Pre GE2025 Mbowe: Mtu wa kwanza kuwajibishwa kwenye matukio ya utekaji ni Rais Samia. CHADEMA kuanza kampeni ya 'Samia Must Go'

Pre GE2025 Mbowe: Mtu wa kwanza kuwajibishwa kwenye matukio ya utekaji ni Rais Samia. CHADEMA kuanza kampeni ya 'Samia Must Go'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Msingi wa hoja hii unajengwa na Ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) Toleo la mwaka 2005 kama ilivyonukuliwa hapa chini:-

8. (1). Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo:-

(a) Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi Kwa mujibu wa katiba hii;

(b) Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;

(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;

(d) Wananchi watashiriki katika shughuli za serikali yao Kwa mujibu wa masharti ya katiba hii


========================================
Kwa mujibu wa Ibara ya 8 ya katiba hii, kumbe kila kiongozi mwenye madaraka na mamlaka ya kiserikali akiwemo aitwaye "Rais" amepewa au tumempa sisi wananchi.......

Kama ni hivyo, kumbe pia wakati wowote (si lazima kusubiri uchaguzi) tukiona hawezi au ameshindwa au anayatumia vibaya madaraka na mamlaka hayo, SISI TENA WANANCHI tunaweza kumtoa kwa njia halali kwa mujibu wa katiba hii hii katika muktadha wa Ibara hiyo hiyo ya 8 [1] (a) - (c) kwa kutumia njia halali 3 zifuatazo:

1. Shinikizo la umma (public pressure):

Hufanyika kwa utaratibu wa kupaza sauti kuonesha na kulisema tatizo. Sauti ikishindwa kusikika na kueleweka kwa wahusika, njia hii huenda hatua inayofuata ya juu zaidi yaani maandamano ya amani (mass mobilization) yakiwa yamebaba ajenda hiyo hiyo tu....

Hii njia ni very effective yenye kuleta matokeo ya haraka. Viongozi walengwa wanaiogopa sana. Na kwa sababu hii, njia hii mara zote huwa ni ngumu yenye risks nyingi kwa sababu huhusisha mapambano na vyombo vya dola kama polisi na hata Majeshi ya ulinzi ambayo huwa chini ya udhibiti na amri za kiongozi (Rais) anayekataliwa na kutakiwa kuondoka....

2. Kwa njia ya mashitaka ya ki - Bunge kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na wabunge maarufu kwa kiingereza kama "impeachment......"

Hii ni njia ngumu na pengine isiyowezekana kabisa ingalau katika mazingira ya sasa kwa sababu ya masharti yake kama yalivyo katika Katiba ya JMT Ibara ya 46A (1) - (11) sambamba na Ibara ya 90 (1) - (2) juu ya nguvu Rais aliyonayo kulivunja Bunge wakati wowote kwa sababu anayoweza hata kuitengeneza tu......

3. Kwa njia ya uchaguzi wa HAKI, HURU na wa WAZI.

Hii ndiyo njia kuu ya kidemokrasia iwapo mambo yako kawaida. Chaguzi mara nyingi zina vipindi vya muda maalumu. Hapa kwetu Tanganyika ni kila baada ya miaka mitano....

Kwa mazingira ya Rais aliyeshindwa kutekeleza wajibu wake, wananchi na nchi haiwezi kusubiri miaka mitano ifike ndiyo tuondoe tatizo......

##Ndo kusema kuwa movement ya CHADEMA ya "SAMIA MUST GO" si kuvunja kuvunja wala sheria yoyote ile. Hili ni shinikizo la umma kwa mtu ambaye yuko chini ya mamlaka yao kushindwa kutekeleza wajibu wake kwa makusudi au kwa kuwa tu uwezo kiuongozi ni mdogo.....

##Polisi wao ndiyo wanavunja sheria na Katiba kwa kuanza kutisha watu ili wasi - exercise haki yao kuwajijibisha kiongozi wao (Rais) ambaye ame - prove total failure ktk kulinda uhai wa wananchi/watulioshindwa kwa mujibu wa Ibara ya 8 [1] (a) - (c)...

##Katika hali hii, wananchi (umma) ni lazima tuyatumie mamlaka yetu kwa ukamilifu...!
Njia pekee ni pressure tuuu huyu bibi atasusa na kujiondokea. Mapinduzi au mbinu yoyote ya aina yake haifai hata kidogo kwa nchi tuliyochagua kujitawala kidemokrasia na amani.

Muhimu ni hiyo political pressure bi hangaya asusie mkate kwa amani au 2025 tumdondoshe kwenye sanduku la kura!
 
Umemaliza yote.
Njia ya kwanza ni nguvu ya umma

Atuachie nchi. Tupate katiba mpya nsipo tuwe na tume maridhawa ya uchaguzi
 
images.jpeg-90.jpg
 
Nasubiri kama kuna Chawa Smart atakayeweza kupinga hivyo vifungu kwa hoja tofauti na kuandika Mitano tena.
 
Mbowe akiwa kwenye mkutano wa waandishi uliohudhuriwa na wanachama wa CHADEMA asema wataanza na kampeni ya Samia Must Go ikiwa hakutakuwa na uwajibikaji kwenye matukio ya utekaji.

Mbowe pia ametoa rai kwa viongozi wa CHADEMA siku 12 kuanzia sasa kuja Dar kwaajili ya kupeana mikakati muhimu kwa hatua zaidi.

Soma Pia:

=====

"Kisiasa, n ani vyema mkasikia bunge la Tanzania, mwaka jana (2023) katika mabadiliko ya sheria ya usalama wa taifa ilipeleka usimamizi ya idara ya usalama wa taifa moja kwa moja Ikulu kusimamiwa na Rais, na sheria ile ilitoa kwa mara ya kwanza haki ya watu wa usalama wa taifa kukamata watu, kuwaweka kizuizini, bila kueleza mahali popote wala bila kushtakiwa.

"Sheria hii ilivyopitishwa Rais aliipitisha na akajimilikisha mamlaka ya usalama wa taifa. Sasa mimi kwa niaba ya CHADEMA na vikao na vikao vyangu, tuna declare mtu wa kwanza kuwajibishwa katika masuala hay ani Rais Samia Suluhu Hassan.

"Na sisi tunasema tunaanza moja kwa moja kampeni inayoitwa ‘Samia Must Go’, hiyo ndiyo rai yetu. Sasa basi, kwasababu bado tuna msiba, tumekubaliana kwamba tuna msiba kwasababu kuna viongozi wetu hatujui wako wapi. Kwahiyo sisi kama chama hatujamaliza msiba. Tutaendelea na msiba wetu kitaifa na bender azote za chama zitapeperushwa nusu mlingoti hadi tujue watu wetu wako wapi, wako hai au mauti

"Lingine, kuanzia siku ya Jumatatu, tar 23/9/2024 mkumbuke nilitangaza tar 21 tunategemea tuone hatua za watu kuwajibika zimeanza. Kama hawatachukuliana hatua wenyewe kwa wenyewe, sisi kuanzia tarehe 23 jiji lote la Dar es Salaam, kila kata kila mtaa.. ndugu zangu tumekuwa tunafanya utani mara nyingi, lakini kwa wakati huu hatuna utani.

"Kuanzia jumatatu sisi tutaingia barabarani kudai tunachoona ni uhai wa watu wetu waliopotenzwa unless serikali imechukua hatua za haraka na za makusudi kuwarejesha, watu kujiuzulu na watu wote kuwajibika kwa mujibu wa tamko letu la leo." -
Amesema Mbowe katika mkutano kwenye ofisi za CHADEMA, Mikocheni leo 11/9/2024

Labda iwe mbowecdm must go
 
GXhc8iGXoAA4NhV.jpeg


Mbali na mauaji, Utekaji na Uhalifu wa serikali dhidi ya watanzania ambao wamekosa amani katika nchi yao
1. Ajira hakuna vijana wanateseka mtaani
2.Huduma za afya ni mbovu, Bima ya afya kwa watoto irudishwe
3.Matumizi ya hovyo ya fedha za umma kwa ziara zisizoisha na zisizokuwa na tija kwa taifa
4.Katiba mbovu inayopelekea utawala wa chama kimoja huku tume ya uchaguzi ikiwa haina uhuru wa kweli
5.Wizara TAMISEMI kusimamia chaguzi za SM
6.Bandari kuuzwa kwa waarabu
7.Wamasai kunyang'anywa ardhi yao ya asili

Kwa hayo machache 'Samia Must Go" inapaswa kuungwa mkono na mtanzania yeyote mzalendo anayeipenda nchi yake.Ni haki yangu kikatiba. Tukutane 23/09/2024

GX2sfoIXQAAKGqc.jpeg
 
Watanganyika wengi wetu ni waoga sana, ingewezekana ingekuwa poa sana.
 
Watanganyika wengi wetu ni waoga sana, ingewezekana ingekuwa poa sana.
 
😹😹Samia must go ukae ww au🚮😂😂hatupendi shazi bana sisi kaandamane mwenyew uko..Tena taratibu msitupigie kelele👍
 
Tushakod Gen z kutoka kenya watatu tu wanatosha kukiwasha hapo kati...
...sa100 must go...
 
ZINGATIA Slogan
"UOGA WETU NDIYO SILAHA YAO"...
Imekaa kimagumashi sana
 
hakuna muandamanaji hapo, utaishia humu huku kupost picha kutoka Twitter.
 
Haijulikani ni shinikizo la wafadhili wao, imani potofu za kishirikina, ramli au muujiza umewatokea...

Hata hivyo awali kulika na migawanyiko baina ya viongozi waandamizi wa Chadema kuhusu slogan ya Samia must go, kwamba kivyovyote Lazima itaambatana na fujo na isingewezekana kua ya amani.

Lakini viongozi wengine walienda mbali zaidi na kudai kwamba tangazo la maandamano lilifanyika kwa mihemko bila tahmini ya kina, na hivyo Samia Must Go Ilikua ni kwenda kinyume na misingi ya kidemokrasia ya chama hicho..

Kupitia barua yao ya usiku wa manane kwa jeshi la polisi iliyoonekana leo, inaonyesha kuna mabadiliko ya kimyakimya au ya kuzinduka usingizini yamefanyika dhidi ya dhima, dhumuni na nia ya maandamano ya kuvuruga amani ya fujo ya Samia must go.

Sasa eti yamebadilika na kua sijui maandamano ya nini vile? Huenda Chadema hawajui hata wanadai wala wanatetea nini. Na Tatizo ni dhahiri Uongozi wao..

kiufupi kwa maoni yangu hawezi kufanikiwa wala kuruhusiwa kuandamana kabisa.

Na upo uwezekano mkubwa sana wakaahirisha maandamano hayo, kwasababu moja haikai, mbili haikai miongoni mwao.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom