Mbowe na Wenzake 3 wakutwa na kesi ya kujibu. Kesi imeahirishwa hadi Machi 04, 2022 watuhumiwa kuanza kujitetea

Maamuzi madogo au hukumu za kesi kama hii, lazima zielezewe vizuri kwa wananchi ili wajenge Imani na mahakama vinginevyo tutajenga kizazi kinachofikiria kuwa hata maamuzi ya mahakama ni kama kamari.

Acha tujipe muda...

Hii Common sense ya Majaji watu wanaona inaendeshwa na watawala.
 
Mimi simshabikii Mbowe wala Serikali. Haki iende kwa mwenye haki. Period.
Hapo sasa tupo pamoja Mr Animo.

Wale mahakimu na Kingai kama waliamua kupindisha sheria ili kummaliza Mbowe kama walivyofanya kwa Tundu Lissu ( Kwa sababu za kisiasa) basi watalaaniwa na mwisho wao utakuwa hapa hapa duniani.

Siasa ni kushindana kwa nguvu za hoja ila sio kwa ubatilifu na hila.
 
Kesi ya Sabaya unaweza kuilinganisha na hii ya Mbowe? Ya Sabaya Hadi ushahidi wa Video ulisimama na mwenyewe alikiri kutumwa na Maguful.
Hii ya Mbowe Ni planned
Comment bora ya wiki hii.
 
Katiba mpya ndiyo suluhisho la unyama woote huu
 
Only in tz ugaidi unafadhiliwa kwa sh efu87 ambayo imetumika nauli na chakula wakabaki hawana ata mia mbovu, vijana wa watu wametafutiwa kibarua cha ulinzi saivi wameitwa ugaidi na watu wasokuwa na utu Mungu wetu yu hai atasimama
Denis Urio ni mtu wa kuteseka maisha yake yoote
 
Kwani samia ndio alimtuma Mbowe atafute x soldier, Mungu aangalii eti kosa ni mpinzani afanye maovu, know mungu ni mtenda haki, intention ya Mbowe haikuwa nzuri, na haya anayoyapitia inawezekana kabisa ni damu za watu zinamuhukumu, mbona mimi nisipitie wala wewe, au Mnyika, au Msigwa, mfano tuu mungu anisamehe Chacha Wangwe ile damu kuna mkono wa Mbowe ndio hizi laana zinamwandama
 
Aliyekwambia Mbowe ni msafi ni nani?? Ameshiriki mara ngapi kutoa uhai wa wenzake?? Ben Saanane yuko wapi, Wangwe yuko wapi? Kwa akili yako unadhani Mbowe hakuhusika?
 
Na Lisu alipigwa zile risasi kwa damu ya Nani? Kuwa huru kifikra acha kutetea ujinga usiokuwa na maana.nimeuliza wale Askari katifutiwa na Urio vipi unamuondoa Urio kwa kumtafutia mtu muovu watu wa kufanya uovu. Haya hao makomando walikuwa awajuani na mbowe wewe unamtoaje Urio kwenye Hatia. Maana kama una uwezo kwa kufikiri kesi ilikuwa ya mbowe pekee yake kwa Urio kujua Nia mbaya ya mbowe angekamatwa ashitakiwe. Mbona usapoti uchunguzi kwa swala la Lisu. Au kwa kuwa mnausika kutaka kumuuwa. Acheni Ushetani.
 
Msamaha wa Rais utamuhusu maana rais hawez ingilia uhuru wa mahakama
 
Aliyekwambia Mbowe ni msafi ni nani?? Ameshiriki mara ngapi kutoa uhai wa wenzake?? Ben Saanane yuko wapi, Wangwe yuko wapi? Kwa akili yako unadhani Mbowe hakuhusika?
Mtieni hatiani. Mbona nyinyi mmeuwa kina alphone mawazo mchana kweupe na mkapiga Lisu risasi peupe. Mpaka zee kenu limekufa na laana za damu za watu
 
Mtieni hatiani. Mbona nyinyi mmeuwa kina alphone mawazo mchana kweupe na mkapiga Lisu risasi peupe. Mpaka zee kenu limekufa na laana za damu za watu
Lissu ni mpango wa Mbowe, ndio maana dereva wake alikimbia mzee.
 
Hii pic kwenye avatar ni ya mtu fulani hv ! ama ni ww umebadili jina?
 
Aliyekwambia Mbowe ni msafi ni nani?? Ameshiriki mara ngapi kutoa uhai wa wenzake?? Ben Saanane yuko wapi, Wangwe yuko wapi? Kwa akili yako unadhani Mbowe hakuhusika?
Hawa wana CHADEMA huwa ni wapuuzi sana! Unaweza kudiriki kusema Mbowe ni msafi kwa lipi hasa? Maana anashutuma kibao za mauaji!
 
Mungu wa mbinguni awabariki nyote.

Mungu wa mbinguni mbariki Freeman Mbowe

Mungu wa mbinguni awabariki makomandoo!
EU Mhimili wa Dunia.......

Mungu ibariki Tanzania. na wapenda Haki popote Ulimwenguni...kutoka Kivu Mashariki Macho yote ya Dunia yameelekezwa Tanganyika
Yametimia hatimaye,Team roho mbaya wataficha wapi nyuso zao za makunyanzi?
Mh.Mbowe siyo gaidi.
Leo FAM hatoki.. watamkuta ana kesi ya mchongo ya kujibu

Angalizo,wakifanya hivyo kitaumana.
Kesi ya FAM na wenzake ipo na itaendelea kwa muda mrefu.
Muhimu kujua ni kuwa hii ni kesi ambayo kila upande una mengi ya kupata na kupoteza
Utetezi wanapoteza uhuru wao lakini wanapata ushawishi na heshima kwenye jamii.
Upande wa mashitaka wanapoteza ushawishi na imani. Wanaongeza chuki na kudharaulika.
Wananchi wao wanapotezewa muda lakini wanapata fursa kubaini mambo mengi ya serikali na mahakama.

NB: Tunapomuomba MUNGU tusiombe kupewa unafuu au kufutiwa mitihani bali tuombe kupewa nguvu, ujasiri, afya, ulinzi, weledi na busara zaidi kukabiliana na changamoto zetu na wanaozisababisha!
Tumeumbwa kuwa imara zaidi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…