Mbowe, mkanye Lissu

Lissu piga spana za vichwa mpaka akili ziwakae sawa.

Halafu baadae aje awaombe kura hao hao Wananchi ambao anatrigger emotions zao? Nilikuwa ni shabiki mkubwa sana wa Lissu na niliumia sana alivyopigwa risasi,kukaa kwake kimya kwa sasa kungepandisha hadhi yake zaidi kuliko huu upuuzi anaofanya,amefanya nianze kufikiria mara mbili kama nilikuwa sahihi kumsuport huko nyuma. Trust me,Mbowe is a real Man na Lissu anaonekana mpuuzi tu kwa sasa! Kunyamaza kungempa heshima zaidi. Endeleeni kumpump,come 2025 kama atakuwa ndiye Mgombea,CDM itaangukia pua tena.
 
Lissu anajua sehemu za kupiga mpaka nyoka anatoka pangoni.Chezea Mwanasheria[emoji23]

CCM wao wanajua wapi pa kuwapiga Spana,2025 ndiyo mtaelewa. Endeleeni na mbwembwe zenu za twitter. Uzuri wapiga kura hawajui hata twitter inafananaje.
 
Any way ila kwa Mimi kama jitu nilinikosakosa kuniua siku likifa ntatamani nipige konzi hadi mait
 

Nimejiuliza mara mbili,ilikuwaje 2020 nikampa kura huyu? Mbowe ni Mwanasiasa,Lisu abaki tu kwenye Uanaharakati.
 

Sijaelewa, Msio na chma then nyie ni wanaCHADEMA??
 
UPUUZI MTUPU!
 
Unaandika "Mwambie atakama anauchungu na kisasi kwa Yale aliyofanyiwa mwambie kwa nafasi take hastahili kufanya anayoyafanya labda Kama Hana mpango wakugombea"

Lissu hawezi kugombea tena Urais Tanzania wala wenyekiti CHADEMA. Nafasi kubwa anayeweza kugombea ni ubunge jimboni kwake tu. Hata kabla uropokaji huu alishaharibu katika kampeni zilizopita za Urais na CHADEMA wanalijua hilo.

Katika kampeni za uchaguzi wa Urais alifanya makosa yafuatayo:


  • Alizibeza shule za kata bila kutoa ufumbuzi (Hapa alipoteza 35% ya kura)
  • Aliibeza lugha ya kiswahili kutumika mashuleni (hapa alipoteza 40% ya kura)
  • Nyinginezo jazeni wenyewe, bila kusahau Uropokaji, hulka anayoendelea nayo mpaka sasa hivi.
Alamsiki na muacheni aendelee kujipambanua, wala msimhusishe Mbowe ktk hili, kwa vile hawezi kumkanya. Ni sikio la kufa hilo.
 
Kwa nini akanywe Lissu?
Akina Musiba hamkuwaona na kuwasikia wakisema watavunja watu miguu bla bla
Lissu ana machungu
Risasi alipigwa yeye
Maisha yake yamebadilika
Msilazimishe jambo
Zungukeni mkimaliza maisha yataendelea
Vijiwe vitaongezeka
 
yaaan alivokuwa anaropoka kwenye ugonjwa mpaka uchungu wa uzaz unatushika.yelewiiii yan kutibua nyongo .najitoa chadaeme
 
Utamaduni wenu unasema mtu akipigwa risasi mnagonganisha gilasi ya mvinyo kusheherekea!
 
Pamoja na kwamba tupo msibani kuomboleza kifo cha mwanaAfrika na Mwanamajumui Hayati John Pombe Magufuli, imenilazimu kuhoji huyu ndiye Mh Lissu Wakili msomi aliyetaka kuwa Rais wetu 2020?

Nimesoma Twitter zake na maandiko yake mbalimbali baada ya msiba wa JPM. Nikajiuliza hivi huyu ndiye alipaswa kuwa Rais? Kwa tamaduni, mila na desturi za Kitanzania na Afrika kwa ujumla si sawa kushangilia kifo hata kama mtu alikuwa humpendi kwa kiwango chochote. Haturuhusu kumhukumu Marehemu, Mungu ndiye mwenye uwezo huo.

Tusiandike kama hatujawahi kufiwa au kama sisi hatutakufa. Kila mtu duniani atakufa na atakufa kwa stahili yake. Kipindi hiki ambacho ndugu jamaa na rafiki wanapopitia kipindi kigumu sisi sote tunapaswa kuwafariji kwa kuwa hakuna anayejua kesho yake.

Nimpongeze Mh Mbowe ambaye statement yake inaonesha namna alivyoiva na anavyothamini uhai. Mh Mbowe ameonyesha nguvu yake ya maarifa na uhodari wa kuchambua maneno kulingana na mkutadha. Kwa mazingira haya simuoni mtu wa kuvaa viatu vya Mh Mbowe Kama Mh Lissu ambaye nilidhani ni matured naye anaweza kuandika vitu vya kitoto ambavyo walau vingeandikwa na BAVICHA.

Tunatambua Lissu alipigwa na kuumizwa, lakini tunamshukuru Mungu mwingi wa rehema alimponya na sasa yupo hai, lakini kitendo cha kupona kwake hakiondoi ubinadamu na kupandikiza umbumbumbu kwenye argument na reasoning.

Lakini pia hii ni indicator kwenu CHADEMA Kama munadhani Lissu will be a good candidate for 2025, basi aingie darasani kwa mzee Mbowe kujifunza hekima na kuchambua mambo kabla ya pablicity.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…