Mbowe: Kukosa pesa za MCC Inachafua jina la nchi ktk medani za kimataifa

Mbowe: Kukosa pesa za MCC Inachafua jina la nchi ktk medani za kimataifa

Ungejiuliza kwanza bajeti ya nchi yako iliyopitishwa na wabunge wako wa CCM ambao walikuwa zaidi ya 80% bunge LA bajeti, bajeti hiyo inaonyesha utegemezi in % ngapi halafu utafakari watumwa wa akili ni akina nani.

Napata tabu kukuelekeza katika hili ,kifupi hakuna nchi isiyojiendesha kwa misaada au madeni- ni tafsiri ya hiyo 'misaada' ndio inayotufanya nchi za kiafrika zionekane kama ombaomba wa misaada. Nchi yoyote ikiingia vitani au kupata msukosuko wa kiuchumi huomba isaidiwe.
Hapa kuna maelezo yanayoweza kukupa upeo wa maswala ya misaada na madeni. Deni lililotokana na msaada wa kivita lilochukua miaka 100 kulipwa... kati ya marekani na uwingereza. deni limemalizwa mwaka huu 2015.
First World War debt paid off | UK | News | Daily Express
 
Ukiona unaamini kuwa huwezi kujikwamua kwenye matatizo yako mwenyewe kama umasikini wetu bila MCC anza kijihurumia. Ni lini msaada umewahi kumaliza shida za watu.
Jifunze kufikiri vizuri.
 
Kwanza Mbowe hamtambui Magufuli sasa kwanini aambiwe Kama haumtambui? Pili, hatuwezi kuuza Uhuru wetu kwa sababu ya vijana wa CHADEMA waliotaka kusevu matakwa ya wachache na kuleta fujo katika nchi hii.

Kwa akili ya Mbowe Marekani akimwambie Tanzania iruhusu ushoga atabadili hata na sheria ya nchi. Kama aliweza kununuliwa na LOWASSA sababu ya pesa kwanini asibadili sheria ili apate fedha za Wamarekani?

Una akili za kutosha ndugu yangu Ila hawa malofa na manyumbu hayawezi kukuelewa kama alivyo mwenyekiti wao tapeli aliyehamishia hela ughaibuni akisubiri uchaguzi wa damu halafu yeye na familia wasepe. MCC kwendeni zenu na hela zenu za Freemason. Mungu ametupa Mali za kila aina tutazitumia hatuhitaji misaada ya kafara za damu kwa ajili ya kuwafurahisha wakina Mbowe
 
Nchi zote duniani huhitaji chama imara cha upinzani kinachoweza saidia serikali iliyopo madarakani kutawala vizuri.Vyama vya upinzani imara huwa ni jicho la pili la serikali kuishitua endapo kuna madudu ndani ya serikali ambayo Raisi au serikali yaweza kuwa hayana taarifa nayo.Pia wafadhili wan je hupenda kuwepo chama pinzani imara kinachoaminika katika nchi ili kuwa jicho lao (WATCH DOG) ya kuangalia kama misaada yao inatumika ipasavyo.
Madudu hayo yaweza kuwa kashfa mbali mbali za ufisadi nk.Chama pinzani chaweza yafichua kupitia wabunge wake kulipuka bungeni n.k


CHADEMA kwa miaka Zaidi ya 20 kilijipambanua kama chama pinzani imara chenye dhamira ya dhati ya kupambana na ufisadi.Kiasi kuwa kikaaminiwa na wananchi wakawa wako tayari hata kukipelekea hati za siri za watu kama Lowasa na wengineo ili wazifanyie kazi.Na wao wakawa waaminifu wakawa wakilipuka bungeni na mikutano ya hadhara hadi baraza la mawaziri likavunjwa mara kibao kwa sababu ya hoja za ufisadi za CHADEMA bungeni.
Wafadhili nao wakatokeaa kuwaamini sana tena sana CHADEMA wakijua kuwa ni chama hodari na kilichodhamiria kupambana na ufisadi kiasi kuwa ripoti za CHADEMA za ufisadi zilipowafikia wafadhili zikiwa na majina ya akina Lowassa nk, wafadhili waliwasikiliza wakazuia misaada ya mabilioni ya pesa zikiwemo za madawa mahospitalini na za kuboresha sekta ya afya na elimu wakitaka suala la ufisadi wa watu kama Lowasa limalizike kwanza ndipo pesa zitoke
Baada ya Tanzania kunyimwa pesa za wafadhili zikiwemo za sekta ya afya na elimu wagonjwa wengi wakaanza kuwa wanalala chini na dawa zikaanza kuwa hazipo mahospitalini,watoto wakawa wanasoma wamekaa chini na serikali kushindwa kuongeza ubora wa elimu sababu ya uwezo mdogo wa serikali.

Tatizo la huduma za afya na elimu zilipoanza kudorora CHADEMA wakaanza kampeni kusema serikali ndio inayosababisha yote hayo wakati ukweli ni CHADEMA ndiyo iliyosababisha wafadhili wasimamishe misaada kwa tuhuma za kusema akina Lowasa mafisadi wakubwa wanazibomoa pesa zao.

Kama kuna chama kilichowasaliti na kuwaumiza watanzania ni CHADEMA.Watu wameumia sana kwa huduma mbovu sekta ya afya na elimu kwa sababu ya CHADEMA .CHADEMA kinatakiwa kiwaombe radhi watanzania walioumia kwa huduma mbovu za afya na elimu zilizosabisha hadi vifo kwa wengine baada ya wafadhili kusimamisha misaada kwa umbeya uliopelekwa na CHADEMA kwa wafadhili uliopelekea misaada ya kibajeti kusimamishwa.Wasizunguke tu na Lowasa wawaombe radhi watanzania kwa hasara waliyowatia kimaendeleo ya afya na Elimu.

Ndio maana nahitimisha kwa kusema mgombea Lowasa wa Chadema ALISHINDWA KUPITA KWA Kuwa CHADEMA kimelaaniwa na wale walioathirika na huduma duni za elimu na afya zilizosababishwa na kukosa hela za wafadhili.Laana ya wagonjwa walalo chini,na wakosa dawa na wale watoto wakaao chini bila madawati na kusoma kwenye nyumba za nyasi,Na walimu wafanyao kazi mazingira magumu ziliwafanya CHADEMA washindwe sana safari hii kuanzia ubunge,udiwani hadi uraisi.

Hili la MCC CHADEMA wamechangia sana kuhujumu ili pesa za wafadhili zikosekane na huduma zishindwe kufanyika halafu wao ndio utakuta baadae wanapita kubwata ona Umeme hamna ni CCM hao!! Wakati wao wamehusika kuchonga MCC.

Hebu fikiria MCC inaweza shupalia kuwa haitioi hela sababu za wale vijana wa CHADEMA na Kituo cha haki za binadamu waliodakwa na kufunguliwa mashtaka.Kesi iko mahakamani hivi MCC hawajui utawala wa sheria hadi waamue tu wenyewe kutoa hukumu kuwa serikali imekosea? Si wangesubiri maamuzi ya mahakama.Hapa wazi kunaonyesha kuna mkono wa CHADEMA.Hivi au inawezekana hiyo software ya kuingilia Uchaguzi ya hao waliokamatwa ilinunuliwa na kufadhiliwa na MCC? Kwa nini MCC wasisubiri maamuzi ya mahakama?

Zanzibar pia kuna malalamiko kuwa kuna vituo vinaonyesha wapiga kura walikuwa wengi kuliko waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.Inaonyesha wazi kuwa kule pia vijana wa IT walichezea mtandao wa ZEC kwa kuungilia.MCC kuna kitu wanaficha lakini yawezekana mtandao ule wa kuingilia matokeo ulikuwa wao.Hatua wanazochukua unaziona kabisa ni za PRO-UKAWA na zinalenga kwenye IT zaidi.MCC nao wawe wakweli.Kuna kitu hawako wazi mahali.

achana nao mkuu....hata hizo hela zao hatuzihitaji.......yan kwao rais ilikuwa awe lowassa na ndiyo maaana walijazana hapa tz kiba eti kushuhudia uchaguzi.......wakaondoka mmoja mmoja bila kuaga.......shame on them!!
 
Ukiona mtu anashabikia wazungu muogope kama ukoma. Misaada unaiua uchumi.
Sio kweli kwamba misaada inaua uchumi. Usijifariji kabisa dada nchi yetu bado ni masikini na inahitaji misaada ili kufanikisha baadhi ya mambo. Au unapinga kwa sababu ni mbowe ndo kasema?
 
Jana ilikuwa rushwa/ufisadi, leo Zanzibar na sheria ya mtandao, kesho utawala bora na keshokutwa haki za binadamu na ushoga.
Wawe sawa au wakosee bado sisi ni nchi huru tunatakiwa tutatue matatizo yetu wenyewe.
 
Tanzania sasa haihitaji pesa ya aina ya hizi za MMC.

Serikali ya JPM izungumze na wachina na ikope pesa hizo kugharamia miradi yake huku ikilipa deni hilo kwa riba yenye nafuu kuwa kabisa hata kwa miaka 15 au 20 sio mbaya.

Zimbabwe na Afrika Kusini wanafanya hivyo na wanaendesha nchi zao bila shida kubwa.

Wachina hawana minyororo kwenye pesa zao ni makubaliano tu na kazi inaanza.

Hizi pesa za kuja na masharti hazina tija sana.
 
Tatizo magufuli sio mwanadiplomasia, hajui afanye nini zanzibar, kakaliwa kooni

Walishajipanga kugawa raslimali zetu sasa imekula Kwao mafisadi nguli wanaotumia siasa na unyonge wetu kujitajirisha. Huyo mbowe haoni aibu hata aibu kuja mbele ya hakiki.kutendo chao cha kumkaribisha majizi yatawachizisha tu .
 
Ukawa hamna uzalendo kabisa yani mnazuia misaada subiri uchaguzi tuwakomeshe
 
Sasa imethibitika kuwa Bodi ya MCC iliyokaa tarehe 16 Dec 2015 imehairisha rasmi kuidhinisha msaada wa Millenium Challenge uliokuwa umekusudiwa kwa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2016.

Sababu kuu mbili zilizosababisha uamuzi huo ni:

1. Mkwamo wa Uchaguzi wa Rais na Wawakilishi Zanzibar na
2. Matumizi mabaya ya sheria ya makosa ya mtandao hususan kuhusiana na uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa 2015.

Kauli yangu juu ya jambo hili ni hii;

1. Ubabe wa baadhi ya viongozi wa CCM ni janga la Taifa. Kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote iliyo chini ya ufadhili wa MCC.

2. Sheria ya makosa ya mtandao (Cyber Crime Act 2015) ni sheria mbaya sana inayokinzana na kukua kwa technologia ya habari na mawasiliano. Aidha, kwa makisudi kabisa inafifisha uhuru wa kupashana habari na ni dhahiri ilitungwa kwa nia mbaya ya kuthibiti kijinai uchaguzi mkuu.

Tuliipinga sheria hii Bungeni na ikapitishwa usiku wa manane kwa ubabe wa wabunge wa CCM na hata tulipomtaka rais Kikwete asiisaini aliisaini kibabe akijua anaandaa mazingira gani ya "kihalifu".

Sheria hii ilitumika kuvamia vituo vyetu vya kukusanya matokeo ya kura za rais na wabunge na mpaka Leo vijana wetu zaidi ya 161 wana kesi za "kubumba" mahakamani.

Aidha Sheria hii ilitumika kuficha dhana ovu kuvamia kituo cha Sheria na haki za binadamu (LHRC) waliokuwa wakikusanya matokeo ya kura za Rais .

Vile vile Sheria hii imetumika kuwakamata na kuwaweka ndani na hata kuwanyima dhamana vijana wetu ambao walituunga mkono katika uchaguzi mkuu.

Namtaka rais Magufuli achukue hatua za kiuongozi na kiutawala kwa kufanya yafuatayo:

1. Aumalize mgogoro wa kisiasa Zanzibar kwa kuhakikisha kuwa mshindi halali anatangazwa .

2. Achukue hatua ya kuifanyia marekebisho makubwa Sheria ya makosa ya mtandao katika bunge lijalo. Aidha wale wote waliobambikiwa kesi amuamuru DPP kuzifuta kesi hizo Mara moja.

Hatua hizo zitalinusuru taifa na hasara ya kupoteza mabilioni hayo ya MCC na zaidi kuepusha kuporomoka zaidi kwa biashara ya Utalii nchini Zanzibar.
Mbowe sisitiza kulipa kodi na kukusanya kodi. Mambo ya kutegemea ufadhiri yamepitwa na wakati. Upinzani mje na ajenda zenye tija kwa taifa. Siyo kuhamasisha uombaomba.
 
Nilijua tu maadam Dr Slaa hayupo CHADEMA kitakosa hoja za kueleweka za kuongea,Dr Slaa angekuwepo angemtia moyo Dr Magufuli kutoogopa kukosa fedha za MCC kwasababu nchi yenyewe ina fedha za kutosha za kujiendesha.Dr Slaa alikuwa anapinga misaada kwakuwa ilikuwa inatengeneza mental slavery na entitlement yaani kuhisi kama mna wajibu wa kufanya chochote mtakachoambiwa na wafadhali wenu kama vile kukubali ndoa za jinsia moja au kusaini mikataba mibovu yenye kuliingizia taifa hasara;pamoja na kujiona mna haki ya kuendelea kuomba misaada (entitlement). Mbowe anapaswa kufahamu kwamba kumtaka rais aendelee kukumbatia misaada ni sawa na kumshauri rais aendelee kuuweka uhuru wa nchi wa kujiamulia mambo yake yenyewe rehani.Yeye kama kiongozi wa upinzani alipaswa kumwonyesha rais alternative ya kujipatia pesa za kuiendesha bila kutegemea misaada,misaada ina gharama zake.
 
Mbowe ni bepari, kibaraka anayeunga mkono utegemezi...
CCM inaamini katika Ujamaa na Kujitegemea, umaskini jeuri...
Anachanganya mambo ya MCC na maslahi yao ya chama... Sioni hoja!
 
Watu wa aina ya Mbowe ndo hugawa nchi zao kwa wakoloni...

Uko sawa, Wachaga waumini wa Sera ya majimbo waliukubali ukoloni wakati wenzao wakipambana nao kwa hasira. Ni jambo la asili..
 
Hizo fedha za MCC ndizo zilizofanya ndugu zenu waishio vijijini kupata umeme. Kama Magufuli ana dhamila ya dhati kusaidia Taifa hili hana budi kutatua mgogoro wa zanzibar haraka sana. Nashangaa kuona watu wanamshabikia Magufuli kama timu ya mpira. Sasa naanza kuamini tafiti zilizoonesha kuwa "BLACK PEOPLE ARE NOT AS SMART AS WHITE"

Nafikiri kuna kipengele naweza kutumia na kukushitaki kituoni kwa kunidhalalisha mtandaoni kama mtu mweusi.

Naogopa hata kutumia vi emoj kusema jinsi ulivyonikuna.Kwangu hilo ni tusi, kama mtu mweusi.

Anyways, "white man can't jump"
 
Back
Top Bottom