki wamebeba wachache tu huku wamebeba mabango yao ambayo alionekana akiyasoma. Huo sio ushindi bali walionyesha insi walivyokuwa inconsequantial.
Haiwezekani kuwa na 'mbadala' wakati Mwenyekiti yupo katika Maridhiano.
Kwa nini? Si walikuwa tayari wameruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara? Kwa nini wale waliokuwa hawataki maridhiano wasi elekeze nguvu zao katika kuwahamasisha watu kuandamana? mwenyekiti aliisha onyesha njia. Na watu kama Ntobi na vijana wenzake walikuwa mbele kuwahamasisha vijana wenzao waendelee kudai Katiba Mpya. Na wengi walilipa gharama kubwa kwa msimamo wao? Si unakumbuka yaliyotokea Mbeya? Huyo Mwenyekiti alikimbilia Mbeya aliposikia tu kuna wenzake wameswekwa ndani na wamedhalilishwa! Wakina Ntobi wanajua kuwa siku zote alikuwa nao aliwawezesha kupambana kwa vitendo na sio maneno matupu. Ndio maana wamechukua personal upotoshaji unaofanywa na Lissu pamoja na wafuasi wake. Na wanawajua wote hawa vizuri kuliko sisi na wanajua nani ni genuine na nani mtu wa maneno tu.
Mfano mzuri ni pale Tanga wakati wa Mazishi ya Mzee Kibao (Pumzika kwa amani).
Kuna watu walitaka yule bwana asiongee kabisa! M/Kiti akasimama na kusema '' hapana ataongea'' na yule Bw akasema ''msikilizeni Mwenyekiti wenu, hakusema Msikilizeni FAM''.
Kabla ya kuanza usomaji wa dua katika msiba huo kiongozi wa msiba aliwaasa kuwa katika misiba ya kiislamu hamna kushangilia au kelele za aina yeyote. Watu walipoanza kumzomea Masauni na kumzuia asiseme Mwenyekiti Mbowe aliwaasa wamsikilize kwa heshima ya Marehemu. Ulitaka awahimize waendelee kuzomea ili watakaposhughulikiwa na Tanpol aende kuwapa pole gerezani? Ulikuwa ni uamuzi wa busara maana kwa tension iliyokuwepo waombolezaji wasingeishia kwenye kuzomea tu bali wangeweza hata kujaribu kumdhuru Masauni. Mbowe ni Mwenyekiti sasa kuna dhambi gani kumpa heshima hiyo? Hiyo nayo mnataka kumnyang'anya?
Mafano 2, BAVICHA waliambiwa na M/Kiti wachunge ndimi zao! kwa maana wasije vuruga Maridhiano.
Kuchunga ndimi sio kuambiwa wanyamaze? Ni kuwaambia wasitumie lugha ambazo zitaweza kumpa sababu ya aliye upande wa pili kujitoa katika mazungumzo. Au kuwatia ndani hao vijana viongozi na ku frustrate juhudi za chama chake za kufikia kwenye maridhiano.
Kutofautiana mitazamo hakufanyi awaye awe Mhafidhina. Neno hilo alilitumia FAM kuwadhalilisha wasiokubaliana naye. Kumbuka ukitaka kumuua Mbwa mpe jina baya kwanzaAngeweza kusema wasioafiki!

Hapo ndipo ukaona wahafidhina wakakaa pembeni jambo unalosema '' waliingia gizani''.
Mhafidhiana maana yake ni mtu "conservative". Hilo sio tusi. Ni mtu ambae si rahisi kubadilika. Sasa kama walikaa pembeni kwa sababu tu wameitwa "conservatives" basi wana matatizo makubwa. Mtu mwenye nia njema angeendelea kujenga hoja yake NDANI ya chama ili Mwenyekiti na wenzake waone wamekosea wapi. Mtu ambae ana amua kusimama nje na kuwabeza waliotofautiana nae ndani ya chama hana nia njema na chama hicho. Mtu Muungwana angejitoa katika nafasi ya uongozi aliyokuwa nao ili asiwe sehemu ya hayo mazungumzo. Mtu mwenye nia njema hafanyi sabotage za wazi wazi.
Wakati wa JPM aliomba maridhiano yakafeli, na sasa ameomba yamefeli.
Huwezi kufeli kila mara ukasema ni ukomavu ukizingatia experience ya miaka 21 kama Mwenyekiti na 33 katika siasa.
Kwa hiyo amefeli mara mbili tu? Mimi nilidhani mara nyingi kuliko hivyo. Rais wa Zambia aligombea zaidi ya mara tano lakini hakukata tamaa. Mbowe amekifikisha mbali sana chama chake toka alipochaguliwa. Na katika mazingira magumu. na hajakata tamaa. Huo ndio ukomavu. Na tofauti na Lissu najua hata akishindwa atafanya kila itihada kuhakikisha kuwa chama chake hakisambaratiki. Na kikisambaratika atajitahidi kukiunganisha tena. Ndio maana humuoni akitoa maneno ya shombo kwa mwenzake kama wanavyofanya wanaompinga. Na ni wachache sana walio upande wake ndio wamejitokeza kupambana na wapinzani wake kwa hofu hiyo hiyo maana maneno yanaacha donda. Kinachosikitisha ni kuwa Lissu halioni hilo. Anataka ushindi by any means neessary. Huyo ni mtu hatari sana.
Ni lini FAM aliwahi kukabiliwa na sauti nyingi kama sasa! Hii ni rebellion baada ya incessant failures

Ni rebellion baada ya kuona CDM haina msimamo imepoteza uelekeo na inachanganya Wanachama wake
Ni rebellion baada ya kuona same old tricks. Ni rebellion inayotokana na kufanya kile kile kwa def ya insanity

Ukiangalia kwa umakini hizi sauti nyingi zinatoka kwa watu ambao hawana mapenzi na CDM. Zinatoka kwa wale ambao hawakupitia nusu ya machungu aliyopitia Mbowe. Na genius ya CCM ni kumpigia debe Mbowe ili aonekane ni kibaraka wao ili watu wamkimbie kwenda kwa Lissu. Hii ni concerted effort ya wale ambao genuinely wanataka mabadiliko na wale ambao wanataka hayo mabadiliko kwa sababu wanaona Lissu sio tishio. Hii sio grass root rebellion. Ni faux rebellion iliyopikwa kwenye Club House ambako kuna wannabe King makers ambao bado hawajamsamehe Mbowe kwa kuwa"snub".
Well, Watu hawakuwa na uhakika kama wakiandamana M/Kiti atakuwepo au ataibukia Ikulu.
Kumbuka kuwa Watu walikuwa Mahakama Kuu wakikabiliana na FFU kabla ya kuona picha za FAM Ikulu.
Tafadhali. You are better than that. Watu ni waoga full stop. Walitoka kwa wingi kwenye maandamano yaliyokuwa na kibali cha serikali. Waliposikia tu kuwa watapigwa kipigo cha mbwa mwizi, wanajeshi watafanya usafi katika eneo la maandamano wakaingia gizani. Ndio maana hiyo confrontational approach haitafanikiwa.Watanzania wengi bado hawataki kupambana na dola. Hivi unadhani pale Magomeni hali ingekuwaje kama angetokeza Lissu na wenzake badala ya kujiweka katika mkao wa kuzuiwa nyumbani. Hiyo ni pamoja na Lema ambae alitakiwa kujua wazi kuwa zitafanyika juhudi kubwa kumzuia kuhudhuria lakinini akapanda ndege siku ya maandamano kwenda kuyahudhuria! Ni farcical kwa kweli.
Katiba ingekuwa na miaka 6 tu. Jiulize ya 1977 imefanyiwa amendments ngapi katika average ya miaka.
Kwa hiyo ingekuwa ya mpito tuu. Na baada ya muda huo ingetayarishwa nyingine? Tulichojifunza kwenye Katiba iliyopo ni kuwa kuna umuhimu iwe kamilifu kwa kiasi kikubwa wakati ina pitishwa ili kama kuna ammendments zitakazofanyika ziwe minor.
FAM kuzungumzia ufinyu wa muda ilikuwa kosa! Yeye hakupaswa kuwa sehemu ya serikali! ni Mpinzani
Muda ulikuwepo lakini Maridhiano yalimtia kibano, akageuka kuwa msemaji wa Kamati ya Maridhiano.
Ana haki ya kusema hivyo. Hakusema kama msemaji wa serikali. Muda haukuwepo ukiangalia mazingira ya wakati ule. Chama kilitakiwa kiwekeze nguvu katika urekebishaji wa Tume ya Uchaguzi ili uchaguzi unaofuata wawe na mandate ndani ya Bunge. Zitto alikuwa sahihi kwenye hili.
Nakuhakikishia wakati huu itakuwa tofauti sana. Huko nyuma alikuwa na support ya Bigwigs na Wanachama.
This time hana zaidi ya nusu ya Wanachama. Please kumbuka siongelei wajumbe wa mkutano mkuu.
Kwa hiyo hao wanachama watamsusia chama akichaguliwa na Mkutano Mkuu kuwa Mwenyekiti? Aliyeshindwa ataongoza juhudi za kumkataa? Nadhani mna underestimate uwezo wa Mbowe kuwa convince hata wale wanaotofautiana nae sasa hivi kuungana nae kwa ajili ya afya ya chama chao. Lissu akiendelea na fitna fitna itakula kwake. Watu wengi wanakipenda chama chao kuliko mtu yeyote. Tatizo ni kuwa Lissu akishinda ataongoza juhudi za kukibomoa ( pengine bila kukusudia).

Yetu macho. FAFO. Walatino na wafanyakazi Marekani wamegundua ukweli huo hata kabla ya Januari 20.

Amandla...
😂 nimeongeza msamiati.

You are welcome.
 
Kwa nini Lussu asimuunge mkono Mbowe ????
Kwa kweli Mbowe wa awali, si huyu wa sasa...

1735559957498.png


Huo Mwaka 2015 CCM ilidaiwa kushinda kwa asilima 55%, Chadema asilimia 30%
Mwenyekit Freeman Aikaeli Mbowe hakujiuzulu, aliendelea kukalia kiti chake

Mwaka huu katika uchaguzi wa serikali za mitaa CCM imedaiwa kushinda kwa asilimia 99%
Mwenyekiti Freeman Aikaeli Mbowe inaonekana ataendelea kutetea kiti chake.

2004 - 2014 (miaka kumi) hakuna mfanikio ya kujivunia ingawa ni kweli tulipiga hatua!
2014 - 2024 (miaka kumi) mafanikio hamna ila tumepiga hatua ya kurudi nyuma!
2024 - 2034 ?​
 
Baada ya hapo mawezi ya waliowengi ndio yanayokuwa ndio msimamo wa Kamati.Ikiwa mawazo ya vigogo waandamizi yanakubaliwa tu hata kama ni minoity hiyo Kamati imekuwa "animal farm ya George Orwell". Hiyo inakuwa ni cabal.
Mwalimu Nyerere alitufundisha jambo baya. Hata pale ndani ya CCM walipokubali 'white paper'' Mwalimu alisema 80/20 tuwasikilize hao 20. Baada ya kupima akasema wana hoja! Je ilikuwa animal farm? ilikuwa cabal?

Maridhiano ni sawa na upatanisho. Mara nyingi yanafanyika pale pande moja inapoona kuwa mwenye nguvu anamuonea na hamtendei au hakumtendea haki.
Unachoongelea hapa ni Vi coactus . Maridhiano hutokea panapokuwa na stalemate.
.Hicho ni kitu cha kawaida. na kwa sababu ya uchache wao hao waandamanaji walishindwa kumzuia asitoke. Walibaki wamebeba wachache tu huku wamebeba mabango yao ambayo alionekana akiyasoma. Huo sio ushindi bali walionyesha insi walivyokuwa inconsequantial.
Hapana! lengo lilikuwa kufikisha ujumbe na si kumfanya Mh Rais Mateka. Kumbuka Rais alikuwa na ulinzi wa FBI
Watu wa Washington walifanya kitu remarkable. Please give the credit where the credit is due
Huyo Mwenyekiti alikimbilia Mbeya aliposikia tu kuna wenzake wameswekwa ndani na wamedhalilishwa! Wakina Ntobi wanajua kuwa siku zote alikuwa nao aliwawezesha kupambana kwa vitendo na sio maneno matupu. Ndio maana wamechukua personal upotoshaji unaofanywa na Lissu pamoja na wafuasi wake. Na wanawajua wote hawa vizuri kuliko sisi na wanajua nani ni genuine na nani mtu wa maneno tu.
Na watu wakimsoma Ntobi na kusikia ndio Team ya Mwenyekiti Mbowe wanaingiwa na wasi wasi.
Hofu kubwa ni kwamba kwa miaka 21 hawa ndio FAM ameweza kuwa groom !!!
Watu walipoanza kumzomea Masauni na kumzuia asiseme Mwenyekiti Mbowe aliwaasa wamsikilize kwa heshima ya Marehemu. Ulitaka awahimize waendelee kuzomea ili watakaposhughulikiwa na Tanpol aende kuwapa pole gerezani? Ulikuwa ni uamuzi wa busara maana kwa tension iliyokuwepo waombolezaji wasingeishia kwenye kuzomea tu bali wangeweza hata kujaribu kumdhuru Masauni. Mbowe ni Mwenyekiti sasa kuna dhambi gani kumpa heshima hiyo? Hiyo nayo mnataka kumnyang'anya?
Wale Vijana hawakutaka Masauni angee! basi. Hawakuwa na nia ya kumdhuru.
Ile ilikuwa passive resistance . Hakukuhitajika busara katika passive resistance kwasababu ni jambo benign
Kuchunga ndimi sio kuambiwa wanyamaze? Ni kuwaambia wasitumie lugha ambazo zitaweza kumpa sababu ya aliye upande wa pili kujitoa katika mazungumzo. Au kuwatia ndani hao vijana viongozi na ku frustrate juhudi za chama chake za kufikia kwenye maridhiano.
ANC walikuwa vitani mazungumzo yakiendelea. Ukraine wapo vitani, mazungumzo yanaendelea.
Hamas wapo vitani mazungumzo yanaendelea. Ni lazima uwe katika ''position of strength'' siyo kuwa submissive kama FAM
Mhafidhiana maana yake ni mtu "conservative". Hilo sio tusi. Ni mtu ambae si rahisi kubadilika.
Mandela alipokataa masharti ya Makaburu hakuwa conservative, alikuwa na msimamo.
Hawa conservatives wana hoja, kwamba, submission ya FAM haileti matokeo chanya.

Kuna illusion kwamba TAL anataka play merry hell sijui ni kwa sababu zipi.
FAM hawaambii watu kwanini anataka miaka 5, na anataka kumaliza kipi alichoacha baada ya 21 yrs
FAM ametengeneza kundi la akina Ntobi kumu attack TAL ni si kueleza miaka 5 ili iwe nini, kasahau nini baada ya 21
Na tofauti na Lissu najua hata akishindwa atafanya kila itihada kuhakikisha kuwa chama chake hakisambaratiki.
Ni taasisi ya Watu ! si chama chake. Haya ndiyo yanampa ugumu kuachia ngazi '' yangu''
Hakusema kama msemaji wa serikali. Muda haukuwepo ukiangalia mazingira ya wakati ule. Chama kilitakiwa kiwekeze nguvu katika urekebishaji wa Tume ya Uchaguzi ili uchaguzi unaofuata wawe na mandate ndani ya Bunge. Zitto alikuwa sahihi kwenye hili.
FAM akiwa magereza jitihada ziliendelea, alipotoka March 23 kulikuwa na miezi 9 kisha 12 ya 2024 kwa maana miaka 2 na nusu. Kumbuka tayari tuna template ya Katiba.

Ndiyo maana tume ya Mkandala ilifanya kazi kwa muda mfupi, walikuwa na reference tayari .
Muda ule wa Tume ya Mkandala ilikuwa kupoteza muda kwasababu hata leo mapendekezo yake hayana maana. FAM alipoteza muda katika vikao na CCM

TAL alikataa kushirikia mambo mengi akilazimisha Katiba, Tume na Mwenyekiti.
TAL hakukubali ujinga wa TCD wala wa Tume ya Mkandala.

Alichotaka ni Katiba, Tume na Mwenyekiti aachiwe kwanza.
Pressure ya TAL ilikuwa kubwa, CCM na Serikali hawakuwa na namna.
FAM akatoka na kuanzisha Maridhiano! Farcical
Nadhani mna underestimate uwezo wa Mbowe kuwa convince hata wale wanaotofautiana nae sasa hivi kuungana nae kwa ajili ya afya ya chama chao.
Amechoka! physically yupo fit !! politically amechoka!
Lissu akiendelea na fitna fitna itakula kwake. Watu wengi wanakipenda chama chao kuliko mtu yeyote. Tatizo ni kuwa Lissu akishinda ataongoza juhudi za kukibomoa ( pengine bila kukusudia).
Hii illusion inatoka wapi? Kwamba anataka merry hell l! kwa sababu zipi?
Kugombea nafasi hakumfanyi awe mtu mbaya! si wanasema ni Chama cha demokrasia!
 
Mwalimu Nyerere alitufundisha jambo baya. Hata pale ndani ya CCM walipokubali 'white paper'' Mwalimu alisema 80/20 tuwasikilize hao 20. Baada ya kupima akasema wana hoja! Je ilikuwa animal farm? ilikuwa cabal?
Nyerere mwenyewe alikubali kuwa Katiba ilimruhusu kuwa dikteta, ingawa yenye alikuwa a benign dikteta. Na ndio chama chake kilikuwa kina behave kama cabal. Tulikuwa tunaimba " zidumu fikra sahihi za Mwenyekiti...." Sasa leo ametokea Mwenyekiti ambae anakubali nguvu ya wengi ( kama alivyoonyesha katika suala la Covid-19) mnambeza. Lissu hapa alitaka awe kama wale nguruwe katika Animal Farm. Na matamshi ya wengi humu yanaonyesha dharau kubwa kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao hawakubaliani nae.
Unachoongelea hapa ni Vi coactus . Maridhiano hutokea panapokuwa na stalemate.
Ni nani hapo amekuwa forced mpaka useme kuwa ni Vi coactus? Maridhiano ni reconciliation ambayo inatumika kutibu majeraha na sio stalemate. Kulikuwa na stalemate gani South Africa wakati Tume ya Tutu ilianzishwa? Kuna political theorists mmoja amesema kuwa tatizo kubwa katika mifumo yetu ya siasa ni kumuona wale ambao mmetofautiana kuwa ni maadui ambao solution ni kuwaua (metaphorically). Amesema kuna haja ya wale wanaotofautiana kuwaona wenzao kuwa " adversaries" na sio "enemies" ambao wana haki ya kuwa na mawazo/ misimamo yao. Unachomtaka Mbowe ni kuichukua CCM kuwa kama adui anaestahili kuuawa. Hiyo haitatufikishisha popote maana nae atapigana vilivyo kuhakikisha anakuua kwanza. Hilo jaribio liliishafanyika dhidi ya CDM lakini halikufanikiwa.
Hapana! lengo lilikuwa kufikisha ujumbe na si kumfanya Mh Rais Mateka. Kumbuka Rais alikuwa na ulinzi wa FBI
Watu wa Washington walifanya kitu remarkable. Please give the credit where the credit is due
Ujumbe kwa watu 10 kusimama na vijikaratasi vilivyoandikwa kile amabcho kila siku anakisikia. Baada ya wapinzani hao kuchukua selfies na clips za kurusha mtandaoni wakaona wamefanya kazi kubwa. Hamna kitu remarkable walihofanya watu wa Washington. Hao ambao wanadai wanaweza kumobilise mamilioni ya watu Tanzania kupambana na serikali iliyopo lakini wanashindwa ku mobilise watu wasiozidi 10 katika nchi ambayo kuna uhuru wa kuandamana na kuonyesha hisia zao bila repercussions. Halafu hao ndio wanaodiriki kumbeza mtu aliyeenda na mtoto wake kuandamana bila kuogopa vitisho walivyotolewa! Ni hao hao ndio wana ubavu wa kumwambia mtu aliyekaa ndani kwa miezi zaidi ya sita bila kutetereka. Please.
Na watu wakimsoma Ntobi na kusikia ndio Team ya Mwenyekiti Mbowe wanaingiwa na wasi wasi.
Hofu kubwa ni kwamba kwa miaka 21 hawa ndio FAM ameweza kuwa groom !!!
Lissu, Heche, Mnyika, Mdee n.k. wote wanakiriki kuwa wamekuwa groomed na Mbowe. Ntobi na wenzake ni generation mpya. Shida ya kizazi chake ni kuwa hawasiti kutumia lugha ambazo surrogates wa Lissu wanatumia. Hebu niambie huyo unaye mpigia debe amejenga viongozi wangapi kuanzia alipokuwa NCCR Mageuzi mpaka hapa alipo. Niambie ali groom wangapi alipokuwa Rais wa TLS? na alileta mafanikio gani kwa wanachama wa TLS? Nakumbuka alimu endorse yule Bwana aliyewahi kuwa Mkuu wa Takukuru kuwa Rais wa TLS.
Wale Vijana hawakutaka Masauni angee! basi. Hawakuwa na nia ya kumdhuru.
Sheikh alikataza sauti za nguvu za aina yeyote lakini wale vijana walianza kuzomea. Kutokana na passion zilizokuwa zimetawala wangeweza hata kupopoa mawe. Mbowe alionyesha leadership quality alipowatuliza. Na katika risala yake hakumkopesha Masauni.
Ile ilikuwa passive resistance . Hakukuhitajika busara katika passive resistance kwasababu ni jambo benign
Passive resistance, my foot. Hata mitaani wakitaka kumshughulikia mtu wanaanza kwa kumzomea. Wote tunajua hilo. Na huwezi kujua kama katika wazomeaji kuna watu wanye nia ya kuchochea fujo ili CDM ionekane ni chama cha fujo.
ANC walikuwa vitani mazungumzo yakiendelea. Ukraine wapo vitani, mazungumzo yanaendelea.
Hamas wapo vitani mazungumzo yanaendelea. Ni lazima uwe katika ''position of strength'' siyo kuwa submissive kama FAM
Mimi nilidhani hamtaki mazungumzo ya aina yeyote kabla ya matakwa yenu yatimizwe? Si ulisema alipotoka gerezani, CDM ilikuwa katika position of strength kutokana na juhudi za Lissu? Lissu alishindwa nini kuongoza mapambano kama wanavyofanya Hamas walio Gaza wakati Mbowe akiendlea na mazungumzo kama Hamas ya Qatar. Tofauti na mnavyotaka kutuaminisha, Mbowe hakuacha kufanya juhudi nyingine ili kuilazimisha serikali ikubalie matakwa ya chama chake. Maandamano yaliendelea kama kawa. Mikutano ya kuelimisha jamii iliendelea kama kawa. Hao wakina Kagaila, Ntobi n.k. kila mara walikuwa vijijini wakihamasisha watu wakishirikiana viongozi shupavu wa maeneo yale. CDM ilianza kumuunga mkono wazi wazi Aida katika mapambano yake dhidi ya DC wake. Mawakili wa CDM wamekuwa wakiendelea kuwapigania wale wote ambao bado wana kesi. Wakati wote huu kiongozi wenu mtarajiwa alikuwa M.I.A na aliwekeza nguvu zake katika Spaces. Shujaa huyu ambae mara kadhaa amekuwa akienda Ulaya kwa check up au kufuatilia madai yake coincidentally pale mambo yanapoanza kupamba moto. Alibanwa na Tanpol Mbeya akatuahidi kuwa atafungua mashtaka dhidi ya wale ambao alisema wamembana. Mpaka leo kimya. Sijamsikia sana akiongoza jopo la mawakili ambao wanawatetea wanachama wa CDM ndio maana nilifurahi nilipomsikia Mdude akimshukuru kwa kumtembelea alipokuwa mahabusu. Ninachosikitika ni kuwa sioni juhudi hizo kwa wale maskini wasio na majina kama Mdude au Sativa. Kwa maelezo yako ni kuwa hakuona shida yeyote wao kubaki kifungoni mpaka siku Katiba Mpya itakapopatikana. Empathy yake inaelekea ni selective.
Mandela alipokataa masharti ya Makaburu hakuwa conservative, alikuwa na msimamo.
Alikataa lakini aliendelea na mazungumzo. Alikuwa flexible na pragmatic. Kumbuka kulikuwa na PAC ambao walikuwa na msimamo mkali kuliko wake. Sijui wameishia wapi.
Hawa conservatives wana hoja, kwamba, submission ya FAM haileti matokeo chanya.
Hawkuwa na hoja. Walikuwa wako tayari kupoteza "the good" kwa kutaka "the perfect". Submission ya Mbowe ilileta matokeo chanya ingawa hakupata kila kitu alichotarajia. Juhudi zake zilikuwa ni kutumia mafaniko aliyopata kumwezesha kupata kilichaobakia. Hakususa, alitumia mikutano ya hadhara na maanddmano yaliyoruhusiwa kuishinikiza serikali kuhusu haja ya Katiba Mpya na Tume Uhuru ya Uchaguzi. Muitiko wa wananchi katika hiyo mikutano na maandamano ilionyesha wazi nguvu za CDM kwa wenye madaraka. Hiyo isingewekana kama wange susa kama ambavyo Lissu alitaka kulazimisha.
Kuna illusion kwamba TAL anataka play merry hell sijui ni kwa sababu zipi.
FAM hawaambii watu kwanini anataka miaka 5, na anataka kumaliza kipi alichoacha baada ya 21 yrs
FAM ametengeneza kundi la akina Ntobi kumu attack TAL ni si kueleza miaka 5 ili iwe nini, kasahau nini baada ya 21
Unashindwa nini kuamini kuwa watu kama Ntobi na Yericko wanamtetea Mbowe dhidi ya attacks za Lissu na surrogates wake kutokana na imani yao kwa Mbowe na kwa sababu wanamjua Lissu kuliko sisi wengine tunavyo mjua. Kwa nini mnakubali criticism dhidi ya Mbowe lakini hamtaki Lissu awe criticised?
Mbowe hajazungumza lolote kuhusu uchaguzi wa Mwenyekiti. Naamini ikifika wakati wake atafanya hivyo. Na inawezekana akafanya hivyo kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu tuu kama ataona taarifa zake zinaweza kuleta mtafaruku katika chama. Mimi naamini kabisa kuwa Mbowe alikuwa tayari kung'atuka lakini approach ya Lissu ya kuachia surrogates wamtukane na wamshinikize asigombee ndio ikamfanya aamue kugombea. Sababu ya kwanza alithibitisha kuwa Lissu ni mtu hatari kwa hatma ya CDM kuliko alivyodhania awali. Pili, angesema hagombei, hao surrogates wangesema kuwa kafanya hivyo kwa sababu anamuogopa Lissu. Tatu, anagombea ili kuthibitisha kuwa kuna demokrasia ndani ya CDM ambayo atathibitisha kwa kumpongeza Lissu au mtu mwingine yeyote atakaemshinda.
Ni taasisi ya Watu ! si chama chake. Haya ndiyo yanampa ugumu kuachia ngazi '' yangu''
Ni msemo tu. Kila mwanachama wa CDM anaona CDM ni chama chake. Shida ni kuwa hata wale ambao sio wanachama na hawachangii lolote sasa wanataka kuwaendesha wanachama wa CDM. Waachiane wakutane, wawasikilize wagombea wao halafu wafanye maamuzi ambayo wanaona yataleta tija kwa chama hata kama hayatapendeza baadhi ya vigogo wa chama na mashabiki wao. Uchaguzi sio beauty contest.
FAM akiwa magereza jitihada ziliendelea, alipotoka March 23 kulikuwa na miezi 9 kisha 12 ya 2024 kwa maana miaka 2 na nusu. Kumbuka tayari tuna template ya Katiba.

Ndiyo maana tume ya Mkandala ilifanya kazi kwa muda mfupi, walikuwa na reference tayari .
Muda ule wa Tume ya Mkandala ilikuwa kupoteza muda kwasababu hata leo mapendekezo yake hayana maana. FAM alipoteza muda katika vikao na CCM
Jitihada gani zilikuwa zikiendelea wakati Mbowe akiwa gerezani? Zilikuwa za aina gani? Katika mazingira ambayo watu walikuwa hawawezi hata kufanya mikutano ya ndani, hizo jitihada zilifanyika wapi? Na kwa nini hawakuendelea nazo wakati mazungumzo yanaendelea? Ni presha ya aina gani unadhani ingeweza kuwa convince CCM waifufue rasimu ya Katiba ambayo waliisha ikataa?
Of course, kila mmoja alijua Tume ya Mkandala ilikuwa ni kupoteza muda. Na Mbowe, Mnyika na wenzake walisema hivyo. Strategy yao ilikuwa ni kuhakikisha kuwa wapinzani wa kutosha wanaingia Bungeni ambako kwa kushirikiana na watakaokuwa nje ya Bunge wangeweza ku apply presha ndani na nje ya nchi! Mnachosema nyinyi ni kuwa Mbowe angesusa na kujikalia nyumbani nakulalamika mitandaoni angefanikiwa kuwa convince CCM kukubali kupitisha Katiba Mpya kwa kutumia ile ya Warioba! Please.
TAL alikataa kushirikia mambo mengi akilazimisha Katiba, Tume na Mwenyekiti.
TAL hakukubali ujinga wa TCD wala wa Tume ya Mkandala.

Alichotaka ni Katiba, Tume na Mwenyekiti aachiwe kwanza.
Pressure ya TAL ilikuwa kubwa, CCM na Serikali hawakuwa na namna.
FAM akatoka na kuanzisha Maridhiano! Farcical

Lissu alikuwa ughaibuni wakati Mbowe yuko ndani. Hiyo presha kubwa unayoizungumzia aliifanyia lini na wapi? Presha ilitokana na watu waliokuwa ndani ya nchi ambao walikuwa wanashirikiana na Mbowe. Presha ilitokana na wakina mama wa Bawacha ambao waliendelea kuandamana wakiimba Mbowe si gaidi. Presha ililetwa na umati kubwa wa wananchi ambao walikuwa wanajazana Mahakamani kila siku bila kuhoka. Presha ilititokana na wawakilishi wa Balozi ambao walikuwa wakihudhuria Mahakamani kila siku. Presha ilitokana na vijana kama Martin ambao kila siku walikuwa wanautaarifu umma jinsi mawakili wa Mbowe na wenzake walivyokuwa wakipangua mashtaka yote. Hao ndio walioifanya serikali waone kuwa ile kesi haina tija. Lissu na wenzake wa kwenye social media walichangia lakini sio kama wale waliokuwa nchini.

Amechoka! physically yupo fit !! politically amechoka!

Hii illusion inatoka wapi? Kwamba anataka merry hell l! kwa sababu zipi?
Kugombea nafasi hakumfanyi awe mtu mbaya! si wanasema ni Chama cha demokrasia!
Nani amesema Lissu anataka merry hell? matamshi yake na ya surrogates wake yanaonyesha kuwa msimamo wao ni bora wakose wote kuliko Mbowe kushinda. Kumkumbatia Msigwa ni mfano mmoja. Mwingine ni hizo spurious comments kuhusu uhalali wa uchaguzi kama atashindwa. Hiyo si Trumpian approach kuwa wafuasi wake waliokuwa nje ya Mkutano Mkuu wapigane ili matokeo yabatilishwe ili atangazwe yeye mshindi. Na hii siyo far fetched hasa ukiangalia character assasanitations zinazofanywa dhidi ya Mbowe na demand ( sio maombi) kuwa asigombee ili apite bila kupingwa. Mbowe anakuwa vilified kwa kufanya kile ambacho Katiba inamruhusu.

Mimi naona niishie hapa. Naamini kuwa tumeelimishana kiasi cha kutosha na tumefika mahali kila mmoja wetu anajua mwenzake anakotokea. Nashukuru tumeweza kufanya hivyo bila kutumia lugha za kejeli na kwangu mimi mjadala huu umenifanya nikuheshimu na kuthamini mawazo yako zaidi.

Kwa vile tumetumia muda mwingi ningependekeza hapo mbeleni tumjadili Lissu kama tulivyomjadili Mbowe.

Amandla....
 
Ni nani hapo amekuwa forced mpaka useme kuwa ni Vi coactus?
Nilikuwa najibu hoja yako kwamba '' Mara nyingi yanafanyika pale pande moja inapoona kuwa mwenye nguvu anamuonea na hamtendei au hakumtendea haki'
Ikitokea hivyo hayo si Maridhiano ni Vi coactus!

Unachomtaka Mbowe ni kuichukua CCM kuwa kama adui anaestahili kuuawa. Hiyo haitatufikishisha popote maana nae atapigana vilivyo kuhakikisha anakuua kwanza. Hilo jaribio liliishafanyika dhidi ya CDM lakini halikufanikiwa.
Ni Raia si mwanachama wa chama cha siasa nasema kwa dhati CCM ni adui.
Kama Chama kinastahili kuuawawa lakini Wanachama wake ni Raia wenzetu hawastahili adhabu yoyote!

Kuna rekodi yangu hapa nikisema, Chama chochote hata cha Fahami Dovutwa kikiwa na nafasi ya kuiondoa CCM nitaikunga mkono. Miaka 63 ni mingi sana ! Tunaelea katika lindi la Umasikini.
Ujumbe kwa watu 10 kusimama na vijikaratasi vilivyoandikwa kile amabcho kila siku anakisikia. Baada ya wapinzani hao kuchukua selfies na clips za kurusha mtandaoni wakaona wamefanya kazi kubwa.
Hao 10 wametimiza wajibu wao! tuwapongeze. Uchache wao ni mdogo kuliko Ubora wa kazi yao
Lissu, Heche, Mnyika, Mdee n.k. wote wanakiriki kuwa wamekuwa groomed na Mbowe. Ntobi na wenzake ni generation mpya.
True ! Kuhusu Ntobi huwezi kusema hajawa groomed na FAM kwa kusingizia generation! cherry-picking uh!
Ntobi ndio makampeni meneja wa FAM na hilo linatia wasi wasi sana! Hawa wanakaaje na M/Kiti
Hebu niambie huyo unaye mpigia debe amejenga viongozi wangapi kuanzia alipokuwa NCCR Mageuzi mpaka hapa alipo. Niambie ali groom wangapi alipokuwa Rais wa TLS? na alileta mafanikio gani kwa wanachama wa TLS? Mara nyingi yanafanyika pale pande moja inapoona kuwa mwenye nguvu anamuonea na hamtendei au hakumtendea haki
Simpigii debe TAL hata kidogo! hili liwekwe wazi. Nafafanua

Ukiwa incumbent una advantage nyingi. Mfano, Mbowe anaweza kutumia resource za Chama akiwa Mwenyekiti. CCM hutumia rasilimali kama ndege na magari kwa wagombea wao kwasababu huwa ni viongozi. Rais anaweza kutumia pesa za Umma kwa faida za kisiasa.
Kamala Harris alikuwa na Airforce 2 na resources nyingine kwasababu alikuwa VP

Hata hivyo, kanuni ya Newton hutumika ! To every action there is an equal and opposite reaction
Incumbents
wana disadvantage katika records . Kwamba wanahukumiwa wakati Mpinzani anatuhumiwa.

TAL hajawahi kuwa Mwenyekiti wa CDM. Ni kiongozi tu kama Makamu na mkuu wa vitengo.
Anatuhumiwa kutelekeza majukumu yake ya kisheria, kumbuka the buck stops with the chairman.

FAM kama Incumbent ana record ya miaka 33 katika politics na miaka 21 kama Mwenyekiti.
Tunamengi ya kuhoji kuhusu record yake si kwa uonevu ni kwasababu ya incumbency.

Kati ya maswali yanayotokana na record ya FAM ni haya
1. Miaka 21 kama M/Kiti ni kipi alichobakiza anachodhani anahitaji kukamilisha
2. Ni kipi atakamilisha kwa miaka 5 ambacho hakufanya miaka 21
3. Nini maono yake kuhusu Chama katika miaka 5 ijayo
4. Nini majibu ya tuhuma kama zile za ''join the chain''
5. Kuna ubaya gani kuweka ukomo wa Viongozi wakiwemo wa viti maalumu
6. Nini kilichomfanya akasua sua kuhusu suala la COVID-19
7. Viongozi wenye Wake na Wachumba COVID wanawezaje kumshauri Mwenyekiti
8. Kuna ubaya gani kutenngeneza mifumo ya uchaguzi na si hii ya nje ya Katiba
9. Kwanini ana feli na kurudia makosa yale yale.
10. Kwanini Chama kimekumbatia nadharia ya Insanity
Orodha inaendelea hadi maswali 37.5

Kwabahati mbaya, Mbowe akiwa ame groom watu wenye weledi ameamua kwenda na akina Ntobi
Nani atatetea record ya incumbent?
Sheikh alikataza sauti za nguvu za aina yeyote lakini wale vijana walianza kuzomea. Kutokana na passion zilizokuwa zimetawala wangeweza hata kupopoa mawe. Mbowe alionyesha leadership quality alipowatuliza. Na katika risala yake hakumkopesha Masauni.
Hizi ramli sikubaliani nazo! ni sawa na zile za Tanpol kuhisi maandamano yatakuwa na uvunjifu wa amani.
Unashindwa nini kuamini kuwa watu kama Ntobi na Yericko wanamtetea Mbowe dhidi ya attacks za Lissu na surrogates wake kutokana na imani yao kwa Mbowe na kwa sababu wanamjua Lissu kuliko sisi wengine tunavyo mjua. Kwa nini mnakubali criticism dhidi ya Mbowe lakini hamtaki Lissu awe criticised?
May be! ninachoelewa Mwamba amejenga empire ambayo survival ya mtu ni kwa quid pro quo . Ikiwa sivyo, watetee record ya Mwamba na si maneno ya kudhalilisha chama chao.
Makamu Mwenyekiti / Mgombea Urais/ Chief Whip halafu Ntobi anamwelezea kwa Umma tofauti!!
Sababu ya kwanza alithibitisha kuwa Lissu ni mtu hatari kwa hatma ya CDM kuliko alivyodhania awali.
Hii ndiyo Merry hell ninayosema! Uhatari wa Makamu wa Chama upo wapi?
Waachiane wakutane, wawasikilize wagombea wao halafu wafanye maamuzi ambayo wanaona yataleta tija kwa chama hata kama hayatapendeza baadhi ya vigogo wa chama na mashabiki wao. Uchaguzi sio beauty contest.
Fair enough
Nani amesema Lissu anataka merry hell?
Soma hapo juu, umesema ni mtu hatari sana. Mtu hatari anaweza kuleta merry hell! ama sivyo?
Mwingine ni hizo spurious comments kuhusu uhalali wa uchaguzi kama atashindwa. Hiyo si Trumpian approach kuwa wafuasi wake waliokuwa nje ya Mkutano Mkuu wapigane ili matokeo yabatilishwe ili atangazwe yeye mshindi. Na hii siyo far fetched hasa ukiangalia character assasanitations zinazofanywa dhidi ya Mbowe na demand ( sio maombi) kuwa asigombee ili apite bila kupingwa. Mbowe anakuwa vilified kwa kufanya kile ambacho Katiba inamruhusu.
Kigaila ndiye asimamie? Nilishauri huko nyuma watafutwe watu waadilifu!
Akina Kigaila walioshindwa kesi ya Rose Mayemba kwasababu si upande wao wakae pembeni.
Sekretariati iliyotengeneza mfumo nje ya Katiba ilitokana na maelekezo ya FAM!
Mimi naona niishie hapa. Naamini kuwa tumeelimishana kiasi cha kutosha na tumefika mahali kila mmoja wetu anajua mwenzake anakotokea. Nashukuru tumeweza kufanya hivyo bila kutumia lugha za kejeli na kwangu mimi mjadala huu umenifanya nikuheshimu na kuthamini mawazo yako zaidi.
Nakushukuru sana sana! natumaini tutaendelea na mijadala mingine ili Vijana waelewe JF ilikuwaje.
 
Nguruvi3 said:
Hata hivyo, kanuni ya Newton hutumika ! To every action there is an equal and opposite reaction
Inawezekana Mh. Mbowe akapata kura asilimia 100% ya wajumbe na hivyo ushindi wake kuingizwa kwenye Guinness Book of Records lakini akapoteza imani yetu kwake.

Bado ukweli utabakia kuwa katika watu 12,148 waliohojiwa mtandaoni watu 10,204 walimpa tick Lissu dhidi ya watu wachache 1,944 waliompa tick Mbowe.

1735718512579.png

Kwa kutumia hekima na kwa kuzingatia ushauri aliopewa Mbowe na familia yake, bado anayo nafasi ya kuachia nafasi hiyo bila kupoteza hata chembe ya heshima tunayompa.
Nguruvi3 said:
Incumbents wana disadvantage katika records . Kwamba wanahukumiwa wakati Mpinzani anatuhumiwa.
Hapo sasa, wenye masikio na wasikie,
 
Kwa kutumia hekima na kwa kuzingatia ushauri aliopewa Mbowe na familia yake, bado anayo nafasi ya kuachia nafasi hiyo bila kupoteza hata chembe ya heshima tunayompa.

Hapo sasa, wenye masikio na wasikie,
Ingawa tulishauri na kuonya lakini wapambe maslahi wakatuzidi kete lakini bado nakusihi Mh. FAM hujachelewa, chukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Mh, TAL leo hii bila kusubiri kesho.

Ukisubiri hadi kesho utakuwa umechelewa na hivyo kutukatisha tamaa wengi tulio na imani na Chadema kama chama mbadala kitakachotuokoa Watanzania mikononi mwa watesi wetu.

Haya kumekucha na vijana wazalendo wa Chadema wameonesha njia.

1736861146235.png

Bavicha wameonesha njia!​
 
Back
Top Bottom